Advertisements

Friday, December 7, 2018

DKT. MWANJELWA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUWA MFANO WA KUIGWA KIUTENDAJI NA TAASISI NYINGINE ZA UMMA

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisisitiza jambo kwa wajumbe wa kikao cha menejimenti ya ofisi yake (hawapo pichani) alipokutana nao kwa lengo kufahamiana na kupanga mkakati madhubuti wa utendaji kazi utakaoziwezesha taasisi za umma nchini kutoa huduma bora kwa umma.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha menejimenti ya Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) alipokutana nao kwa lengo kufahamiana na kupanga mkakati madhubuti wa utendaji kazi utakaoziwezesha taasisi za umma nchini kutoa huduma bora kwa umma.


DKT. MWANJELWA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUWA MFANO WA KUIGWA KIUTENDAJI NA TAASISI NYINGINE ZA UMMA

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) amewataka watumishi wa ofisi yake kuwa mfano wa kuigwa na taasisi nyingine kiutendaji kwa kufanya kazi kwa bidii, maarifa, uadilifu na weledi ili kujenga misingi bora ya utumishi wa umma nchini.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa ametoa maelekezo hayo leo wakati akizungumza na menejimenti ya ofisi yake, lengo likiwa ni kufahamiana na kupanga mkakati madhubuti wa utendaji kazi utakaoziwezesha taasisi za umma nchini kutoa huduma bora kwa umma.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wamepewa dhamana ya kuhakikisha utumishi wa umma unakuwa na tija na maslahi kwa maendeleo ya taifa hivyo hawana budi kutekeleza wajibu wao kikamilifu.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa ameongeza kuwa, watumishi wakifanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma iliyopo, malalamiko yasiyo ya lazima kwenye eneo la utumishi na utawala bora yatapungua kwa kiwango kikubwa.

Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesisitiza kuwa, mtumishi wa umma anatakiwa kupimwa kwa utendaji kazi wake kwa matokea chanya ili atakapopanda daraja ajivunie utendaji kazi wake na kuongeza kuwa, upimaji huo utapunguza malalamiko ya kutopandishwa madaraja kwa watumishi ambao hawawajibiki ipasavyo.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amekutana na menejimenti ya ofisi yake kwa mara ya kwanza mara baada ya kuripoti na kuanza kazi rasmi tarehe 14 Novemba, 2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alimteua Mhe. Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, tarehe 10 Novemba, 2018 na kumuapisha tarehe 12 Novemba, 2018.


IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA RAIS (UTUMISHI)

TAREHE 07 DESEMBA, 2018

No comments: