Advertisements

Wednesday, August 31, 2016

BREAKING NEWS: CHADEMA WASITISHA MAANDAMANO YA UKUTA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesitisha maandamano ya UKUTA ambayo yalipangwa kufanyika Septemba 1 (kesho) baada ya kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa viongozi wa dini.
Akiongea na waandishi wa habari muda huu, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amesema chama kimeona kisitishe maandamano kwa muda ili kiwaachie viongozi wa dini watafute suluhu kuhusu suala hilo.
“CHADEMA tunaomba kuwatangazia watu wote kwamba tunahairisha mikutano ya kisiasa na maandamano yote kwa muda wa mwezi mmoja,” alisema Freeman Mbowe

5 comments:

Anonymous said...

Hapakuwa na chochote hapo. Nani mjinga angeacha kazi zake kufuata ujinga wa wanasiasa wanaojitafutia umaarufu. Magufuli alishinda muacheni afanye yake mkutane uchaguzi ujao. Msiwapotezee watu muda wao.

Anonymous said...

What breaking news? One must have been too dumb not to see this coming. These guys are just playing games. They keep loosing their credibility each passing day.

Anonymous said...

Hawa jamaa wa Moshi/Arusha wasirubuni wananchi. They have the time and money to waste.

Anonymous said...

Unadaiwa rent unaitisha maandamano nchi nzima!

Anonymous said...

hii ndio kula ya watu wengine. kisha wemgine wanafuata mkumbo. kalipe pango kwanza