ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, September 26, 2012

Membe na Rais Barack Obama na mama Michelle Obama


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Bernard Membe (Mb) akiwa katika picha ya  pamoja na  Rais wa Marekani, Barack Obama  na Mkewe Michelle Obama.  Wakati wa hafla ambayo  Rais  Obama  aliiandaa kwaajili ya  Viongozi  Wakuu wa Nchi na Serikali  ambao wamekusanyika Jijini New York kuhudhuria Mkutano wa 67 wa  Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe  anaongoza ujumbe wa  Tanzania katika Mkutano huu akimuwakilisha Mhe.  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na atauhutubia mkutano  huo kwa niaba ya Rais  siku ya  Ijumaa. Hafla  hiyo imefanyika  katika Hotel ya maarufu ya Waldorf  Astoria jijini  New York

No comments: