Watalii zaidi ya 40 kutoka Taifa la Mungu wana wa Israel wamerudi Nyumbani, Kutoka Jerusalem hadi Ngorongoro Tanzania kuja kujionea maajabu ya Ulimwengu.
Watalii hao wameshuhudia maajabu (Wonders) ya uumbaji wa Mungu ikiwemo Kasoko ya Ngorongoro, Bonde la Olduvai na kupata taarifa kuhusu eneo la Laetoli lenye Nyayo za Binadamu wa kale.
Watalii hao wakiongozwa na Ellyn Zelikman wamesema kuwa Ngorongoro imekuwa ndoto ya maisha na wameamua kujivinjari eneo hilo ili kujionea maajabu ya Dunia.
Wamesema wamezoea kuona alama za kiroho, Utamaduni wa kisasa wa Mediterania unaozunguka miji mashuhuri na Hifadhi za asili lakini Ngorongoro imewafanya kufungua ukurasa mpya kwa kuona Simba juu ya miti, Faru pembeni mwa ziwa lenye magadi, Tembo, Nyati, Chui, Ngiri, Pundamilia, Nyumbu na wengineo.
Hifadhi ya Ngorongoro kwa takribani miaka mitano (05) iliyopita imepokea zaidi ya watalii 9,367 kutoka nchini Israel ambapo juhudi za kuongeza watalii wengi zaidi zinaendelea.


No comments:
Post a Comment
bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake