"Kuna mwanangu mmoja hivi, wa mitaa ya Ilala kaangusha mjengo huku, basi sijui anataka kuwapangisha jamaa? Kila msimu ukianza unamwona misele haiishi. Ila ndiyo maisha yenyewe, uongo? Tusibaniane."
Halafu uliza nimekuja kufuata nini? Mchizi wangu mmoja kanialika nije nishangae magumashi ya huku, hiki kipindi cha Bunge, ujue kunakuwaga na mishe. Huku unaweza kudhani watu wamekubali makao makuu yawepo. Kumbe mitikasi tu watu wanalia denge posho za majaa.
...na wanakamua kweli ujue...
Kuna mwanangu mmoja hivi, wa mitaa ya Ilala kaangusha mjengo huku, basi sijui anataka kuwapangisha jamaa? Kila msimu ukianza unamwona misele haiishi. Ila ndiyo maisha yenyewe, uongo? Tusibaniane.
Pamoja na ishu nyingine, ni kwamba Ngwea tushampumzisha na mida mida nitakuwa nachomoka huku kuelekea Dar kwenye Kili Awards kwenda kushuhudia mtanange na wiki ijayo najitupa kwenye shoo mbili kubwa, jijini, Ijumaa na Jumamosi, utaona mwenyewe.
Sasa bwana katika mishe zangu si nikazama maishani? Nikakutana na mwanangu mmoja hivi tulikuwa naye skonga longtaimu. Mchizi kafungua ishu zake sijui za duka la spea huku, basi mambo yamenyooka, ndambi la kutosha, anakula tu kiulaini.
Sasa ana demu wake fulani hivi, ukimwona anakuja hivi, ...mkali, lazima utampitisha kwa vigezo vya kimataifa ila sasa ngoja mkae. Anaongea kupita kiasi samtaimz hata mchizi wake mwenyewe anamponda.
Sasa siku mbili hizi, maana kwa hisani ya mshkaji aliyenialika Bata zimekuwa haziishi, nikakutana na kisanga kimoja. Yule demu bwana kamchenjia shosti yake, kamchana chana na viwembe. Kisa bwana kamkuta na meseji za jamaa yake, akaanza ku’dauti haukamz?
Unaona bwana?.... Zee kama Zee ikabidi niingilie kati kutaka kujua mchongo mzima, kwamba ishu inakuwaje?
Dah kumbe domo limemponza mwanangu. Kakaa chini, akaanza kumfagilia jamaa yake kwamba mtundu na nini anamfanyia mambo ya ajabu wakiwa chimbo, mwenyewe anajua kwamba anaharibu kumbe wenzake hizo tabia chafu ndiyo wanazozitaka.
Wasivutiwe na jamaa nini?
Demu unaambiwa alifunguka jamaa anapiga utunda, mtu wa kuzama na nini, si unajua zile, mwenyewe akawa anahadithia kama hapendi pendi vile kumbe wenzake ndiyo mambo yao hayo, kimoyo moyo wakawa kama wanamwambia, si utuachie sisi?
Watu wakaanza kuisaka namba ya jamaa kwa udi na uvumba na unajua watoto wa kike wakitaka lao hasa wakiwa watoto wa mjini. Waliipigia misele hiyo namba unaambiwa mwanangu mwenyewe mpaka wakaikamata, wakaanza kukomaa naye.Kwani alichukua raundi?
We si unajua watoto wa kike wakitaka lao, siku tatu nyingi jamaa huyu, ..akajaa kwa wa kwanza unaambiwa, wakakubaliana akatesti kama kweli au ilikuwa miyeyusho ya mropokaji.
...weeeeeeee....Sista duu kurudi hata maneno hayamtoki vizuri. Mwenzake akaona anacheleweshwa na yeye akaingia kwenye misheni posibo.
Si kuna misheni imposibo?........Wao yao ikawa posibo, maana mitego michache tu jamaa akajaa wakawa washamkamatia, wakawa wanapokezana tu, leo huyu, kesho yule mpaka yule mropokaji sasa akaanza kujiuliza mbona jamaa kama kanipotezea?
Kuja kuanza uchunguzi, akaja kushtukia kwamba watu washamkamata, ndiyo akaanzisha valangati bwana. Mtu mzima nilipata muda ujue wa kupiga naye stori huyo demu, tena mchizi wake akiwa pembeni.
Tukamuuliza haukamu unauza siri za kampuni?..................Eti, “Oooh nilikuwa nasema hivyo ili wasimpende, nikawa namchafua si unajua wanawake wengi hawapendi mambo hayo?”.
Likanitoka swali tu sasa wewe umeona lini mchafu akachafuka? Mtu kashachafuka zamani unajidanganya kumchafua, umechemka!
Jamani kwa aliye Domu kama una supu ya karibu naomba, baadaye baadaye natimua zangu mie!
No comments:
Post a Comment
bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake