
Bw Said Abdallah [41], ambaye ni albino, akiwa amelala kitandani katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, huku akiwa amefungwa bandeji kwenye mkono wake wa kushoto baada ya kukatwa kiganja chake na watu wanaodaiwa kuwa Wamasai na kisha kuondoka na kiganja hicho.
Said Abdallah[41] mkazi wa kijiji cha Melela Wilaya ya Mvomero Mkoani hapa
amelazwa katika hospital ya mkoa baada ya kudaiwa kukatwa mkono wake wa kushoto
na wamasai kisha kutimka nao!
amelazwa katika hospital ya mkoa baada ya kudaiwa kukatwa mkono wake wa kushoto
na wamasai kisha kutimka nao!
Tukio hilo lilitokea siku ya Jumamosi April 10 Majira ya saa 9 Alasili katika kijiji cha Melela ambacho kiko umbali wa kilometa 30 hivi kutoka morogoro mjini, ambapo imeelezwa kwamba wamsai hao walimvamia albino huyo ndani ya shamba lake na kuanza kumchapa bakora na baadae kumfyeka mkono wake wa kushoto kwa kutumia masime waliokuwa nayo.
Akizungumza na mtandao huu kwa taabu ndani ya wodi nomba 1 ya hospitali ya mkoa wa morogoro, Bw Said alisema kwamba siku ya tukio majira ya saa 9 alikuwa akilima katika shamba lake hilo lililopo maeno ya Kongolelo katika kijiji hichoambacho wakazi wake wengi ni wamasai.
Akisimulia zaidi mkasa huo Albino huyo alikuwa na haya ya kusema:
"Jana majira ya 9 nilikuwa nalima katika shamba langu ghafla niliona wamasai wawili wakiingiza Ngo'mbe kwenye shamba langu nilipowauliza kulikoni badala ya kunijibu waliniomba ugoro nikawaeleza kwamba sina.
"Kitendo hicho cha kuwanyima ugoro kiliwauzi na kuamua kunichalaza bakoro kichwani kutokana na wingi wa bakola hizo walizokuwa wakinipiga kichwani nilianguka chini nakupoteza fahamu, nilipopata fahamu nilijikuta nimeshakatwa
mkono wangu.
mkono wangu.
"Nilitafuta hicho kipande cha mkono wangu pale eneo la tukio sijakiona mpaka naondolewa eneo lile, nahisi wamasai wale waliondoka nao na kwamba lengo lao lilikuwa ni kuchukua kiungo changu kwani sina ugomvi nao
wowote", alisema Albino huyo ambaye bado hajaoa.
wowote", alisema Albino huyo ambaye bado hajaoa.
Muuguzi wa zamu wa wodi, Bi Rose Sengo, akizungumza na wanahabari kuhusiana na hali ya Albino huyo jana asubuhi


No comments:
Post a Comment