ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, July 7, 2026

DIB YALETA UNAFUU KWA MABENKI

  

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano ya Umma wa DIB, Lwaga Mwambande pichani.


Na Hellen Ngoromera


BODI ya Bima ya Amana nchini (DIB) imeanzisha utaratibu mpya wa kuzipunguzia hasara benki zinazoingia kwenye migogoro au changamoto za kiuendeshaji.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano ya Umma wa bosi hiyo Lwaga Mwambande amesema hayo Julai 6 Jijini Dar es Salaam katika Maonyesho ya Jubilei ya dhahabu ya miaka 50 ya Sabasaba yanayoendelea katila viwanja vya  Sabasaba.

Amesema badala ya kusubiri mpaka benki ife ndipo bodi yake ilipe fidia wameona ianzishe utaratibu huo ambao ni mzuri na wenye manufaa makubwa.

"Badala ya kusubiri mpaka benki ife ndipo tulipe fidia sasa tuna jukumu la kupunguza hasara kwa benki zinazopita changamoto hizo," amesema Lwaga.

Ameeleza kwamba utaratibu huo umeanza katika mwaka mpya wa fedha ulioanza Julai na kwamba Benki Kuu ya Tanzania(BoT) ndiyo yenye jukumu la kushughulikia jambo hilo. Hata hivyo ameweka wazi kwamba hadi sasa hakuna benki iliyofikia katika hali hiyo.

"Mpango huo ni mzuri na wenye manufaa kwani ni nafuu kuliko kulipia fidia. "Wataalamu wanasema kupunguza hasara wakati mwingine ni nafuu kuliko kulipa fidia, unaweza kukuta benki inahitaji Shs.mlioni 500 ili irejee kwenye utendeji wa kawaida na mkiiacha ikafa mnaweka mkakuta fidia inakuwa hadi milioni 2," amesema Lwaga.

Amebainisha kuwa katika vitu ambavyo bodi hiyo inajitahidi  ni kuwa mwangalifu katika mfuko wa amana. 

Bodi ya amana imeanzishwa kwa lengo la kukinga amana za wananchi katika benki na taasisi za kifedha na inapotokea benki ambazo wananchi hao wanaweka fedha zao zinafilisika amana zao zingawiwa  kikamilifu.

Monday, July 6, 2026

TAMASHA LA SANJO YA BUSIYA 2026 LAZINDULIWA RASMI, WATANZANIA WAHIMIZWA UPENDO NA AMANI

 


Na. Matukio Daima Media App, Kishapu, Shinyanga.


MTEMI wa Busiya Ntemi Makwaia wa iii amezindua rasmi tamasha la Sanjo ya Busiya  maarufu kama  Sabasaba (7-7) huku Wananchi wakihimizwa upendo na Amani.

Uzinduzi huo umefanyika jioni ya Julai 5,2026  umefanyika katika eneo la Ikulu ya Busiya  na Mtemi wa Busiya Ntemi Makwaia wa iii pamoja na Machifu wengine kutoka meeneo mbalimbali ikiwemo: Kilimanjaro, Morogoro, Dodoma, Tabora, Mara, Mwanza, Ruvuma, Mkoa mwenyeji wa Shinyanga na Taifa la  Afrika Kusini, ambao kwa pamoja walipata pia kutoa neno la Shukrani.

Awali, Ntemi Makwaia iii alishuhudia matukio mbalimbali ya tamasha hilo ikiwemo ngoma za asili kutoka Jamii ya Wasukuma.



Mtemi wa Busiya Ntemi Makwaia wa iii  akivikwa mavazi maalum ya kiutawala


Aidha, amewatakia Wananchi kuendelea kupendana na kudumisha amani sambamba na kuendeleza utamaduni.

Tamasha hilo limekuwa likikusanya umati mkubwa kutoka ndani na nje ya Nchi wakifika kwa wingi kushuhudia matukio ya Ngoma za asili na kila za Jamii ya Wasukuma kutoka Busiya na maeneo jirani.

Ambapo pia Wananchi wanapata fursa za  huduma za afya ikiwemo kupimwa Afya zao bure kutoka kwa Watalaam na Madaktari wa Afya Check, pamoja na Hospitali ya jirani.

Tamasha hilo linatarajiwa kufika kilele chake Julai 7, 2026 ambapo shughuli za Ngoma , vyakula vya asili na manunuzi ya bidhaa mbalimbali zinaendelea kunogesha tamasha hilo kila mwaka tokea kuanzishwa kwake miaka 16 iliyopita.



















Sunday, July 5, 2026

DKT. ART ULENE KUSHEREHEKEA MIAKA 90 JUU YA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO

 


Na. Calvin Katera - Kilimanjaro


Dkt. Art Ulene, Daktari mstaafu kutoka  nchini Marekani na aliyewahi kuwa mwandishi wa masuala ya afya wa kituo cha televisheni cha NBC, ameanza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro kuvunja rekodi ya kuwa mtu wa kwanza mwenye umri wa miaka 90 kukwea hadi katika kilele cha Uhuru chenye mita 5895 kutoka usawa wa bahari. 

Kwa sasa rekodi hiyo inashikiliwa na raia wa Marekani anayeitwa Anne Lorimor, aliyepanda Mlima Kilimanjaro akiwa na umri wa miaka 89 na siku 37, akipandia lango hilo hilo la Rongai Julai 18, 2019 na kufanikiwa kufika katika kilele hicho ambacho kinavutia kwa macho kutokana na uwepo wa mrundikao wa barafu.

Safari  hiyo ya Dkt.  Ulene ya kuvunja rekodi ya Bi. Lorimor ilianza Julai 03, 2026 katika Lango la Rongai iyotarqjiwa kuchukua siku 10 ameilekeza katika kumbukizi yake ya kuzaliwa inayosherehekewa kila ifiapo Julai 13, siku anayoitarajia imkute akiwa katika kilele kirefu kuzidi vyote barani Afrika, huku akitimiza ndoto yake kuvunja rekodi hiyo iliyodumu kwa takribani miaka saba. 

Akizungumza kabla ya kuanza safari hiyo, Dkt. Ulene alisema wazo la kurejea Kilimanjaro lilianza kama mzaha kati yake na marafiki, lakini baadaye likageuka kuwa safari yenye maana kubwa ya kujipima uwezo na kuhamasisha watu kutokukata tamaa kutokana na umri.

Alisema baada ya kuupanda Mlima Kilimanjaro mara tatu zilizopita, ameendelea kuvutiwa na uzuri wa mlima huo pamoja na ukarimu wa Watanzania. Kwa mujibu wake, Mlima Kilimanjaro ni mfano wa maisha yenye changamoto na mafanikio, huku akisisitiza kuwa safari hiyo si ya kuvunja rekodi pekee bali ni ya kujitambua na kuthibitisha uwezo wa binadamu.

Dkt. Ulene alisema umri unaweza kufanya mambo kuwa magumu zaidi, lakini haupaswi kuwa kikwazo cha kutimiza ndoto. Amehimiza watu kuendelea kufuata malengo yao, akieleza kuwa kila mmoja ana "mlima wake” wa kupanda katika maisha.

Aliongeza kuwa akifanikiwa kufika katika Kilele cha Uhuru, atasherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 90 pamoja na timu yake kwa keki na nyimbo za kumbukumbu. Hata hivyo, amekiri kuwa bado anaiheshimu changamoto ya Mlima Kilimanjaro, hususan baridi na upepo mkali unapofikia zaidi ya mita 3700 kutoka usawa wa bahari.

Kwa upande wake, Afisa Uhifadhi Daraja la Kwanza, Hifadhi ya Taifa  Kilimanjaro, Hilda Mikongoti, alisema kuwa safari hiyo ni fursa muhimu ya kuitangaza Tanzania na Mlima Kilimanjaro duniani sanjari na kurejea kwa Dkt. Ulene kwa mara ya nne ni uthibitisho wa ubora wa huduma zinazotolewa na hifadhi hiyo.

Muhifadhi Mikongoti aliongeza, “KINAPA imefanya maandalizi ya kutosha kwa kushirikiana na Kampuni ya World Wild Travel Tanzania inayompandisha Dkt. Ulene, ikiwemo kuongeza muda wa safari hadi siku 10 ili kumpa nafasi ya kuzoea mabadiliko ya mwinuko na kuhakikisha anafika kileleni.”

Aidha, alisisitiza kuwa Mlima Kilimanjaro unaweza kupandwa na mtu yeyote mwenye maandalizi sahihi, akibainisha kuwa hata wenzetu wenye mahitaji maalumu wamewahi kufika kileleni kutokana na kuboreshwa kwa miundombinu na huduma ndani ya hifadhi.

Naye Mkurugenzi wa World Wild Travel Tanzania, Raymond Maasai, alisema maandalizi ya safari hiyo yalianza mwaka jana, huku ratiba maalumu ikiandaliwa ili kumpa Dkt. Ulene muda wa kutosha wa kupanda taratibu, kupumzika mara kwa mara na kutumia vifaa maalumu vinavyoongeza faraja wakati wote wa safari.

Wadau wa utalii wanaamini kuwa mafanikio ya Dkt. Ulene yataongeza umaarufu wa Mlima Kilimanjaro katika soko la utalii duniani na kuimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha utalii wa milima, huku yakibeba ujumbe kwamba ndoto hazina umri na zinaweza kutimizwa kwa maandalizi sahihi, dhamira na ujasiri.










MBIO ZA BAISKELI ZAKARIBISHA TAMASHA LA SANJO YA BUSIYA 2026

 


Na. Matukio Daima Media App, Kishapu, Shinyanga.


MBIO za Baiskeli za Busiya ziemefanyika Julai 4, 2026  kwa mara ya kwanza katika shamrashamra za kukaribisha tamasha la Sanjo ya Busiya  maarufu kama  Sabasaba (7'7).

Uongozi wa Utemi huo umefanya kwa mara ya kwanza Mbio hizo za Baiskeli kwa lengo la kurejesha utamaduni wa Baiskeli kwa kabila la Wasukuma.

mashindano ya mbio hizo yalianzia eneo la njia panda la Kolandoto hadi  Ikulu ya Busiya  na washiriki walipokelewa na Mtemi wa Busiya Ntemi Makwaia wa iii pamoja na Machifu wengine kutoka meeneo mbalimbali.

Awali, Ntemi Makwaia iii akizindua mbio hizo, amebainisha kuwa, utamaduni wa Wasukuma ni pamoja na kuendesha Baiskeli hali ambayo inawapa kuwa na Afya njema kwani utaratibu huo ni Moja ya mazoezi ya mwili na kuweka mwili vyema bila magonjwa.

Tamasha la Sanjo ya Busiya ambalo litazinduliwa rasmi Julai 05 na  hitimisho ni Julai 07 ambapo ngoma mbalimbali kutoka Busiya na nchi jirani zitashiriki sambamba na matukio mengine ikiwemo huduma za afya, ambapo Wananchi watapata nafasi ya kupimwa Afya zao kutoka kwa Watalaam na Madaktari wa Afya Check, pamoja na Hospitali ya jirani.

















Saturday, July 4, 2026

CAPE VERDE LOST THE MATCH TO ARGENTINA, BUT WON THE HEARTS OF THE FOOTBALL WORLD

WAZIRI MKUU MSTAAFU, MHE.KASSIM MAJALIWA ASHIRIKI MBIO ZA MAC D MARATHON2026, APIGA KURA TUZO ZA WTA

 

Mgeni Rasmi katika Mbio za Riadha za MAC D Marathon ambaye pia ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa akipewa maelezo ya jinsi ya kupigia kura wa vivutio vya Tanzania katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kutoka kwa Afisa Utalii Lusajo Nsweve wa TAWA, Julai 4,2026, Kunduchi, Jijini Dar es Salaam.

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa ameshiriki katika Mbio za Riadha za MAC D Marathon zilizofanyika Julai 4, 2026 Kunduchi, Dar es salaam.

Mhe. Majaliwa alikuwa mgeni rasmi katika Mbio hizo zenye lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupitia zenye kaulimbiu ya "Go Green with Gas" na kuunga mkono juhudi za Serikali katika utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi.

Ambapo alipata fursa kuelekezwa jinsi ya kupigia kura vivutio vya Tanzania katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kutoka kwa Afisa Utalii Lusajo Nsweve wa Mamlaka ya usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

Pia viongozi wengine mbalimbali wameweza kushiriki zoezi hilo,

TAWA imetumia jukwaa hilo kutangaza vivutio vya utalii inavyovisimamia pamoja na kuhamasisha zoezi la upigaji kura wa tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kwa Viongozi wa Serikali na washiriki mbalimbali.