Advertisements

Friday, September 4, 2015

SHUKRANI


Jumuiya ya watanzania Washington DC, Maryland na Virginia inapenda kutoa shukrani kwa wanajumuiya wote wa hapa DMV na kutoka sehemu mbalimbali za hapa Marekani, Ubalozi wetu hapa Washington DC, Uongozi wa shirika lisilo la Kiserekali (AWCAA- Taasisi ya Kinamama wa Kiafrika ya Maswala ya Saratani ya hapa Washington DC)  na Timu nzima ya madaktari, wahudumu wa afya wote wakiojumuika nasi kufanikisha kutoa huduma za afya Tanzania. Pia tunapenda kuwashukuru wafadhili wetu; Benki ya Azania, Benki ya CRDB, PSPF, Farida Catering, ofisi ya Diaspora Dar-es-salaam na Zanzibar, Wizara ya Afya Zanzibar na Ofisi ya Rais Zanziba kwa michango yao na ukarimu wao kwa wageni wetu katika muda huo walipokuwa wakitoa huduma hii ya afya. Mungu Ibariki Tanzania yetu. Picha za matukio muhimu zinaweza kupatikana hapo chini. 

Report kamili na Documentary zitafuata siku chache zijazo.

Tunatanguliza shukrani,
Iddi Sandaly
President
Association of Tanzanian Community in Washington DC, Maryland and Virginia









1 comment:

Anonymous said...

Siku hizi DMV inaendeshwa kwa mtandao tu hatukutani tena kuona jinsi tunavyoweza kujikwamua na yake yaliyotushinda hapa nyuma kama dual Citizen. Na tumempata balozi mpya. Je tunatarajia kuendelea kumkaribisha Rais ajaye aendelee kutuona vilevile na haki tuendelee kuikosa? Kwa nini tusiwe na muamko!! Wengine wako kupiga kura.