Sunday, May 11, 2014

TOUCH FOUNDATION KUENDELEA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA TANZANIA

 Balozi Manongi na   Upendo  Manongi  wakiwa na  Padre  Dkt. Peter Le Jacq wa  Shirika la  Maryknoll ambaye alianza kufanya kazi na Bugando Medical Center katika miaka ya  80  ambaye kwa kushirikiana kwa karibu na  Marehemu  Mhashamu Askofu Aloysius Balina walianza juhudi za  kuyatafutia ufumbuzi  matatizo ya sekta ya afya  hasa upungufu wa  Madaktari. Padre Dkt. Jacq pamoja na rafiki zake  alikuwa chumbuko la Kamati ya Touching Tanzania katika  miaka hiyo ya  80 na hatimaye kuzaliwa kwa Touch Foundation mwaka 2004. Dkt. Jacq naye kwa upande wake amesifu na kutambua  mchango wa Mhe. Rais Jakaya Kikwete na kujituma kwake kuimarisha sekta ya afya kwa kushirikiana na wadau wengine.
 Rais wa Touch Foundation,  Bw. Lowell Bryan akiwa  katika picha ya pamoja na  Balozi Tuvako  Manongi,  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania  Umoja wa Mataifa na Mke wa Balozi, Bibi Upendo Manongi wakati wa  Hafla ya Asante Supper 2014 iliyofanyika  mwishoni mwa wiki,  hafla  hiyo ilikuwa ni kuadhimisha miaka 10 ya Taasisi hiyo  iliyokwenda sambamba na  harambee ya kuchangia  uimarishaji wa sekta ya Afya nchini Tanzania. Touch Foundation inafanya kazi kwa karibu  na  Serikali ya Tanzania na Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki cha Afya na Sayansi Mwambata ( CUHAS)  Bugando Tanzania.   Katika  hafla hiyo, ambayo ilihudhuriwa na   Viongozi wa  CUHAS wakiongozwa na  Mhashamu Askofu Mkuu,  Yuda Thaddaaeus  Ruwa'ichi, Bw. Bryan alisifu na kupongeza utashi wa Kisiasa na Uongozi wa Mhe. Rais Jakaya  Mrisho Kikwete katika kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi , ushirikiano wake  na kutambua kwake mchango wa sekta binafsi katika  eneo hilo.
Makamu Mkuu wa  CUHAS  Professa  Jacob Mtabaji kushoto kwa  Balozi Manongi na  Professa Paschalis Rugarabamu ambao walikuwa sehemu ya Ujumbe  uliohudhuria Asante Supper 2014 wakiwa katika picha ya pamoja na  baadhi ya Maofisa wa  Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa. 

Na Mwandishi Maalum
Touch Foundation ,  Taasisi  isiyo ya kiserikali  na yenye makao yake nchini Marekani,  mwishoni mwa wiki ( Mei 8),  imeadhimisha miaka  kumi ya kazi zake  na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali  ya Tanzania na  Taasisi nyingine katika uboreshaji na uimarishaji wa  sekta ya afya nchi.
Katika hafla  iliyojulikana kama   Asante  Supper 2014,  ilihusisha pia utoaji wa tuzo kwa wadau mbalimbali ambao wamekuwa  nguzo muhimu ya  Taasisi hiyo. Asante Supper  ilihusisha pia  harambee ya  uchangishaji wa fedha kwaajili ya kusaidia sekta  hiyo  ya afya. Hafla hiyo  ilifanyika katika ukumbi wa  Morgan Library Museum, Jijini New York.
Akiwakaribisha wageni waalikwa,  Rais wa Touch Foundation,  Lowell Bryan pamoja na  kuelezea mafanikio ya taasisi yake iliyoanzishwa mwaka 2004 katika uboreshaji wa sekta ya afya  nchini Tanzania, amewataka wafadhili mbalimbali  kuendelea kujitolea na kuchangia  zaidi ili  sekta ya afya nchini Tanzania iweze kuimarika na hatimaye kumaliza au kupunguza changamoto  mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo.
Akasema  utashi wa kisiasa  na wa kiuongozi ambao Mh. Rais  Jakaya Mrisho Kikwete ameonyesha katika, si tu kutambua na kuthamini  mchango wa Touch Foundation na  Taasisi nyigine kama  hiyo, bali pia amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba  sekta ya afya inaimarika  nchini Tanzania na huduma za afya zinawafikia wananchi kule walipo.

Naye Padre Dkt. Peter le Jacq ambaye naye amekuwa na mchango  mkubwa wa  uimarishaji wa sekta ya afya nchini kupitia Hopistali  ya   Buganda ana ambaye haswa ni  chimbuko la Touch Foundation,  hakusita kutoa  shukrani zake kwa Rais Kikwete na  kumuelezea kama  kiongozi anayejituma,  kujitolea na mwenye  ushirikiano  mzuri za sekta binafsi.
Katika  Miaka  kumi ya uhai wake Touch Foundation imekuwa ikishirikiana  na kufanya kazi kwa  Karibu na  Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, na hususani Chuo Kikuu  cha Kikatoliki cha  Afya na    Sayansi Mwambata  cha Bugando (CUHAS). Ushirikiano huo  unahusisha  katika maeneo mbalimbali mtambuka yakiwamo mafunzo ya madaktari na wataalam  wa fani mbalimbali  kupitia CUHAS na hivyo kuchagia  ongezeko la madaktari na wataalam.
 Mbali ya  watendaji wakuu wa  Touch Foundation,  wakiongonzwa na Rais wake, Bw. Lowell Bryan,  pamoja na wafadhili.Asante Supper 2014 ilihudhuriwa  pia na wageni  maalum  kutoka Tanzania na ujumbe huo   ulihusisha   Muhashamu Thaddaeus Ruwa’ichi Askofu Mkuu wa  Mwanza  na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,Balozi Tuvako Manongi  alikuwa miongoni wa wageni waaalikwa.
Wengine kutoka  CUHAS walikuwa ni Askofu Augustine Shao,   Makamu Mkuu wa  CUHAS ,Profesa Jacob Mtabaji,  Makamu  Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine,  Padre Dkt. Charles Kitima, Profesa Paschalis Rugarabamu, Dkt, Isidor Nyahomela, Dkt. Frederick Kigadye, Dkt. Charles Majinge,  Dkt. Manage Manyama,  Dkt. Stella Mongella,  Dkt. Godwin, Godfrey Sharau na Sister Marie- Jose Voeten kutoka  hospitali  Teule ya  Sengerema.
Baadhi ya  Madaktari hao kutoka Bugando   na hasa wale walionufaika na  ufadhili wa Touch Foundation walielezea walivyonufaika na  ufadhili huo ambao umewawezesha kusoma, kujipatia ujuzi na hivyo kupata fursa ya kuwahudumia watanzania  wenzao.

No comments:

Post a Comment

bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake