Advertisements

Monday, October 25, 2021

TANZANIA YANG’ARA MCHEZO WA KARATE NCHI ZA MAZIWA MAKUU

 
Na Mwandishi Maalum, DRC

Timu ya Taifa ya Karate ya Tanzania imeng’ara katika mashindano ya kimataifa ya Karate kwa Nchi za Maziwa Makuu yaliyofanyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kumalizika leo Jumamosi.

“Kwa ujumla tumepata medali 27 kwa categories tofauti tofauti ambapo wanawake wameleta medali 13 na wanaume ni medali 14,” alisema kiongozi wa Chama cha Karate nchini na kuongeza:

“Katika medali hizo tuna Gold 7, Silver 8 na Bronze 12.” Timu hiyo iliondoka nchini kupitia Rwanda baada ya Serikali ya Tanzania kupitia Wizara yenye dhamana na Michezo kukwamua changamoto ya usafiri na vibali kwa ajili ya Timu hiyo kuvuka kupitia mpaka wa Rwanda uliokuwa umefungwa.

No comments: