Tuesday, October 13, 2015

DK MAGUFULI ASEMA BADO SIKU 12 KUWA RAIS WATtANZANIA

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akijinadi kwa wananchi kuomba kura za ndiyo katika mkutano wa kampeni mjini Mkuranga, Pwani leo.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Wasanii wakishangilia wakati Dk Magufuli akiwasili kwenye mkutano wa kampeni katika Jimbo la Kibiti, mkoani Pwani leo.
 Mama mfuasi wa CCM akionesha furaha yake baada ya kumuona Dk Magufuli  wakati msafara wake uliposimamishwa na wananchi katika Kijiji cha Mbwemkulu, Wilaya ya Kilwa

 Mfugaji wa Jamii ya Kisukuma, akifurahia kofia aliyopatiwa zawadi na Dk Magufuli katika mkutano wa kampeni eneo la Nyamwage, wilayani Rufuji leo.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akimhesabia Mgombea Ubunge Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega aliyekuwa akipiga Push Up wakati wa mkutano wa kampeni mjini Mkuranga
 Wananchi wa Kata ya Nangaru, Jimbo la Nchinga, wakishangilia baada ya kumuona Dk Magufuli akiwasili kwenye mkutano wa kampeni za CCM, katika Kata ya Nangaru, Jimbo la Nchinga, wMkoa wa Lindi
 Dk Magufuli akimvisha kofia mmoja wa wananchama wa upinzani waliamua kuhamia CCM katika mkutano wa kampeni
 Dk Magufuli akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya CCM, Mgombea ubunge Jimbo la Nchinga, Said Mtanda katika mkutano wa kampeni Kata ya Nangaru PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mama akishangaa kumuona Dk Magufuli wilayani Kilwa
 Mmoja w a waliokuwa viongozi wa CUF, akitangaza kujitoa  Chama Cha Wananchi (CUF), NA KUJIUNGA ccm katika kutano wa kampeni za CCM,mjini Kilwa.
 Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Kilwa Kusini, wakati wa mkutano wa kampeni za CCM  mjini Kilwa Masoko.

 Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Kilwa Kaskazini, Murtaza  Mangungu eneo la Malendegu, wilayani Kilwa.

 Wananchi wakishangilia kwa furaha na kuahidi kumpigia kura za ndiyo katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu, Dk Magufuli..PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG


 Wananchi wa Kijiji cha Jaribu wakishangilia wakati Dk  akihutubia na kuomba apigiwe kura za ndiyo.

 Wananchi wakiwa na furaha kukubali kunyoosha mikono juu ikiwa ni ishara kumkubali Dk Magufuli na kuahidi kumpigia kura Oktoba 25 mwaka huu.
 Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Mkuranga,Abdalah Ulega
 Mke wa Mgombea ubunge Jimbo la Mkuranga,Abdalah Ulega, Mariam akiwa na furaha baada ya kuona mwenzi wake akipigiwa debe na Dk Mafuli.
Aliyekuwa Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima, akiwapigia debe Dk Magufuli na Ulenga mjini Mkuranga

9 comments:

  1. Rais labda awe mwenyekiti wa CCM

    ReplyDelete
  2. Weee ukawa tuuu na badooooooo

    ReplyDelete
  3. Kwa mapengo ya huyu bibi hata 45 hana
    CCM hiyo
    Ndo maisha bora
    Tuchaguwe CCM tunaumwa

    ReplyDelete
  4. Labda Rais wa Msoga
    Hata Chato hatumtaki
    Uchifu tumempa Lowassa

    ReplyDelete
  5. Ukawa mmekuwa kama wehu!!! Hamguswiii!!!
    Tunahesabu siku...mtanywea nywee...kama maji ya mtungini.

    ReplyDelete
  6. Lowasa atabakia na uchifu wake wa kununua, uraisi wa magufuli. Ukawa jitaraarisheni kisaikolojia msije mkapata uchizi wa kudumu.

    ReplyDelete
  7. Rais awamu ya tano ni: John Pombe Joseph Magufuli.

    ReplyDelete
  8. Labda aende akawe baloji wa nyumba 10 wa huko Chato

    ReplyDelete
  9. Rais mpya wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ni Dr Magufuli.

    ReplyDelete

bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake