WAZIRI WA MAMBO YA NDANI ATOA TAMKO
WAKTI HUOHUO, serikali leo mchana imependekeza pande zinazosigana katika siasia mkoani Arusha zikae meza moja na kutafuta suluhu kwa mazungumzo na sio kwa vurugu. Hayo yamesemwa mchana huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mh. Shamsi Vuai Nahodha alipoongea na wanahabari ofisini kwake jijini Dar, akiwa na Inspketa Jenerali wa Polisi, Afande Saidi Mwema, ikiwa ni siku moja baada ya kutokea vurugu baina ya polisi na wafuasi wa CHADEMA baada ya kufanya maandamano yanayodaiwa kuwa si halali. Inasemekana watu wawili wamepoteza maisha na sita wamejeruhiwa vibaya katika vurumai ya jana.
Mh. Nahodha, ambaye amekuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibra kwa muda mrefu na mwenye uzoefu wa mambo hayo, amesema serikali imeamua kuingilia kati mgogoro huo kwa kuziweka meza moja pande mbili zinazokinzana ili kuleta amani mpya na kuidumisha jijini Arusha.
Pia Mh. Nahodha amesema askari polisi yeyote ambaye itathibitika alikwenda nje ya mipaka yake ya kazi atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Mh. Nahodha, ambaye amekuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibra kwa muda mrefu na mwenye uzoefu wa mambo hayo, amesema serikali imeamua kuingilia kati mgogoro huo kwa kuziweka meza moja pande mbili zinazokinzana ili kuleta amani mpya na kuidumisha jijini Arusha.
Pia Mh. Nahodha amesema askari polisi yeyote ambaye itathibitika alikwenda nje ya mipaka yake ya kazi atachukuliwa hatua kali za kisheria.
No comments:
Post a Comment
bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake