ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, May 24, 2011

Kumbukumbu ya Mzee Matthew Elirehema Mmari
Ni mwaka mmoja sasa umepita toka baba yetu mpendwa mzee Matthew Elirehema Mmari ulipotuacha. Hakuna maneno yanayoweza kuelezea machungu yanayoletwa na kukukosa wewe katika maisha yetu lakini Mungu wetu wa Rehema aliona kuwa ulikuwa tayari kurudi kwake aliyekuumba nasi inabidi tukubali.
Wewe ndiye uliyekuwa Nguzo na Msingi katika kutuongoza na kufurahia maisha yetu. Tunakumbuka sana ukarimu na ucheshi wako; mafundisho na maadili yako. Hatutaweza kamwe kusahau msisitizo wako kuhusu Upendo na Umoja kati yetu pia kumcha Mungu.
Unakumbukwa sana na ndugu, jamaa na marafiki. Kipekee zaidi unakumbukwa na mkeo Mrs. Dekarisa Mmari; Wanao Vincent, Hubert, Judith, Robert, Joyce, Neema; Wajukuu wako G, Tevin, Amani, Baraka, Daudi, Dekarisa na Dekarisa-Silvia. Hakuna atakayeweza kuliziba pengo ulilotuachia Baba.  

1 comment:

Anonymous said...

Bwana ametoa...bwana ametwaa jilna la lihimidiwe...R.I.P Baba amen