Advertisements

Tuesday, July 17, 2018

WAZIRI MKUU AZINDUA GHALA LA KUHIFADHIA MAZAO YA WAKULIMA KATIKA KIJIJI CHA BULIGE NA KUKAGUA SHAMBALA DENGU JIMBO LA MSALALA

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikata utepe kuzindua ghala la kuhifadhia mazao ya wakulima katika kijiji cha Bulige kwenye Halmashauri ya Msalala, Julai 17, 2018.  Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kahama, Anamringi, Macha, wapili kushoto ni Mbunge wa Msalala, Ezekiel  Maige na  wanne kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum, Aza Hilal. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum, Lucy Mayenga na wapili kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,  Elius Kwandikwa. 
 Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akiweka jiwe la Msingi la ghala la kuhifadhia mazao ya wakuliama katika kijiji cha  Bulige kwenye Halmashauri ya Msalala Juali 17, 2018. Anayemsaidia ni Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige na Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum, Lucy Mayenga.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua shamba la dengu lenye ukubwa wa ekari 10, mali ya Bw. Philipo Kapande (wapili kushoto) katika kijiji cha Jomu kwenye Halmashauri ya Msalala Julai 17, 2018. Wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack. Na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Mabala Mlolwa.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua shamba la dengu lenye ukubwa wa ekari 10, mali ya Bw. Philipo Kapande (kushoto) katika kijiji cha Jomu kwenye Halmashauri ya Msalala Julai 17, 2018. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: