ANGALIA LIVE NEWS

Saturday, July 4, 2026

WAZIRI MKUU MSTAAFU, MHE.KASSIM MAJALIWA ASHIRIKI MBIO ZA MAC D MARATHON2026, APIGA KURA TUZO ZA WTA

 

Mgeni Rasmi katika Mbio za Riadha za MAC D Marathon ambaye pia ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa akipewa maelezo ya jinsi ya kupigia kura wa vivutio vya Tanzania katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kutoka kwa Afisa Utalii Lusajo Nsweve wa TAWA, Julai 4,2026, Kunduchi, Jijini Dar es Salaam.

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa ameshiriki katika Mbio za Riadha za MAC D Marathon zilizofanyika Julai 4, 2026 Kunduchi, Dar es salaam.

Mhe. Majaliwa alikuwa mgeni rasmi katika Mbio hizo zenye lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupitia zenye kaulimbiu ya "Go Green with Gas" na kuunga mkono juhudi za Serikali katika utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi.

Ambapo alipata fursa kuelekezwa jinsi ya kupigia kura vivutio vya Tanzania katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kutoka kwa Afisa Utalii Lusajo Nsweve wa Mamlaka ya usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

Pia viongozi wengine mbalimbali wameweza kushiriki zoezi hilo,

TAWA imetumia jukwaa hilo kutangaza vivutio vya utalii inavyovisimamia pamoja na kuhamasisha zoezi la upigaji kura wa tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kwa Viongozi wa Serikali na washiriki mbalimbali.







MCHECHU: HAKUNA UCHUMI BILA UHIFADHI


Na. Edmund Salaho/Ruaha 


Msajili wa Hazina ambaye pia ni mlezi wa Great Ruaha Marathon na mwakilishi wa Mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba katika mbio hizo Bw. Nehemiah Mchechu amebainisha kuwa uchumi wa Taifa unategemea uhifadhi huku akiongeza kuwa Mto Ruaha Mkuu ni moja ya mito muhimu zaidi nchini unaotoa uhai kwa Hifadhi ya Taifa Ruaha, unaosaidia wananchi katika shughuli za kilimo na mifugo, ikiwa ni pamoja na kuwewezesha uzalishaji wa umeme na kuchangia ustawi wa wananchi nchini.

Mchechu, ameyasema hayo leo Julai 04, 2026 wakati akizindua mbio za kimataifa zinazofanyika katika Hifadhi ya Taifa Ruaha maarufu kama "Great Ruaha Marathon".

Aidha, Mchechu ametoa rai kwa Watanzania kujijengea tabia ya kutembelea Hifadhi za Taifa, kujivunia utanzania na kuwa mabalozi wa nchi yao.

"Tunataka Watanzania wengi zaidi watembelee hifadhi zetu, wajivunie urithi tulionao na wawe mabalozi wa utalii wa nchi yao” alieleza Mchechu.





Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, Massana Gibril Mwishawa amebainisha kuwa utalii wa michezo umekuwa kivutio kikubwa kwa watalii wa ndani na nje na kuelezea kuwa TANAPA imeweka mikakati madhubuti katika zao hilo jipya la utalii.

"Duniani kote, matukio makubwa ya michezo hutumiwa kuongeza idadi ya watalii, kuvutia wawekezaji, kukuza biashara na kuijenga taswira ya nchi kimataifa, TANAPA tumejidhatiti vilivyo kuhakikisha tunavutia watalii wengi kupitia zao hili la utalii wa michezo"

Mratibu wa Great Ruaha Marathon Bw. Hamim Kilahama amesema  "Great Ruaha Marathon si mashindano ya riadha pekee. Ni jukwaa la kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa kulinda mazingira, kuhifadhi vyanzo vya maji vya Mto Ruaha Mkuu, kuendeleza utalii wa Kusini mwa Tanzania. Tunatumia michezo kama chombo cha kuleta mabadiliko chanya katika jamii, ikiwa ni mara ya tano mfululizo Great Ruaha Marathon imefungua ukurasa mpya wakuitangaza Ruaha kupitia utalii wa michezo".

Hifadhi ya Taifa Ruaha ni moja kati ya Hifadhi kubwa barani Afrika. Ni hazina ya kipekee yenye idadi kubwa ya wanyama kama tembo, simba, chui, mbwa mwitu wa porini, twiga, nyati na mamia ya aina za ndege wanaovutia watalii kutoka kila pembe ya dunia.




















Thursday, July 2, 2026

ZANZIBAR SOAP WAJA NA BIDHAA ZA SABUNI ZA ASILI SABASABA

 


Zanzibar Soap ambao ni wauzaji wa bidhaa za Sabuni za urembo zilizotengenezwa kwa kutumia miti ya asili wemesogeza huduma kwa Wananchi katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea barabara ya Kilwa Temeke Jijini Dar es salaam.

Kwa mujibu wa Meneja mauzo wa Zanzibar Soap, Bw. Mjaka Sogora amesema bidhaa hizo zimetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu huku zikiwa katika aina tofauti kama sabuni za kipande, sabuni za maji, na sabuni za miche.

"Wateja na wadau mbalimbali tunawakaribisha kwenye hema la Serengeti ambalo lipo jirani na hema la NIDA.

Ukifika utaona bango la Zanzibar Soap, lakini pia utaona bidhaa zetu mbalimbali. 

Njoo na pesa kidogo, ujaze kapu, kuna offa ya   pungozo kubwa na  bidhaa zetu wanatumia watu wote, Wanawake kwa Wanaume na watoto pia.



Lakini pia Zanzibar Soap tuna bidhaa tofauti tofauti zenye kutibu, kuponya na kurekebisha yule mwenye;-Chunusi, muwasho mwilini, ngozi iliyofifia na huondoa mabaka baka mwilini, Ewe Mteja Pendezesha mwili wako na ngozi yako kwa kutumia Zanzibar Soap." Amesema Mjaka Sogora.

Baadhi ya sabuni zinazopatikana kwenye banda lao hilo ni pamoja na: Turmeric/Honey Soap, Lemon/Honey Soap, Nuru Soap -Coffee Scrub, Molato, Kojic na Luxury Shea Butter.

Kwa wateja na mawakala,kwa wanaotaka bidhaa hizo za Zanzibar Soap wanaweza wasiliana na Zanzibar Soap waliopo Mtaa wa Tomondo Temeke Pire Dar es salaam, mtandao wa kijamii wa Instagram kwa jina la Zanzibarsoap.









SIGMAGAS & ENGINEERING WASOGEZA HUDUMA SABASABA, WATOA ELIMU JUU YA MABOMBA YA GESI



SIGMA Gas and Engineering inayojihususha na mifumo ya mabomba ya gesi ya hospitali (MGPS) gesi Tiba wapo kwenye maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea barabara ya Kilwa Temeke Jijini Dar es salaam kwa kutoa elimu mbalimbali juu ya matumizi ya gesi katika Sekta ya Afya.


Akizungumza Meneja Mauzo wa Sigma gas & Engineering, Bw.Frank Hyera amesema wamekuwa na utaratibu wa kushiriki maonesho hayo ya Sabasaba ikiwa ni kusogeza huduma kwa Umma kwa kutangaza shughuli wanazofanya.


"Karibu Sabasaba kwenye banda letu, Selous 49/50, tupo hapa kutoa elimu  jinsi mifumo ya mabomba ya gesi inavyofanya kazi na viwango vya usalama vinavyotumika katika tasnia.


Sigma gas and Engineering zaidi tumajishughulisha na masuala ya Vifaa Tiba hususani vya gesi ambapo tunafunga na tumefunga maeneo mbali mbali ikiwemo Hospitali za binafsi na za Serikali lakini pia maeneo maalum yanayohusiana na gesi upande wa matibabu." Amesema Frank Hyera.



Aidha, pia wanafanya 

mifumo ya kuweka mabomba ya gesi ya viwandani, mifumo ya gesi ya maabara, na mifumo ya mabomba ya LPG.


"Sisi pia ni wasambazaji rasmi wa Renner Compressors, Peak Scientific, na British Oxygen Company (BOC) kwa hapa Nchini.

Mifumo ya Mabomba ya Gesi ya Hospitali,

Tunatoa suluhisho za kina kwa ajili ya usanifu, usakinishaji, na matengenezo ya mifumo hiyo, kwa kutumia mifumo ya kisasa tunaweka ilikurahisisha huduma hii ya gesi katika Sekta ya Afya.


Lakini pia tunafunga mifumo ya gesi viwandani, Mifumo ya Mabomba ya Gesi za Maabara, Mifumo ya Mabomba ya LPG hii ni kwa hoteli, shule, na majengo ya makazi.


"Lakini pia tunapatikana Buguruni Malapa, Dar es salaam unaweza kuwasiliana nasi

+255 677 071 127 au

info@sigmagas.co.tz 

Facebook: SigmaGas & Engineering 

Instagram: sigmagas_and_engineering" amemalizia Frank Hyera.


Mwisho.

KATIBU MKUU WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA ATEMBELEA BANDA LA TET MAONESHO YA 50 YA SABASABA



KATIBU Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Mh. Balozi, Waziri Rajabu Salum ametembea banda la Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya biashara ya Dar es salaam (SABASABA) na kujionea shughuli za taasisi hiyo ikiwemo Vitabu mbalimbali.

Balozi Waziri Rajabu Salum pia amepata nafasi ya kusaini kitabu cha wageni.

TET inashiriki maonesho hayo ya Sabasaba sambamba na uuzaji wa Vitabu mbalimbali elimu ikiwemo Vitabu vya kidato Tano na Sita na vingine vingi elimu ya awali, Sekondari 






MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA WAIMARISHA UPATIKANAJI, UDHIBITI WA BEI NA MAPATO YA TAIFA

 


Na Mwandishi Wetu


Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (Petroleum Bulk Procurement Agency - PBPA) umesema mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja umeendelea kuimarisha upatikanaji wa mafuta nchini, kudhibiti mfumuko wa bei, kuhakikisha ubora wa mafuta na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Afisa wa Logistic wa Petroli wa PBPA, Hilda Kowero, alisema taasisi hiyo inatumia maonesho hayo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake na mafanikio yaliyopatikana kupitia mfumo huo.

Alisema jukumu kuu la PBPA ni kuratibu uagizaji wa mafuta kwa pamoja ili kuhakikisha mafuta yanapatikana kwa uhakika katika maeneo yote ya nchi, hatua inayochangia maendeleo ya sekta mbalimbali za uchumi na huduma za kijamii.

Kowero alisema pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta, wakala huo hushirikiana na mamlaka mbalimbali za Serikali kuhakikisha mafuta yote yanayoingia nchini yanakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na mamlaka husika kabla ya kuanza kutumika.

Alieleza kuwa ushirikiano huo unahusisha taasisi kama Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) pamoja na Wakala wa Vipimo, jambo linalowapa wananchi uhakika wa kutumia mafuta yenye ubora na usalama unaokubalika.




Aidha, alisema mfumo huo umeongeza uwazi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa kuwezesha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa na uhakika wa kiwango cha mafuta kinachoingia nchini na hivyo kurahisisha ukusanyaji sahihi wa kodi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Kowero, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja kulikuwa na changamoto ya kuyumba kwa bei za mafuta, lakini kwa sasa mfumo huo umechangia kudhibiti mfumuko wa bei na kuhakikisha wananchi wanapata mafuta kwa bei zinazodhibitiwa kupitia taratibu zilizowekwa na EWURA.

Alisema mfumo huo pia umeendelea kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usambazaji wa mafuta katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, ambapo mafuta yanayoagizwa kupitia bandari za Tanzania husafirishwa kwenda Rwanda, Burundi, Uganda, Zambia, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kowero alibainisha kuwa hali hiyo imeimarisha mahusiano ya kidiplomasia na biashara kati ya Tanzania na nchi jirani huku ikiongeza mchango wa sekta ya nishati katika kukuza uchumi wa taifa.

Aliwataka wananchi kutembelea banda la PBPA katika Maonesho ya Sabasaba ili kujifunza zaidi kuhusu majukumu ya wakala huo na namna mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja unavyoendelea kuchochea maendeleo ya uchumi wa Tanzania kupitia upatikanaji wa mafuta ya kutosha, salama na yenye ubora.




TET NDIYO MOYO WA ELIMU NCHINI, VITABU VYA KIDATO CHA TANO NA SITA VIPO HAPA SABASABA -DEO FAZAH



Mkuu wa Idara ya Fedha na Uhasibu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Deo Fazah akipokea zawadi alipotembelea banda la TET ndani ya Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya biashara ya Dar es salaam (Sabasaba)2026.


MKUU wa Idara ya Fedha na Uhasibu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Deo Fazah amesema taasisi hiyo ndiyo moyo halisi wa elimu Nchini kwa elimu yetu ya Msingi, elimu ya Sekondari na Ualimu.

Deo Fazah amesema hayo katika Banda la TET ndani ya Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea barabara ya Kilwa, Temeke Jijini Dar es salaam.

Amebainisha:

"Tunapopata nafasi kama hii, tunashiriki ili kuwaambia Watanzania kile tunachofanya, tunapenda kuwakaribisha wadau wote wanaoweza kujitokeza Kufanya kazi na TET katika uandaaji wa Vitabu vya Kiada.

Pia Vitabu vyote vya Kiada vilivyofanyiwa maboresho tunavyo hapa na maeneo yote.

Taasisi ipo na maduka yake Kikanda, ikiwemo pale Ofisi TET Bamaga, lakini pia Kariakoo na kwa mawakala wengine wote.

Pia tupo Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa, Nyanda za juu Kusini kote huko vitabu vyote vipo na vinauzwa kwa bei elekezi kwa bei ileile ambayo kitabu kinachouzwa Dar es salaam na Kigoma ama Mbeya kitauzwa kwa bei ileile," Amesema Deo Fazah.

Aidha, amewakaribisha wadau wanaotaka kufanya masuala ya Utafiti katika elimu milango ipo wazi katika mashirikiano na TET katika kuendeleza elimu nchini.

Wazazi, walezi, Wanafunzi na wadau karibuni sana Vitabu vya kidato cha Tano na Sita pia vipo hapa na wote wanaweza kutembelea hapa Sabasaba lakini pia katika ofisi zetu za makao makuu ya TET