Wednesday, July 22, 2015

RAIS OBAMA KUWASILI KENYA SIKU YA IJUMAA JIONI, BAADHI YA MITAA NA ANGA KUFUNGWA KWA MUDA

US President Barack Obama boards Air Force One at Andrews Air Force Base in Maryland. PHOTO | AFP
Ulinzi ni mkali kweli kweli zaidi na polisi 10,000 wamemwagwa jiji la Nairobi kwa ajili yakulinda usalama kwa ujio wa Rais wa Marekani Mhe. Barack Obama anayetarajiwa kuwasili jijini Nairobi siku ya Ijumaa kati ya saa 1;45 na 2;35 jioni ya siku hiyo ya July 24, 2015.

Baadhi ya barabara za jiji la Nairobi zimefungwa kwa ajili ya kuimarisha usalama wa jiji hilo wakati wa ujio wa Rais huyo wa Marekani.

Anga la nchi hiyo litafungwa siku ya Ijumaa mida hiyo ya Rais Obama atakapo wasili ni siku ya Jumapili jioni Rais Obama atakapoondoka nchini humo..Shirika la Anga nchini Kenya KCAA limetangaza siku ya Ijumaa kati 1;45 na 8;35 hakutaruhusiwa kwa ndege yeyote kuruka au kutua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo kenyata na hivyo hivyo ndivyo itakavyokua  siku ya Jumapili kati ya 11;05 na 11;45 jioni Rais Obama atakapokua amemaliza ziara nchini humo/

No comments:

Post a Comment

bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake