Advertisements

Monday, May 20, 2019

RAIS DKT. SHEIN AONGOZA WANANCHI WA ZANZIBAR KATIKA MAZIKO YA WAZIRI WA ZAMANI MAREHEMU ALI JUMA SHAMUHUNA KIJIJI CHA DONGE MKOA WA KASKAZINI UNGUJA LEO

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hassan Khatib alipowasili katika hafla ya maziko ya aliyekuwa Waziri wa Zamani wa SMZ Marehe Ali Juma Shamuhuna, kushoto Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Mohammed Aboud na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Haji Omar Kheri, alipowasili katika Kijiji cha Donge Imiyani.(Picha na Ikulu)
 BAADHI ya Wananchi kutoka sehemu mbalimbali Zanzibar wakijumuika katika hafla ya maziko ya Marehemu Ali Juma Shamuhuna yaliofanyika katika Kijiji cha Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja leo, 20-5-2019.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.,Dk. Ali Mohamed Shein, akishiriki katika Sala ya kuusalia Mwili wa Marehemu Ali Juma Shamuhuna, maziko yaliofanyika katika Kijiji chao Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja.leo 20-5-2019.(Picha na Ikulu)
 WANANCHIna Waumini wa Dini ya Kiislam wakiitikia dua baada ya kumalizika Sala ya kuuombea mwili wa Marehemu Ali Juma Shamuhuna iliofanyika katika msikiti wa Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.20-5-2019
 WANANCHI wakiwa wamebeba jeneza likiwa na mwili wa Marehemu Ali Juma Shamuhuna wakati wa maziko hayo yaliofanyika Kijijini kwao Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.
 VIJANA wa Chama Cha Mapinduzi walioandaliwa kwa ajili ya kubeba jeneza la Marehemu Ali Juma Shamuhuna wakati wa maziko hayo wakielekea katika eneo lililotengwa kwa maziko hayo katika Kijiji cha Imiyani Donge Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Ali Juma Shamuhuna wakati wa maziko hayo yaliofanyika katika Kijiji cha Imiyani Donge Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.20-5-02019
 MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Ali Juma Shamuhuna
 WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud Mohammed akisoma wasifu wa Marehemu Ali Juma Shamuhuna, baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya maziko iliofanyika katika Kijiji cha Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja
  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi, na Wananchi wakiitikia dua baada ya kumalizika kwa Sala ya kuusalia mwili wa marehemu iliofanyika kjatika Masjid ya ilioko Kijiji Kwao Donge Imiyani Mkoa wa Kasakazini Unguja leo.20-5-2019.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akitowa mkono wa pole na kuifariji familia ya Marehemu Ali Juma Shamuhuna,wakati wa msiba huo uliofanyika Kijiji kwao Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja leo
RAIS wa Zabnzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiitikia dua ikisomwa na Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, wakati wa hafla hiyo ya maziko ya Marehem,Ali Juma Shamuhuna yaliofanyika Kijiji kwao Donge Imiyani Mkoa wa Kaskazini Unguja leo. (Picha na Ikulu)

No comments: