Advertisements

Tuesday, October 16, 2018

SUKOS yakabidhi vifaa vya zima moto Idara ya Uratibu wa Maafa Nchini

Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, Suleiman Kova (kulia) akikabidhi Hati ya Shukrani kwa Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe walipomtembelea kukabidhi vifaa vya zima moto Ofisini kwake Dodoma
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe (katikati) akipokea maelezo kutoka kwa Meneja wa Oparesheni Bi.Rahma Kova wakati wa kukabidhi cheti cha Shukrani ya ushirikiano uliopo kati ya SUKOS na Ofisi ya Waziri Mkuu
Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji - SUKOS, Suleiman Kova akimkabidhi vifaa vya zima moto Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said kwa ajili ya kutoa huduma ya uokoaji endapo itatokea majanga ya moto katika maeneo ya kazi
Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, Suleiman Kova (kulia) akizungumza jambo wakati wa kukabidhi vifaa vya zima moto pamoja na hati ya shukrani kwa Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe (katikati) na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi (Mipango na Utafiti) Idara hiyo Bw.Bashiru Taratibu walipotembelea Oktoba 15, 2018.
Mkurugenzi Msaidizi Mipango na Utafiti Idara ya Uratibu wa Maafa Bw.Bashiru Taratibu akiangalia vifaa vya zima moto vilivyokabidhiwa na Taasisi ya Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji –SUKOS Oktoba 15, 2018 kwa ajili ya kutoa huduma ya uokoaji endapo itatokea majanga ya moto
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali Jimmy Said Matamwe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa SUKOS Foundation walipotembelea Idara hiyo ili kukabidhi Vifaa vya Zima Moto pamoja na hati ya shukrani kwa namna Taasisi yake inavyoshirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, kulia kwake ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Suleiman Kova.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments: