Advertisements

Friday, January 19, 2018

MBUNGE MBILINYI 'SUGU', ANYIMWA DHAMANA TENA NA AMERUDISHWA RUMANDE HADI JUMATATU IJAYO

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa, Emmanuel Masonga wamerudishwa rumande hadi Januari 22, 2018 siku ya Jumatatu ambapo kesi yake itaanza kusomwa mfululizo.

Mbunge huyo wa Mbeya mjini na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa wanashikiliwa na jeshi la polisi wakituhumiwa kutenda kosa la uchochezi katika mkutano wao wa hadhara ambao ulifanyika Disemba 31, 2017 jijini Mbeya ambapo jeshi la polisi linasema kuwa viongozi hao walizungumza maneno yenye kuleta chuki kati ya Serikali na wananchi.

Mchana wa January 16, 2018 Mahakama ya Hakimu Mkazi Jijini Mbeya iliamuru Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa Emmanuel Masonga wapelekwe rumande mpaka January 19 ambayo ni leo kwa kesi ya uchochezi.


Viongozi hao wamerudishwa rumande tena mpaka siku ya Jumatatu ambapo kesi yao itaanza kusomwa tena

No comments: