Advertisements

Friday, February 15, 2019

DKT. MWANJELWA AWAPA WIKI MOJA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA MKINGA WANAOISHI NJE YA VITUO VYA KAZI KUHAMIA KATIKA MANEO YAO YA KAZI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wilayani Mkinga, wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani humo. 
Baadhi ya watumishi wa umma wilayani Mkinga wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani humo. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiteta jambo na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said, kabla ya kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani humo. 
Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) akimkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani humo. 
Afisa Utumishi Mwandamizi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Baraka N. Nangosongo akitoa ufafanuzi wa masuala ya kiutumishi kwa watumishi wa umma wilayani Mkinga wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF wilayani humo. 

JAMES KATUBUKA MWANAMYOTO,
AFISA HABARI,
OFISI YA RAIS-UTUMISHI,
0713 360 813
15/02/2019.

No comments: