Mmoja kati ya mashuhuda wa tukio hilo aliliambia Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa, tukio hilo lilitokea hivi karibuni na chanzo cha kijana huyo kufanya mauaji hayo ni kutokana na Laheri ambaye ni mwanafunzi kumkataa kimapenzi.

Absalum Mbogela (22).
Alisema kuwa binti huyo alikutwa na mauti akiwa njiani kwenda bustanini kumwagilia mazao ambapo kijana huyo alimvizia njiani akiwa na nondo na kisu na kumpiga nayo kichwani kisha kumchoma kisu shavuni.
Baada ya kufanya ukatili huo inadaiwa kijana huyo alikimbia na alipofikia umbali wa kama hatua mia tano, alikunywa sumu na kufariki muda mchache baadae.
“Absalum kwa muda mrefu amekuwa akimtaka kimapenzi msichana huyo na kuna wakati alikuwa akimtishia kumfanya kitu kibaya na sasa amekitimiza na yeye kujiua,”kilisema chanzo chetu.

Laheri Maneno (16).
Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Itagutwa, Bahati Kamilongo alisema kuwa, kijana huyo alikutwa amekunywa sumu na alifariki dunia wakati jitihada za kumpeleka hospitalini zikifanyika.
Naye Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Evarist Mangalla alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kwamba jeshi lake linaendelea na uchuguzi zaidi . chanzo:GPL
No comments:
Post a Comment
bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake