ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, July 2, 2026

ZANZIBAR SOAP WAJA NA BIDHAA ZA SABUNI ZA ASILI SABASABA

 


Zanzibar Soap ambao ni wauzaji wa bidhaa za Sabuni za urembo zilizotengenezwa kwa kutumia miti ya asili wemesogeza huduma kwa Wananchi katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea barabara ya Kilwa Temeke Jijini Dar es salaam.

Kwa mujibu wa Meneja mauzo wa Zanzibar Soap, Bw. Mjaka Sogora amesema bidhaa hizo zimetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu huku zikiwa katika aina tofauti kama sabuni za kipande, sabuni za maji, na sabuni za miche.

"Wateja na wadau mbalimbali tunawakaribisha kwenye hema la Serengeti ambalo lipo jirani na hema la NIDA.

Ukifika utaona bango la Zanzibar Soap, lakini pia utaona bidhaa zetu mbalimbali. 

Njoo na pesa kidogo, ujaze kapu, kuna offa ya   pungozo kubwa na  bidhaa zetu wanatumia watu wote, Wanawake kwa Wanaume na watoto pia.



Lakini pia Zanzibar Soap tuna bidhaa tofauti tofauti zenye kutibu, kuponya na kurekebisha yule mwenye;-Chunusi, muwasho mwilini, ngozi iliyofifia na huondoa mabaka baka mwilini, Ewe Mteja Pendezesha mwili wako na ngozi yako kwa kutumia Zanzibar Soap." Amesema Mjaka Sogora.

Baadhi ya sabuni zinazopatikana kwenye banda lao hilo ni pamoja na: Turmeric/Honey Soap, Lemon/Honey Soap, Nuru Soap -Coffee Scrub, Molato, Kojic na Luxury Shea Butter.

Kwa wateja na mawakala,kwa wanaotaka bidhaa hizo za Zanzibar Soap wanaweza wasiliana na Zanzibar Soap waliopo Mtaa wa Tomondo Temeke Pire Dar es salaam, mtandao wa kijamii wa Instagram kwa jina la Zanzibarsoap.









SIGMAGAS & ENGINEERING WASOGEZA HUDUMA SABASABA, WATOA ELIMU JUU YA MABOMBA YA GESI



SIGMA Gas and Engineering inayojihususha na mifumo ya mabomba ya gesi ya hospitali (MGPS) gesi Tiba wapo kwenye maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea barabara ya Kilwa Temeke Jijini Dar es salaam kwa kutoa elimu mbalimbali juu ya matumizi ya gesi katika Sekta ya Afya.


Akizungumza Meneja Mauzo wa Sigma gas & Engineering, Bw.Frank Hyera amesema wamekuwa na utaratibu wa kushiriki maonesho hayo ya Sabasaba ikiwa ni kusogeza huduma kwa Umma kwa kutangaza shughuli wanazofanya.


"Karibu Sabasaba kwenye banda letu, Selous 49/50, tupo hapa kutoa elimu  jinsi mifumo ya mabomba ya gesi inavyofanya kazi na viwango vya usalama vinavyotumika katika tasnia.


Sigma gas and Engineering zaidi tumajishughulisha na masuala ya Vifaa Tiba hususani vya gesi ambapo tunafunga na tumefunga maeneo mbali mbali ikiwemo Hospitali za binafsi na za Serikali lakini pia maeneo maalum yanayohusiana na gesi upande wa matibabu." Amesema Frank Hyera.



Aidha, pia wanafanya 

mifumo ya kuweka mabomba ya gesi ya viwandani, mifumo ya gesi ya maabara, na mifumo ya mabomba ya LPG.


"Sisi pia ni wasambazaji rasmi wa Renner Compressors, Peak Scientific, na British Oxygen Company (BOC) kwa hapa Nchini.

Mifumo ya Mabomba ya Gesi ya Hospitali,

Tunatoa suluhisho za kina kwa ajili ya usanifu, usakinishaji, na matengenezo ya mifumo hiyo, kwa kutumia mifumo ya kisasa tunaweka ilikurahisisha huduma hii ya gesi katika Sekta ya Afya.


Lakini pia tunafunga mifumo ya gesi viwandani, Mifumo ya Mabomba ya Gesi za Maabara, Mifumo ya Mabomba ya LPG hii ni kwa hoteli, shule, na majengo ya makazi.


"Lakini pia tunapatikana Buguruni Malapa, Dar es salaam unaweza kuwasiliana nasi

+255 677 071 127 au

info@sigmagas.co.tz 

Facebook: SigmaGas & Engineering 

Instagram: sigmagas_and_engineering" amemalizia Frank Hyera.


Mwisho.

KATIBU MKUU WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA ATEMBELEA BANDA LA TET MAONESHO YA 50 YA SABASABA



KATIBU Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Mh. Balozi, Waziri Rajabu Salum ametembea banda la Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya biashara ya Dar es salaam (SABASABA) na kujionea shughuli za taasisi hiyo ikiwemo Vitabu mbalimbali.

Balozi Waziri Rajabu Salum pia amepata nafasi ya kusaini kitabu cha wageni.

TET inashiriki maonesho hayo ya Sabasaba sambamba na uuzaji wa Vitabu mbalimbali elimu ikiwemo Vitabu vya kidato Tano na Sita na vingine vingi elimu ya awali, Sekondari 






MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA WAIMARISHA UPATIKANAJI, UDHIBITI WA BEI NA MAPATO YA TAIFA

 


Na Mwandishi Wetu


Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (Petroleum Bulk Procurement Agency - PBPA) umesema mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja umeendelea kuimarisha upatikanaji wa mafuta nchini, kudhibiti mfumuko wa bei, kuhakikisha ubora wa mafuta na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa wa Logistic wa Petroli wa PBPA, Hilda Kowero, alisema taasisi hiyo inatumia maonesho hayo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake na mafanikio yaliyopatikana kupitia mfumo huo.

Alisema jukumu kuu la PBPA ni kuratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja ili kuhakikisha mafuta yanapatikana kwa uhakika katika maeneo yote ya nchi, hatua inayochangia maendeleo ya sekta mbalimbali za uchumi na huduma za kijamii.

Kowero alisema pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta, wakala huo hushirikiana na mamlaka mbalimbali za Serikali kuhakikisha mafuta yote yanayoingia nchini yanakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na mamlaka husika kabla ya kuanza kutumika.

Alieleza kuwa ushirikiano huo unahusisha taasisi kama Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) pamoja na Wakala wa Vipimo, jambo linalowapa wananchi uhakika wa kutumia mafuta yenye ubora na usalama unaokubalika.




Aidha, alisema mfumo huo umeongeza uwazi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa kuwezesha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa na uhakika wa kiwango cha mafuta kinachoingia nchini na hivyo kurahisisha ukusanyaji sahihi wa kodi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Kowero, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja kulikuwa na changamoto ya kuyumba kwa bei za mafuta, lakini kwa sasa mfumo huo umechangia kudhibiti mfumuko wa bei na kuhakikisha wananchi wanapata mafuta kwa bei zinazodhibitiwa kupitia taratibu zilizowekwa na EWURA.

Alisema mfumo huo pia umeendelea kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usambazaji wa mafuta katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, ambapo mafuta yanayoagizwa kupitia bandari za Tanzania husafirishwa kwenda Rwanda, Burundi, Uganda, Zambia, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kowero alibainisha kuwa hali hiyo imeimarisha mahusiano ya kidiplomasia na biashara kati ya Tanzania na nchi jirani huku ikiongeza mchango wa sekta ya nishati katika kukuza uchumi wa taifa.

Aliwataka wananchi kutembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Sabasaba ili kujifunza zaidi kuhusu majukumu ya wakala huo na namna mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja unavyoendelea kuchochea maendeleo ya uchumi wa Tanzania kupitia upatikanaji wa mafuta ya kutosha, salama na yenye ubora.




TET NDIYO MOYO WA ELIMU NCHINI, VITABU VYA KIDATO CHA TANO NA SITA VIPO HAPA SABASABA -DEO FAZAH



Mkuu wa Idara ya Fedha na Uhasibu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Deo Fazah akipokea zawadi alipotembelea banda la TET ndani ya Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya biashara ya Dar es salaam (Sabasaba)2026.


MKUU wa Idara ya Fedha na Uhasibu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Deo Fazah amesema taasisi hiyo ndiyo moyo halisi wa elimu Nchini kwa elimu yetu ya Msingi, elimu ya Sekondari na Ualimu.

Deo Fazah amesema hayo katika Banda la TET ndani ya Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea barabara ya Kilwa, Temeke Jijini Dar es salaam.

Amebainisha:

"Tunapopata nafasi kama hii, tunashiriki ili kuwaambia Watanzania kile tunachofanya, tunapenda kuwakaribisha wadau wote wanaoweza kujitokeza Kufanya kazi na TET katika uandaaji wa Vitabu vya Kiada.

Pia Vitabu vyote vya Kiada vilivyofanyiwa maboresho tunavyo hapa na maeneo yote.

Taasisi ipo na maduka yake Kikanda, ikiwemo pale Ofisi TET Bamaga, lakini pia Kariakoo na kwa mawakala wengine wote.

Pia tupo Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa, Nyanda za juu Kusini kote huko vitabu vyote vipo na vinauzwa kwa bei elekezi kwa bei ileile ambayo kitabu kinachouzwa Dar es salaam na Kigoma ama Mbeya kitauzwa kwa bei ileile," Amesema Deo Fazah.

Aidha, amewakaribisha wadau wanaotaka kufanya masuala ya Utafiti katika elimu milango ipo wazi katika mashirikiano na TET katika kuendeleza elimu nchini.

Wazazi, walezi, Wanafunzi na wadau karibuni sana Vitabu vya kidato cha Tano na Sita pia vipo hapa na wote wanaweza kutembelea hapa Sabasaba lakini pia katika ofisi zetu za makao makuu ya TET 








Wednesday, July 1, 2026

ETHIOPIA IMEFANIKIWA KUINGIZA MBUNGE WA PILI MWENYE ASILI YA ETHIOPIA KATIKA BUNGE LA MAREKANI (U.S. CONGRESS).

MOHAMED MATOPE, Washington, DC

Jana, Melat Kiros, mwanamke mwenye umri wa miaka 29, aliandika historia baada ya kumshinda mbunge aliyekuwa madarakani kwa takribani miaka 30 katika uchaguzi wa mchujo (Democratic Primary) uliofanyika Denver, Colorado. Ushindi huo umeonekana kuwa moja ya matokeo makubwa zaidi ya kisiasa mwaka 2026.

Kwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ya wapiga kura katika jimbo hilo huunga mkono Chama cha Democratic, Kiros anapewa nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi mkuu mwezi Novemba na kuwa Mbunge wa pili aliyezaliwa Ethiopia kuhudumu katika Bunge la Marekani.

Melat Kiros, a corporate attorney, alizaliwa Addis Ababa, Ethiopia, na alihamia Marekani akiwa mtoto mchanga baada ya familia yake kupata nafasi kupitia mpango wa Diversity Visa Lottery. Alikulia katika jimbo la Colorado, ambako alifanya vizuri katika masomo na baadaye akapata shahada ya Political Science na Economics. Baadaye alihitimu shahada ya sheria (Juris Doctor,J.D.), na kwa sasa ni mwanafunzi wa Ph.D. katika Public Policy katika University of Colorado Denver.

Mafanikio yake pia yanaonyesha umuhimu wa nchi za Afrika kuwatambua Diaspora, kuwapa haki za kiraia na nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa lao. Diaspora ni rasilimali muhimu yenye mtandao mpana wa ushawishi, utaalamu na fursa zinazoweza kutumika kuitangaza na kuitetea nchi kimataifa.

Waswahili husema, Usipokuwa mezani, utaishia kwenye menyu. Kwa sasa, Ethiopia ina watu wawili waliozaliwa nchini humo na kwa kuwa nchi yao inaruhusu uwepo wa uraia pacha, ni raia wa nchi hio, walioshikilia na wanatarajiwa kushikilia viti katika Bunge la Marekani. Hiyo ina maana ya kwamba, kuna sauti za Ethiopians kwenye meza kubwa kupita zote duniani, mahali ambapo maamuzi muhimu kuhusu sera za Marekani na uhusiano wake na mataifa mengine hufanyika. Ingawa wabunge hao wanawakilisha wananchi wa majimbo yao na maslahi ya Marekani, uelewa wao wa historia, utamaduni na changamoto za Ethiopia unaweza kuchangia kujenga daraja la maelewano na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Mafanikio ya Melat Kiros ni fahari kwa Ethiopians na Africans na diaspora wote wanaoamini kuwa ndoto zinaweza kutimia kupitia elimu, kazi ngumu na huduma kwa jamii. Pia ni ukumbusho kwamba kuwekeza katika watu wako, hata wanapoishi nje ya nchi, kunaweza kuzaa viongozi wenye ushawishi mkubwa katika jukwaa la kimataifa.


 

Tuesday, June 30, 2026

HII HAPA RATIBA YA MADAKTARI BINGWA NA BOBEZI ZAMU YA JULAI MOSI, 2026 MOI



Ratiba ya  Madaktari bingwa na bobezi watakaokuwa zamu siku ya Jumatano Julai Mosi 2026, kwa Team husika wakitoa huduma ya matibabu ya mifupa ( Team A, Team T , P/OT) uti wa mgongo, ubongo na mishipa ya fahamu (GNS, ENDOSCOPIC, PNS).

Pia daktari mtaalam wa "usingizi na ganzi", moyo, kisukari (PHYSICIAN) n.k watakuwepo.

Karibu  upate huduma.



Monday, June 29, 2026

SAHARA CONSULT AND TIE SIGN MoU TO ADVANCE EDUCATION INNOVATION AND DIGITAL TRANSFORMATION

 


Dar es Salaam, Tanzania – 29 June 2026 – 

SAHARA Consult Company Limited and the Tanzania Institute of Education (TIE) have today signed a Memorandum of Understanding (MoU) to establish a strategic partnership aimed at accelerating the adoption, integration, and scaling of Education Technology (EdTech) solutions within Tanzania's basic education system. The partnership is designed to strengthen digital transformation in education while ensuring that innovation is aligned with national curriculum standards and education priorities. 

The collaboration aligns with the aspirations of Tanzania Development Vision 2050, which recognises education, innovation, digital transformation, and human capital development as key enablers of a competitive and knowledge-based economy. By supporting the integration of technology into teaching and learning and creating structured pathways for the adoption of locally developed EdTech solutions, the partnership will contribute to building an education system that equips learners with the skills required for the future.

The five-year partnership brings together TIE's mandate in curriculum development and educational quality assurance with Sahara Consult's expertise in innovation, entrepreneurship, digital transformation, and EdTech ecosystem development. Through this collaboration, the two institutions will work together to develop national EdTech Adoption Guidelines, strengthen curriculum ICT integration, enhance teacher capacity, facilitate collaboration between curriculum developers and EdTech innovators, and establish an EdTech Testbed (Sandbox) for the piloting and evaluation of digital learning solutions. The partnership will also promote joint research, knowledge sharing, monitoring, evaluation, and evidence generation to support informed policy development and effective programme implementation. 

Speaking at the signing ceremony, Dr. Aneth Komba, Director General of TIE, said: “This partnership comes at a timely moment as TIE continues to implement the improved curriculum, which places strong emphasis on the integration of ICT and other technologies in teaching and learning. We believe the implementation of this agreement will strengthen the objectives of the curriculum reforms, particularly the goal of preparing learners with 21st-century skills, including the effective use of education technologies.”

Mr Jumanne Rajabu Mtambalike, Chief Executive Officer of Sahara Consult, said:“Sahara Consult is honoured to partner with the Tanzania Institute of Education in advancing a shared vision for a more innovative, inclusive, and future-ready education system. This collaboration represents an important step in strengthening the connection between curriculum development, technology, research, and practical innovation.

As Tanzania continues to embrace digital transformation in education, we believe that meaningful progress will come from strong partnerships between public institutions, private sector actors, academia, development partners, and innovators. Through this partnership, Sahara Consult will bring its experience in innovation, impact consulting, ecosystem building, and EdTech acceleration to support practical solutions that improve teaching, learning, and education outcomes.

Together with TIE, we are committed to creating pathways for evidence-based innovation, supporting the integration of relevant education technologies, and contributing to transformative change that prepares learners, teachers, and institutions for the future.”

The partnership between the Tanzania Institute of Education and Sahara Consult marks a significant step toward strengthening Tanzania’s education innovation ecosystem. By bringing together curriculum expertise, technology, research, entrepreneurship, and practical implementation support, the collaboration will help create a stronger bridge between education policy, classroom needs, and locally developed EdTech solutions. Both institutions reaffirm their commitment to advancing inclusive, relevant, and future-ready learning that empowers teachers, supports learners, and contributes to Tanzania’s broader digital transformation and human capital development agenda.

About Tanzania Institute of Education (TIE)


The Tanzania Institute of Education (TIE) is a national institution mandated to support curriculum development and educational materials in Tanzania. Through its work, TIE contributes to the improvement of teaching, learning, and education quality across the country.


About Sahara Consult


Sahara Consult is a comprehensive management consulting firm that collaborates closely with industry experts to deliver solutions that leverage innovation and digital entrepreneurship. The company works with partners across the public sector, private sector, academia, and development community to drive transformative change through impact, technology, and innovation consulting.



Sunday, June 28, 2026

TIMU SABA KUCHUANA RESI ZA NGALAWA ZIFF2026



Ngalawa saba zitachuana vikali katika mbio za kasi na ufundi zinazotarajiwa kufanyika kwenye Ufukwe wa Serena. 

Mbio hizo za ngalawa zinabeba msisimko mkubwa wa kuhitimisha Tamasha la 29 la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF) kwa mwaka huu wa 2026. 

Mtendaji Mkuu wa ZIFF, Joseph Mwale, amethibitisha kuwa ushindani huo utazikutanisha ngalawa zenye majina makubwa ikiwemo Azam Media, UNICEF, UN WOMEN, Fish Market, BATISTA, WIOMSA, na COMNET, ambapo mabaharia watachuana kuanzia ufukweni hapo, kuzunguka baharini na kurejea nchi kavu huku washindi wakiondoka na zawadi nono za fedha taslimu.

Kihistoria na kitamaduni, mbio za ngalawa zimekuwa kielelezo kikuu cha maisha, ukakamavu na urithi wa Waswahili wa mwambao ambao wametumia vyombo hivi kwa karne nyingi katika uvuvi na usafiri. 

Kuingizwa kwa mashindano haya kama kilele cha tamasha kupitia jukwaa la Wanawake na Vijijini (Women Panorama) kunalenga kuhuisha mchezo huu wa asili na kuupa sura ya kisasa inayovutia watalii na wenyeji. 

Tukio hili la kasi na ufundi majini halimalizi tu tamasha kwa burudani, bali linaweka msisitizo mkubwa katika agenda ya mashindano yenyewe kama nguzo inayounganisha jamii, huku ufukwe wa Serena ukigeuka kuwa uwanja wa mayowe, shangwe na ushindani wa kweli wa baharini.





WANAWAKE 30 VINARA WATUNUKIWA TUZO ZA MALKIA WA ARUSHA 2026



Tuzo za Malkia wa Arusha 2026 zimewakutanisha wanawake zaidi ya 300 kutoka sekta mbalimbali nchini kwa lengo la kutambua na kuenzi mchango wao katika maendeleo ya jamii na uchumi. Katika hafla hiyo, wanawake 30 vinara walitunukiwa tuzo kwa umahiri wao katika sekta mbalimbali ikiwemo Ujasiriamali, Biashara, Kilimo, Utalii, Afya, Elimu, Teknolojia, Maendeleo ya jamii, Sanaa na Utamaduni. Hafla hiyo ilifanyika tarehe 27 Juni 2026 katika Hoteli ya Gran Meliá Arusha.

Akimwakilisha Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), Mgeni Rasmi ambaye ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Witness Shoo, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Arusha, aliwapongeza wanawake wote walioshiriki na waliotambuliwa kwa mchango wao katika jamii.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni Rasmi alisema ongezeko la watalii nchini linafungua fursa nyingi za kiuchumi kwa watanzania hususan wanawake na kuwataka kujipanga kunufaika na matukio makubwa yanayotarajiwa kufanyika nchini, ikiwemo Mkutano wa 153 wa Umoja wa Mabunge Duniani (Inter-Parliamentary Union - IPU)2026, World Travel Awards Grand Finale 2026 na AFCON 2027, kwa kujiandaa kutoa huduma zenye viwango vya kimataifa ili kuongeza mapato na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Vilevile, aliwahimiza wanawake kuendelea kudumisha nidhamu, uadilifu, ushirikiano na kujituma, akieleza kuwa misingi hiyo ndiyo nguzo ya kujenga viongozi bora, jamii yenye maadili na uchumi imara.

Kupitia jukwaa hilo, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) liliendelea kuhamasisha Utalii wa ndani pamoja na kutangaza fursa mbalimbali za Utalii na uwekezaji zinazopatikana ndani ya Hifadhi za Taifa Tanzania.
















#MalkiaWaArusha #TuzoZaWanawake #TanzaniaParks #ATM2030 #UtaliiNiMaisha #DestinationTanzania