Advertisements

Wednesday, June 14, 2017

UEFA yaongeza tuzo 5 kwa wachezaji

Makao makuu ya shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA)

Shirikisho la mpira wa miguu barani Ulaya (UEFA) limeongeza idadi ya tuzo zitakazo tolewa kwa wachezaji bora wa mwaka ambao watapatikana kupitia kura za makocha pamoja na waandishi wa habari za michezo.
Tuzo hizo ambazo idadi yake zitafikia tano zinatarajiwa kuanza kutolewa Agosti 24 katika jiji la Monaco nchini Ufaransa, katika droo ya makundi ya ligi ya mabingwa Ulaya.
Ujio wa tuzo hizi ni kwaajili ya wachezaji waliofanya vizuri katika mashindano ya msimu uliopita mwaka 2016/17.

No comments: