Advertisements

Wednesday, October 22, 2014

Wiki ya Umoja wa Mataifa kuadhimisha miaka 69 yazinduliwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw.John Haule (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa tarehe 21 hadi 25 Oktoba, 2014. Wiki hiyo ambayo huadhimishwa kila mwaka itajumuisha gwaride rasmi na kupandishwa bendera katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam tarehe 24 Oktoba. Sherehe hizo zitahitimishwa na bonanza la michezo mbalimbali litakalo husisha wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje kwenye viwanja vya Gymkhana tarehe 25 Oktoba. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni "Agenda ya Maendeleo baada ya 2015 - Asiachwe mtu nyuma (The Post 2015 Development Agenda - leaving No one Behind)". Wakwanza kushoto ni Bwa. Alvaro Rodriguez, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, na wakwanza kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celestine Mushy. 
Wawakilishi wa Idara na Vitengo kutoka Mambo ya Nje 
Bw. Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa Habari 
Waandishi wa Habari kutoka mashirika mbalimbali ya habari hapa nchini wakisikiliza maelezo kuhusu maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa. 
Kikao kikiendelea 

Picha na Reginald philip

No comments: