Advertisements

Tuesday, April 18, 2017

MWIMBAJI JIMMY GOSPIAN ASHINDA TUZO YA ZABURI AWARDS 2016/17 KANDA YA ZIWA

Jimmy Gospian akipokea tuzo yake, Mwimbaji Bora Chipukizi wa Kiume
Jimmy Gospian anatamba na nyimbo mbalimbali ikiwemo wimbo uliomtambulisha vyema uitwao, Nakujua Bwana

Jimmy Gospian (kushoto) akipokea pongezi kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Famara Entertainment
Baadhi ya waimbaji wa Kwaya ya AIC Chang'ombe Vijana Choir

Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliojitokeza kwenye utoaji wa tuzo hizo
Mwimbaji chipukizi wa muziki wa Injili Jijini Mwanza, Jimmy Gospian (kushoto), ameibuka mshindi kwenye Tuzo za ZABURI AWARDS 2016/17 zilizotolewa jana kwa waimbaji wa Injili Kanda ya Ziwa na Kampuni ya Famara Entertainment, Uwanja wa CCM Kirumba.

Gospian kutoka ngome ya BMG, aliibuka mshindi katika kipengere cha Mwimbaji Bora Chipukizi wa Kiume ambapo washindi wa tuzo hizo walipatikana kwa wingi wa kura za mashabiki.

Washindi wengine kwenye tuzo hizo ni; Kwaya Bora-Mwanza Singers, Albamu Bora-Pokea Sifa ya Rebeka Pius, Mwimbaji Bora wa Kike-Betty Lucas, Mwimbaji Bora wa Kiume-Derick Ndonge, Mwimbaji Bora Chipukizi wa Kike-Julieth Busagi, Kundi Bora-Kihayile Group na Tuzo ya Heshima-AIC Chang'ombe Vijana Choir.

Mbali na utoaji wa tuzo hizo, pia kulikuwa na uzinduzi wa Albamu ya PAZIA LA HEKALU iliyoimbwa na kwaya ya AIC Chang'ombe Vijana Choir

No comments: