Advertisements

Monday, April 17, 2017

EKA 17 ZA MASHAMBA YA BANGI ZAFYEKWA

Polisi Mkoa wa Arusha wameteketeza eka 17 za mashamba ya bangi katika Kata ya Kisimiri, wilayani Arumeru.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema mashamba hayo yalitekelezwa wakati wa msako maalumu.
 
Mkumbo alitoa onyo kwa wananchi wanauzunguka Mlima Meru ambao wamekuwa wakilima bangi kwa kisingizio kuwa, polisi hawawezi kufika.
 
“Kuna mtindo wa kulima bangi milimani hasa Mlima Meru, tunasema tutaendelea na msako kubaini wote wanaohusika,” alisema.

Aliwataka viongozi wa mitaa na madiwani kuwa makini na kudhibiti kilimo hicho haramu kwenye maeneo yao. Kamanda Mkumbo alisema kwa sasa umeanzishwa mtindo wa baadhi ya wananchi kuchanganya bangi na mazao mengine ili kupoteza ushahidi.
 
“Wanachokifanya sasa wanachanganya miche ya mazao na bangi, kwa hiyo inakua pamoja tutaendelea na msako huo kila kona lengo ni kuhakikisha kunakuwa na ukomo wa kilimo hicho cha dawa za kulevya mkoani hapa,” alisema Mkumbo.

No comments: