ANGALIA LIVE NEWS

Monday, August 17, 2026

MASHINDANO YA NGALAWA YANOGESHA MSIMU WA PILI WA FuToPiA ZANZIBAR 2026



ZANZIBAR - Ngalawa ya "Baba Karudi" iliyoongozwa na Hassan Thajo imeibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya mbio za ngalawa yaliyofanyika Bahari ya Fumba.

Mashindano hayo yalishuhudia ushindani mkubwa kutoka kwa ngalawa 12 na ni sehemu ya program ya michezo ya asili katika msimu wa pili wa tamasha la FuToPiA Zanzibar lililofanyika tarehe 8-9 Agosti, 2026.

Katika mbio hizo, Ngalawa ya "Wape Kazi" iliyoongozwa na Nahodha Aboubakari Kondo ilishika nafasi ya pili, huku nafasi ya tatu ikinyakuliwa na Ngalawa ya "Utoto Raha" iliyoongozwa na Nahodha Hussein Thajo.

Akizungumza baada ya mashindano, Mratibu wa Michezo ya Asili wa FuToPiA Zanzibar, Joseph Klanda amesema mashindano hayo yanalenga kuwakaribisha wananchi wa maeneo ya Nyamanzi, Dimani na Fumba Town kujumuika na kufurahia tamasha hilo pamoja.

"Chombo cha 'Baba Karudi' washindi wa kwanza kilipewa nguvu na kampuni ya Fortitude Security. Chombo cha 'Wape Kazi' mshindi wa pili kilipeperusha bendera ya FuToPiA Zanzibar, na chombo cha mshindi wa tatu kilipeperusha bendera ya Clouds Media," amesema Klanda.

Aidha, amesema washindi wote kuanzia nafasi ya kwanza hadi ya 12 walipata zawadi ya fedha taslimu pamoja na shukrani za ushiriki.












TANAPA, GERMANY AGENCIES EXECUTE SH 19 BN COMMUNITY DEVELOPMENT PROJECTS AS THEY SEEK TO BALANCE CONSERVATION AND LIVELIHOOD IN NGORONGORO



By Edmund Salaho, Loliondo–Ngorongoro 


Aug. 17, 2026. Tanzania National Parks (TANAPA), in partnership with Germany’s development agencies, is implementing community development and conservation projects worth about 6.3 million euros ($7.4 million), equivalent to roughly Sh19 billion, in Ngorongoro District, Arusha Region. 

The programme seeks to improve community livelihoods and public services while strengthening conservation of the wider Serengeti ecosystem. 

It is being implemented under the Serengeti Ecosystem Development and Conservation Project (SEDCP), financed by the German government through KfW Development Bank, with support from the Frankfurt Zoological Society (FZS).

During Monday’s inauguration of the Enguserosambu Dispensary, representatives of Germany’s Federal Ministry for Economic Cooperation and Development (BMZ), KfW and other partners witnessed the handover of the facility. 

The state-of-the-art dispensary, located in Enguserosambu Ward, was constructed at a cost of Sh504 million (180,000 euros) and will serve about 5,000 people. 

Nuhu Daniel Massay, TANAPA Assistant Conservation Commissioner–National Parks Development, who also coordinates donor-funded projects, investments and parks planning, said the interventions demonstrate the importance of linking conservation with the wellbeing of communities living alongside protected areas. 

“Conservation cannot be separated from the livelihoods and wellbeing of communities. These investments demonstrate that protecting wildlife and ecosystems must go hand in hand with improving the lives of people living around protected areas,” Massay said. 

He added that better access to education, healthcare, water, markets and sustainable livelihoods could make communities stronger partners in protecting natural resources. 

Joachim Schmitt, Head of Delegation, said he was impressed by the scale and impact of the projects, adding that “the best is yet to come,” while commending Tanzania-Germany cooperation for showing how conservation and community development can reinforce each other.

Across the Serengeti ecosystem, SEDCP has supported 69 social infrastructure projects in Serengeti and Ngorongoro districts. 

These include 14 dispensaries, 16 classrooms, 23 houses for teachers and health workers, one dining hall, one dormitory, six feeder roads and eight charco dams. 

In Ngorongoro District, 36 community development projects have been implemented, with 15 completed and handed over to communities and 21 at various final stages. 

The projects include 11 classrooms, a dining hall, seven dispensaries, 10 houses for teachers and health workers, four feeder roads covering 46 kilometres and three charco dams.

The programme is also supporting livelihoods and sustainable land management through FZS. According to district officials, 23 Community Conservation Banks (COCOBAs) have provided self-employment and income-generating opportunities to 835 people—444 women and 391 men. 

SEDCP has additionally supported village land-use planning, issuance of Certificates of Customary Rights of Occupancy (CCROs) and community-based protection of forests and grazing areas in Serengeti, Ngorongoro, Bariadi, Bunda and Tarime districts. 

Ngorongoro District Administrative Secretary Hamza Hamza said the projects had improved access to education, healthcare and water while strengthening the relationship between conservation and community development. 

“These investments are not merely infrastructure. They have made a real difference in the lives of our people,” Hamza said, adding that communities were becoming more involved in protecting forests, grazing areas and other natural resources.

The German-backed programme is also designed to diversify household livelihoods and reduce pressure on natural resources. 

During Monday’s field visit, the BMZ and KfW delegation inspected the Charco Dam at Olorien Village, where officials explained its benefits to communities and livestock. 

The dam cost Sh1.1 billion (363,363.16 euros) and is located in Olorien Village/Magaiduru Ward, benefiting communities in Olorien and Magaiduru villages. 

It serves a population of 5,011 people and 109,838 livestock, including cows, goats, sheep and donkeys. 

TANAPA is the client, with the Ngorongoro District Executive Director, ward and village leaders, Rural Water Supply and Sanitation Agency (RUWASA) and the District commissioner, among key stakeholders.

The delegation later travelled to Lopolum village, where Maasai community members presented aspects of their traditional way of life and discussed the benefits and challenges of the programme. 

COCOBA groups demonstrated their savings and income-generating activities, while members of the Enguserosambu Forest Trust and village forest scouts explained their work protecting the community forest. 

The partnership brings together TANAPA, BMZ, KfW, the German Embassy, FZS and Tanzanian government authorities. 

Massay said TANAPA would continue working with development partners and local authorities to ensure projects are completed to the required standards and maintained for lasting benefits. 

He said the programme demonstrates the value of Tanzania-Germany cooperation in linking conservation with the socio-economic development of communities living near protected areas.












WAZIRI SORAGA: FuToPiA ZANZIBAR NI JUKWAA LA KUONGEZA UBUNIFU NA KUKUZA UCHUMI WA KIDIJITALI

  


Na: Mwandishi Wetu, Zanzibar


ZANZIBAR - Waziri wa Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga amepongeza tamasha la FuToPiA Zanzibar kwa kuanzisha jukwaa la ubunifu linalowezesha wadau mbalimbali kutoa mawazo juu ya ukuaji wa uchumi, masuala ya kidijitali na masoko.

Soraga amesema hayo katika jukwaa maalum la ubunifu wakati wa msimu wa pili wa tamasha la Muziki, Utamaduni na Ubunifu la FuToPiA Zanzibar, lililofanyika Fumba Town, Unguja tarehe 8 na 9 Agosti, 2026.

Katika jukwaa hilo, Soraga ameshiriki majadiliano maalum kuelezea mikakati ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, SMZ katika safari ya mageuzi ya kidijitali katika visiwa vya Zanzibar.

Amesema Zanzibar kwa sasa inapitia vipindi tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma kama kisiwa. Uchumi unakua kwa haraka na kila pembe kuna fursa za kiuchumi zinazojitokeza ikiwemo miradi ya maendeleo.

Aidha, amesema wao kama viongozi wa Serikali wanapongeza wadau kuja na majukwaa ya ubunifu kwani yanaisaidia Serikali kufikia malengo yake kwa ushirikiano na wadau.

"Kupitia majukwaa kama haya ya tamasha la FuToPiA Zanzibar, tunapata fursa ya kuelezea harakati na vipaombele vya Serikali tunavyotarajia kuvifanyia kazi kwa wananchi," amesema Soraga.

Ameeleza kuwa Serikali ya SMZ ina mipango ya kuweka miundombinu ya TEHAMA na mawasiliano ili wananchi wote waweze kuunganishwa na mtandao. Hii ni pamoja na kuweka mtandao wa wazi 'Public Wi-Fi' Zanzibar nzima.

Pia amesema Serikali imejipanga kuboresha mifumo ya ulinzi ili kulinda udukuzi wa taarifa katika mitandao ya simu, kibenki na huduma nyingine ili zibaki katika hali ya usalama.

Kuhusu ubunifu hususani kwa vijana wa Zanzibar, Soraga amesema Serikali imeweka nguvu kubwa ya kuunda mazingira bora na rafiki kwa vijana kuonesha vipaji vyao ikiwemo ubunifu wa mifumo na huduma za kidijitali. Amesema vijana watapewa nyenzo na maarifa ili waweze kutengeneza mifumo na kutoa masuluhisho mbalimbali.

Ameongeza kuwa Serikali ipo katika mpango wa kuboresha miundombinu ya msingi ya TEHAMA ikiwemo njia za kimataifa za mtandao wa intaneti 'International Gateway' na kuwa na kituo cha data 'Data Center' cha kuhifadhi taarifa. Amesema Serikali imekusudia kuwekeza zaidi ya dola za Marekani milioni 100 mpaka kukamilika kwa mradi huo.

Katika kuhakikisha huduma zinapatikana kwa urahisi, amesema watafanya kazi ya kuunganisha mifumo ndani ya Serikali hasa ya utoaji wa huduma ili kumsaidia mwananchi.

Kuhusu matumizi ya fedha taslimu, amesema dunia ya sasa inatakiwa kuachana na matumizi ya fedha taslimu na kuelekea kwenye matumizi ya mifumo ya fedha kupitia mitandao.

"Nichukue fursa hii kumpongeza na kumshukuru Rais wetu Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa utashi wake mkubwa na muelekeo alioutoa wa kuona Zanzibar ifikapo 2030 suala zima la matumizi ya fedha taslimu liwe historia na kwamba wananchi wote waweze kulipia huduma zao kwa njia ya mtandao, kibenki na kwenye simu," amesema Soraga.

Tamasha la FuToPiA Zanzibar linaandaliwa na Busara Promotions na linajumuisha muziki, sanaa, ubunifu, masoko na michezo.

Wasanii na ma-DJ mbalimbali walioshiriki ni pamoja na DJ Joozey, DJ Zoro, Baba Kash, Sauti Marley, Ruth Mlawa, DJ LAG kutoka Afrika Kusini, Vania Ice, Hammer Q na wengineo.






Thursday, August 13, 2026

MUHIMBILI YATUA MALAWI, YAFANYA KAMBI KUBWA YA UPASUAJI WA MACHO

  



Timu ya wataalamu kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili inashiriki katika kambi maalum ya upasuaji wa macho wa kibingwa na kibingwa bobezi inayofanyika katika Hospitali ya Kamuzu Central (KCH), jijini Lilongwe, Malawi. Ushiriki huo umefanyika kufuatia mwaliko maalum kutoka kwa Rais wa Vision Care, Dkt. Donghae Kim, ambapo timu ya Muhimbili imepata fursa ya kuungana na wataalamu wa Vision Care katika kutoa huduma za matibabu ya macho kwa wananchi wa Malawi.

Vision Care ni shirika la kimataifa lenye makao makuu nchini Korea Kusini, linalojikita katika kupambana na kupunguza tatizo la upofu duniani kupitia huduma za afya ya macho, matibabu na upasuaji. Kupitia ushiriki huo, wataalamu wa Muhimbili wamekuwa sehemu ya timu ya kimataifa inayoshirikiana katika kutoa huduma za kibingwa na kibingwa bobezi kwa wagonjwa wenye changamoto mbalimbali za macho.

Ushiriki wa Muhimbili katika kambi hiyo unaendelea kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya afya, huku ukitoa fursa kwa wataalamu wa Tanzania kushirikiana na wenzao kutoka mataifa mbalimbali katika kuboresha huduma za macho. Pia, kambi hiyo inaonesha nafasi ya Muhimbili katika kushiriki juhudi za kimataifa za kupunguza mzigo wa upofu na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za macho kwa wakati.






ISAIAH(ISAYA) YUNKE: MTANZANIA AMBAYE DUNIA ILIMTAMBUA, LAKINI NCHI YAKE IKAMSAHAU

Mohamed Matope

Ilikuwa ni video ya harusi iliyonipeleka kwenye story ya maisha ambayo sikuitarajia kabisa. Jumamosi nilitumiwa video za sherehe ya harusi ya Sharlene Ruto huko Kilgori, iliyofanyika katika ranchi ya Rais William Ruto. Pamoja na video hiyo kulikuwa na caption fupi iliyosema: “Mtanzania achumbia binti wa Ruto.” Kwa udadisi, nilianza kutafuta jina la Mtanzania huyo. Nilichotarajia kukutana nacho ni story ya kijana Mtanzania ambaye kwa namna fulani amejikuta akiingia katika familia moja ya kisiasa yenye nguvu zaidi nchini Kenya. Lakini nilichokutana nacho kilikuwa kikubwa zaidi.

Kiu changu cha kumuelewa vizuri huyu kijana kikaongezeka wakati wa sherehe hiyo, Rais William Ruto alimuelezea Isaiah kama kijana jasiri na mstahimilivu, ambaye aliweza kupenya na kujenga uhusiano ndani ya familia yenye watu mashuhuri, hadhi kubwa na ulinzi mkali, hadi kufikia hatua ya kumchumbia binti yake. Kauli hiyo ilinifanya nijiulize zaidi: Huyu kijana ni nani? Kadiri nilivyozidi kutafuta na kujifunza kuhusu maisha yake, ndivyo nilivyozidi kugundua kwamba nyuma ya yule kijana aliyekuwa akitajwa kwenye story ya harusi kulikuwa na historia ya maisha ambayo, kwa maoni yangu, ilipaswa kujulikana zaidi Tanzania.

Isaiah hakuzaliwa katika mazingira ya upendeleo. Alizaliwa na baadaye kutelekezwa na wazazi wake, akaenda kuishi na bibi yake kijijini Mwanza, katika mazingira ambayo umasikini haukuwa neno tu bali ulikuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Hakukua katika mazingira ambayo yangempa mtu sababu ya kuamini kwamba siku moja angekuwa mhitimu wa chuo kikuu au kijana anayetambuliwa kimataifa. Alikuwa mchungaji wa mifugo na hata alianza shule akiwa na umri mkubwa. Kwa mtoto anayekulia katika mazingira kama hayo, maisha yanaweza kuonekana tayari yameamua hatima yake. Lakini kwa Isaiah, haikuwa mwisho wa safari. Alikuwa na kitu ambacho hata umasikini haukuweza kumpokonya: azma, uthubutu na ubunifu.

Wednesday, August 12, 2026

RAIS MWINYI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA MALIASILI KWENYE TAMASHA LA KIZIMKAZI

  


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar


Rais wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye ni mgeni rasmi katika ufunguzi wa Tamasha la Kizimkazi, ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii lililopo katika viwanja vya tamasha hilo, Kizimkazi, Zanzibar.

Mhe. Mwinyi amefanya ziara hiyo mapema leo, Agosti 12, 2026, mara baada ya kufungua rasmi tamasha hilo linalofanyika kwa siku tatu, kuanzia Agosti 12 hadi 14, 2026.

Katika ziara hiyo, Rais Mwinyi alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, pamoja na huduma na fursa zinazotokana na sekta ya maliasili na utalii.

Tamasha hilo linahusisha uzinduzi wa miradi ya maendeleo, maonyesho ya biashara, michezo, pamoja na shughuli za kutangaza utamaduni, utalii na fursa za uwekezaji.

Tamasha la Kizimkazi mwaka huu limebeba kauli mbiu isemayo “Kizimkazi Kumenoga.”





Tuesday, August 11, 2026

LEONARD RWIZANDEKWE VS MWL. JULIUS NYERERE URAIS NDANI YA TANU


Mzee Leonard Rwizandekwe aliwashangaza watanzania mwaka 1965 kwa kukiomba chama cha TANU kimpendekeza kwa wananchi awe mgombea pekee wa urais badala ya Mwalimu Nyerere, akiwa kijiji kwake Katendaguro Wilaya ya Misenye Mkoa wa Kagera alipofanyiwa mahojiano na Elisa Muhingo na Mathias Byabato, Bukoba, anasema wakati huo ilikuwa ni nadra na vigumu mtu yoyote kutaka kugombea nafasi hiyo kwa kuwa wananchi wengi walidhani kuwa hapakuwepo mtu mwingine zaidi ya Mwalimu Nyerere ambaye angeweza kuwa Rais wa nchi.

Alizaliwa tarehe 14 juni mwaka 1929 katika kijiji cha Katendaguro na kusoma shule ya msingi ya Rukurungo na baadae alipelekwa katika jumba la Mugorola lililokuwa Bunge la jadi ambapo hapo alikaa humo akilelewa na wazee ikiwa ni pamoja na kufundishwa maadili, utii, na uwajibikaji.

Mwaka 1948 alichaguliwa kujiunga na shule ya Serikali Ihungo iliyopo Bukoba kwa masomo ya Sekondari ambapo baada ya kuhitimu aliajiriwa katika idara ya mahesabu katika Wilaya ya Buhaya .

Rwizandekwe aliamua kujisomea mwenyewe masomo ya sheria na alipofanya mtihani wa Chuo cha Kibete cha nchini Uganda alifaulu vizuri na baada ya kupata cheti aliajiriwa katika sekta mbalimbali serikalini ambapo juni 1 mwaka 1959 aliteuliwa kuwa Hakimu wa Mahakama ya Rufaa ya Buhaya.

Mwaka 1960 alichaguliwa kama mtumishi bora kutoka Halmashauri ya Buhaya kwenda kuhudhuria semina ya sheria za Afrika nchini Uganda ambapo kupitia huko alichaguliwa pia kuhudhuria masomo ya shahada ya sheria za mila za Afrika katika Chuo Kikuu cha London nchini Uingereza.

Aliporudi nchini mwaka 1963 alikuwa Msomi mzuri tu na kwaajili hiyo aliajiriwa kama Mkurugenzi msaidizi wa Halmashauri ya Buhaya ambapo baada ya muda mfupi Mwalimu Nyerere alimuhamishia Makao Makuu ya Wizara ya sheria alipoajiriwa kama mshauri mkuu wa sheria za mila za Serikali.

Rwizandekwe ,wazo la kugombea nafasi ya urais lilimjia mwaka 1965 baada ya kubaini kuwa mambo ambayo alikuwa amekubaliana na Mwalimu kuwa angeyafanya baada ya kupata Uhuru yote yalikuwa hayakufanyika.

Monday, August 10, 2026

MUHIMBILI YAWEKA HISTORIA, YAFANIKISHA UPASUAJI WA KWANZA WA KUTENGANISHA MAPACHA WALIOUNGANA AINA YA PARASITIC CONJOINED TWINS

 

 

Madaktari bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo, Agosti 10, 2026, wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kwanza wa kutenganisha mapacha walioungana aina ya parasitic conjoined twins, ambapo mmoja wa mapacha hakukua kikamilifu na alikuwa akimtegemea mwenzake kwa ukuaji na uhai.

Akizungumza mara baada ya upasuaji huo, Dkt. Victor Ngotta, Bingwa wa Upasuaji wa Watoto wa MNH, amesema mafanikio hayo yanaonyesha uwezo wa hospitali kushughulikia kesi ngumu na adimu zinazohitaji utaalamu wa hali ya juu, na ni hatua muhimu katika kuendelea kuimarisha huduma za upasuaji wa kibingwa nchini.

Dkt. Ngotta amesema upasuaji huo ulihitaji maandalizi ya kina na ushirikiano wa wataalamu kutoka fani mbalimbali kutokana na hali ya kipekee ya mtoto huyo, ambaye alikuwa na pacha aliyekuwa na mikono, miguu na sehemu ya kiuno pekee huku akimtegemea mwili wa mwenzake kwa ukuaji na uhai.

Mafanikio ya upasuaji huo yanaendelea kuimarisha nafasi ya Hospitali ya Taifa Muhimbili kama kituo kinachoongoza nchini katika utoaji wa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi. Mtoto anaendelea vizuri na yupo chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.








  



RAIS DKT. MWINYI: KAMERA ZA USALAMA BARABARANI KUDHIBITI AJALI ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali imeanza kuweka mfumo wa kamera za usalama barabarani ili kuimarisha utii wa sheria, kurejesha nidhamu na kudhibiti ajali zinazotokana na ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 10 Agosti 2026, alipokutana na Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Kusimamia Viongozi Wakuu wa Kitaifa, iliyoongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Machano Othman Said, Ikulu Zanzibar.

Amesema utekelezaji wa mfumo huo umeanza katika Mkoa wa Mjini Magharibi na utaendelea kuimarishwa na kupanuliwa katika maeneo mbalimbali ya mijini na vijijini, kwa lengo la kuongeza usalama wa madereva, waendesha vyombo vya usafiri pamoja na watembea kwa miguu.

Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuimarisha vituo vya mafunzo ya amali na kufanya mageuzi katika elimu ya ufundi ili kuwapatia vijana ujuzi na maarifa yatakayowawezesha kujiajiri, kuajiriwa na kuwa na ushindani katika soko la ajira.

Kuhusu kupanda kwa bei za bidhaa, amesema Serikali inaendelea kuweka bei elekezi na kusimamia utekelezaji wake, huku akiwataka wafanyabiashara kuzingatia viwango vilivyowekwa kwa lengo la kulinda maslahi ya wananchi na kupunguza gharama za maisha.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amewataka wakandarasi na wasimamizi wa ujenzi kuhakikisha mahitaji ya watu wenye ulemavu yanazingatiwa katika majengo ya umma na binafsi, ili kuwawezesha kupata huduma kwa urahisi na bila vikwazo.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Machano Othman Said, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa maono na utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo, na kueleza kuwa Kamati itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuimarisha maendeleo na kukuza uchumi wa Zanzibar.













Thursday, August 6, 2026

TFS YAANDIKA HISTORIA KWA KUSHIRIKI MAONESHO YA KILIMO ZANZIBAR KWA MARA YA KWANZA, YAPOKELEWA KWA KISHINDO

  



Na Mwandishi Wetu, Dole Kizimbani, Zanzibar

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeandika historia kwa kushiriki kwa mara ya kwanza Maonesho ya Kilimo Zanzibar, hatua iliyopokelewa kwa pongezi na viongozi pamoja na wananchi kutokana na kupeleka elimu na fursa za kiuchumi zinazotokana na uhifadhi wa misitu na nyuki visiwani humo.

Mafanikio hayo yalidhihirika Agosti 5, 2026, baada ya Waziri wa Katiba na Sheria Zanzibar, Haroun Ally Suleiman, kutembelea banda la TFS katika Viwanja vya Dole, Kizimbani na kupongeza uamuzi wa wakala huo kuvuka bahari na kuwaletea Wazanzibari huduma za elimu ya uhifadhi pamoja na fursa za uwekezaji.

    "Niwapongeze sana TFS kwa kuona umuhimu wa kutangaza fursa za uhifadhi hapa Zanzibar. Ni hatua nzuri ambayo itawanufaisha wananchi kwa kuwawezesha kuibua vyanzo vipya vya mapato kupitia uhifadhi wa misitu," alisema Waziri Haroun.

Alisema ushiriki wa TFS katika maonesho hayo unafungua milango mipya ya ushirikiano kati ya Tanzania Bara na Zanzibar katika kukuza uchumi kupitia matumizi endelevu ya rasilimali za misitu na nyuki, huku akiitaka taasisi hiyo kuendelea kushiriki maonesho na kampeni za uelimishaji visiwani humo.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Francis Kiondo, alisema ushiriki huo wa kwanza Zanzibar ni sehemu ya mkakati wa TFS wa kusogeza huduma karibu na wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuhakikisha fursa za uhifadhi zinawafikia Watanzania bila kujali walipo.

Alisema kupitia maonesho hayo, wananchi wanapata elimu kuhusu uhifadhi wa misitu na nyuki, uzalishaji wa mbegu bora za miti na miche, ufugaji nyuki, fursa za uwekezaji katika sekta ya misitu pamoja na utalii wa ikolojia, ambao unazidi kuwa chanzo muhimu cha ajira na mapato.

Maonesho ya Kilimo Zanzibar yanaendelea katika Viwanja vya Dole, Kizimbani kuanzia Agosti 1 hadi 14, 2026, ambapo TFS imewahimiza wananchi kutembelea banda lake ili kujifunza na kutumia fursa mbalimbali zinazotokana na uhifadhi endelevu wa rasilimali za misitu.

UONI HAFIFU WAONGOZA CHANGAMOTO KWA WANAOPIMA MACHO BANDA LA MUHIMBILI NANE NANE



Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema tatizo la uoni hafifu linaongoza miongoni mwa changamoto zinazobainika kwa wananchi wanaofika kupima afya ya macho katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) yanayoendelea katika viwanja vya Dk. Samweli Malechela, jijini Dodoma, ambapo huduma za uchunguzi wa macho, elimu na ushauri wa kitaalamu zinatolewa bure. 

Akizungumza Dkt. Bingwa wa Magonjwa ya Macho kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Johannes Mafwili, amesema wananchi wengi wanaofika katika banda la hospitali hiyo hupatikana na tatizo la uoni hafifu, huku wakifanyiwa uchunguzi wa kina na kupatiwa ushauri wa kitaalamu kulingana na hali zao. 

Amesema uchunguzi wa mapema husaidia kubaini magonjwa mbalimbali ya macho kabla hayajasababisha madhara makubwa, hivyo amewahimiza wananchi kutumia fursa ya maonesho hayo kupima afya ya macho bila kusubiri dalili kuwa mbaya. 

Dkt. Mafwili amewataka wananchi wanaotembelea Maonesho ya Nane Nane kufika katika banda la Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kunufaika na huduma hizo za bure na kupata elimu itakayowasaidia kulinda afya zao.