Advertisements

Saturday, August 11, 2018

KIKAO CHA KUJADILI RIPOTI YA MTHIBITI NA MKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA TUNDUMA, AGOSTI 10, 201

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali Nicodemas E. Mwangela akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma (hawapo pichani) wakati wa kujadili ripoti ya Mthibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali.
Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali Nicodemas E. Mwangela (hayupo pichani) wakati wa kujadili ripoti ya Mthibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali Nicodemas E. Mwangela;

Ninawapongeza kwa kuvuka lengo la makusanyo na kufikia asilimia 104 hii inaonyesha kuwa katika halmashaurii hii Kuna watu waaminifu, wanaofanya kazi kwa bidiii na waadilifu.

Licha ya pongezi ninazowapa na katika mambo mazuri mnayoyafanya bado kuna dosari kadhaa ndio maana kuna hoja 17 za ripoti ya CAG.

Ofisi yangu iko wazi endapo mtendaji yoyote akiwa na lolote ambalo anajua natakiwa nilifahamu ofisi yangu iko wazi masaa 24 siku 7.

Ninaomba ushirikiano wenu na mimi ninaamini katika ushirikiano kwakuwa mtu mmoja hawezi kufanya mambo yote.

Ili tufanye kazi vizuri malengo tuliyojiwekea tuyatekeleze kwa muda uliopangwa, suala la muda ni muhimu sana, watendaji tuweke utaratibu wa kujipangia kila siku utafanya nini na upange muda wa utekelezaji, hii itatusaidia kuenda kwa kasi.

Kuna tatizo kubwa viongozi tunaletewa taarifa na takwimu za uongo ambapo tukifika maeneo husika kujiridhisha tunakuta hali ni tofauti, sasa ninataka tukiomba taarifa mtuletee takwimu za uhakika ili muweze kuepuka baadhi ya hoja.

Kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wataalamu mkisikia kuna ukaguzi wa ofisi ya CAG mnakwepa kwa visingizio vya ugonjwa, likizo na ruhusa.

Naagiza wakurugenzi msitoe ruhusa kwa wataalamu kipindi cha ukaguzi wa CAG mpaka kuwe na sababu za msingi ili wataalamu kutoka ofisi ya CAG wakija wawakute wataalamu husika ambao wanaweza kujibu hoja vizuri.

Ninaelekeza kuwa hoja iliyojibiwa mwaka jana wa fedha isionekane tena kwa mwaka huu wa fedha.

Mkaguzi wa Hesabu kutoka Ofisi ya CAG Joyce Luena;

Halmashauri ya Tunduma ina kesi zenye thamani ya bilioni 1.38 sawa na asilimia 35 ya bajeti ya mapato ya ndani, halmashauri izisimamie kesi hizo kwa umakini ili kuokoa fedha za serikali pamoja na kusimamia mikataba ili kutojiingiza tena katika kesi.

Halmashauri zizingatie maoni ya Mkaguzi wa ndani kwakuwa ndiye anayewapa picha halisi ya utendaji wa halmashauri unaendaje na hivyo kuweza kuzuia baadhi ya hoja.

Watendaji wajikite zaidi kwenye kuzuia hoja na sio kujibu hoja yaani wasiwe mabingwa ya kujibu hoja bali kuzuia hoja.

Halmashauri iendelee kusimamia mipango ya makusanyo ya mapato waliyojiwekea ili waweze kukusanya Zaidi wasitegee kwakuwa walivuka lengo.

Imetolewa Na:
Grace Gwamagobe
Afisa Habari


Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

No comments: