Advertisements

Sunday, November 19, 2017

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI AZINDUA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA MKOA WA MARA


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala (kushoto), Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Andrew Masawe (katikati), wakishuhudia uchukuliwaji wa alama za vidole za mmoja wa wananchi waliofika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo, mkoani Mara kuandikishwa kwa ajili ya kupata kitambulisho cha utaifa. Kupitia zoezi hilo wananchi wa mkoa huo na wilaya zake watapata fursa ya kupata vitambulisho vya Taifa vinavyotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiingiza taarifa za muombaji wa kitambulisho cha Taifa, baada ya kuzindua zoezi la usajili wa vitambulisho hivyo leo Mkoani Mara.Kupitia zoezi hilo wananchi wa mkoa huo na wilaya zake watapata fursa ya kupata vitambulisho vinavyotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiakisi fomu ya taarifa za muombaji wa kitambulisho cha Taifa, baada ya kuzindua zoezi la usajili wa vitambulisho hivyo leo Mkoani Mara.Kupitia zoezi hilo wananchi wa mkoa huo na wilaya zake watapata fursa ya kupata vitambulisho vinavyotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Andrew Masawe (kulia),wakiteta jambo baada ya Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), kuzindua zoezi la usajili wa vitambulisho vya Taifa lililofanyika leo katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo,mkoani Mara.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiwa tayari kuhudumia wananchi waliofika katika zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa baada ya kuzinduliwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mkendo,mkoani Mara. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments: