Advertisements

Tuesday, July 27, 2021

RAIS DK.MWINYI AJUMUIKA KATIKA MAZIKO YA ALIYEKUWA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA KUSINI UNGUJA MAREHEMU RAMADHAN ABDALLA KICHUPA KIJIJINI KWAO JAMBIANI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia Dua ya kumuombea aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja Marehemu Ramadhan Abdalla Ali (Kichupa) baada ya kumalizika kwa Sala ya Jeneza iliofanyika katika Masjid Salam Jambiani Kijijini kwao Mkoa wa Kusini Unguja.
VIJANA wa Chipukizi wa Mkoa wa Kusini Unguja wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa Marehemu Ramadhan Abdalla Ali ( Kichupa) aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Unguja, maziko yaliofanyika Kijijini kwao Jambiani.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Ramadhan Abdalla Ali (Kichupa) maziko yaliofanyika Kijiji kwao Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akitowa mkono wa pole kwa Familia ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja Marehemu Ramadhan Abdalla Ali (Kichupa) alipofika nyumbani kwa marehemu kijijini kwao Jambiani.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume.( hayupo pichani) baada ya kutowa mkono wa pole kwa Familia ya Marehemu Ramadhan Abdalla Ali (Kichupa) aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja, maziko yaliofanyika Kijijini kwao Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi na (kulia kwa Rais) Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Rais Mstaaf wa Zanzibar Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Mstaaf Balozi Seif Ali Iddi na (kushoto kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja.Mhe. Rashid Hadidi Rashid, wakiitikia dua ikisomwa na Sheikh.Hassan Simai Makame, baada ya kumalizika kwa maziko ya Marehemu Ramadhan Abdalla Ali (kichupa) yaliofanyika Kijijini kwao Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.(Picha na Ikulu

No comments: