ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, July 5, 2026

MBIO ZA BAISKELI ZAKARIBISHA TAMASHA LA SANJO YA BUSIYA 2026

 


Na. Matukio Daima Media App, Kishapu, Shinyanga.


MBIO za Baiskeli za Busiya ziemefanyika Julai 4, 2026  kwa mara ya kwanza katika shamrashamra za kukaribisha tamasha la Sanjo ya Busiya  maarufu kama  Sabasaba (7'7).

Uongozi wa Utemi huo umefanya kwa mara ya kwanza Mbio hizo za Baiskeli kwa lengo la kurejesha utamaduni wa Baiskeli kwa kabila la Wasukuma.

mashindano ya mbio hizo yalianzia eneo la njia panda la Kolandoto hadi  Ikulu ya Busiya  na washiriki walipokelewa na Mtemi wa Busiya Ntemi Makwaia wa iii pamoja na Machifu wengine kutoka meeneo mbalimbali.

Awali, Ntemi Makwaia iii akizindua mbio hizo, amebainisha kuwa, utamaduni wa Wasukuma ni pamoja na kuendesha Baiskeli hali ambayo inawapa kuwa na Afya njema kwani utaratibu huo ni Moja ya mazoezi ya mwili na kuweka mwili vyema bila magonjwa.

Tamasha la Sanjo ya Busiya ambalo litazinduliwa rasmi Julai 05 na  hitimisho ni Julai 07 ambapo ngoma mbalimbali kutoka Busiya na nchi jirani zitashiriki sambamba na matukio mengine ikiwemo huduma za afya, ambapo Wananchi watapata nafasi ya kupimwa Afya zao kutoka kwa Watalaam na Madaktari wa Afya Check, pamoja na Hospitali ya jirani.

















Saturday, July 4, 2026

CAPE VERDE LOST THE MATCH TO ARGENTINA, BUT WON THE HEARTS OF THE FOOTBALL WORLD

WAZIRI MKUU MSTAAFU, MHE.KASSIM MAJALIWA ASHIRIKI MBIO ZA MAC D MARATHON2026, APIGA KURA TUZO ZA WTA

 

Mgeni Rasmi katika Mbio za Riadha za MAC D Marathon ambaye pia ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa akipewa maelezo ya jinsi ya kupigia kura wa vivutio vya Tanzania katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kutoka kwa Afisa Utalii Lusajo Nsweve wa TAWA, Julai 4,2026, Kunduchi, Jijini Dar es Salaam.

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa ameshiriki katika Mbio za Riadha za MAC D Marathon zilizofanyika Julai 4, 2026 Kunduchi, Dar es salaam.

Mhe. Majaliwa alikuwa mgeni rasmi katika Mbio hizo zenye lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupitia zenye kaulimbiu ya "Go Green with Gas" na kuunga mkono juhudi za Serikali katika utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi.

Ambapo alipata fursa kuelekezwa jinsi ya kupigia kura vivutio vya Tanzania katika Tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kutoka kwa Afisa Utalii Lusajo Nsweve wa Mamlaka ya usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).

Pia viongozi wengine mbalimbali wameweza kushiriki zoezi hilo,

TAWA imetumia jukwaa hilo kutangaza vivutio vya utalii inavyovisimamia pamoja na kuhamasisha zoezi la upigaji kura wa tuzo za Utalii Duniani (World Travel Awards) kwa Viongozi wa Serikali na washiriki mbalimbali.







MCHECHU: HAKUNA UCHUMI BILA UHIFADHI


Na. Edmund Salaho/Ruaha 


Msajili wa Hazina ambaye pia ni mlezi wa Great Ruaha Marathon na mwakilishi wa Mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba katika mbio hizo Bw. Nehemiah Mchechu amebainisha kuwa uchumi wa Taifa unategemea uhifadhi huku akiongeza kuwa Mto Ruaha Mkuu ni moja ya mito muhimu zaidi nchini unaotoa uhai kwa Hifadhi ya Taifa Ruaha, unaosaidia wananchi katika shughuli za kilimo na mifugo, ikiwa ni pamoja na kuwewezesha uzalishaji wa umeme na kuchangia ustawi wa wananchi nchini.

Mchechu, ameyasema hayo leo Julai 04, 2026 wakati akizindua mbio za kimataifa zinazofanyika katika Hifadhi ya Taifa Ruaha maarufu kama "Great Ruaha Marathon".

Aidha, Mchechu ametoa rai kwa Watanzania kujijengea tabia ya kutembelea Hifadhi za Taifa, kujivunia utanzania na kuwa mabalozi wa nchi yao.

"Tunataka Watanzania wengi zaidi watembelee hifadhi zetu, wajivunie urithi tulionao na wawe mabalozi wa utalii wa nchi yao” alieleza Mchechu.





Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, Massana Gibril Mwishawa amebainisha kuwa utalii wa michezo umekuwa kivutio kikubwa kwa watalii wa ndani na nje na kuelezea kuwa TANAPA imeweka mikakati madhubuti katika zao hilo jipya la utalii.

"Duniani kote, matukio makubwa ya michezo hutumiwa kuongeza idadi ya watalii, kuvutia wawekezaji, kukuza biashara na kuijenga taswira ya nchi kimataifa, TANAPA tumejidhatiti vilivyo kuhakikisha tunavutia watalii wengi kupitia zao hili la utalii wa michezo"

Mratibu wa Great Ruaha Marathon Bw. Hamim Kilahama amesema  "Great Ruaha Marathon si mashindano ya riadha pekee. Ni jukwaa la kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa kulinda mazingira, kuhifadhi vyanzo vya maji vya Mto Ruaha Mkuu, kuendeleza utalii wa Kusini mwa Tanzania. Tunatumia michezo kama chombo cha kuleta mabadiliko chanya katika jamii, ikiwa ni mara ya tano mfululizo Great Ruaha Marathon imefungua ukurasa mpya wakuitangaza Ruaha kupitia utalii wa michezo".

Hifadhi ya Taifa Ruaha ni moja kati ya Hifadhi kubwa barani Afrika. Ni hazina ya kipekee yenye idadi kubwa ya wanyama kama tembo, simba, chui, mbwa mwitu wa porini, twiga, nyati na mamia ya aina za ndege wanaovutia watalii kutoka kila pembe ya dunia.




















Thursday, July 2, 2026

ZANZIBAR SOAP WAJA NA BIDHAA ZA SABUNI ZA ASILI SABASABA

 


Zanzibar Soap ambao ni wauzaji wa bidhaa za Sabuni za urembo zilizotengenezwa kwa kutumia miti ya asili wemesogeza huduma kwa Wananchi katika maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea barabara ya Kilwa Temeke Jijini Dar es salaam.

Kwa mujibu wa Meneja mauzo wa Zanzibar Soap, Bw. Mjaka Sogora amesema bidhaa hizo zimetengenezwa kwa ubora wa hali ya juu huku zikiwa katika aina tofauti kama sabuni za kipande, sabuni za maji, na sabuni za miche.

"Wateja na wadau mbalimbali tunawakaribisha kwenye hema la Serengeti ambalo lipo jirani na hema la NIDA.

Ukifika utaona bango la Zanzibar Soap, lakini pia utaona bidhaa zetu mbalimbali. 

Njoo na pesa kidogo, ujaze kapu, kuna offa ya   pungozo kubwa na  bidhaa zetu wanatumia watu wote, Wanawake kwa Wanaume na watoto pia.



Lakini pia Zanzibar Soap tuna bidhaa tofauti tofauti zenye kutibu, kuponya na kurekebisha yule mwenye;-Chunusi, muwasho mwilini, ngozi iliyofifia na huondoa mabaka baka mwilini, Ewe Mteja Pendezesha mwili wako na ngozi yako kwa kutumia Zanzibar Soap." Amesema Mjaka Sogora.

Baadhi ya sabuni zinazopatikana kwenye banda lao hilo ni pamoja na: Turmeric/Honey Soap, Lemon/Honey Soap, Nuru Soap -Coffee Scrub, Molato, Kojic na Luxury Shea Butter.

Kwa wateja na mawakala,kwa wanaotaka bidhaa hizo za Zanzibar Soap wanaweza wasiliana na Zanzibar Soap waliopo Mtaa wa Tomondo Temeke Pire Dar es salaam, mtandao wa kijamii wa Instagram kwa jina la Zanzibarsoap.