Advertisements

Friday, October 24, 2014

SHEREHE ZA MIAKA 50 YA USHIRIKIANO WA KIDIPLOMASIA KATI YA TANZANIA NA CHINA HUKO BEIJING

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Ndugu Li Yuanchao wakati walipokutana kwenye Sherehe ya kutimiza Miaka 50 ya Uhusiano wa Kidiplomasia baina ya Tanzania na China. Sherehe hizo zilizoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini China na kufanyika jijini Beijing.
Makamu wa Rais wa China Ndugu Li Yuanchao akigonganisha glasi ikiwa ni ishara ya kusherehekea kutimiza miaka 50 ya ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China. Sherehe hizo zilifanyika jijini Beijing. 
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akigonganisha glasi na Mama Salma wakisherehekea kutimiza miaka 50 ya ushirikiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na China.
Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Bernard Membe wakisherehekea kutimiza miaka 50 ya Ushirikiano wa Kidiplomasia baina ya Tanzania na China kwa kugonganisha glasi zao huku Mama Salma na Makamu wa Rais wa China Ndugu Li Yuanchao (aliyesimama kulia) wakishuhudia. Sherehe hizo zilifanyika Beijing nchini China. PICHA NA JOHN LUKUWI

No comments: