ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, May 18, 2025

HONGERA SANA NASRA CHUNDA KWA KUHITIMU MASOMO YAKO

Nasra Chunda, tunakupongeza kwa kufanikiwa kuhitimu masomo yako ya Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Fedha (Master of Financial Management) kutoka Chuo Kikuu cha Boston! Hii ni hatua kubwa na ya kujivunia katika safari yako ya kielimu na kitaaluma.

Bidii yako, kujitolea, na uvumilivu wamezaa matunda, na tunao uhakika kwamba utatumia maarifa haya kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Kutoka timu yote ya Vijimambo Blog, tunakutakia kila la heri katika hatua zako za baadaye. Hongera sana, Nasra, kwa kufanikisha ndoto yako!

Monday, May 12, 2025

RAIS WA ZANZIBAR DK.HUSSEIN ALI MWINYI AFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU CHARLES HILARY KUTOA MKONI WA POLE KWA FAMILIA



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametoa mkono wa pole kwa familia ya marehemu Charles Hillary, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo, tarehe 11 Mei 2025, jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. Mwinyi amefika nyumbani kwa marehemu, Mtaa wa Kibamba CCM, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, kutoa mkono wa pole kwa mjane wa marehemu, Bi Sarah Mwakanjuki, pamoja na wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki.

Rais Dkt. Mwinyi amewataka wote walioguswa na msiba huo kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Marehemu Charles Hillary amefariki akiwa na umri wa miaka 66.

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR MHE.HEMED SULEIMAN ABDULLA AWASILI MKOANI KILIMANJARO KUSHIRIKI MAZIKO YA MAREHEMU MSUYA



Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameondoka Zanzibar na kuwasili Mkoani Kilimanjaro kushiriki katika mazishi ya aliyewahi kuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa Tanzania marehemu Cleopa David Msuya.

Imetolewa na Kitengo cha Habari (OMPR)

Tarehe 12.05.2025.

MCHAKATO WA NEMC KUWA MAMLAKA WAENDELEA


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akijibu maswali bungeni wakati wa Kikao cha 21 Mkutano wa 19 wa Bunge jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025.

Ofisi ya Makamu wa Rais imesema mchakato wa kulipa mamlaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kupitia mchakato unaoendelea.

Kuifanya NEMC kuwa mamlaka kutaipa nguvu ya kisheria ya kusimamia majukumu yake ipasavyo na hivyo kujiwezesha kimapato.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis ameliarifu Bunge jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025 wakati akijibu swali la nyongeza Mbunge wa Mpendae Mhe. Toufiq Salim Turky lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Viti maalumu Mhe. Amina Ali Mzee aliyetaka kujua ni lini mchakato wa NEMC kuwa mamlaka kamili.

WAZIRI MKUU ASHIRIKI UFUNGUZI WA JUKWAA LA MAAFISA WATENDAJI WAKUU AFRIKA 2025


▪️Rais Ouattara asisitiza uongezaji thamani wa mazao
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili wa Maafisa Watendaji Wakuu barani Afrika ulioanza leo Mei 12, 2025, katika ukumbi wa hoteli ya Sofitel jijini Abidjan, Ivory Coast.

Mheshimiwa Majaliwa amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo ambao umefunguliwa na Rais wa Ivory Coast, Alassane Ouattara na kuwakutanisha Maafisa Watendaji Wakuu zaidi ya 3000, wawekezaji na Wakuu wa Nchi na Serikali.
Akizungumza na washiriki wa jukwaa hilo, Rais Ouattara amesema kuwa mkutano huo utawawezesha washiriki kujadili changamoto zinazolikabili bara la Afrika na kutoa majawabu ya changamoto hizo katika maeneo ya uchumi, fedha, mazingira na biashara.

Ameongeza kuwa ili bara la Afrika liweze kuendelea kuimarisha uchumi wake, viongozi wanapaswa kuendelea kuweka na kutekeleza mikakati ya kuongezea thamani mazao yanayozalishwa.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ameshiriki Mjadala wa Marais ulioendeshwa na Mwandishi wa Kujitegemea wa CNN, Larry Madowo na kuwashirikisha Marais wa Afrika Kusini, Rwanda, Mauritania na Makamu wa Rais wa Ivory Coast.

INEC YAKUBALI KUANZISHA MAJIMBO MAPYA 8 NA KUBADILI MAJINA MAJIMBO 12.


Mwenyekiti Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Jacobs Mwambegele amesema kuwa Tume imekubali kuanzisha Majimbo mapya 8 katika Mkoa wa Dar es Salaam,Dodoma,Mbeya,Simiyu,Geita na Shinyanga pamoja na kubadilishwa kwa majina ya Majimbo 12.

Jaji Mwambegele amesema hayo leo Mei 12,2025,Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Taarifa yake kuhusu Kugawa na Kubadilisha majina ya Majimbo ya Uchaguzi, kwa Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025.

Ambapo amesema kuwa Tume imezingatia zaidi vigezo vinne ambavyo imevipa uzito kwenye mchakato wa ugawaji wa Majimbo hayo ikiwa ni pamoja idadi ya watu, ambapo kwa Majimbo ya mjini kigezo kilikuwa kuanzia watu 600,000 na kwa Majimbo ya Vijijini ilikuwa kuaniza watu 400,000,Uwezo wa Ukumbi wa Bunge wa kuchukua Wabunge wapya,Idadi ya Wabunge Wanawake wa Viti Maalum na Jimbo moja la Uchaguzi kutokuwa katika Wilaya au Halmashauri mbili.
Akibainisha Majimbo mapya yaliyoanzishwa kuwa ni pamoja na Mkoa wa Dar es Salaam ambapo Jimbo la Uchaguzi la Ukonga limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Kivule,Jimbo la Mbagala limegawanywa na kuanzishwa Jimbo la Chamazi. Mkoa wa Dodoma limeanzishwa Jimbo jipya moja ambapo Jimbo la Uchaguzi la Dodoma mjini limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Mtumba.

VITUO 413 KUTUMIKA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI DODOMA


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule amewahimiza Wananchi wa Mkoa wa Dodoma wenye sifa ya kupiga kura kujitokeza katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura kwa awamu ya pili ambapo zoezi hilo linalotarajiwa kuanza mnamo tarehe 16 hadi 22 Mei 2025 katika ofisi zote za Kata Mkoani Dodoma.

Mhe Senyamule amesema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari akitoa Taarifa juu ya uboreshaji wa Daftari hilo la mpiga kura kwa awamu ya pili Mkoani Dodoma.

Na kusema kuwa ni muhimu kwa wapiga kura kuhakikisha kuwa taarifa zilizopo kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ni sahihi ili waweze kutimiza haki yao ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

"Zoezi hili ni muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu,hivyo naomba niendelee kusisitiza kila mwananchi mwenye sifa ya kupiga kura tarehe 16 hasi 22 Mei alike kituoni kwaajili ya kuhakiki Taarifa zake".

Saturday, May 10, 2025

RAIS DKT. SAMIA AONGOZA WATANZANIA KUAGA MWILI WA ALIYEKUWA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS HAYATI MZEE CLEOPA DAVID MSUYA KATIKA VIWANJA VYA KARIMJEE DAR ES SALAAM


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aongoza Watanzania kuaga mwili wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Mei, 2025.


Friday, May 9, 2025

ZAIDI YA MATUKIO 2,000 YA UKATILI YARIPOTIWA MANYARA NDANI YA MIEZI MINNE.


Na John Walter -Babati
Zaidi ya matukio 2,000 ya ukatili yameripotiwa katika Mkoa wa Manyara ndani ya kipindi cha miezi minne pekee, hali inayoashiria ongezeko kubwa la vitendo hivyo vinavyotishia ustawi wa jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amefichua takwimu hizo leo alipokuwa akiongoza kikao maalumu kilichowakutanisha viongozi mbalimbali wa serikali, wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Kamati za Usalama, Wakurugenzi, Makatibu Tawala pamoja na wadau wa maendeleo kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kukabiliana na ukatili huo.

Kwa mujibu wa RC Sendiga, kutoka Januari hadi Mei 2025, jumla ya matukio 2,201 ya ukatili yameripotiwa katika mkoa mzima. Wilaya ya Hanang imeongoza kwa kuwa na matukio 668, ikifuatiwa na wilaya nyingine kwa idadi tofauti.

“Kasi ya kuongezeka kwa ukatili ni ya kutisha, tunahitaji kuchukua hatua za haraka, za pamoja na madhubuti kuhakikisha jamii inalindwa dhidi ya vitendo hivi,” amesema RC Sendiga.

Thursday, May 8, 2025

JAMII YATAKIWA KUWA NA HOFU YA MUNGU NA KUKEMEA UKATILI.



Na John Walter -Babati
Siku chache baada ya tukio la kusikitisha la kubakwa na kuuawa kwa mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Ayatsea, uongozi wa SMAUJATA Wilaya ya Babati umetembelea kijiji cha Ayatsea kutoa elimu na kukemea vikali vitendo vya ukatili vinavyoendelea kushamiri kwa kufichwa ndani ya jamii.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa SMAUJATA Wilaya ya Babati, Ezekiel Tlanka, ambaye pia ni Katibu wa SMAUJATA Kanda ya Kaskazini, matukio zaidi ya manne ya ukatili yameripotiwa kutokea kijijini humo, lakini mara nyingi yamekuwa yakimalizwa kifamilia, jambo linalozidi kushusha utu na haki za waathirika.

“Vitendo hivi vinatia aibu na havifai kufumbiwa macho, tunatoa rai kwa jamii kuwa na hofu ya Mungu na kusimama kidete kukemea na kuwafichua wanaojihusisha na tabia hizi chafu,” alisema Tlanka wakati wa ziara hiyo.

Katika hatua ya kushangaza, Tlanka alivamia mkutano wa kina mama uliokuwa ukilenga kufanya usuluhishi wa mgogoro baada ya kijana mmoja kumtukana mama yake kwa matusi makali.

Wednesday, May 7, 2025

MAADHIMISHO YA WIKI YA ZIMAMOTO DUNIANI YAFANA MANYARA.


Na John Walter -Babati

Maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto Duniani yamefanyika leo mkoani Manyara, yakiongozwa na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani humo, RFO Gilbert Mvungi.

Maadhimisho hayo yameambatana na shughuli mbalimbali za kijamii na utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu tahadhari na uokoaji katika majanga ya moto.
Kamanda Mvungi ametumia mamlaka aliyopewa kupandisha vyeo baadhi ya maafisa wa jeshi hilo, kuanzia ngazi za chini hadi za kati akieleza kuwa, hatua hiyo inalenga kuongeza motisha kwa askari hao ili waendelee kutoa huduma bora kwa wananchi.

Maafisa wa Zimamoto, wakiwa wamevalia sare zao na kubeba mabango yenye ujumbe wa kaulimbiu ya mwaka huu isemayo "Shujaa wa Moto, Mlinzi wa Maisha: Okoa Maisha na Mali, Piga 114", walipita mitaa mbalimbali ya mji wa Babati wakihamasisha matumizi ya namba hiyo wakati wa dharura.

MWENGE WA UHURU KUPOKEWA NJOMBE MJINI,MWENYEKITI WA HALMASHAURI AELEZA A-Z MAANDALIZI ATAKA WANANCHI KUJITOKEZA


Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe Erasto Mpete amewataka wananchi wa halmashauri hiyo kujitokeza katika maeneo ya miradi yatakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru ili waweze kupokea ujumbe mahususi wa Mwenge na kujionea jinsi halmashauri yao inavyotekeleza miradi ya maendeleo.

Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake Mpete amesema,halmashauri ya mji wa Njombe inatarajia kupokea Mwenge wa Uhuru Mei 8 mwaka huu ukitokea wilayani Ludewa ambapo utatembelea katika kata tano na kumpongeza mkurugenzi wa halmashauri hiyo pamoja na wataalamu kwa maandalizi makubwa ya mapokezi.
"Mwenge wa Uhuru utapita katika kata tano za halamashauri ya mji wa Njombe na utaanza kata ya Luponde kijiji cha Madobole kwa hiyo tunaomba sana wananchi wa Madobole kujitokeza kwa wingi maana yake ndio sehemu ya mapokezi ili kuonyesha kwamba halmashauri ya mji wa Njombe tuko vizuri na baada ya kutoka Madobole Mwenge utakimbizwa kata ya Uwemba katika kijiji cha Ikisa na pale kutakuwa na tukio la kukagua msitu unaoitwa Ilonganjaula na mkimbiza mwenge atakabidhi mizinga ya Nyuki"amesema Mpete

Amesema Mwenge wa Uhuru katika kata ya Mji Mwema utapita katika maeneo mbalimbali ikiwemo katika kiwanda cha uchakataji na kusafirisha mazao ya Parachichi,Kituo cha Afya ambao huduma ya mionzi itazinduliwa na ugawaji wa vyandarua na bima huku pia katika kata hiyo kikietembelewa kikundi cha ujasiriamali wanaojishughulisha na uchoraji na baada ya hapo Mwenge wa Uhuru utaweza kwenda kuzindua madarasa sita katika shule ya sekondari Mpechi.

Tuesday, May 6, 2025

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MAREKANI WAFANYA PASSPORT DC EVENT

 

Joseph Kapinga, afisa ubalozi utalii na siasa ubalozi wachezaji Tanzania nchini Marekani, Washington DC akikaribisha wageni mbalimbali waliojitokeza siku ya Jumamosi May 3, 2025 tamasha la Passport DC ambalo kila ubalozi ulifanya tamasha hilo la kila mwaka kutangaza utalii wa nchi zao.


Monday, May 5, 2025

MKURUGENZI MKUU WA TCAA AFUNGUA RASMI KOZI YA PILI YA CHETI KWA WAKUFUNZI WA USALAMA WA ANGA (AVSEC) KATIKA CHUO CHA CATC, DAR ES SALAAM


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi akizungumza wakati wa kufungua kozi ya pili ya cheti kwa Wakufunzi wa Usalama wa Anga (AVSEC Instructors Certification Phase Two Course) katika Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa anga Tanzania (CATC) Aristid Kanje akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa Kozi ya pili ya cheti kwa Wakufunzi wa Usalama wa Anga (AVSEC Instructors Certification Phase Two Course).

ESHI LA POLISI LINACHUNGUZA TUHUMA ZA KUHUSIKA ASKARI KATIKA KUPOTEA KWA MDUDE NYANGALI

 


MAONO YA RAIS DKT. SAMIA YAMEIPAISHA SEKTA YA ANGA-MAJALIWA


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia wadau mbalimbali wa viwanja vya ndege wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 73 wa Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege kwa Ukanda wa Afrika (ACI Afrika) unaofanyika jijini Arusha
Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa akziungumza kuhusu jukwaa hilo adimu linalowaleta pamoja viongozi na wasimamizi wa usafiri wa anga, waendeshaji wa viwanja vya ndege kujadili na kubadilishana mawazo katika kuboresha na kuikuza sekta ya usafiri wa Anga.
Rais wa Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege kwa Ukanda wa Afrika (ACI Afrika) Emanuel Chaves akizungumzia mafanikio endelevu sekta ya anga afrika wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 73 wa Baraza la Kimataifa la Viwanja vya Ndege kwa Ukanda wa Afrika (ACI Afrika) unaofanyika jijini Arusha

Sunday, May 4, 2025

WANANCHI 412 WAPATA HUDUMA YA VIPIMO VYA AFYA BURE ST.JOSEPH IKELU,SERIKALI YAOMBWA KUPUNGUZA KODI



Serikali imeombwa kuzipunguzia kodi hospitali zinazo milikiwa na taasisi za dini ili kurahisisha uendeshaji kwa kuwa hazijaanzishwa kwa lengo la kufanya biashara zaidi ya kutoa huduma kwa wananchi kutimiza takwa la kanisa kutoa huduma ya kimwili na kiroho.

Wito huo umetolewa na Pandre Inocent Chaula ambaye ni katibu wa afya na katibu wa Mhashamu Askofu Ausebius Kyando Jimbo Katoliki la Njombe wakati wa maadhimisho ya Jubilei kuu ya Ukristo 2025 iliyofanyika katika hospitali ya St.Joseph Ikelu iliyopo halmashauri ya mji wa Makambako.
"Hospitali imeletwa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na sio biashara tuombe tusaidiane katika huduma hizi,tunapata changamoto ya katika uendeshaji michango mingi,kodi nyingi sasa tuwaombe viongozi wa serikali mliopo mtusemee kama kituo cha huduma na sio biashara"amesema Padre Chaula

RC DODOMA AITAKA TANROADS KUTAFUTA NJIA MBADALA KWA WANANCHI WAKATI WA UJENZI WA DARAJA LA MORENA JIJINI DODOMA

Maelekezo yametolewa kwa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS)Mkoa wa Dodoma ambao unasimamia Mradi wa upanuzi wa daraja la Morena, kutafuta njia mbadala itakayotumiwa na wananchi watakaohitaji huduma upande wa pili wa daraja baada ya barabara iliyokua ikiunganishwa na daraja hilo kufungwa kwa muda ili kupisha ujenzi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa maelekezo hayo wiki iliyopita Aprili 29, 2025 alipofanya ziara fupi ya kutembelea eneo hilo la mradi lililopo kwenye makutano ya barabara ya kuelekea Morena na Mkoa wa Morogoro (Shabiby) ili kujionea maendeleo ya ujenzi huo.
“Hapa mmepata mawazo ya kutafuta sehemu nyingine ambazo zinaweza kuwa ‘altenative’, muiwekee vibao ili mtu aone ana ‘option’ tofauti tofauti za kufika katika hilo eneo. Hilo lifanyeni, tarehe 1 tupate taarifa kuwa hawa wananchi wanapita wapi maeneo mengine ili kulifikia hili eneo”.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri amepongeza upanuzi wa daraja hilo kwani utamaliza changamoto ya mafuriko kwenye makazi ya watu kipindi cha mvua kubwa lakini pia litaondoa changamoto za kiafya kutokana na kuzaliana kwa mbu pindi maji ya mvua yanapotuama eneo hilo sambamba na magonjwa ya mlipuko.

SERIKALI INALAANI VIKALI NA KUKEMEA TUKIO LA KUSHAMBULIWA NA KUUMIZWA KATIBU MKUU WA TEC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia mara baada ya Misa ya Kumsimika Askofu wa Jimbo Jipya Katoliki la Bagamoyo Mhashamu Askofu Stephano Lameck Musomba pamoja na Sherehe ya Uzinduzi wa Jimbo hilo iliyofanyika katika Uwanja wa St. Mary Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani leo tarehe 04 Mei 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa St. Mary Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kushiriki Sherehe ya Uzinduzi wa Jimbo Jipya Katoliki la Bagamoyo na kusimikwa kwa Askofu wa kwanza wa Jimbo hilo Mhashamu Askofu Stephano Lameck Musomba leo tarehe 04 Mei 2025.
Askofu wa Jimbo Jipya Katoliki la Bagamoyo Mhashamu Askofu Stephano Lameck akikabidhiwa fimbo ya Kiaskofu wakati wa Misa ya Kumsimika Askofu huyo na Sherehe ya Uzinduzi wa Jimbo Jipya Katoliki la Bagamoyo leo tarehe 04 Mei 2025.

Friday, May 2, 2025

HOSPITALI YA ST. JOSEPH IKELU YAREJESHA TABASAMU KWA WANANCHI NJOMBE,WATOA HUDUMA ZA VIPIMO BURE


Wakati Kanisa Katoriki likiadhimisha Jubilei ya mwaka 2025 ya Ukristo na siku ya wafanyakazi Duniani,Hosptali ya St Joseph Ikelu iliyopo kata ya Utengule halmashauri ya mji wa Makambako inatoa huduma ya vipimo bure kwa wananchi wenye nia ya kujua afya zao ili waweze kuanza matibabu.

Akizungumza wakati zoezi la vipimo likiendelea Daktari wa hospitali hiyo,Dkt.Polikap Nyengela amesema vipimo vinavyotolewa ni pamoja na kipimo cha Kisukari,Macho,Tezi dume,Saratani ya Matiti,shinikizo la damu na hali ya lishe,ambapo lengo la kutoa huduma hiyo bure ni kurejesha kwa jamii kile walichokipata ili kuwasaidia wananchi kutambua hali.
Amesema kwa sasa watu wengi wanakumbwa na magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu hali ambayo inapekekea kuathirika kwa mfumo wa mwili na kusababisha wengi wao kuishi na magonjwa kwa muda mrefu bila kujua kama wanaumwa kutokana na kutokuwa na kawaida ya kupima afya zao.

"Tunarudisha kwa jamii kile ambacho tumefanikiwa kukipata na zoezi hili tunalifanya kwa muda wa siku mbili tarehe moja leo (jana) na leo tarehe mbili"amesema Nyengela

CMSA YAZINDUA SHINDANO LA MASOKO YA MITAJI KWA WANAFUNZI VYUO VIKUU NA TAASISI ZA ELIMU YA JUU


MAMLAKA ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) imezindua shindano la Masoko ya Mitaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na Taasisi za elimu ya juu kwa lengo likiwa ni mkakati wa mamlaka hiyo kuongeza uelewa kwa wananchi.

Uzinduzi wa Shindano hilo umefanyika leo Mei 2 mwaka huu jijini Dar es Salaam ,sambamba na kutunuku vyeti kwa wahitimu wa kozi ya watendaji katika Masoko ya mitaji wanaokidhi viwango vya kimataifa.
Akizungumza kuhusu kuzindua shindano la Masoko ya mitaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na Taasisi za elimu ya juu ,Ofisa Mtendaji Mkuu wa CMSA Dk.Nicodemus Mkama amesema katika kutekeleza moja ya mikakati ya Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha 2019/20 – 2029/30 CMSA inatoa elimu kwa umma kwa lengo la kuongeza uelewa na ushiriki wa wananchi kuhusu fursa zinazopatikana katika masoko ya mitaji.

Dkt.Mkama amesema katika utekelezaji wa mkakati huo CMSA inaendesha Shindano kwa Wanafunzi wa Vyuo vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu kwa lengo la kuongeza uelewa na kuwajengea vijana uwezo wa kushiriki katika masoko ya mitaji kwa kutumia njia ya mitandao ya kielektroniki ,yaani simu za mikononi na intaneti.

Thursday, May 1, 2025

WATUMISHI WA NBAA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI MEI MOSI, 2025


Baadhi ya Watumishi wa Bodi ya Taifa ya wahasibu na wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakipita mbele ya Jukwaa kuu huku wakiwa na bango lenye ujumbe kuhusiana Wafanyakazi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

RAIS WA ZANZIBAR DK. HUSSEIN MWINYI MGENI RASMI MAADHIMISHO KILELE CHA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Dunia Mei Mosi 2025, yaliyofanyika Mkoa wa Kusini Unguja katika viwanja vya Kizimkazi leo 1-5-2025.
WAFANYAKAZI wa Taasisi za Serikali na Binafsi Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi 2025, maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Mkoa wa Kusini Unguja katika viwanja vya Kizimkazi leo 1-5-2025
WAFANYAKAZI wa Taasisi za Serikali na Binafsi Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi 2025, maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Mkoa wa Kusini Unguja katika viwanja vya Kizimkazi leo 1-5-2025