Sunday, May 19, 2013

PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-

Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.


Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.


Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.


Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.


Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

INASEMEKANA KUWA AFYA YA SHEIKH PONDA NI TETE



Sheikh Ponda Issa Ponda
KATIBU wa Taasisi na Jumuiya za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, ni mgonjwa, MTANZANIA Jumapili linaripoti. Sheikh Ponda, ambaye kwa sasa anatumikia kifungo cha nje cha miezi 12, huku wenzake 49 wakiachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, anadaiwa afya yake ina kasoro na kwamba amekutana na madaktari wake kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kiafya.

Taarifa ambazo MTANZANIA Jumapili limezipata kutoka kwa watu wake wa karibu, zinaeleza kuwa Sheikh Ponda yuko katika uchunguzi wa afya yake katika hospitali moja Jijini Dar es Salaam.

Msemaji wa Sheikh Ponda, Yusuph Shaaban, ameliambia gazeti hili kuwa Sheikh Ponda yuko katika uchunguzi wa afya yake, huku akikataa kuzungumza zaidi mwenendo wa uchunguzi na hali yake kiafya kwa sasa kwa madai kuwa suala hilo ni la binafsi, hivyo hawezi kuliongelea zaidi.
Hata alipoulizwa ugonjwa unaomsumbua na sehemu anayopata matibabu, alikataa kuzungumza na kulielekeza gazeti hili kumtafuta Sheikh Ponda mwenyewe kutoa ufafanuzi zaidi.

PITIA HII NI UCHAMBUZI WA MKTAKIBARI WA MBIO ZA URAIS 2015

Na Nova Kambota,

Gazeti la Dira ya Mtanzania toleo no 224 la jumatatu ya Machi
11 mwaka 2013 katika ukurasa wa 7 lilichapisha makala ya Dk Noordin
Jella yenye kichwa cha habari “Je, tunataka Rais dikteta au
muadilifu?” nimesoma kwa makini makala hiyo, nimechekesha na kupima
hatua kwa hatua kile ambacho mwandishi alilenga hatimaye
nimejiridhisha kuwa makala hiyo ilikuwa na mapungufu makubwa ya
kimantiki na hoja.

HAPPY BIRTHDAY, HAPPY BIRTHDA, HAPPY BIRTHDAY

Naomi Mbiduka wa Minnesota, U.S.A
Praying that your day is as special as you are, Vijimambo wish you happy birthday

USO WA KITABU INAWEZEKA HII KWELI HII IMECHANGIA


MWENYEKITI WA CCM RAIS KIKWETE AZUNGUMZA NA WABUNGE WA CCM DODOMA

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
Wajumbe kwenye kikao cha Mwenyekiti wa CCM na Wabunge wa CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migoiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.
kwa picha zaidi bofya read more

KWA WAPENDA MOVIE-Mtoto Wetu

VUGURU ZATOKEA MJINI IRINGA, POLISI WATUMIA MABOMU KUREJESHA AMANI


Hivi ndivyo hali ilivyokuwa baada ya Machinga kufunga barabara kuu ya Iringa - Dodoma na ile ya Mashine Tatu mjini Iringa. 
Hali ikiwa tete eneo hilo.
Polisi wakiwa tayari kukabiliana na Machinga.
Abiria na wapiga debe wa stendi kuu Iringa wakinawa maji baada ya kupigwa mabomu na kumwagiwa maji ya kuwasha na askari.

(PICHA ZOTE NA FRANCIS GODWIN, IRINGA)

DIAMOND, NEY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE

Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.
Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.
Diamond na Ney wakiwapagawisha mashabiki.
Ney wa Mitego akisema na wapenzi wake.
Diamond Platnumz akionyesha umahiri wake stejini.
kwa picha zaidi bofya read more

MCHUNGAJI PETER MSIGWA MIKONONI MWA POLISI

Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (Chadema), Peter Msigwa.

Taaarifa kutoka Iringa zinasema mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amekamatwa na jeshi la polisi na yuko chini ya Ulinzi.Mchungaji Msigwa amekamatwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Michael Kamuhanda kwa madai kwamba anawaunga mkono wafanyabiashara ndogondogo wa manispaa hiyo 'Machinga' wanaopambana na polisi wanaowakataza kufanya biashara mjini.
Mchungaji Msigwa amekuwa mtetezi mkubwa wa wafanyabiashara ndogondogo kiasi kwamba kila anapoonekana maeneo ya manispaa hiyo hujikuta gari yake ikisukumwa na Machinga hao. Kabla ya kukamatwa, Mchungaji Msigwa alikuwa katika harambee iliyokuwa inaendesha na Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Chuo Kikuu cha Tumaini.-GPL

Rais Kikwete: Udini unaoibuka una mkono wa nje

Dodoma. Rais Jakaya Kikwete amebainisha kuwa vurugu za kidini na kisiasa zinazotokea nchini, zina uhusiano na watu wa nchi za nje.
Alitoa kauli hiyo jana kwenye ibada maalumu ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mkuu wa Sitta wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dk Jacob Chimeledya.
Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi kwenye ibada hiyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu.

Mnyama aliwa, ubingwa wanoga Yanga

kikosi cha Simba kilichoanza
Simba na Yanga wakiingia uwanjani
Wachezaji wa Yanga na Simba wakisalimiana
Hili ndilo lilikuwa bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Didier Kavumbagu kwa kichwa.
Mpambano ukiendelea.
Haruna Shamte akipambana na Simon Msuva wa Yanga.
Kocha wa Simba wakati mchezo ukiendelea.
Kocha wa Yanga akifuatilia mtanange.
Nahodha wa Yanga Nadir Haroub akinyanyua kombe la ubingwa wa ligi kuu ya VODACOM msimu wa 2012/2013
Mrisho Ngassa akiwa amevalishwa jezi ya YANGA kwa mara nyingine tena huku akiwa amefurahi kweli kweli.
Mwamuzi wa mchezo wa leo Saanya akiwa chini mara baada ya kuumia.
picha kwa hisani ya Shaffih Dauda Blog
kwa picha zaidi bofya read more

A major TV network in Tanzania is Launching THE FIRST EVER search for a reality Tv star!!


Think you have a BIG PERSONALITY?   We are looking for you.
We are looking for people who do not mind sharing their lives and can speak KISWAHILI FLUENTLY. You should be energetic, exciting, outgoing, and with a strong opinion...and aren't afraid to share it. 
NO SCRIPT, nothing to memorize.
MAKE MONEY living your regular life
 
This is an opportunity of a life time with a very substantial pay. DO NOT let it pass you by.
 
If you think you got what it takes to become the next big thing,  call Suzan at 832 774 0089, and be on your way to STARDOM. 
 Go on.... BE THE NEXT BIG THING!!!!!!!

Sensei Rumadha Fundi kala Nondozzzzz! nchini Marekani

 Sensei Rumadha Fundi (mstari wa nyuma) akiwa na wataalamu wenzie wa mapafu
 Sensei Rumadha Fundi akielekea kuchukua Nondozi
 Sensei Rumadha akiwa na ndugu na marafiki.
 Sensei Rumadha na mkewe Anita pamoja na mdogo wake Rumadha,Kibwana Fundi katika shangwe.
sensei Rumadha akiwa binamu Dotto Haruna.

KUTOKA USWAHILINI ADI UGHAIBUNI

Sensei Rumadha Fundi ,kachukua Degree "Associate in Applied Science Cardiopulmonary Respiratory Care"

Sensei Rumadha Fundi ajiongezea taaluma kutoa Usensei wa Karate na Mwalimu wa Yoda na sasa mtaalamu wa tiba za binadamu upande wa mapafu !

Si mwingine bali yule mtanzania mtaalamu wa michezo ya Karate na Yoga
Sensei Rumadha Fundi (3rd Dan,Black Belt ) mwenye maskani yake kule
marekani .

SEIF NA NARGIS WASHEREHEKEA MIAKA 25 YA NDOA YAO, MARTIN'S CROSSWINDS, GREENBELT, MD

Seif Ameir pamoja na mdhamini wa pendo lake kwa miaka 25, Nargis Ameir wakichumu kwenye sherehe ya miaka 25 ya ndoa yao iliyofanyika Jumamosi May 18, 2013 katika ukumbi wa Martin's Crosswimds uliopo Greenbelt, Maryland nchini Marekani.
Seif Ameir akiwa na mama mwenye nyumba wake na mdhamini wa pendo lake  kwenye sherehe yao ya miaka 25 ya ndoa yao.
Nargis akimlisha keki mdhamini wa pendo lake kwa miaka 25, barafu na waridi wa moyo wake, Seif Ameir kwenye sherehe ya miaka 25 ya ndoa yao.
Nargis na Seif wakichumu kama ishara ya upendo na mashikamano wa malavidavi yao kwa miaka 25
Seif akimlisha keki mdhamini wa pendo lake na mama mwenye nyumba wake, Nargis Ameir kwenye sherehe yao ya miaka 25 ya ndoa yao.
Nargis akimchum mumewe.
Seif na Nargis katika densi yao ya kwanza ya miaka 25 ya ndoa yao.

Seif na Nargis katika picha ya pamoja na watoto wao
Watoto wakiongea machache kuhusu wazazi wao
Seif Ameir akilonga yake ya moyoni kwa kuwashukuru watu wote waliofika na wote waliowawezesha bila kumsahau Mwenyezi Mungu  na hatimae Jumamosi ya May 18, 2013 kufanikisha sherehe ya miaka 25 ya ndoa yao.
Nargis akiwashukuru waandaaji, Mumewe na watu wote waliowezesha sherehe yao ya miaka 25 ya ndoa.
kwa picha zaidi bofya read more

VIVAZI VILIVYOTAMBA KWA SEIF NA NARGIS MIAKA 25 YA NDOA YAO

kwa picha zaidi bofya read more