Advertisements

Friday, November 17, 2017

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI AFUNGUA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro (aliyesimama), akizungumza na wajumbe wa baraza la wafanyakazi (hawapo pichani) katika mkutano wa kujadili taarifa za Utekelezaji katika baraza hilo, mkutano huo ulifanyika jana jijini Dar es salaam na kufunguliwa rasmi na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Balozi Hassan Simba Yahaya. Picha na Jeshi la Polisi.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Balozi Hassan Simba Yahaya, akizungumza na wajumbe wa baraza la wafanyakazi (hawapo pichani) katika mkutano wa kujadili taarifa za Utekelezaji katika baraza hilo, mkutano huo ulifanyika jana jijini Dar es salaam, na kukutanisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro. 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Balozi Hassan Simba Yahaya pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, wakiwa katika picha na wajumbe wa baraza la wafanyakazi baada ya kufunguliwa rasmi kwa kikao cha kujadili taarifa za utekelezaji wa baraza hilo jana jijini Dar es salaam. 

No comments: