Advertisements

Saturday, June 3, 2023

AFISA MANUNUZI AWEKWA NDANI MANYONI

Mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba amemsweka ndani afisa manunuzi ya halmashauri ya Manyoni Joseph Swila kwa kukiuka maagizo aliyoyatoa jana wakati alipofika kukagua ujenzi wa wodi ya wanawake, wanaume na chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya Manyoni.

RC Serukamba alimuagiza mhandisi wa halmashauri na afisa manunuzi kuongea mafundi ili kuongeza kasi ya ujenzi ambapo unatakiwa kukamilika kabla ya June 30 mwaka huu.

Mara ya kuona utekelezaji wa agizo Serukamba amekerwa na afisa manunuzi Joseph Swila baada ya kuonekana kumtetea mkandarasi anayejenga Majengo hayo huku akiwa hapatikani kwenye simu na haypo site.

No comments: