ANGALIA LIVE NEWS

Friday, June 12, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAKOSHWA NA TMDA



Na. Mwandishi Wetu,

Dodoma.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya  UKIMWI  yatembelea ofisi za TMDA Makao Makuu Dodoma Juni 10, 2026 kwa lengo la kujionea utendaji wa taasisi na inavyotekeleza majukumu yake. 

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.  Johannes Lukumayi (Mb) amesema lengo la kamati ni kujionea kwa macho namna taasisi hii muhimu katika kulinda afya ya jamii imejipanga katika kuwahakikishia wananchi wanalindwa afya yao kupitia  bidhaa za dawa na vifaa tiba.

"Tunafahamu umuhimu wa taasisi hii ndani ya nchi katika kulinda afya zetu na nje ya nchi pia katika kuongoza taasisi nyingine" alisema   Mhe.  Lukumay.

Akichangia wakati wa kuhitimisha ziara hiyo, Mhe. Adonis Bitegeko (Mb), aliipongeza Mamlaka kwa mapinduzi makubwa katika kuwekeza katika mifumo ya TEHAMA na aliitaka Mamlaka kuendelea kutatua changamoto ya mifumo ya uingizaji mizigo kwa kushirikiana na wadau wengine kufuatia mabadiliko yaliyopo katika mfumo huo. Aidha alitoa wito kwa Mamlaka  kujipanga ili kuendana na ukuaji wa sayansi na Tecknolojia katika masuala ya udhibiti.

Ziara hiyo pia ilihusisha viongozi wa Wizara ya Afya akiwemo Katibu Mkuu Dkt. Seif Shekalage ambao kila mmoja aliipongeza Mamlaka kwa utendaji na namna inatekeleza majukumu yake.




















DKT. KIJAJI ATETA NA WAZIRI WA CHINA KUHUSU USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA UTALII



WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Utamaduni na Utalii wa China Mhe. Gao Zheng katika Mkutano wa 126 wa Baraza Tendaji la Shirika la Utalii Duniani uliofanyika nchini Teledo, Hispania.

Mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha ushirikiano wa diplomasia ya uchumi hususani katika Sekta ya Utalii kati ya Tanzania na China.

Viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu mikakati ya kuvutia watalii, kukuza uwekezaji, na kubadilishana uzoefu na matumizi ya teknolojia katika utalii.

Aidha katika kikao hicho, Dkt. Kijaji alibainisha kuwa Tanzania iko tayari kushirikiana kwa karibu na China ili kukuza Sekta  ya Utalii baina ya nchi hizo mbili, huku akieleza kuwa China ni moja ya soko muhimu la utalii na la kimkakati kwa Tanzania.  

Aidha, alibainisha umuhimu wa kuendeleza programu za mafunzo na kubadilishana utaalamu ili kuhakikisha kuwa pande zote zinanufaika kutokana na fursa zilizopo.

Pande zote mbili zilikubaliana kuendeleza mazungumzo hayo na kuanzisha hatua za utekelezaji wa ushirikiano zaidi, ikiwemo miradi ya pamoja ya utalii, uwekezaji wa kimkakati, na kampeni za kukuza bidhaa za utalii zinazovutia soko la kimataifa. 

Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza idadi ya watalii, kuongeza mapato ya utalii, na kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na China.







MFAHAMU JETA (TRIDACNA)



Wavuvi wa Pwani ya Bahari ya hindi hapa Tanzania humtaja Jeta kuwa ni samaki asiyetembea. Wakati wanasayansi humtaja kama kiumbe kwenye kundi la mollusca/Mollusk ambaye anaweza kuishi zaidi ya miaka 500. Huhifadhi mamilioni ya mwani wa *usanisinuru au usanidimwanga* (photosynthetic) katika gamba lake ambao hutoa hadi asilimia 90% ya chakula chake. 

Hapa Makumbusho ya Taifa la Tanzania tunayo mabaki ya  Tridacna Gigas kutoka pangani mkoani Tanga na mengine kutoka mkoa wa Lindi yanayokadiliwa kuwa viumbe hao waliishi umuri wa miaka 420 hadi 460. Wakiwa miongoni mwa viumbe walioshi umuri mrefu zaidi duniani.

Ni kweli kwamba kiumbe huyu huwa hatafuti chakula. Bali hutegemea zaidi mionzi ya  jua ili kujitengenezea chakula chake yeye mwenyewe kwa mchakato wa *usanisinuru au usanidimwanga* (photosynthesis). Lakini Wavuvi kutoka pwani ya Tanzania wanasimulizi yao ndefu na nzuri sana kuhusu njia ya kiumbe huyu kujipatia chakula. Wao wanaamini kwamba: *gamba linalofunika mwili wa  Jeta (Tridacna) huwa linafunguka pale anapokuwa na njaa. Ile sehemu yake ya ndani huwavutia baadhi ya viumbe kutamani kuidonoa kama chakula chao, kumbe huo ni mtego, huvizia samaki wadogo kama dagaa na baadhi viumbe wengine wadogo wanaopotaka kumdonoa yeye huwa anafunga gamba lake. Hapo humgeuza kila anayeingia ndani kuwa kitoweo chake*. 

Hiyo ndio simulizi kutoka kwa wavuvi wa pwani ya Tanzania.

Tridacna waliopo hapa Makumbusho ya Taifa la Tanzania ndio jamii ya Jeta wanaokuwa wakubwa zaidi kiumbo, inayofikia hadi mita 1.4 na kilo 250. Pia ni kati ya viumbe wanaoishi kwa muda mrefu zaidi, na umri wa juu uliothibitishwa unakaribia miaka 500 kulingana na uchambuzi wa ukuaji wa gamba lake.

Mfumo wa lishe ndio kitu cha ajabu zaidi duniani maana hawatembei ila wanajilisha wenyewe kwa kujichakatia chakula. Hawa viumbe huwa wanastawi zaidi eneo la bahari lenye idadi kubwa ya mwani (wanga wa jua). Mara nyingi huwa wanapatikana maeneo ya matumbawe. Hapo husitawi na kutanua gamba lake kama tishu maalum za vazi lake (mdomo wa nje huwa una rangi, unaoonekana wakati mtulivu akiwa amefunguka). 

Mwani huu wa photosynthesis kwa kutumia mwanga wa jua, huzalisha sukari ambayo huhamishwa kwenda mwilini mwake kama chakula. Hadi asilimia 90% ya mahitaji ya lishe ya Jeta (Tridacna) yanaweza kutimizwa kwa mchakato huo wa mwani, ikisaidiwa na kuchuja kwa chembe za maji.

Ni kweli kabisa kuwa Tridacna hahitaji kuwinda, kufuata mawindo, au kusogea. Inafungua ganda lake, hujiweka wazi kwenye mwanga wa jua, na kungoja.

Mazingira yake ukuaji wake lazima awe katika kina kifupi, maji safi, na jua - kwa kawaida kina cha mita 1-20 katika miamba. Maisha yake yanategemea kabisa miamba ya matumbawe ambayo amechagua.

Akiwa mtulivu siku zote kiumbe huyu anaweza kuishi kwa miaka zaidi ya 500 kwa kujipatia chakula chake mwenyewe bila kujongea popote. 

Siku ukifika Makumbusho ya Taifa la Tanzania basi jitaidi uwaone Jeta kwa macho yako (Tridacna), simulizi hii itakufaa sana ukiikumbuka siku siku hiyo.

REQUESTS FOR UNESCO GRANTS, SCHOLARSHIPS AND OFFICIAL MISSIONS REQUIRE ENDORSEMENT FROM NATIONAL COMMISSIONS OR PERMANENT DELEGATIONS

 



UNESCO operates through its established cooperation bodies in the Member States and has established procedures governing requests for grants, scholarships, patronage, and official missions. *As stipulated in UNESCO’s legal and institutional framework, external requests are generally not accepted unless they are formally endorsed by the relevant National Commission for UNESCO or the Permanent Delegation to UNESCO.*


All ministries, organizations, institutions, researchers, civil society organizations, and individuals seeking UNESCO support are therefore required to obtain an official letter of endorsement or support from the appropriate national authorities before submitting their requests.


*Why Endorsement is Required*

*Verification and Alignment*

Official endorsement confirms that the proposed project, mission, or activity is consistent with national development priorities and UNESCO’s mandate in the fields of education, science, culture, communication, and information.


*Decentralized Cooperation*

UNESCO works primarily through its Member States. *National Commissions for UNESCO serve as the principal link between UNESCO and national stakeholders, ensuring that initiatives are coordinated and aligned with national objectives.*


*Quality Assurance*

The endorsement process helps ensure that proposals meet the required standards of technical quality, international relevance, accountability, and financial transparency before they are considered by UNESCO Headquarters in Paris.


*Official Missions and Invitations*

UNESCO missions typically require an official invitation from the State Party concerned. *Such invitations are coordinated, supported, or endorsed through the country’s National Commission for UNESCO and, where necessary, its Permanent Delegation to UNESCO.*


*UNESCO does not process requests for official missions, patronage, or related activities that lack formal endorsement from these authorized entities.* This requirement is strictly enforced to ensure proper coordination and compliance with UNESCO procedures.


*Why This Policy Exists*

*Sovereignty and National Oversight*

National Commissions act as the constitutional bridge between UNESCO and Member States. They help ensure that international initiatives are consistent with national policies, priorities, and regulatory frameworks.


*Coordination and Efficiency*

The endorsement mechanism prevents duplication of activities, promotes effective collaboration among stakeholders, and ensures that national authorities are fully informed of international projects and missions conducted within their territories.


*Who Should Be Contacted?*

Applicants seeking UNESCO support should first engage with the relevant authorities in the country where the activity will take place.


*National Commissions for UNESCO*

National Commissions serve as the primary in-country partners for UNESCO-related initiatives and provide guidance on national procedures, priorities, and endorsement requirements.


*Permanent Delegations to UNESCO*

Permanent Delegations, based at UNESCO Headquarters in Paris, represent Member States within UNESCO’s governing bodies and facilitate official diplomatic communication with the Organization.


*Responsibilities of Permanent Delegations to UNESCO*

Permanent Delegations serve as the official diplomatic representatives of Member States to UNESCO.


*Their responsibilities include:*


· Acting as the primary diplomatic channel between UNESCO and the Member State.


· Representing the State Party at the UNESCO General Conference, Executive Board, and other intergovernmental meetings.


· Facilitating high-level diplomatic communications, invitations, and official arrangements concerning UNESCO missions and activities.


*Responsibilities of National Commissions for UNESCO*

National Commissions are national cooperating bodies established by Member States to strengthen UNESCO’s work at the country level.


*Their responsibilities include:*


· Promoting collaboration among ministries, universities, research institutions, civil society organizations, and other stakeholders.


· Coordinating UNESCO-related activities within the country.


· Providing for coordination, logistical and technical support for UNESCO missions, experts, evaluators, and field activities.


· Advising governments on UNESCO programmes and facilitating the implementation of UNESCO projects and initiatives.


*Reference Documents*

For further information, please consult the following UNESCO and partner resources:


*UNESCO Legal and Institutional Framework:* https://unesdoc.unesco.org/ark:/48223/pf0000374460

*Architecture of National Commissions for UNESCO:* https://unesco.org.uk/site/assets/files/2999/architecture_of_national_commissions_for_unesco_2022.pdf


*Guidance on Approaching UNESCO:* https://www.fiva.org/storage/Unesco%20and%20FIVA/approaching-UNESCO_compressed.pdf?v20260129215505


*Conclusion*

Organizations and individuals seeking UNESCO grants, scholarships, patronage, partnerships, or official missions should ensure that their requests are submitted through the appropriate national mechanisms. 


*Obtaining endorsement from the relevant National Commission for UNESCO or Permanent Delegation to UNESCO is not merely a procedural requirement; it is an essential component of UNESCO’s governance framework that promotes accountability, coordination, quality assurance, and alignment with national and international priorities.*

DKT. KIJAJI AIPONGEZA UN TOURISM, NA KUAIHIDI TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUKUZA UTALII ENDELEVU



WAZIRI wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amelipongeza Shirika Maalum la Utalii la Umoja wa Mataifa  (UN Tourism) kwa kuendelea kusimamia na kuratibu masuala ya utalii duniani, na kuahidi kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kikamilifu na shirika hilo katika kuendeleza na kuimarisha Sekta ya Utalii kimataifa.

Akizungumza katika Mkutano wa 126 wa Baraza Tendaji la UN Tourism, Dkt. Kijaji ametumia fursa hiyo kulipongeza shirika hilo na uongozi wake, akisisitiza kuwa Dira ya Usimamizi wa Shirika ya Mwaka 2026–2029 imeonesha uongozi thabiti na mwelekeo wa wazi katika kutekeleza ajenda ya maendeleo ya utalii duniani.

Aidha, amelipongeza shirika hilo kwa kuendelea kuziunga mkono nchi wanachama, ikiwemo Tanzania, katika juhudi za kukuza utalii endelevu huku akifafanua kuwa Programu ya Maendeleo na Uendelezaji wa Utalii, ikiwemo Mpango wa Kuendeleza Utalii Vijijini, imeleta matokeo chanya kwa kuboresha maisha ya wananchi, kuunda fursa za kiuchumi na kuinua ustawi wa jamii.

Mathalan, amesema mipango hiyo imeonesha dhahiri nguvu ya utalii kama kichocheo cha maendeleo jumuishi na endelevu, hususan kwa jamii zinazozunguka maeneo ya vivutio vya utalii.

Kwa msisitizo, Dkt. Kijaji amesema Tanzania itaendelea kufanya kazi kwa karibu na UN Tourism  na nchi wanachama ili kukuza Sekta ya Utalii  imara ili ichangie kikamilifu katika ukuaji wa uchumi, uhifadhi wa mazingira na ustawi wa jamii.

Sambamba na hilo, amebainisha kuwa Tanzania iko tayari kuimarisha zaidi ushirikiano na shirika hilo ili kuhakikisha malengo ya kukuza na kuboresha Sekta ya Utalii yanafikiwa kwa ufanisi.

Kuhusu utekelezaji wa Mpango Kazi Mkuu wa shirika hilo unaohusu mabadiliko ya tabianchi, Dkt. Kijaji amebainisha kuwa Serikali itaendelea kuimarisha ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya utalii wa wanyamapori na fukwe kwa kuzingatia usimamizi endelevu na kuchukua hatua madhubuti za kukabiliana na athari hizo.

Ameongeza kuwa kuimarisha ustahimilivu wa maeneo ya utalii ni muhimu katika kulinda ajira na kipato cha wananchi, kuhifadhi bainowai na kuhakikisha uendelevu wa muda mrefu wa sekta hiyo, ambayo ni mhimili muhimu wa uchumi wa Taifa.











BODI YA WADHAMINI TANAPA YAKABIDHIWA TUZO ZILIZOIWEZESHA TANAPA KUNG’ARA KITAIFA NA KIMATAIFA



Kamishna wa Uhifadhi TANAPA, CPA Musa Nassoro Kuji amekabidhi kwa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA Tuzo ya Mafanikio katika Utoaji wa Huduma bora Mwaka 2026 (Quality Achievement Award 2026) pamoja na Cheti cha Ushindi wa Pili (First Runner-Up) katika Tuzo za Ubora wa Taifa 2025/2026 kwenye kikao cha bodi hiyo, Juni 11, 2026 jijini Dar es salaam.

Tuzo ya “Quality Achievement Award 2026” ilitolewa tarehe 31 Mei 2026 jijini Brussels, Ubelgiji na Taasisi ya “European Society for Quality Research (ESQR)” huku Cheti cha Ushindi katika Tuzo za Ubora wa Taifa 2025/2026 kilitolewa na Shirika la Viwango Tanzania kwa kutambua taasisi zinazofanya vizuri katika utoaji wa huduma na kuzingatia viwango vya ubora, kilitolewa juni 05, 2026 jijini Dar es salaam.

Bodi ya Wadhamini TANAPA inayoongozwa na Mwenyekiti wake  Jenerali George Waitara, Mkuu wa Majeshi Mstaafu, imepokea tuzo hizo na kuipongeza Menejimenti ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, Maafisa na Askari Uhifadhi kwa kuendelea kutambulika kimataifa na kitaifa katika kusimamia utekelezaji wa majukumu ya TANAPA ya uhifadhi na maendeleo ya utalii nchini. 

Vilevile, Bodi ya Wadhamini imetoa wito kwa watumishi wote wa Shirika kuhakikisha kuwa kila mmoja anatimiza wajibu wake kikamilifu ili kuendelea kufanikisha malengo ya Shirika na Taifa kwa ujumla pamoja na kupata tuzo nyingi zaidi.








Thursday, June 11, 2026

MAISHA YA SHABANI YOHANA WANTED NCHINI BOTSWANA

 


Kwa mujibu wa simulizi la Frankata Thekiso, safari ya mwanamuziki Shabaan Yohana nchini Botswana ilianza miaka ya 1990, huenda kati ya 1996 au 1997, alipowasili huko kwa msaada wa Mtanzania mwenzake Nathaniel Mwamboma, maarufu kama Naya Capricorn. 

Wakati huo Nata alikuwa akiongoza bendi ya Dar es Salaam Stars, iliyokuwa na makao yake katika ukumbi wa Sethegetsane, eneo la Mmopane, magharibi mwa jiji la Gaborone.

Katika kipindi hicho, Dar es Salaam Stars ilikuwa miongoni mwa bendi zilizokuwa zikifanya vizuri Botswana, huku ushindani wao mkubwa ukiwa bendi ya rumba iliyojulikana kama MOS & LED Sounds. 

Shabaan Yohana alipojiunga na Dar es Salaam Stars, walirekodi santuri iliyoitwa Bula Maitho, iliyowafanya wajulikane zaidi katika medani ya muziki wa dansi nchini humo.

Hata hivyo, baada ya takribani mwaka mmoja, Dar es Salaam Stars ilisambaratika. 

Shabaan hakukata tamaa. Badala yake, aliungana na wanamuziki wengine akiwemo Charlie, Evans Ngalube kutoka Zambia, na Mtanzania Ali Baba Kilunga kuanzisha kundi jipya lililoitwa Sakaye King. Kundi hilo lilikuwa likitumbuiza katika ukumbi maarufu wa Zebra Night Club, magharibi mwa Gaborone.

Ni katika kipindi hicho ndipo walipotoa santuri iliyotikisa sana yenye jina John O Nyala (yaani John Anaoa). 

Wimbo huo ulipata umaarufu mkubwa na kuvutia mashabiki wengi, huku nakala zake zikiuzwa kwa wingi. 

Umaarufu wa Sakaye King uliendelea kukua, lakini baadaye Shabaan akaondoka na kujiunga na mwanamuziki mkongwe wa Botswana Frank Franco Lesokwane, pamoja na Mtanzania mwingine aliyejulikana kama Makambi.

Ushirikiano huo ulipelekea kuanzishwa kwa bendi ya Franco Afro Musica, ambayo ilikuja kuwa moja ya bendi maarufu zaidi Botswana. 

Ndani ya bendi hiyo, Shabaan alikuwa mpiga gitaa la solo. 

Umaarufu mkubwa ulipatikana kupitia kibao cha Ke Lela Le Lona, ambacho kilivuka mipaka ya Botswana na kusikika katika nchi jirani. 

Baadaye walitoa nyimbo nyingine zilizopendwa kama Ba Ntolela Me Tshela na Robala Nana.

Mwaka 2004, Shabaan alihamia Selibe Phikwe na kujiunga na bendi ya Rainbow Sounds, ambako alitumikia kwa takribani miaka minne. 

Hata hivyo, alirejea tena Afro Musica na kuendelea kuitumikia hadi mwaka 2008. 

Wakati huo, mwaka 2005, Afro Musica ilimsajili mpiga solo mwingine kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo aliyejulikana kwa jina la Samurai Ngingo, ambaye alifanya kazi bega kwa bega na Shabaan.

Mbali na Afro Musica, mwaka 2006 Shabaan alifanya kazi pia na Extra Melody Band, bendi iliyokuwa imejitenga kutoka Afrika Sound na iliyokuwa na makao yake Mogoditshane.

Mwaka 2015 alipata changamoto ya kiafya, lakini baada ya kupona alirejea tena jukwaani na kujiunga na kundi la More Fire, ambalo lilitoa albamu ya Me Boela. 

Katika miaka yake ya mwisho, aliendelea kuwa mwanamuziki wa More Fire huku akijihusisha pia na muziki wa injili.

Wale waliomfahamu wanamkumbuka Shabaan Yohana si tu kwa umahiri wake wa kupiga gitaa la solo, bali pia kwa utu wake wa kipekee. 

@Alikuwa mtu mpole, mwenye heshima na aliyependwa na wengi ndani na nje ya tasnia ya muziki. Safari yake ya muziki nchini Botswana imeacha alama kubwa na inabaki kuwa sehemu muhimu ya historia ya wanamuziki wa Kitanzania waliovuka mipaka na kutamba katika ukanda wa Kusini mwa Afrika.



WAGONJWA 12 WAFANYIWA UPASUAJI WA TEZI DUME KWA NJIA YA TUNDU DOGO MUHIMBILI



Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imefanikisha upasuaji wa saratani ya tezi dume kwa njia ya matundu madogo (Laparoscopic Radical Prostatectomy), teknolojia ya kisasa inayomwezesha mgonjwa kupata nafuu kwa haraka, kupunguza muda wa kulazwa hospitalini na kurejea kwenye shughuli zake za kawaida mapema.

Akizungumza baada ya kufanyika kwa upasuaji huo, Bingwa wa Magonjwa ya Mfumo wa Mkojo wa MNH, Dkt. Gift Daniel amesema mafanikio hayo yamepatikana kupitia kambi maalum ya siku mbili ya upasuaji na mafunzo kwa vitendo iliyowakutanisha wataalam wa mfumo wa mkojo kutoka nchi mbalimbali kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuimarisha huduma za kibingwa.

“Katika kambi hii tumefanyia wagonjwa 12 upasuaji wa changamoto mbalimbali za mfumo wa mkojo, ikiwemo saratani ya tezi dume, saratani ya figo, saratani ya kibofu cha mkojo, uvimbe wa maji kwenye figo (renal cyst) pamoja na huduma nyingine za kibingwa. Mafanikio haya yanaonesha uwezo wa wataalamu wetu kutumia teknolojia za kisasa katika kutoa huduma za ubingwa bobezi,” amesema Dkt. Gift.

Kambi hiyo imewakutanisha wataalamu kutoka Tanzania, China, Cameroon, DRC na Uganda, huku zaidi ya wataalamu wazawa 200 wakifuatilia upasuaji huo mubashara kwa njia ya mtandao, hatua iliyowezesha kubadilishana uzoefu na kueneza matumizi ya teknolojia za kisasa ya upasuaji wa mfumo wa mkojo katika hospitali mbalimbali vya afya.