Na. Matukio Daima Media App, Kishapu, Shinyanga.
MBIO za Baiskeli za Busiya ziemefanyika Julai 4, 2026 kwa mara ya kwanza katika shamrashamra za kukaribisha tamasha la Sanjo ya Busiya maarufu kama Sabasaba (7'7).
Uongozi wa Utemi huo umefanya kwa mara ya kwanza Mbio hizo za Baiskeli kwa lengo la kurejesha utamaduni wa Baiskeli kwa kabila la Wasukuma.
mashindano ya mbio hizo yalianzia eneo la njia panda la Kolandoto hadi Ikulu ya Busiya na washiriki walipokelewa na Mtemi wa Busiya Ntemi Makwaia wa iii pamoja na Machifu wengine kutoka meeneo mbalimbali.
Awali, Ntemi Makwaia iii akizindua mbio hizo, amebainisha kuwa, utamaduni wa Wasukuma ni pamoja na kuendesha Baiskeli hali ambayo inawapa kuwa na Afya njema kwani utaratibu huo ni Moja ya mazoezi ya mwili na kuweka mwili vyema bila magonjwa.
Tamasha la Sanjo ya Busiya ambalo litazinduliwa rasmi Julai 05 na hitimisho ni Julai 07 ambapo ngoma mbalimbali kutoka Busiya na nchi jirani zitashiriki sambamba na matukio mengine ikiwemo huduma za afya, ambapo Wananchi watapata nafasi ya kupimwa Afya zao kutoka kwa Watalaam na Madaktari wa Afya Check, pamoja na Hospitali ya jirani.

















































