HABARI ZA NYUMBANI TANZANIA KUPITIA SIMU TV BOFYA HAPA
Friday, November 14, 2025
Thursday, October 3, 2019
SERIKALI YATAJA MAENEO YANAYOASHIRIA KUVUMBULIWA RASILIMALI YA MAFUTA NCHINI TANZANIA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji Angellah Kairuki akimwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Kassim Majaliwa wakati akifungua Kongamano la Tatu la Mafuta na Gesi Tanzania linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 2-3, 2019. Kongamano hilo linawakutanisha wadau zaidi ya 592 kutoka Mataifa mbali mbali ikiwemo Austaralia, Brazili, Canada, China, Visiwa Vya Comoro, Ghana. Mengine ni Itali, India, Japani, Kenya, Msumbiji, Netherand, Nigeria, Afrika Kusini, Oman, Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.
Waziri wa Nishati na Madini Meldard Kalemani akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Tatu la Mafuta na Gesi Tanzania linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 2-3, 2019.
Serikali ya Tanzania ametaja maeneo manne yanayoashiria matumaini ya ugunduzi wa rasilimali ya Mafuta nchini kwa siku za usoni kupitia shughuli za utafiti zinazoendelea.
Maeneo aliyoyataja ni pamoja na ya ukanda wa Ziwa Rukwa, Ziwa Tanganyika na Kitalu cha Eyasi Wembere chenye ukubwa
MANA Ministry USA ( Washington DC ) KONGAMANO LA MAOMBI Nov 15 to 17th 2019
Mwl Christopher & Diana Mwakasege
Bwana Yesu Asifiwe.
PLEASE REGISTER TO ALLOW US TO PLAN FOR YOU!!
Ni ombi letu kwako kuwa utajiandikisha na kulipa reg fee $30 ili kuchangia gharama ya maandalizi za kongamano.
Ili Kujiandikisha ,tumia link
Venue:
*Hilton Hotel Rockville*
1750 Rockville Pike
Rockville MD 20852
For assistance/ details call/text: 240-565-7133 // 301-693-3807//703- 344-5611 // 516-238-3618// 703-992-3753
Wednesday, October 2, 2019
Kwanini mapenzi ndani ya ndoa zetu yanapungua?

Je, umewahi kujiuliza, unampenda mpenzi wako kwa kiwango gani? Je, yeye anakupenda kwa kiasi gani? Upendo wake unamaanisha nini hasa? Upendo wako kwake una maana gani? Ni pendo la ndani kweli au tamaa za mwili?
Unaweza kujiuliza, inawezekana vipi ukampenda mtu hadi mkafikia kuingia kwenye ndoa, bado ikawa ni tamaa ya ngono tu? Hapa namaanisha kuwa yawezekana vipi, mpendane halafu muingie ndani maelewano yaondoke?
Heshima itoweke? Upendo utoweke? Inawezakana vipi? Wengi wanajiuliza: “Tumependana na mume wangu kwa miaka mingi, tumeingia kwenye ndoa na tumeishi humo kwa siku nyingi lakini kwa nini leo hii amebadilika?” Wasomaji wengi wananiuliza maswali yanayofanana na hayo (hasa wanawake). Ngoja nikupe kisa cha msomaji mmoja mwanamke, kisha tuingie kwa undani zaidi katika mada yetu.
MBUNGE KIBAHA VIJIJI JUMAA ACHANGIA MADARASA MAWILI NA HEKARI KUMI UJENZI SHULE YA KATA GWATA
Mbunge wa Jiambo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa kushoto akikabidhiwa zawadi ya fimbo na mmoja wa viongozi wa jamii ya wafugaji alipowasili katika kijiji cha Kigoda, kulia kwake ni Naibu waziri wa elimu sayansi na teknolojia William Ole Nasha baada ya kuwasili katika eneo hilo kwa lengo la kuweka jiwe la msingi katika ofisi ya kijiji hicho pamoja na kutembelea eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya kata (PICHA NA VICTOR MASANGU)
Naibu waziri wa elimu sayansi na teknolojia wa kati kati akipiga makofi katika halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi katika ofisi ya kijiji cha kigoda kilichopo kata ya Gwata katika halmashauri ya Kibaha vijini kushoto kwake ni Mbunge wa Kibaha Vijijini Haoumd Jumaa, na viongozi wengine wa kijiji hicho.
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YATILIANA SAINI UJENZI WA MJI MPYA KWAHANI ZANZIBAR
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Iddi Haji Makame (kushoto)akitiliana saini na Meneja Mkuu wa Kampuni ya ESTIM Construction co.ltd Girdhar M, Pindolia kuhusiana na Ujenzi wa Mji mpya wa Kwahani hafla iliofanyika muembe njugu Zanzibar.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Iddi Haji Makame (kushoto)wakikabidhiana hati ya saini na Meneja Mkuu wa Kampuni ya ESTIM Construction co.ltd Girdhar M,Pindolia kuhusiana na Ujenzi wa Mji mpya wa Kwahani hafla iliofanyika muembe njugu Zanzibar.
Elimu ya Mpiga Kura ipo mkoani Tabora kabla ya Uboreshaji wa Daftari Oktoba 14-20, 2019
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) upande wa Habari Daniel Kasokola akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Tabora Boys (Tabora School) wakati Gari la Matangazo la NEC lilipotembelea shule hiyo iliyopo Mjini Tabora kutoa Elimu ya Mpiga Kura kuelekea Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mkoa wa Tabora, Katavi, Rukwa na Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma unaotarajiwa kuanza Oktoba 14 hadi Oktoba 20, 2019.
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) upande wa Habari Daniel Kasokola, akieleza jambo mbele ya mwanafunzi mwenye ulemavu wa macho wa Shule ya Sekondari Tabora Boys Elisha John kuhusu kipaumbele ambacho NEC inakitoa kwa makundi maalum wakiwemo watu wenye ulemavu.
UBINAFSISHAJI WA KIWANDA CHA NYUZI TABORA BAADA YA KUBAINI HAKIFANYI VIZURI
Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa (aliyeshika uzi) akipata maelezo kutoka kwa Katibu wa Kiwanda cha Nyuzi Tabora Pascal Jotham (mwenye shati nyeusi) leo alipokuwa Mkoani Tabora kukagua viwanda mbalimbali. Waziri huyo hauridhishwa na utendaji wa kiwanda hicho na kuahidi kupitia Mkataba wa Ubinafishaji wake.
Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa (katikati ) akiwa ameshika mmoja ya kitambaa kilichozalishwa na Kiwanda cha Nyuzi Tabora wakati wa ziara yake Mkoani Tabora jana ya kukagua viwanda mbalimbali. Waziri huyo hauridhishwa na utendaji wa kiwanda hicho na kuahidi kupitia Mkataba wa Ubinafishaji wake.
WAUGUZI WAOMBA ADA YA LESENI ZA UUGUZI ZIPUNGUZWE
Baadhi ya wauguzi wakishangilia wakati Mgeni rasmi akiingia ukumbi wakati wa ufunguzi wa Kongamano la kisayansi na Mkutano Mkuu wa 47 wa Wauguzi Tanzania Bara 01 Oktoba, 2019 ambao unafanyika kwa siku nne Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wauguzi wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la kisayansi na Mkutano Mkuu wa 47 wa wauguzi Tanzania Bara 01 Oktoba, 2019 ambao unafanyika kwa muda wa siku nne Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
WAZIRI MKUU AKAGUA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA KUSINI
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini inayojengwa katika eneo la Mitengo, Mtwara Oktoba 2, 2019. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Viongozi na wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza baada ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini kwenye eneo la Mitenga, Mtwara, Oktoba 2, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa (wa tatu kulia), Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme (wa pili kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi (kulia) wakati Waziri Mkuu alipokagua ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini, eneo la Mitengo Mtwara, Oktoba 2, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu (katikati) wakisoma ramani ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini katika eneo la Mitengo , Mtwara Oktoba 2, 2019. Kushoto ni Meneja wa Mradi, Godwin Maro. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini katika eneo la Mitengo, Mtwara Oktoba 2, 2019. Kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, wa tatu kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa na wanne kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
MABARAZA YA ARDHI YA KATA NA VIJIJI YASIYOTENDA HAKI MAFIA YAVUNJWE-DKT MABULA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na wananchi wa Baleni wilayani Mafia mkoa wa Pwani alipokwenda kusikiliza kero za ardhi katika eneo hilo akiwa katika ziara yake ya siku mbili katika wilaya hiyo kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi pamoja na kukagua masijala ya ardhi jana.
Mwananchi Hassan Omar maarufu mzee wa Lumbesa mkazi wa Dagoni Mafia akimuonesha nyaraka Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kuhusiana na mgogoro wa ardhi wakati Dkt Mabula alipofanya ziara wilaya ya Mafia kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi pamoja na kukagua masijala ya ardhi jana.
BODI YA REA YAKAGUA MRADI WA UMEME JUA UYUI
Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Styden Rwebangira (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu (kushoto), wakikagua moja ya mitambo ya umeme jua iliyopo katika kijiji cha Tura, wilayani Uyui, Mkoa wa Tabora, Oktoba 1, 2019.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Styden Rwebangira (katikati) na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu (kushoto), wakijadiliana jambo na Afisa Mtendaji wa Kata ya Tura, Nelson Mungwila (kulia), walipowasili kwenye kata hiyo kukagua mradi wa umeme jua, Oktoba 1, 2019.
WAZIRI MKUU ATEMBELEA KIWANDA CHA KUBANGUA KOROSHO CHA YALIN CHA MTWARA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wanawake waliokuwa wakibangua korosho wakati alipotembelea kiwanda cha kubangua korosho cha Yalin cha Mtwara, Oktoba 2, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wanawake waliokuwa wakibangua korosho wakati alipotembelea kiwanda cha kubangua korosho cha Yalin kilichopo Mtwara, Oktoba 2, 2019. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
AFISA TARAFA ITISO: TUTATUMIA MAKUNDI YA NGOMA ZA ASILI KUHAMASISHA NA KUELEZA UMUHIMU WA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Afisa Tarafa Remidius Emmanuel akizungumza na baadhi ya vikundi vya Sungusungu pamoja na wananchi wa kata ya Itiso wakati wa tamasha dogo la utamaduni lililoandaliwa na viongozi wa kabila la Wagogo wa Tarafa ya Itiso na kufanyika katika Kijiji cha Mapanga (Makulu).
Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Tarafa ya Itiso A/Insp. Mohamed Ally akitoa neno kwa wananchi pamoja na baadhi ya vikundi vya Sungusungu wakati wa tamasha dogo la utamaduni lililoandaliwa na viongozi wa kabila la Wagogo wa Tarafa ya Itiso na kufanyika katika Kijiji cha Mapanga (Makulu)
Tuesday, October 1, 2019
RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AMUAPISHA MKURUGENZI WA NEC PAMOJA NA MKUU WA ITIFAKI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Wilson Mahera
Charles kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC), katika hafla fupi
iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Kanali Wilbert
Augustine Ibuge kuwa Balozi ambaye ameteuliwa leo kuwa Mkuu wa Itifaki Chief of
Protocol wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ikulu
jijini Dar es Salaam.
WAZIRI MKUU ASHUHUDIA USAFIRISHAJI WA KOROSHO
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Renatus Mkinga wakati alipotembelea bandari ya Mtwara kukagua kazi ya usafirishaji wa korosho, Oktoba 1, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa (kushoto) wakati alipokagua kazi ya kusafirisha korosho kwemye bandari ya Mtwara, Oktoba 1, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
RAIS DKT. SHEIN AFANYA UZINDUZI WA MELI YA MAFUTA YA MT.UKOMBOZI II
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika bandari ya Malindi Zanzibar kwa ajili ya Uzinduzi wa Meli ya Mafuta ya MT.Ukombozi II, akiongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Damen Shipyard Gorinchem, Kanda ya Afrika Mr.Ronald Maat, alipowasili katika viwanja vya Bandari ya Malindi Zanzibar kwa ajili ya Uzinduzi wa Meli ya Mafuta ya MT. Ukombozi II, hafla hiyo imefanyika leo 1-10-2019.
WAZIRI MKUU AZAWADIWA KITI CHA WAZEE KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAZEE DUNIANI - MJINI MTWARA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhiwa zawadi ya kiti cha wazee na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wazee Tanzania, Abdallah Majumba (kushoto) baada ya kuhutubia katika Maadhiisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye Uwanja wa Nangwada Sijaona mjini Mtwara, Oktoba 1, 2019. Katikati ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amekalia kiti cha wazee alichozawadiwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wazee Tanzania, Abdallah Majumba (kushoto) baada ya kuhutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Nangwada Sijaona mjini Mtwara, Oktoba 1, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
SERIKALI ITAENDELEA KUWALINDA WAZEE DHIDI YA UKATILI
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika Kitaifa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mjini Mtwara, Oktoba 1, 2019. Kulia ni Mkalimani wa lugha ya alama, Ally Nalinga Uwesu.(Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika Kitaifa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mjini Mtwara, Oktoba 1, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Alphayo Kidata wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mtwara ambako alikuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika Kitaifa kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona. Oktoba 1, 2019 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Subscribe to:
Posts (Atom)



















