Saturday, April 16, 2022

RAIS MWINYI AFUNGUA KONGAMANO LA PILI LA MADAKTARI NA WAHUDUMU WA AFYA CHUO CHA UTALII MARUHUBI ZANZIBAR.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Pili la Madaktari na Wahudumu wa Afya lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja Jijini Zanzibar, lililoandaliwa na Taasisi ya Jamiyyatul Akhlaqul Islaamia (JAI) na kuwashirikisha Madaktari.Wauguzi,watoa huduma ya Afya na Masheikh.(Picha na Ikulu)
PROFESA Mussa Assad akizungumza na kutoa Mada kuhusiana na Dhima ya Kutoa Huduma Kwa Jamii , wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la Madaktari na Wahudumu wa Afya, lililfanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Zanzibar lililofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi 
WASHIRIKI wa Kongamano la Pili la Madaktari na Wahudumu wa Afya wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Pili la Madaktari na Wahudumu wa Afya lililoandaliwa na Taasisi ya Jamiyyatul Akhlaqul Islaamia ( JAI) lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja Jijini Zanzibar

WAZIRI wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, kulifungua Kongamano la Pili la Madaktari na Wahudumu wa Afya, lililoandaliwa na Taasisi ya Jamiyyatul Akhlaqul Islaamia (JAI) lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Unguja Jijini Zanzibar


No comments:

Post a Comment

bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake