Advertisements

Monday, March 18, 2024

MAKALA: WANANCHI KATA 22 WASIKILIZENI WAGOMBEA, MPIGE KURA


Wagombea wa vyama mbalimbali wakiangalia fomu za uteuzi wa wagombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kugombea nafasi ya udiwani Kata ya Kimbiji iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Dar es Salaam.
Wagombea wa vyama mbalimbali wakiangalia fomu za uteuzi wa wagombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kugombea nafasi ya udiwani Kata ya Kimbiji iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Dar es Salaam.

Na Mroki Mroki
TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza Machi 20,2024 kuwa ni siku ya kupiga kura katika Uchaguzi Mdogo wa udiwani katika Kata 23 za Tanzania Bara.

Tume ilitangaza uchaguzi huo baada ya kuketi katika kikao chake cha Februari 15 mwaka huu na siku hiyohiyo, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K akatoa taarifa kwa umma juu ya uwepo wa uchaguzi huo mdogo.

Tayari mchakato wa Uchaguzi huo umeshaanza ambapo Februari 27 hadi Machi 4, 2024 wagombea walichukua fomu za uteuzi, uteuzi ulifanyika Machi 4,2024 na kampeni za uchaguzi zilianza Machi 5,2024 na zinaendelea hadi tarehe 19 Machi, 2024.

‘’HATUJARIDHIKA NA UREJESHEJA FEDHA ZA MIKOPO YA KKK’’

 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe, Timotheo Mzava akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon mara baada ya Kamati yake kuwasili mkoa wa Pwani kukagua utekelezaji Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika halmashauri ya Chalinze mkoa wa Pwani tarehe 18 Machi 2024. Katikati ni Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe, Geophrey Pinda akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Chalinze na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe, Ridhiwani Kikwete wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii katika halmashauri ya wilaya ya Chalinze Machi 18, 2024.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe, Timotheo Mzava na Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Geophrey Pinda wakimsikiliza Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze Deo Msilu (wa pili kulia) kuhusu mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi unaotekelezwa katika eneo la Msolwa Halmashauri ya Chalinze Machi 18, 2024.
Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Chalinze Deo Msilu akisisitiza jambo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ilipokwenda kukagua mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika eneo la Msolwa Chalinze Machi 18, 2024.

DKT NCHEMBA ATETA NA BALOZI WA DENMARK NCHINI TANZANIA-MEMA YAJA


Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark hapa nchini, Mhe. Mette Dissing-Spandet, ambapo ameishukuru nchi hiyo kwa kuchangia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii pamoja na ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida. Mkutano huo umefanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri wa Fedha, Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark hapa nchini, Mhe. Mette Dissing-Spandet, ambapo ameishukuru nchi hiyo kwa kuchangia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii pamoja na ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida. Mkutano huo umefanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri wa Fedha, Jijini Dodoma. Kulia ni Mchumi na Mkuu wa masuala ya Biashara-Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania, Bw. Oscar Mkude.

Na Benny Mwaipaja, Dodoma
WAZIRI wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameishukuru Denmark kwa kuchangia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii pamoja na ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida.

Dkt. Nchemba ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mheshimiwa Mette Dissing-Spandet, Ofisini kwake Jijini Dodoma ambapo walijadili masuala kadhaa ya ushirikiano.

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

 

WASHIRIKI KUTOKA TANZANIA NA NCHI KADHAA ZA AFRIKA WANAHUDHURIA KOZI YA ICAO YA WAKAGUZI WA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA INAYOTOLEWA CATC


Mkuu wa Chuo cha CATC ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mafunzo hayo ya ICAO upande wa Usalama wa Usafiri wa Anga (ASTC) Dar es Salaam Bw. Aristid Kanje akizungumza wakati wa kufungua kozi ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) kwa wakaguzi wa kitaifa wa Usalama wa usafiri wa anga inayofanyika katika Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC)
Mkufunzi kutoka Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), Neema Msumi akitoa maelezo mbalimbali kuhusu chuo hicho pamoja na kujitambulisha kwa washiriki wakati wa ufunguzi wa kozi ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) kwa wakaguzi wa Kitaifa wa Usalama wa Usafiri wa Anga.
Mkufunzi kutoka  Afrika Kusini  Kagiso Mooketsi akitoa utambulisho pamoja na kuzungumzia kwa ufupi kuhusu chuo cha CATC cha Afrika Kusini kinavyojiendesha na kusimamiwa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) wakati wa kozi hiyo inayofanyika katika Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC).
Mkufunzi kutoka Kenya Millicent Henga  akijitambulisha pamoja na kutoa maelezo mafupi ya kozi zitakazofundishwa kwenye kozi maalum ya Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) kwa wakaguzi wa kitaifa wa Usalama wa usafiri wa anga inayofanyika katika Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC).

KAMATI YA LAAC IMEKAGUA MIRADI HALMASHAURI YA MISENYI MKOANI KAGERA


Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakikagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), akieleza jambo mbele ya watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), pamoja na wajumbe wa Kamati hiyo wakiangalia mashine ya mionzi (x-rays) wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakiwaangalia wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kitobo Wilaya ya Misenyi waliokuwa wanatoa maelezo ya viumbe hai na wanyama katika maabara ya bailojia wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera.

DKT. BITEKO: RAIS SAMIA AENDELEA KUENZI MAONO YA HAYATI MAGUFULI KWA VITENDO

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko akiwa na Mke wa Hayati Dkt. Magufuli, Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa pamoja na viongozi wengine wakisali katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Misa Takatifu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeyi Wilayani Chato Mkoani Geita tarehe 17 Machi, 2024.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko akizungumza katika Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitatu ya Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeyi Wilayani Chato Mkoani Geita tarehe 17 Machi, 2024. Misa hiyo imehudhuliwa na familia ikiongozwa na Mke wa Hayati Dkt. Magufuli, Mama Janeth Magufuli, watoto wa Hayati, wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko akiwa na Mke wa Hayati Dkt. Magufuli, Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shingella pamoja na viongozi wengine wakiwa katika Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitatu ya Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeyi Wilayani Chato Mkoani Geita tarehe 17 Machi, 2024.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akitoa salamu katika Misa Takatifu ya Kumbukizi ya Miaka Mitatu ya Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeyi Wilayani Chato Mkoani Geita tarehe 17 Machi, 2024. Kushoto ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shingella.

RAIS SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI ALIOWATEUA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Mhandisi Mwajuma Waziri kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Tunguu Zanzibar tarehe 17 Machi, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu, Ally Senga Gugu kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo Ndani ya Nchi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Tunguu Zanzibar tarehe 17 Machi, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu Kaspar Kaspar Mmuya kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Tunguu Zanzibar tarehe 17 Machi, 2024.

Sunday, March 17, 2024

RAIS DKT. HUSSEIN ALI MWINYI APOKEA MKONO WA POLE KUTOKA KWA NDG. SUKWA SAID SUKWA


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Ndg. Sukwa Said Sukwa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Tanzania (UVCCM) alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa ajili ya kutowa mkono wa pole, kufuatilia kifo cha Baba yake Mzazi Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi, mazungumzo hayo yaliyofanyika leo 16-3-2024 katika ukumbi wa Ikulu.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Tanzania (UVCCM)Ndg.Sukwa Said Sukwa alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa ajili ya kutowa mkono wa pole leo 16-3-2024, kufuatia kifo cha Baba yake Mzazi Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Alhajj Ali Hassan Mwinyi.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Tanzania Ndg.Sukwa Said Sukwa, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa ajili ya kutowa mkono wa pole kufuatila kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Hayati Ali Hassan Mwinyi


MAKARANI WA USIMAMIZI WA UCHAGUZI WA UDIWANI MSANGANI WAFUNDWA


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA
Katika kuelekea katika uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya Udiwani kata ya Msangani iliyopo Halmashauri ya mji Kibaha makarani wa kusimamia uchaguzi huo wamepatiwa mafunzo maalumu kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Uchaguzi huo wa kujaza nafasi ya udiwani wa kujaza nafasi hiyo unnatarajiwa kifanyika machi 20 mwaka huu ambapo utawashirikisha wananchi wa kata ya Msangani.

Kadhalika Makarani hao waongozaji licha ya kupata mafunzo hayo wamepata kiapo cha kutunza Siri Chini ya Kanuni ya 16(1) (a) na 50 (4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge,2020 na Kanuni ya 14 (1)(a),(2) na 43(4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani),2020 Mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Salum Papen.
Aidha,Mafunzo hayo yametolewa na Maria Israel,Benjamin Mputtu wakisaidiana na Afisa Uchaguzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Optuna Kasanda ambao wamewasisitiza kwenda kufanyakazi kwa kuzingatia Sheria,Kanuni na taratibu za Uchaguzi

Akifungua Mafunzo hayo,Msimamizi wa Uchaguzi,Mwanasheria nguli wa Mahakama kuu na zilizo chini yake Salum Papen amesema.." Tume imewateua ninyi kwa mujibu wa sheria na Kwa kuzingatia uzoefu wenu katika masuala ya Uchaguzi "katendeni haki amesisitiza Papen

SERIKALI IMEWATAKA WAKURUGENZI NA WATENDAJI WA MASHIRIKA YA MASLAHI YA WACHACHE KUSIMMIA MASLAHI YA UMMA


Msajili wa Hazina Nehemia Mchechu, akitoa hotuba yake wakati wa kufunga mkutano kati ya Msajili wa Hazina na Wakurugenzi wa bodi ya maslahi ya wachache uliofanyika Kibaha Mko wa Pwani.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo (kulia) na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Kida wakifuatilia kwa makini hotuba ya Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu, aliyoitoa wakati wa kufunga mkutano wa kati ya Msajili wa Hazina na Wakurugenzi wa bodi ya maslahi ya wachache uliofanyika Kibaha Mko wa Pwani.
Serikali imewataka wakurugenzi na wajumbe wa bodi katika taasisi na makampuni ambayo Serikali ina hisa chache kwa maslahi ya wachache kusimamia maslahi ya umma katika taasisi wanazozisimmia kwa niaba ya Serikali na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo wakati akifunga Mkutano wa siku tatu kati ya Msajili wa Hazina na Wakurugenzi wa bodi ya maslahi ya wachache, uliofanyika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha Mkoani Pwani.
“Mhe Rais anamini na ana Imani kwamba na taasisi za umma na makampuni ambayo serikali ina uwekezaji, yana nanafsi kubwa sana ya kuchangia katika maendeleo ya nchi hii na kwa sababu hiyo ameamua kuweka mkono kwenye kufanya mabadiliko katika taasisi hizo ili zifanye kazi na ufanisi wake uweze kuonekana.” Amesema Kitila.

CDE.MBETO- ASEMA G.N.U IMEUNDWA KWA NGUVU YA KURA YA MAONI.


KATIBU wa Kamati ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis akizungumza na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali.

NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR.
KATIBU wa Kamati ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis amesema kuwa madai ya ACT-Wazalendo ya kujitoa katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) yapuuzwe na hayana mashiko kwani Serikali hiyo imeundwa kwa nguvu ya kura ya maoni ya Wananchi wote kupitia mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984.

Hayo ameyasema wakati akitoa ufafanuzi juu ya hoja mbalimbali kwa Waandishi wa Habari hapo Ofisi kwake Kisiwandui Zanzibar.

Alisema Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) haikuundwa kwa matakwa,hisani na ridhaa ya Chama kimoja cha ACT-Wazalendo bali ipo kwa matakwa ya Wananchi waliopiga kura ya maoni ya kukubali wote kupitia kura ya maoni na kwamba hata kujitoa katika Serikali hiyo unafuatwa mfumo ule ule wa kupiga kura ya maoni.

Kupitia Mkutano huo Mbeto,alifafanua kuwa ACT-Wazalendo wana ajenda binafsi ya kuirejesha Zanzibar katika machafuko ya kisiasa ni kutokana na vitendo na kauli zao hizo za vitisho dhidi ya Serikali iliyopo madarani.

RAIS DKT. MWINYI APOKEA POLE KUTOKA KWA UWT TAIFA


Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amepokea salamu za pole Ikulu Mnazi Mmoja kutoka kwa Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Ndg. Mary Chatanda (MCC) pamoja na Makamu wake Ndg.Zainab Shomari kufuatia kifo cha Baba yake Mzazi, Mwenyekiti wa CCM Taifa Mstaafu, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyefariki dunia tarehe: 29 Februari 2024, Dar es Salaam na kuzikwa tarehe: 02 Machi 2024, Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja Machi 16, 2024, Ikulu, Zanzibar.


MURILO AZINDUA HUDUMA YA TAX MTANDAO



Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Murilo akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya usafiri mtandaoni maarufu kama SUKA leo jijini Dar es salaam.
Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alex Katundu akizungumza nkwenye uzinduzi huo wa taxi mtandaoni inayojulikana kwa jina la SUKA
Afisa Leseni na Usajili wa LATRA, Jonathani Kitururu akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Saturday, March 16, 2024

KAMATI YA BUNGE YAIPONGEZA NIDA KWA KAZI NZURI YA KUCHAPISHA VITAMBULISHO VYA TAIFA KWA WANANCHI


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Jumanne Sagini (mwenye tai kushoto) akiwatambulisha Menejimenti na viongozi wengine wa Wizara kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Vita Kawawa na wajumbe wengine wa Kamati mara baada ya kuwasili katika Kituo cha uchakataji Taarifa kukagua Mradi wa Vitambulisho vya Taifa jana.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi, na Usalama (NUU) Mhe. Vita Kawawa akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakati Kamati hiyo ilipotembelea Kituo cha Kuchakata Taarifa kukagua mradi wa Vitambulisho vya Taifa jana. Kushoto ni Naibu Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini (Mb)
Mjumbe Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi, na Usalama Mhe. Cosato Chumi akizungumza wakati alipokuwa akichangia taarifa ya Utekelezaji wa mradi wa Vitambulisho vya Taifa wakati Kamati hiyo ilipotembelea Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa jana. Kulia anayesikiliza kwa makini ni Mhe.Nicolaus Ngassa Mbunge wa Igunga ambaye pia ni mjumbe wa Kamati hiyo.