Tuesday, November 17, 2015

TANZIA



UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WASHINGTON, D.C.



TAARIFA YA MSIBA

Mheshimiwa Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania nchini Marekani, anasikitika kutangaza kifo cha Bi. Nyamiti Ivan Lusinde, aliyekuwa mfanyakazi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Washington DC.

Bi. Nyamiti Ivan Lusinde  alifariki dunia Jumanne tarehe 17 Novemba, 2015 Dar Es Salaam, Tanzania ambapo alikuwa likizo yake ya mwaka.

Kitabu cha rambirambi kipo nyumbani kwa marehemu
20408 Honey Crisp Lane, Apartment E
Germantown, MD 20876

Maelezo zaidi kuhusu taratibu za mazishi yatatolewa mara baada kupokea taarifa zaidi  kutoka nyumbani Tanzania.

5 comments:

  1. Eeh Mungu uilaze roho ya Nyamiti Ivan Lusinde mahali pema peponi. Nyamiti, upumzike katika raha ya Mungu ya milele. AMEN.

    Dada Joyce Mwombela na familia yote ya Mwombelas.

    ReplyDelete
  2. May your soul RIEP. Duh so sad.

    ReplyDelete
  3. Oh my God, oh my God. NYAMIZI UMEONDOKA TO SOON. TUMEFIKA 2 WEEKS AGO UBALOZINI UKATUSAIDIA KUPATA VISA NA FAMILIA YANGU, KUMBE ULIKUWA U ATUAGA JAMANI. NATAMANI NIUE MSIBA UKO WAPI IN TANZANIA ILI NIFIKE KWA RAMBIRAMBI. JAMANI. MUNGU WANGU WEE..
    JOYCE RWHUMBIZA.

    ReplyDelete
  4. Poleni sana , mungu ailaze roho ya marehemu peponi, Ameen.
    please tufahamishane yoyote atakayepata mipango ya mazishi na rambirambi.
    SHUKRANI
    Mohamed and family

    ReplyDelete
  5. Msiba uko wapi Tanzania? Details za mazishi zitasaidia.

    ReplyDelete

bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake