Advertisements

Tuesday, April 18, 2017

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete atembelewa na Balozi wa Canada Nchini

 Rais Mstaafu Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amekutana na Balozi wa Canada nchini Mhe. Ian Myles aliyemtembelea ofisini kwake Masaki jijini Dar es Salaam.
 Mheshimiwa Balozi Ian Myles aliwasilisha ujumbe maalum kutoka kwa Mheshimiwa Lloyd Axworthy, Mwenyekiti wa Global Refugee Initiative na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje wa Canada. 
Mheshimiwa Rais Mstaafu amepokea ujumbe huo na kufanya mazungumzo na Balozi huyo wa Canada nchini kuhusu shughuli zake baada ya kustaafu hususan ushiriki wake katika Kamisheni ya Elimu.

No comments: