Advertisements

Friday, June 23, 2017

WIZARA YA AFYA YAKANUSHA TAARIFA ZA GAZETI LA HABARI LEO KUHUSU TAKWIMU ZA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA


1 comment:

Anonymous said...

Ningependa kusema machache kuhusu Kauli ya Mheshimiwa Rais Magufuli kwamba watoto wapatao mimba wasirudi shuleni. Kwa kauli hii, Rais anaturudisha nyuma miongo kadhaa katika kampeni nyingi za wanaharakati za kuwakomboa watoto wakike na kuondoa umasikini kwenye jamii.
1. Kabla ya kumtwisha mtoto adhabu ya kutokurudi shule, (tukisahau adhabu ya kudumu ya mtoto huyu kupoteza utoto wake, wasiwasi kwa kuwa mzazi katika umri mdogo na mabadiliko ya maisha yake kwa ujumla) kwanza tuangalie sheria inasemaje
2. Kosa kubwa wengi wanalifanya - watu wa media na mablogu wanaongoza kwa hili ni kusema mtoto wa shule wa miaka 13 afanya mapenzi na mwanaume mtu mzima. Hapa hakuna MAPENZI, kisheria hii ni defilement. Huyu binti hana uwezo wa ku consent kufanya mapenzi.
3. Tuanze na tatizo, ni akina nani wanao wabaka watoto? Je ni walimu? Jirani? ndugu? n.k. Hawa ni pedophiles ambao wanatakiwa wawe aidha wamefungwa au wako kwenye register maalumu ili tujue ni kina nani na wapo wapi na wawekwe mbali kabisa na watoto
4. Watoto waelimishwe kuhusu miili yao, ukuaji, madadiliko na kuhamasishwa kutoa taarifa mapema wakiona dalili za haja majitu mazima yanayowamendea watoto. Kama kuna mtu anazagaa zagaa karibu na shule bila mpango wowote, au ni ndugu au jamaa anamfatilia mtoto, mtoto apewe uwezo wa kuripoti aidha kwa mzazi au chombo maalum cha kulinda watoto
5. Child Protection Unit / Centre - Tanzania hatua hiki chombo na tunakihitaji sana. Waatalamu wenye uzoefu wa kuwa hoji watoto (bila kuwanyanyasa) kuwalinda inapotokea mnyanyasaji ni mzazi au mlezi, kuwashauri wanapokuwa wananyanyaswa na waalimu shuleni wakati mzazi hana muda au hajali n.k. Hizi Gender desks sifahamu kweli umuhimu wake, ila kwa jina lenyewe a desk sio mahali pa mtoto mwenye tatizo la kunyanyaswa kujinsia au kubakwa anaweza kuongea kwa uwazi, desk zingine zipo nje adharani kwenye kituo cha polisi. ukisogelea pale kila mtu anaanza kuhisi jambo.
6. Reporting ya haya matukio ya ubakaji wa watoto - waandishe wafunzwe namna ya kuandika ripoti hizi, isiwe mambo ya kishilawadu. Mtoto kabakwa ni tukio kubwa la kuhuzunisha, sio mambo ya umbea - ripoti iwe kamili na ieleze wazi kilicho tokea, sio njemba lakamatwa kwa kula penzi la katoto. Hii ni reporting isiyo na sensitivity ya jambo lenyewe. Repoti iwe kamili na victims (watoto) wasiwekwe adharani kusimulia kwenye mablogu au magazeti ya udaku, hii ni ushahidi na utolewe na wahusika wanaofanya uchunguzi
7. Forensic interviewing of children, huu ni utaalamu muhimu sana wa kuwahoji watoto, ambao sidhani kama tunao wa kutosha. Nimeona baadhi ya kesi ambapo victims ni watoto wadogo (chini ya miaka kumi) nikabaki najiuliza tunakokwenda. Hawa watoto pia wanahitaji counseling (hawa counselors na forensic investigators) wanatakiwa wawe pamoja kwenye Child Protection unit.
8. Tusisahau Tanzania ni signatory wa UN Convention on the rights of the Child and African Charter on Human and Peoples' Rights.
For once think about this, your 13 years old daughter is in a boarding school somewhere in Tanzania, and you learn that an adult male has been abusing her and she is now pregnant. what would you do?