Advertisements

Wednesday, October 12, 2016

WAKULIMA WADOGO WADOGO WAWASILISHA MADAI YAO KWA WIZARA YA ARDHI NA MAENDELEO YA MAKAZI

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi akizungumza na wakulima wadogowadogo waliofika kuwasilisha madai yao juu ya kumiliki Ardhi sambamba na kupanda mlima Kilimanjaro  zitakazofanyika kuanzia Oktoba 14 hadi 16 mwaka huu ilikiwa ni ishara kuwa mwanamke anaweza kupewa Ardhi na kuimiliki.Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog
Kaimu Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mary Gasper Makondo aliyemuwakilisha Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi akizungumza na wakulima wadogowadogo waliowasilisha  madai yao ya serikari kuhusu umiliki wa Ardhi pamoja na kutolea ufafanuzikuhusu maswala hayo.
Beatrice Sichone ambaye ni Katibu wa Kituo cha Taarifa na Maarifa katika Kata ya Nsara, Mbeya Vijijini akisoma madai yao yanayohusiana na kudai usawa katika umiliki wa Ardhi.
Mwanachama TGNP, Gemma Akalimali akisherehesha wakati ya wanawake wakulima walipokuwa wakiwasilisha madai yao ya serikari kuhusu umiliki wa Ardhi kwa wizara husika kwenye kongamano liliofanyika katika viwanja vya TGNP Mtandao leo
Wakulima wadogowadogo wakiwa wameshika mabango yaliyobeba ujumbe kuhusu umiliki wa Ardhi na usawa katika umilikishwaji walipofika katika viwanja vya TGNP Mtandao leo
Mgeni rasmi aliyemuwakilisha Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP wakiimba kwa pamoja  wakati wa kuwapokea wanawake waliofika wakiwa na mambango mbalimbali yaliyokuwa na ujumbe tofauti tofauti.
Kaimu Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mary Gasper Makondo aliyemuwakilisha Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi akikata utepe kuashiria kupokea madai ya Msingi ya wakulima wadogowadogo waliowasilisha madai yao kwa serikali leo katika uwanja wa TGNP Mtandao
Kaimu Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mary Gasper Makondo aliyemuwakilisha Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi  akionesha madai ya wakulima wadogo wadogo mara baada ya kukabidhiwa.

Mwanachama na mwanzilishi wa Shirika lisilo la kiserikali la TGNP Mtandao, Bi. Zipora Shekilango(kulia) akiwa na  Profesa Marjorie Mbilinyi ambaye ni mwananchama wa TGNP (Kushoto) walipokuwa kwenye kongamano la wakulima wadogowadogo waliokuwa wakiwasilisha madai yao kwa viongozi wa kiserikali.
Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake (WLAC) Theodora Mlelwa akizungumza jambo.
Baadhi ya wakulima wadogowadogo pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya wanawake wakifuatilia kwa makini kinachoendelea
Baadi ya waandishi wa habari wakiwa kazini
Wakulima wadogo wadogo, viongozi na wananchama wa TGNP Mtandao wakicheza wakati wa longamano hilo
Kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani wakati wa kongamano ilo
Kaimu Kamishna wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mary Gasper Makondo aliyemuwakilisha Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi akimkabidhi bendera mmoja wa wakulima wanawake wadogowadogo waliokuwa wanaanza safari ya Kilimanjaro ili kuwapokea wanawake waliopanda Mlima Kilimanjaro na kuhudhuria Kongamano la wanawake wa Afrika litakalojumihisha nchi mbalimbali za Afrika litakalofanyika chini ya Mlima Kilimanjaro.
Wakulima wadogowadogo wakiagwa tayari kwa kuanza safari ya kuelekea mkoani Kilimanjaro
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi  akizungumza na waandishi wa Habari
Meneja Kilimo na Haki ya Ardhi kutoka Action Aids , Elias Mtinda akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari leo katika viwanja wa TGNP Mtandao kuhusu haki ya Mwanamke kumili ardhi

No comments: