Advertisements

Thursday, July 20, 2017

NAIBU WAZIRI WA MAJI AFANYA ZIARA CHALINZE

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akisisitiza jambo wakati wa ziara yake  ya kukagua hatua iliyofikiwa katika mradi wa ukarabati  na upanuzi wa mtambo wa maji chalinze na na ujenzi wa mfumo wa kusafirishia maji pamoja na matenki yakuhifadhia maji. Kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Chalinze (CHALIWASA)Mhandisi Christer Mchomba na kushoto ni Msimamizi wa mradi huo kutoka kampuni ya WAPCO inayotekeleza mradi huo.
Mafundi wakiendelea na Kazi ya ujenzi wa matanki ya kuhifadhi na kusambaza maji katika Jimbo la Chalinze.
Baadhi ya mitambo ikiwa katika moja ya maeneo unakotekelezwa mradi  huo utakaonufaisha wakazi wa Jimbo la chalinze na sehemu ya Wilaya ya Handeni.
Sehemu ya mabomba yakiwa katika moja ya maeneo unakotekelezwa mradi huo.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe (wapili kushoto) akioneshwa ramani ya mradi huo na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wake wakati wa ziara yake  ya kukagua mradi huo  wa ukarabati  na upanuzi wa mtambo wa maji chalinze na na ujenzi wa mfumo wa kusafirishia maji pamoja na matenki yakuhifadhia maji.

(Picha zote na Frank Mvungi-MAELEZO)

No comments: