Advertisements

Friday, September 4, 2015

ALIYEFANYA MAUAJI YA KINYAMA JIJINI ARUSHA AKAMATWA


Na Woinde  Shizza

Mtuhumiwa mauaji ya kutisha ya kumkata viungo vya mwili marehemu zikiwemo sehemu za siri, viganja vya mikono na matiti mauaji yaliotokea kwenye hotel ya A Square Belmot amekamatwa na jeshi la polisi mkoani Arusha.

Akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake kamanda wa polisi, Naibu kamishna wa jeshi la polisi mkoani hapa Liberatus Sabas (pichani)  alisema kuwa mtuhumiwa alikamatwa juzi majira ya asubuhi katika eneo la TRA House jijini hapa.

Kamanda Sabas alisema kuwa alipohojiwa na polisi alikiri kushiriki mauaji hayo na ndipo alipowapeleka kuwaonyesha polisi alipovitupa viungo vya marehemu eneo la mto Misheni  Usa River, wilayani Meru.

Alisema kuwa marehemu ametambuliwa jina kamili Alfred Kimbaa mwenye umri wa miaka18 mkazi wa mianzini jijini Arusha,  huku mtuhumiwa ambaye jina lake limetambuliwa kwa Elijus Lyatuu mkazi wa Dar es Salaam ambaye marehemu alikuwa akiuza duka la kaka yake alietambuliwa kwa jina moja la Lyatuu ambaye pia anaishi jijini Dar es salaam.

Alisema kuwa mtuhumiwa ni mwanafunzi wa mwaka wa tano chuo cha falsafa cha kanisa katoliki Segerea na alipofika Arusha kwa mara ya kwanza aliishi na marehemu chumba kimoja kabla ya mgogoro kuanza na ndipo alipofikia kumuua marehemu na kuiacha maiti yake katika hotel nae kutokomea kusikojulikana hadi alipokamatwa juzi.

Alisema kuwa mtuhumiwa Elijus alimua marehemu kwanza kabla ya kuanza kucharanga viungo ndio maana chumbani alikokutwa marehemu hakukua na damu.

“Tukio hili lisihusishwe na imani za kishirikina kwani inashukiwa kulikuwa na mgogoro kati ya mtuhumiwa na marehemu uliopelekea mtuhumiwa kufanya tukio hilo”alisema Kamanda Sabas.

Upelelezi ukikamilika na taratibu za jeshi la polisi zinaendelea na zikikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

No comments: