Advertisements

Monday, November 29, 2021

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA CHUO CHA VETA , CHUNYA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Chunya, Novemba 29, 2021. Kulia. ni Naibu Waziri wa Elimu , Sayansi na Tekinolojia, Omari Kipanga na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Pancras Bujulo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilaya ya Chunya
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Pancras Bujulo (wa pili kulia) kuhusu ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilaya ya Chunya baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo hicho, Novemba 29, 2021. Kushoto ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Omari Kipanga na kulia ni Mkuu wa Chuo cha VETA cha Mpanda, Joshua Mategane.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Omari Kipanga (katikati) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya VETA, Peter Maduki baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) wilaya ya Chunya, Novemba 29, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Muonekano wa Chuo cha Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Chunya ambacho Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliweka jiwe la msingi

No comments: