Advertisements

Monday, November 20, 2023

The CookFund awards 9.4 billion to boost market rollout of clean cooking solutions in Tanzania.

 Forty-four (44) clean cooking energy enterprises have been selected for the award of grant funding from the CookFund programme which is funded by European Union (EU) and managed by UN Capital Development Fund (UNCDF).

The award totaling 9.4 billion Tanzania shillings completes the second call for proposals phase from eligible businesses operating in five urban areas of Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Mwanza and Pwani to substantially increase the uptake of clean cooking technologies by the end user. Supported solutions include bioethanol, electric pressure cookers, liquified petroleum gas and improved charcoal stoves, effectively supporting the government of Tanzania target of reaching 80% of households in Tanzania adopt and transition to clean cooking energy by 2033.

To mark the achievement, the partners including the Ministry of Energy, EU and UNCDF hosted an Awards Ceremony. In her remarks, the guest of honor, Deputy Minister of Energy Hon. Judith Kapinga said, ‘The government values programmes like the CookFund and hopes that it will help to alleviate the current dependence on traditional cooking energy. 


The support to the private sector and entrepreneurship in the clean cooking space through financial grants provided by the program is meant to incentivize the private sector in the promotion of clean cooking solutions and help us in familiarization with this approach so that even after the program ends, we shall carry on using other resources and stakeholders until the market is fully established, said Deputy Minister Kapinga.’

Speaking on behalf of the European Union, Mr. Merel said, ‘This project is giving a visible contribution to the development of private sector investments in the sector of clean cooking and responds to the rapid urbanisation, in Tanzania as well as globally, where solutions for clean cooking are urgently needed’.

The new grantees join the initial 16 recipients, totaling 60 grants disbursed under CookFund. As the Fund Manager and primary program implementer, UNCDF offers ongoing support to grant recipients, ensuring effective fund utilization, promoting technical capacity building, and monitoring program operations for accountability.

Mr. Imanuel Muro, CookFund Programme Manager said, ‘With the presentation of the second round of grants, we are advancing a mechanism that empowers enterprises and promote a strategic shift in Tanzania's energy landscape. The CookFund fosters a diversified energy mix, channeling resources towards clean cooking technologies that replace harmful cooking practices and ensure a more sustainable and resilient energy future for our nation.’

Based on the Tanzania Mainland Household Budget Survey (2017/18), access to clean fuels and technologies for cooking is only 17.1% of urban population and 2% of rural population. The increase in demand for wood-fuel is driven by rapid urbanization, high prices, and the limited availability of alternative fuels. To overcome these challenges, the CookFund’s intention is to increase the share of population using sustainable clean cooking energy solutions in urban areas.

The CookFund provides financial and technical assistance to eligible enterprises and companies to accelerate market roll-out of clean cooking solutions (stoves and fuels) leading to improved social, economic, and environmental conditions. It finances capital expenditures and/or working capital for building the internal capacity of businesses involved in the production, importation, distribution, wholesale or retail of stoves, fuels, or related products and services.
Deputy Minister for Energy, Judith Kapinga (3rd Right), hands over a dummy cheque worth TZS 124 million to Duka la Mama company. The company is among the grantees of the TZS  9 billion in grants awarded to 44 enterprises engaged in the CookFund programme to boost the uptake of clean cooking technologies. Second left is UNCDF Program Manager, Immanuel Muro, EU Head of Delegation, Cedric Merel (2nd Left), and Styden Rwebangila, Assistant Commissioner for Electricity Development from the Ministry of Energy (Left).

Saturday, November 18, 2023

WIMBO MPYA MY SWEET, MR TZ AKIMSHIRIKISHA VAILEN

UNESCO YAKABIDHI VIFAA VYA MAFUNZO YA MRADI WA BEAR II KWA MVTTC MOROGORO

SHIRIKA la Elimu , Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) limekabidhi vifaa mbalimbali vya mafunzo kupitia programu mpya ya mradi wa ‘Better Education for Africans Rise[BEAR II] kwa Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro [MCVTTC]

Vifaa hivyo ni maalum katika Uandaaji na utoaji wa mafunzo ya Stashahada ya ufundi katika Sanaa za ubunifu na Kilimo-biashara [Creative arts and agri-business] vyenye thamani ya wastani wa Tsh 120,415,350 ambazo ni ufadhili wa ubia kati ya UNESCO na Jamhuri ya Watu wa Korea.

Awali akizungumza katika makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mkazi  wa UNESCO Dar es salaam, Bw. Michel Toto ameshukuru kwa namna ya kipekee na heshima kubwa kwa waliofanikisha mradi huo kuanzia mwanzo ikiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Elimu pamoja na wadau wote.

‘’Katika muda mchache, wataalam hao wataonyesha utendaji kazi wa vifaa hivi vikiwemo vya usindikaji wa chakula na ufundi wa mikono vikiwemo Oveni ya gesi, Oveni ya kuokea ya umeme (vacuum oven, automatic gas oven, Electric baking oven & fermenting oven). Lakini pia vifaa vya mashine za kufunga maji na unga, kinu cha mahindi, kiuasha umeme wa jua na vingine vingi.

UNESCO inazingatia mpango wa Maendeleo endelevu wa [SDG 4], katika kutetea usawa na elimu bora ya ufundi na kuongezeka kwa idadi ya vijana na watu wazima wenye ujuzi wa kiufundi na ufundi kwa ajili ya ajira, kazi za staha na ujasiriamali, na kuondoa ukosefu wa usawa katika upatikanaji wa taaluma.’’ Ameeleza Michel Toto.

Aidha, amesema Serikali na Chuo hicho kupitia mradi huo wa BEAR II, inaacha alama yake katika kushughulikia changamoto ya dunia ya kuhakikisha vijana wanawezeshwa kupitia elimu na kukuza ujuzi wao katika kukubiliana na soko la ajira.

Kwa upande wake,Mgeni rasmi Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu, Dkt. Ethel Kasembe ameshukuru UNESCO na Watu wa Jamhuri ya Korea kwa msaada wa vifaa hivyo kwani vinaenda saidia ajira kwa Vijana na Watanzania kwa ujumla huku pia akipokea changamoto za Chuo hicho ikiwemo uchakavu wa majengo ambapo amesema wameichukua kuona namna ya kusaidia.

Nae Mkuu wa chuo hicho cha MVTTC, Samwel Kaali amepongeza UNESCO kwa vifaa hivyo huku wakiadi kuvitunza sambamba kuzalisha wataalam katika fani hizo mpya zitakazoanza chuoni hapo.

‘’Shukrani za dhati kwa UNESCO, VETA tutahakikisha vifaa hivi tunatunzwa vizuri ili vidumu na kuendelea kutumika kutolea mafunzi kwa muda mrefu zaidi.’’ Amesema Kaali.

Chuo hicho cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro[MVTTC] ni miongoni mwa Vyuo maalum vinavyomilikiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi [VETA]ambapo kilianzishwa mwaka 1997 kupitia Sheria ya Bunge Na1 ya mwaka 1994 sura 82, marejeo ya mwaka 2019 pamoja na marekebisho yake mwaka 2021 na 2022 huku pia kikiwa na usajili wa Ithibati ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi [NACTVET] kikiwa na lengo la kutoa mafunzo ya taaluma za elimu ya Ualimu wa Ufundi na Ufundi stadi pamoja na usimamizi wake.

Imeandaliwa na Andrew Chale, Morogoro-Mwandishi na Mpiga Picha.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) nchini, Bw. Michel Toto akizungumza wakati wa tukio la kukabidhi vifaa vya mradi wa kuboresha elimu ya ufundi (BEAR II) wenye lengo la kuwajengea uwezo vijana katika ajira mbalimbali sokoni na binafsi unaofadhiliwa na Shirika hilo na ubia wa pamoja na Jamhuri ya Watu wa Korea, tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) nchini, Bw. Michel Toto akizungumza wakati wa tukio la kukabidhi vifaa vya mradi wa kuboresha elimu ya ufundi (BEAR II) wenye lengo la kuwajengea uwezo vijana katika ajira mbalimbali sokoni na binafsi unaofadhiliwa na Shirika hilo na ubia wa pamoja na Jamhuri ya Watu wa Korea, tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.



Mgeni rasmi Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu, Dkt. Ethel Kasembe akizungumza katika tukio hilo la ukabidhiwaji wa vifaa wa mradi wa (BEAR II).Katikati ni Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO nchini, Bw. Michel Toto na kushoto ni Mkuu wa Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro, Bw. Samwel Kaali,tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.

Mkuu wa Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro, Bw. Samwel Kaali akizungumza katika tukio hilo la ukabidhiwaji wa vifaa wa mradi wa (BEAR II).Katikati ni Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO nchini, Bw. Michel Toto na kushoto ni Mgeni rasmi Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu, Dkt. Ethel Kasembe,tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.



Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO nchini, Bw. Michel Toto [kulia] wakiwa wameshika nyaraka ya makabidhiano ya vifaa hivyo na Mgeni rasmi Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu, Dkt. Ethel Kasembe,tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.



Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) nchini, Bw. Michel Toto akishuhudia vifaa hivyo wakati wa tukio la kukabidhi vifaa vya mradi wa kuboresha elimu ya ufundi (BEAR II) wenye lengo la kuwajengea uwezo vijana katika ajira mbalimbali sokoni na binafsi unaofadhiliwa na Shirika hilo na ubia wa pamoja na Jamhuri ya Watu wa Korea, tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) nchini, Bw. Michel Toto pamoja na mgeni rasmi wakipata maelezo ya vifaa hivyo namna vinavyofanya kazi wakati wa tukio la kukabidhi vifaa vya mradi wa kuboresha elimu ya ufundi (BEAR II) wenye lengo la kuwajengea uwezo vijana katika ajira mbalimbali sokoni na binafsi unaofadhiliwa na Shirika hilo na ubia wa pamoja na Jamhuri ya Watu wa Korea, tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.



Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) nchini, Bw. Michel Toto na mgeni rasmi na viongozi wengine wakionja mikate iliyotengenezwa na vifaa hivyo Chuoni hapo wakati wa tukio la kukabidhi vifaa vya mradi wa kuboresha elimu ya ufundi (BEAR II) wenye lengo la kuwajengea uwezo vijana katika ajira mbalimbali sokoni na binafsi unaofadhiliwa na Shirika hilo na ubia wa pamoja na Jamhuri ya Watu wa Korea, tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.

Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO nchini, Bw. Michel Toto [kulia] wakiwa wameshika moja ya vifaa wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo na Mgeni rasmi Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu, Dkt. Ethel Kasembe,tukio lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.



Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO nchini, Bw. Michel Toto [kulia] akiagana na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu VETA, Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala Bw. Felix Staki, Kushoto ni Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Wizara ya Elimu, Dkt. Ethel Kasembe na kulia ni Mkuu wa Chuo cha Ualimu wa Ufundi Stadi Morogoro, Samwel Kaali wakati wa tukio kukabidhiwa vifaa lililofanyika katika Chuo cha Ualimu wa Ufundi Morogoro.

Friday, November 10, 2023

WATEJA WA Y9 MICROFINANCE KUONGEZEWA DAU LA MKOPO SASA WAWEZA KUKOPA HADI LAKI TATU

 

 Na Mwandishi wetu.


Dar es Salaam. Taasisi ya kifedha ya Y9 Microfinance imeendelea na utaratibu wake wa kukabidhi zawadi kila wiki ambapo wiki hii wamekabidhi zawadi ya pikipiki mbili kwa washindi wa Droo ya nne kwa wakazi wa Njombe na Songea.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo Mkurugenzi wa Mauzo na Usambazaji wa Taasisi ya Y9 Microfinance Bw. Fredrick Mtui amesema kuwa taasisi ya Y9 ilianzishwa mahususi kuwasadia na kuinua mitaji ya wale wenye kipato cha chini na watanzania wote nchini.

Lengo kuu la Y9 Microfinance ni kuhakikisha kila mtanzania anapata fursa hii kwa kuhakikisha anapakua app ya Y9 Microfinance na kupata huduma ya tatu ambazo ni mkopo wa fedha taslimu.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Taasisi ya Y9 Microfinance, Sophia Mang’enya ambaye pia alieleza kuwa hii ni fursa kubwa sana kwa watanzania kwani Taasisi ya Y9 umeongeza pia kiwango cha mkopo pia siku za kulipa deni la mkopo

Mang’enya ameeleza kuwa jwasasa mteja wa Y9 anaweza kukopa kuanzia elfu mbili hadi laki tatu na muda wa kurejesha ni siku 9 ambapo awali kiwango cha juu kilikuwa laki moja na muda wa kurejesha ni siku tatu

Ameeleza kuwa nia na madhumuni ya kuongeza kiwango cha mkopo nikuridhishwa na mwenendo mzuri wa ulipaji kwa wateja wao hivyo amewasihi watanzania wachangamkie fursa hii ambayo haina mashart magumu.

amewapongeza washindi wote kwa kujiunga na huduma zao na kuweza kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo simu, pikipiki vilevile ameongeza kwamba kwenye droo ya mwisho ambayo itanyika katikati ya mwezi Disemba kutakuwa na zawadi kubwa zaidi ya gari aina ya Toyota IST. na zawadi nyengine kemkem

Alisema kuwa washindi hao wameshinda zawadi hizo baada ya kupakuwa App yetu na kukopa kupitia app na kurejesha mikopo yao ndani ya muda uliowekwa kwa mujibu wa taratibu zetu.

Alisema kuwa zawadi bado zipo nyingi kikubwa Watanzania kuendelea kutumia humu zetu ili kujishindia zawadi.

Leo pia tumechezesha droo ambapo tumepata washindi wawili ambao ni Riziki Makame ambae amejishindia pikipiki ya matairi mawili pamoja na mkazi wa Arusha Bw. Peter ambae amejishindia simu janja.




Friday, November 3, 2023

WASHINDI SHINDANO LA BE ROAD SAFE KWA NJIA YA SANAA WATUNUKIWA TUZO, RC DAR AIPONGEZA PUMA ENERGY TANZANIA

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Amend wametoa tuzo kwa wanafunzi ambao wameibuka washindi wa michoro ya usalama barabarani kupitia  kampeni ya Be Road Safe kwa njia ya sanaa.

Katika utoaji wa tuzo huo umefanyika katika Shule ya Msingi Kibugumo iliyopo Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ambaye aliwakilishwa ba Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo .

Kampeni hiyo inalenga kuleta mageuzi ya usalama wa watoto na vijana barabarani nchini Tanzania huku ikielezwa wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Kubugumo,  Kufaru,  Msewe, Kibasila na Mtambani wameshiriki katika kampeni hiyo kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo shindano la kuchora.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila,  wakati wa utoaji tuzo hizo kwa washindi,  Mkuu wa Wilaya Halima Bulembo amesema wanaipongeza kampuni ya Puma Energy Tanzania pamoja na Ammend kwa kutoa elimu ya usalama barabarani kwa watoto walioko shule za msingi.

Asema mafunzo ya usalama barabarani kwa watoto walioko katika shule za msingi yatasaidia kupunguza ajali za barabarani hususan katika maeneo ambayo mafunzo hayo yametolewa huku akishauri elimu hiyo yatolewe nchi nzima kuongeza uelewa.

Amesisitiza Serikali inaamini kwa kufanya hivyo kitaokolewa kizazi cha sasa na kijqacho kwa kuwa elimu ya matumizi bora ya barabara inaendelea kusambaa.

Amesema kuwa kupitia mafunzo ya usalama barabarani kwa watoto hususan walioko katika shule za msingi Puma imefanya jambo kubwa katika kuepusha ajali za barabarani ambazo zimekuwa sikiisababishia nchi hasara kubwa kwa kupoteza nguvu kazi na mali.

"Mafunzo ya elimu ya usalama barabarani yaliyotolewa na Puma Energy Tanzania kwa kushirikiana na Ammend katika shule tano ni vyema yakatolewa pia katika shule nyingi zaidi kuwajengea uwelewa watoto wangi wa Dar es Salaam na hata nje ya mkoa huo.

"Serikali ya mkoa (Dar es Salaam) tunaamini kuwa kwa kufanya hivi tunaokoa kizazi cha sasa na kijacho kwa kuwa elimu ya matumizi bora na sahihi ya barabarani inaendelea kusambaa," amesema Bulembo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Fatma Abdallah, amesema mafunzo yaliyotolewa kwa wanafunzi hao ni utekelezaji wa mpango wa 'Be road safe Africa) unaotekelezwa na Ammend katika nchi tano za Afrika ambazo ni Zambia, Zimbabwe, Tanzania, Botswana na Ghana.

Amesema kuwanzishwa kwa mpango huo kunatokana na takwimu mbaya za ajali za barabarani ambazo zinasababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali.

"Nchini Tanzania pekee Jeshi la Polisi kupitia kikosi cha Usalama Barabarani kimetoa takwimu zinazoonyesha kutokea kwa vifo 1,545 na majeruhi 2,278 kwa mwaka 20222 kutokana na ajali 1,720 za barabarani.

Fatma akizungumzia kampeni hiyo ya 'Be Road Safe' amesema kuwa ni jukwaa muhimu shirikishi linalokuza jamii salama kwa watoto.

 "Kupitia mashindano hayo ya kuchora tumeongeza ubunifu na uelewa thabiti wa kanuni za usalama barabarani miongoni mwa wanafunzi na kuongeza ufahamu kwa jamii ya Watanzania.

Amesema tangu kuanzishwa kwa mpango huo mwaka 2013 'Be Road Safe' umekuwa mwanga wa matumaini na kwamba ni msingi wa kimkakati wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) wa kampuni hiyo chini ya mpango mkuu wa 'Be Puma Safe' ambao pia unajumuisha uwezeshaji wa wananchi hususan vijana.

Hafla hiyo iliyofanyika Shule ya Msingi Kibugumo ilihidhuriwa na wadau mbalimbali akiwemo Mkuu wa Dawati la Elimu ya Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi Michael Deleli, Mkurugenzi wa Shirika la Ammend Simon Kalolo, walimu na wanafunzi kutoka shule zilizoshiriki mafunzo na shindano hilo.

 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo(wa tatu kulia) akimkabidhi kikombe mwanafunzi wa darasa sita katika Shule ya Msingi Kibugumo Feisali Msiakwe baada ya kuibuka mshindi wa mchoro wa usalama barabarani na kuifanya shule yake kuwa kinara katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Amend.Wengine katika picha hiyo ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Fatma Abdallah( wa kwanza kushoto), Kaimu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kibugumo Salvatory Lasway ( wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo( wa kwanza kulia).

Mwanafunzi wa darasa sita katika Shule ya Msingi Kibugumo Feisali Msiakwe akinyanyua juu kikombe cha ushindi baada ya mchoro wake wa kuelimisha kuhusu usalama barabarani kushinda katika shindano la michoro ya usalama barabarani kwa Mkoa wa Dar es Salaam.Feisali amepata kitita cha Sh.500, 000 na shule yake baada ya kuibuka mshindi wa mchoro wa usalama barabarani na kuifanya shule yake imepata Sh.milioni tano ambazo zimetolewa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kupitia Mkurugenzi wake Fatma Abdallah(wa kwanza kushoto waliosimama.)



Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo(wa tatu kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Fatma Abdallah( wa kwanza kushoto) wakiwa wameshika mfano wa hundi ya Sh.milioni tano iliyotolewa kwa Shule ya Msingi Kibugumo baada ya mwanafunzi wake Feisali Msiakwe ( wa nne kushoto) kuibuka mshindi wa mashindano ya mchoro wa usalama barabarani katika mkoa wa Dar es Salaam.Mashindano hayo yameandaliwa na Puma kwa kushirikiana na Shirika la Amend Tanzania.Wengine katika picha hiyo ni walimu na wadau wa usalama barabarani.













Sunday, October 8, 2023

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIWA SAFARINI KUELEKEA NEW DELHI, INDIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiendelea na kazi wakati akiwa safarini kuelekea Mji wa New Delhi nchini India kwa ajili ya Ziara ya Kitaifa tarehe 08 Oktoba, 2023. Mhe. Rais Samia alitumia usafiri wa Ndege ya Shirika la ATCL ambalo limeanza safari zake kutoka Tanzania mpaka India.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiendelea na kazi wakati akiwa safarini kuelekea Mji wa New Delhi nchini India kwa ajili ya Ziara ya Kitaifa tarehe 08 Oktoba, 2023. Mhe. Rais Samia alitumia usafiri wa Ndege ya Shirika la ATCL ambalo limeanza safari zake kutoka Tanzania mpaka India.

 

Friday, October 6, 2023

MTOTO AMUUA BABA YAKE KWA KUMKATA MAPANGA WAKIGOMBEA MKOROSHO MKOANI LINDI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Pili Mande

Na Said
Hauni, Lindi.

MKULIMA wa Kijiji na Kata ya Namapwia,wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi, Musa Michenje (60) amefariki dunia baada ya kukatwa mapanga na mtoto wa kaka yake aitwae Nkono Malenga (35) kutokana na ugomvi wa kugombania mti wa mkorosho.


Taarifa kutoka kijijini humo ambazo zime thibitishwa na uongozi wa Kata na Jeshi
la Polisi, inaeleza mauwaji hayo yamefanyika Oktoba 4, 2023 saa 11;00 alasiri.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo akiwemo Diwani wa Kata hiyo Omari Lingumbende wameeleza Michenje na Malenga ni mtu na mwanawe,walikuwa wakigombea mkorosho uliokuwa kwenye mpaka wa shamba kati ya marehemu na kaka yake Malenga.

Mashuhuda hao Yusufu Ismaili, David Michael walisema kutokana na mkorosho huo kuwa mpakani kaka mtu Malenga aliamua kumuachia mdogo wake Michenje.

Walisema siku hiyo Michenga akiwa anaokota korosho kwenye mkorosho huo,mtoto wa kaka yake aitwse Nkono alifika na kumtaka aache kuokota.

Walisema kutokana na mabishano yaliyokuwa yamejitokeza mtoto huyo aliyekuwa na panga mkononi alianza kumshambulia baba yake huyo mdogo kwa kumkata maeneo mbalimbali ya mwili wake na kusababisha kifo hapo hapo.

MRADI WA ELIMU YA JUU KWA MAGEUZI YA KIUCHUMI CHUO KIKUU MZUMBE WAENDESHA MAFUNZO KWA WAHADHIRI KUHUSU UFUNDISHAJI WA KIBUNIFU

Kaimu Mratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) Dkt. Hawa Tundui, akimkaribisha Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha kufungua Mafunzo ya Wahadhiri juu ya kuunganisha ufundishaji wa kibunifu na masuala mtambuka katika mitaala yanayoendelea katika Hoteli ya Oasis, Morogoro. Mafunzo hayo yameratibiwa na Mradi wa Elimu ya juu kwa mageuzi ya kiuchumi (HEET- Project) Chuo Kikuu Mzumbe.
Dkt. Perpetua Kalimasi akifundisha kamati zinazotengeneza na kupitia mitaala za Chuo Kikuu Mzumbe kuhusu Rasimu ya mitaala ya Elimu ya msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu ili waweze kuhusisha na mitaala wanayoihuisha katika mafunzo ya wahadhiri juu ya kuunganisha ufundishaji wa kibunifu na masuala mtambuka katika mitaala yaliyofanyika katika Hotel ya Oasis Morogoro.
Washiriki wa Mafunzo ya Wahadhiri juu ya kuunganisha ufundishaji wa kibunifu na masuala mtambuka katika mitaala wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilika kwa hafla ya ufunguzi. Mafunzo hayo yameratibiwa na Mradi wa Elimu ya juu kwa mageuzi ya kiuchumi (HEET-Project) Chuo Kikuu Mzumbe

MFANYAKAZI WA NDANI ARUSHA ALIA KUNYANG'ANYWA MTOTO WA MIEZI 6 NA BOSI WAKE, ALIDAI NI MJUKUU WAKE

WENYE VVU KUPATA HUDUMA JUMUISHI UCHUNGUZI, TIBA DHIDI YA NCD’S, KUPITIA THPS NA CDC


Na Veronica Mrema

Watu zaidi ya 200,020 wanaoishi na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi {VVU}, wameanza kunufaika na huduma jumuishi ya uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza {NCD’s} kwa kufanyiwa uchunguzi.

Pamoja na hilo, wanapatiwa dawa bila malipo hususan wale wanaogundulika wanakabiliwa na tatizo la Shinikizo la Damu.

Dawa ambayo hivi sasa wameanza kugawiwa bila malipo ni ya kudhibiti Shinikizo la Damu.

Taasisi ya THPS inatekeleza mradi wa Afya Hatua chini ya ufadhili wa Serikali ya Marekani kupitia CDC katika kuwafikia watu hao katika mikoa minne.

Yamebainishwa hayo leo na Mkurugenzi wa Miradi THPS Dkt. Eva Matiko alipozungumza katika mkutano wa masuala ya afya {Tanzania Health Summit}, Dar es Salaam.

“THPS ina malengo ya kuhakikisha huduma jumuishi kwa ajili ya magonjwa yasiyoambukiza inafikia wapokea huduma {wenye VVU} wote,” amesema na kuongeza,

“.., hivi sasa vituo zaidi ya 245 vinatoa huduma hii, kupima kutambua na kutoa rufaa, kwa mwaka wa fedha 2022/23 baadhi ya mikoa itanufaika na mradi wa CDC.

“Kwa kuweza kutoa dawa kama inavyotolewa kwa dawa za HIV, vile vile dawa za kudhibiti Shinikizo la Damu watakuwa wanapatiwa wateja hawa.

RAIS DKT. SAMIA KUFANYA ZIARA YA SIKU NNE NCHINI INDIA

Lengo la ziara ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kudumisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na India hususan sekta za kimkakati kama afya, viwanda na biashara, ulinzi na usalama, elimu, teknolojia ya habari na mawasiliano, uchumi wa buluu, maji, na kilimo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan atafanya ziara ya Kitaifa nchini India kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya India Mhe. Droupadi Murmu, kuanzia tarehe 8 – 11 Oktoba.

Na Sophia Kingimali

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kikazi ya siku nne nchini India yenye lengo la kutanua wigo wa biashara na uwekezaji nchini.

Akizungumzia ziara hiyo Oktoba 5 jijini Dar es salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makambo amesema ziara hiyo inatarajiwa kuwa yenye tija kubwa kwa nchi kwani mikataba zaidi ya 15 itasainiwa.

“Ziara hii inafanyika kutokana na uhusiano mzuri uliopo baina ya India na Tanzania lakini pia kudumisha na kuendeleza uhusiano katika sekta za kimkakati ikiwemo elimu,maji,kilimo na afya”amesema Makamba.

Amesema matarajio yanayotegemewa kutokana na ziara hiyo ni pamoja na kuanzisha taasisi ya upandikizaji moyo nchini lakini pia kuanzishwa kwa kiwanda cha chanjo za binadamu na wanyama.

Amesema pamoja na hayo wanatarajia mapinduzi ya kidigitali katika sekta viwanda kwa kuanzisha kiwanda cha kutengenezea simu janja nchini.

MBINU ZA MONTESSORI ZINAMWANDAA MTOTO KUWA JASIRI NA UWEZO WA KUJITEGEMEA


MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk.Philip Mpango,akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Montessori Community of Tanzania (MCT),Bi. Sarah Kiteleja mara baada ya kutembelea banda la Taasisi hiyo wakati wa Kilele Cha Jukwaa la Mwaka la Mashirika yasiyo ya Kiserikali kilichoenda sambamba na Uzinduzi wa Mfumo wa Ramani wa kidijitali wa utambuzi wa Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini leo Oktoba 5,2023 jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna-DODOMA


Mkurugenzi wa Montessori Community of Tanzania (MCT),Bi. Sarah Kiteleja amesema mbinu za ufundishaji za Montessori zinamwandaa mtoto kuwa na ujasiri na uwezo wa kujitegemea pamoja na kuishi katika mazingira yoyote.

Bi.Sarah ameyasema hayo leo Oktoba 5,2023 Jijini Dodoma wakati wa Kilele Cha Jukwaa la Mwaka la Mashirika yasiyo ya Kiserikali lililoenda sambamba na Uzinduzi wa Mfumo wa Ramani wa kidijitali wa utambuzi wa Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini.

Bi.Sarah amesema wanafanya kazi kwa karibu na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia na Maendeleo ya Jamii kutatua changamoto ya Kusoma,Kuandika na Kuhesabu.

Amesema kupitia vifaa vya Montessori wameanza kufundisha mtoto kusoma,kuandika na kuhesabu.

Amesema kwenye hesabu wanafundisha msingi wa hesabu na kumwelewesha mtoto kwa kugawanya,kujumlisha na kuzidisha na kufanya hesabu mpaka 1999.

Amesema kupitia mfumo huo unamsaidia mtoto kuwa na ujasiri uwezo wa kujitegemea,kuishi mahali popote katika mazingira yoyote.

“Montessori inampatia mtoto life skills ambazo zitamsaidia kuishi popote,”amesema Bi.Sarah

Amesema wameweza kufanya utafiti kuangalia mbinu hiyo ya ufundishaji na imeleta faida gani katika Jamii.

“Katika utafiti huu imeonekana kwamba Montessori inaibua vipaji kuweza kuwa na ujuzi na kujiamini na uwezo wa kufanya vitu vipya,” amesema

Hata hivyo amesema mipango ya Shirika ni kuanza kufundisha walimu wa shule za msingi katika Chuo cha Mwanza ambapo kozi inatarajia kuanza Januari mwakani.

“Lakini pia mipango mingine tumeanza utafiti katika Mkoa wa Bukoba kwa ajili ya kuwafundisha walimu wa Serikali ili waweze kuyamudi madarasa yao”amesema Bi.Sarah

Pia amesema wana vyuo 7 vya Montessori na tumefanikiwa kufundisha zaidi ya walezi 5000 na kuanzisha vituo vya malezi 2500 nchi nzima.

Amesema kupitia vituo vya malezi wamefanikiwa kufundisha watoto zaidi ya 100,000.

DKT. KUSILUKA AIPONGEZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Na Sixmund Begashe -Dodoma

Wizara ya Maliasili na Utalii imepongezwa kwa kazi nzuri ya usimamizi wa ujenzi wa Jengo jipya la Ofisi awamu ya pili la Wizara hiyo lililopo Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma, ambalo lipo tayari kwa matumizi ya Shughuli za kiofisi.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, alipolitembelea Jengo hilo kwenye ziara yake na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi unaondelea kwenye mji huo wa kipeke nchini.

Aidha licha ya kuipongeza Wizara hiyo Dkt. Kusiluka amehimiza ukamikishwaji wa kazi chache zilizobaki kwenye ujenzi huo.

Akizungumzia ujenzi wa Jengo hilo, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi ameleza kuwa hadi sasa ujenzi wa jengo hilo umeshafikia asilimia 99% na kuwa asilimia Moja iliyobaki ni ya kazi ndogo ndogo za mwisho


Tuesday, September 19, 2023

KUELEKEA IMBA TOGETHER 2023 MPANGO WA RATIBA HUU HAPA!!

THIS TIME SIO SIKU 1 TENATUKIO LINAANZA TAR 27 KISHA TUNAHITIMISHA TAR 28 KWA KISHINDO!!

KUANZIA NI LEO MPAKA SIKU YA TUKIO TUTAKUWEKEA UPDATE KILA SIKU!!

KARIBU WINSTON SALEM
KARIBU NORTH CAROLINA
KARIBU UNITED STATES
KARIBU IMBA 2023
@imbatogether
@imbatogether
@ajs_tv_usa
@ajs_tv_usa
@anna_simtaji
@anna_simtaji

US EMBASSY SUPPORTS PEMBA WOMEN ENTERPRENEURS



 U.S. Embassy Dar es Salaam 

TANZANIA


September 19, 2023

FOR IMMEDIATE RELEASE

U.S. Embassy Supports Pemba Women Entrepreneurs 

Pemba – Thirty women entrepreneurs from Pemba today concluded 13-weeks of specialized training in business and entrepreneurship funded by the U.S. government through its Academy of Women Entrepreneurs (AWE) program. U.S. Embassy Ambassador Michael Battle congratulated the women and urged them to use what they learned to continue building successful businesses. The graduation ceremony was also attended by Minister of State President’s Office Labor, Economy, and Investment -Zanzibar Honorable Mudrick Ramadhan Soraga, Southern Pemba Regional Commissioner Hon. Salama Mbarouk Khatib, District Commissioner of Chake Chake District Hon. Abdalla Rashid Ali, Coordinator of Pemba Public Library Mr. Ahmed Amour, and many other distinguished guests. 

AWE is a global initiative of the U.S. government seeking to promote women’s economic empowerment with the goal of helping 50 million women worldwide fulfill their economic potential.  AWE is committed to providing women the knowledge, networks, and access they need to turn their ideas into reality. 

Speaking to the graduates during the ceremony, Ambassador Battle described the impact of the training that AWE provides. “These 13 weeks of training have provided you with the practical skills to create sustainable businesses, as well as a network of mentors and like-minded entrepreneurs in the United States,” he said.

He further added that empowering women economically is the fastest way to change society. “Women have a strong multiplier effect on the wider community because when women succeed, they are more likely to invest their earnings into their families and their communities, paying for things like their children’s education and health care.  The economic benefits of your accomplishments support future generations.  Your creativity is already having an impact on the society and the economy of Tanzania,” he said.

The Pemba cohort is the tenth group of women to participate in AWE.  Other groups of women have participated in Dar es Salaam, Iringa, Zanzibar, Mwanza, Dodoma, Mbeya, Bagamoyo, Kigoma, and Kagera

Through a partnership with the U.S. African Development Foundation (USADF), entrepreneurs participating in the AWE program are eligible for additional seed funds from USADF ranging up to $20,000 to expand their businesses.  

The U.S. Embassy partners with Selfina to implement the AWE program in Tanzania. Founded in 2002 by Dr. Victoria Kisyombe, Selfina is a pioneer of micro-credit in Tanzania through micro-leasing with particular attention to widows and young girls. In the past 19 years SELFINA has economically empowered more than 31,000 women through an active revolving fund. Over 300,000 lives have been impacted through the benefits accrued. Women are now owners of their own businesses and more than 150,000 jobs have been created. 


Friday, September 15, 2023

MKURUGENZI MKUU TCAA AKAGUA MABORESHO YA MRADI WA MNARA WA KUONGOZEA NDEGE UWANJA WA NDEGE MTWARA

  

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bw. Hamza Johari (wa kwanza kushoto) akiongoza timu ya TCAA na Wakala wa Majengo (TBA) katika ukaguzi mradi wa maboresho ya mnara wa kuongozea ndege unaoendelea katika Uwanja wa ndege Mtwara.
Mhandisi Swalehe Nyenye kutoka TCAA akielezea mpango wa maboresho uliopo kwenye ramani ya ujenzi wa mnara huo

Timu ikiendelea kukagua hatua za mnara wa muda unaoendelea kujengwa uwanjani hapo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bw. Hamza Johari ameongoza timu ya wataalamu kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) na Wakala wa Majengo (TBA) katika ukaguzi wa mradi wa maboresho ya mnara wa kuongozea ndege unaoendelea katika Uwanja wa ndege Mtwara.

Mradi huo unahusisha vipengele viwili ikiwa ni kujenga mnara wa muda ambapo utaruhusu waongozaji ndege kuendelea na kazi wakati mnara wa sasa ukifanyiwa maboresho unatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Novemba.

Huu ni muendelezo wa uboreshaji wa miundombinu unaofanywa na Serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha wataalamu wanatekeleza majukumu yao katika mazingira mazuri ya kazi.