ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, May 22, 2025

PRESIDENT SAMIA SULUHU HASSAN: A LEADER COMMITTED TO JUSTICE AND DEMOCRACY


By Japhari Saidi


Since assuming office in 2021, Her Excellency President Samia Suluhu Hassan has demonstrated exceptional leadership grounded in justice, reconciliation, and democratic values. Her bold and deliberate actions have ushered in a new era of hope and openness for Tanzanians.

When she came into power, political party meetings had been suspended for over six years. Under her leadership, all political parties are now free to organize and hold public gatherings across the country in line with their capacity and rights — a significant step forward for multiparty democracy.

Several opposition leaders who had fled the country due to safety concerns have returned home safely and resumed their political activities without interference or intimidation.

The media environment, once clouded by fear and censorship, has seen a transformation. President Samia reopened previously banned media outlets and promoted freedom of expression. Today, journalists report with increased freedom and transparency.

She also took action to address long-standing legal cases, many of which were seen as politically motivated. Numerous cases, particularly those involving opposition figures, were withdrawn, restoring public trust in the justice system.

In the economic sphere, she lifted restrictions on bank accounts that had been frozen without clear justification, allowing businesspeople to resume their operations and contribute to the economy.

Through these reforms and others, President Samia Suluhu Hassan has proven herself a leader who listens, respects democratic principles, and promotes fairness for all. She is a modern stateswoman fostering development through dialogue, inclusion, and justice.

By Japhari Saidi

Wednesday, May 21, 2025

WATANZANIA TUENDELEE KUMTUNZA MDUDU NYUKI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizundua Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Ufugaji Nyuki kwa Tanzania iliyo Bora katika Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani kwenye viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, Mei 20, 2025. Kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana.
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akikabidhiwa na Waziri wa Maliasilia na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana nakala ya Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Ufugaji Nyuki kwa Tanzania iliyo Bora aliouzindua katika Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani kwenye viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, Mei 20, 2025.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda tuzo ya kutambua mchango wake Kwenye maendeleo ya sekta ya ufugaji nyuki nchini katika Maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani kwenye viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, Mei 20, 2025

MAKAMANDA WA POLISI WAFANYA UKAGUZI WA MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA MTWARA


Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania, CP Awadhi Juma Haji, ameongoza Makamanda wa Polisi wa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara—mikoa inayopitiwa na miundombinu ya gesi asilia na kufanya ziara ya ukaguzi wa miundombinu hiyo inayotoka Msimbati, Madimba hadi Kinyerezi kupitia Somanga.

,Ziara hii ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya GASCO inayosimamiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, CP Awadhi amebainisha kuwa Jeshi la Polisi lina wajibu wa kuhakikisha miundombinu ya gesi asilia inakuwa katika hali ya usalama wa kutosha, kwa kuwa rasilimali hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya polisi CP Awadhi Juma Haji

“Jeshi la Polisi lina makubaliano ya ushirikiano na Kampuni ya GASCO kupitia TPDC kwa ajili ya kutoa ulinzi kwenye miundombinu ya gesi asilia. Ziara hii ni utekelezaji wa takwa la makubaliano hayo, ambapo kila mwaka tunatakiwa kufanya ukaguzi ili kutathmini hali ya kiusalama,” amesema CP Awadhi.

DCEA YATEKETEZA MASHAMBA YA BANGI EKARI 157 KONDOA, WATUHUMIWA 7 WAKAMATWA

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa pamoja na wananchi wa Kata ya Haubi, wamefanikisha operesheni maalum ya kutokomeza kilimo haramu cha bangi katika maeneo ya Hifadhi ya Milima ya Haubi, wilayani Kondoa, mkoani Dodoma.

Akizungumza kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa DCEA, Naibu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali wa mamlaka, Daniel Kasokola, amesema operesheni hiyo iliyofanyika kuanzia Mei 14 hadi 19, imefanikisha uteketezaji wa ekari 157 za mashamba ya bangi yaliyokuwa katika vijiji vya Ntomoko, Kinyasi na Haubi. Aidha, watuhumiwa saba wanashikiliwa kwa mahojiano huku pikipiki mbili zikikamatwa katika maeneo ya operesheni.
“Operesheni hii ni ya pili kufanyika mwaka huu katika wilaya ya Kondoa. Januari tulibaini na kuteketeza zaidi ya ekari 500 za bangi. Kupungua kwa mashamba haya hadi ekari 157 ni ushahidi kuwa wananchi wameanza kuelewa na kushiriki kikamilifu katika jitihada hizi. Tunawapongeza kwa ushirikiano huu.” amesema Kasokola.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Mhe. Fatuma Nyangasa, amesisitiza kuwa serikali ya wilaya itaendelea kushirikiana kwa karibu na DCEA katika kuhakikisha kilimo cha bangi kinatokomezwa kabisa na kusisitiza kuwa elimu kwa wananchi itaendelea kutolewa ili waachane na kilimo hicho haramu na badala yake wajikite katika uzalishaji wa mazao halali ya chakula na biashara kama vile tumbaku, ufuta na maharage.

ECOBANK TANZANIA YAUNGA MKONO MKUTANO WA MWAKA WA USHAURI WA BODI YA USAJILI WA MAKANDARASI (CRB) 2025

 Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega (katikati) akimkabidhi cheti Mkuu wa Kitengo cha Biashara kwa Wateja Wakubwa (Commercial Banking) Joyce Ndyetabura (kushoto) cha udhamini wa Mkutano wa Mwaka wa Ushauri wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) kwa mwaka 2025
Wafanyakazi wa Ecobank Tanzania wakiwa kwenye mkutano wa Mwaka wa Ushauri wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB).

Tuesday, May 20, 2025

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AMKARIBISHA RAIS WA JAMHURI YA NAMIBIA MHE. NETUMBO NANDI-NDAITWAH, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2025.

NYONGO AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA NCHINI UBELIGIJI


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stanslaus Nyongo amewasili nchini Ubeligiji kuongoza ujumbe wa Tanzania katika Kongamano la Bajeti la Umoja wa Ulaya linalofanyika mjini Brussels nchini Ubeligiji kuanzia tarehe 20 hadi 21 Mei, 2025.

Tanzania imealikwa katika kongamano hili kama nchi pekee kutoka Afrika kushiriki katika kongamano hili kutokana na mahusiano mazuri ya muda mrefu na Umoja wa Ulaya.
Katika kongamano hilo ujumbe wa Tanzania utatatoa maoni kuhusu mwelekeo wa vipaumbele vya bajeti ya EU kwa kipindi kijacho hususan katika maeneo yanayogusa maendeleo endelevu, uwekezaji, na ushirikiano wa kimaendeleo na nchi za Afrika.

Mbali na kushiriki katika kongamano hilo, Mhe. Nyongo ataongoza pia ujumbe wa Serikali ya Tanzania katika mkutano wa ngazi ya Mawaziri wa Afrika na Umoja wa Ulaya Mkutano huu muhimu unalenga kujadili masuala ikiwemo ulinzi na usalama, ustawi wa kiuchumi, , ushirikiano wa kimataifa na masuala ya uhamiaji.

WAWILI WAHUKUMIWA MIAKA 20 JELA KWA KUKUTWA NA NYARA YA SERIKALI.


Na John Walter -Babati

Mahakama ya Wilaya ya Babati leo Mei 20, 2025 imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela kwa wanaume wawili waliopatikana na hatia ya kumuua pundamilia na kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria.

Washtakiwa hao ni Ramadhan Hussein Dodi (39) na Mohamed Bakari Chora (30), wakazi wa Kijiji cha Chubi, Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma. Walipatikana na hatia ya kutenda kosa hilo mnamo Oktoba 25, 2024 katika eneo la Chubi lililopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire, Wilaya ya Babati mkoani Manyara.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyosomwa mahakamani, washtakiwa walikamatwa wakiwa na kichwa cha pundamilia, miguu ya pundamilia, mkia mmoja pamoja na ngozi ya mnyama huyo. Nyama ya pundamilia waliokuwa wakimiliki ilikadiriwa kuwa na thamani ya Dola za Kimarekani 1,200, sawa na takribani shilingi milioni 3,204,000 za Kitanzania.

NBAA NA ZIAAT ZASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO KWA MIAKA MINNE


Mgeni rasmi Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil  akishuhudia utiaji saini kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA) CPA Pius Maneno na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wahasibu,  Wakaguzi na Washauri elekezi wa Kodi Zanzibar (ZIAAT) CPA Ame B. Shadhil
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania (NBAA) CPA Pius Maneno (kulia) wakipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wahasibu,  Wakaguzi na Washauri elekezi wa Kodi Zanzibar (ZIAAT) CPA Ame B. Shadhil(kushoto)mara baada ya saini hati ya makubaliano ya kufanya kazi pamoja katika maeneo mbalimbali yanayohusu taaluma ya uhasibu na ukaguzi wa hesabu. 

Monday, May 19, 2025

WANANCHI NJOMBE WAOMBA WIGO WA MIRADI YA KUSAMBAZA UMEME UONGEZWE.


Na mwandishi wetu -Njombe
Wananchi wa vitongoji mbalimbali vya Mkoa wa Njombe wameiomba Serikali kuongeza wigo wa miradi ya kusambaza umeme ili iweze kutekelezwa katika vitongoji vyote.

Wakizungumza katika nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara inayoendelea wakati wa kampeni ya kutoa elimu na kuhamasisha umma kuunganisha umeme katika Mkoa wa Njombe, wananchi hao wameiomba Serikali kuongeza wigo wa miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji ili iweze kuwafikia wananchi wengi zaidi na taasisi nyingi zilizopo katika maeneo yao.
Mikutano hiyo imefanyika katika vijiji vya Ibatu, Usetule, Manga, Kifumbe, Mtulingala, Mbugani na Nyamande, ambapo wananchi wa vitongoji vya Magomati, Mjimwema, Kidete, Mtanga, Ilongo, Kisaula, Matangini, Mvengi B na Nyamande A, wameiomba Serikali kuongeza miradi ya kusambaza umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa.

Aloyce Ng'angalila mkazi wa Kitongoji cha Magomati Kijiji Cha Usetule amesema, "nyumba zilizopitiwa na nguzo za umeme ni chache na ambazo hazijapitiwa na mradi huo wa umeme ni nyingi, naomba REA itusaidie kupata Umeme katika maeneo yaliyobaki".

Sunday, May 18, 2025

HONGERA SANA NASRA CHUNDA KWA KUHITIMU MASOMO YAKO

Nasra Chunda, tunakupongeza kwa kufanikiwa kuhitimu masomo yako ya Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Fedha (Master of Financial Management) kutoka Chuo Kikuu cha Boston! Hii ni hatua kubwa na ya kujivunia katika safari yako ya kielimu na kitaaluma.

Bidii yako, kujitolea, na uvumilivu wamezaa matunda, na tunao uhakika kwamba utatumia maarifa haya kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Kutoka timu yote ya Vijimambo Blog, tunakutakia kila la heri katika hatua zako za baadaye. Hongera sana, Nasra, kwa kufanikisha ndoto yako!

Thursday, May 15, 2025

KIJIJI CHA WANANCHI WATAKIWA KUVUTA UMEME MAJUMBANI


Na John Walter -Hanang'
Kijiji cha Dumbeta kilichopo Wilaya ya Hanang', mkoani Manyara sasa kimeunganishwa kikamilifu kwenye huduma ya umeme, hatua inayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika maisha ya wakazi wake.

Haya yamebainika wakati Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mkoa wa Manyara ilipotembelea mradi wa usambazaji umeme katika kijiji hicho.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Peter Toima, aliwataka wananchi wa Dumbeta kuchangamkia fursa hiyo kwa kuvuta umeme majumbani mwao ili waweze kunufaika na huduma hiyo muhimu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Monday, May 12, 2025

RAIS WA ZANZIBAR DK.HUSSEIN ALI MWINYI AFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU CHARLES HILARY KUTOA MKONI WA POLE KWA FAMILIA



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametoa mkono wa pole kwa familia ya marehemu Charles Hillary, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo, tarehe 11 Mei 2025, jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. Mwinyi amefika nyumbani kwa marehemu, Mtaa wa Kibamba CCM, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, kutoa mkono wa pole kwa mjane wa marehemu, Bi Sarah Mwakanjuki, pamoja na wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki.

Rais Dkt. Mwinyi amewataka wote walioguswa na msiba huo kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Marehemu Charles Hillary amefariki akiwa na umri wa miaka 66.

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR MHE.HEMED SULEIMAN ABDULLA AWASILI MKOANI KILIMANJARO KUSHIRIKI MAZIKO YA MAREHEMU MSUYA



Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameondoka Zanzibar na kuwasili Mkoani Kilimanjaro kushiriki katika mazishi ya aliyewahi kuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa Tanzania marehemu Cleopa David Msuya.

Imetolewa na Kitengo cha Habari (OMPR)

Tarehe 12.05.2025.

MCHAKATO WA NEMC KUWA MAMLAKA WAENDELEA


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akijibu maswali bungeni wakati wa Kikao cha 21 Mkutano wa 19 wa Bunge jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025.

Ofisi ya Makamu wa Rais imesema mchakato wa kulipa mamlaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kupitia mchakato unaoendelea.

Kuifanya NEMC kuwa mamlaka kutaipa nguvu ya kisheria ya kusimamia majukumu yake ipasavyo na hivyo kujiwezesha kimapato.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis ameliarifu Bunge jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025 wakati akijibu swali la nyongeza Mbunge wa Mpendae Mhe. Toufiq Salim Turky lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Viti maalumu Mhe. Amina Ali Mzee aliyetaka kujua ni lini mchakato wa NEMC kuwa mamlaka kamili.

WAZIRI MKUU ASHIRIKI UFUNGUZI WA JUKWAA LA MAAFISA WATENDAJI WAKUU AFRIKA 2025


▪️Rais Ouattara asisitiza uongezaji thamani wa mazao
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili wa Maafisa Watendaji Wakuu barani Afrika ulioanza leo Mei 12, 2025, katika ukumbi wa hoteli ya Sofitel jijini Abidjan, Ivory Coast.

Mheshimiwa Majaliwa amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo ambao umefunguliwa na Rais wa Ivory Coast, Alassane Ouattara na kuwakutanisha Maafisa Watendaji Wakuu zaidi ya 3000, wawekezaji na Wakuu wa Nchi na Serikali.
Akizungumza na washiriki wa jukwaa hilo, Rais Ouattara amesema kuwa mkutano huo utawawezesha washiriki kujadili changamoto zinazolikabili bara la Afrika na kutoa majawabu ya changamoto hizo katika maeneo ya uchumi, fedha, mazingira na biashara.

Ameongeza kuwa ili bara la Afrika liweze kuendelea kuimarisha uchumi wake, viongozi wanapaswa kuendelea kuweka na kutekeleza mikakati ya kuongezea thamani mazao yanayozalishwa.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ameshiriki Mjadala wa Marais ulioendeshwa na Mwandishi wa Kujitegemea wa CNN, Larry Madowo na kuwashirikisha Marais wa Afrika Kusini, Rwanda, Mauritania na Makamu wa Rais wa Ivory Coast.

INEC YAKUBALI KUANZISHA MAJIMBO MAPYA 8 NA KUBADILI MAJINA MAJIMBO 12.


Mwenyekiti Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Jacobs Mwambegele amesema kuwa Tume imekubali kuanzisha Majimbo mapya 8 katika Mkoa wa Dar es Salaam,Dodoma,Mbeya,Simiyu,Geita na Shinyanga pamoja na kubadilishwa kwa majina ya Majimbo 12.

Jaji Mwambegele amesema hayo leo Mei 12,2025,Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Taarifa yake kuhusu Kugawa na Kubadilisha majina ya Majimbo ya Uchaguzi, kwa Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025.

Ambapo amesema kuwa Tume imezingatia zaidi vigezo vinne ambavyo imevipa uzito kwenye mchakato wa ugawaji wa Majimbo hayo ikiwa ni pamoja idadi ya watu, ambapo kwa Majimbo ya mjini kigezo kilikuwa kuanzia watu 600,000 na kwa Majimbo ya Vijijini ilikuwa kuaniza watu 400,000,Uwezo wa Ukumbi wa Bunge wa kuchukua Wabunge wapya,Idadi ya Wabunge Wanawake wa Viti Maalum na Jimbo moja la Uchaguzi kutokuwa katika Wilaya au Halmashauri mbili.
Akibainisha Majimbo mapya yaliyoanzishwa kuwa ni pamoja na Mkoa wa Dar es Salaam ambapo Jimbo la Uchaguzi la Ukonga limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Kivule,Jimbo la Mbagala limegawanywa na kuanzishwa Jimbo la Chamazi. Mkoa wa Dodoma limeanzishwa Jimbo jipya moja ambapo Jimbo la Uchaguzi la Dodoma mjini limegawanywa na kuanzishwa Jimbo jipya la Mtumba.

VITUO 413 KUTUMIKA UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI DODOMA


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule amewahimiza Wananchi wa Mkoa wa Dodoma wenye sifa ya kupiga kura kujitokeza katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura kwa awamu ya pili ambapo zoezi hilo linalotarajiwa kuanza mnamo tarehe 16 hadi 22 Mei 2025 katika ofisi zote za Kata Mkoani Dodoma.

Mhe Senyamule amesema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari akitoa Taarifa juu ya uboreshaji wa Daftari hilo la mpiga kura kwa awamu ya pili Mkoani Dodoma.

Na kusema kuwa ni muhimu kwa wapiga kura kuhakikisha kuwa taarifa zilizopo kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ni sahihi ili waweze kutimiza haki yao ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

"Zoezi hili ni muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu,hivyo naomba niendelee kusisitiza kila mwananchi mwenye sifa ya kupiga kura tarehe 16 hasi 22 Mei alike kituoni kwaajili ya kuhakiki Taarifa zake".

Saturday, May 10, 2025

RAIS DKT. SAMIA AONGOZA WATANZANIA KUAGA MWILI WA ALIYEKUWA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS HAYATI MZEE CLEOPA DAVID MSUYA KATIKA VIWANJA VYA KARIMJEE DAR ES SALAAM


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aongoza Watanzania kuaga mwili wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Mei, 2025.


Friday, May 9, 2025

ZAIDI YA MATUKIO 2,000 YA UKATILI YARIPOTIWA MANYARA NDANI YA MIEZI MINNE.


Na John Walter -Babati
Zaidi ya matukio 2,000 ya ukatili yameripotiwa katika Mkoa wa Manyara ndani ya kipindi cha miezi minne pekee, hali inayoashiria ongezeko kubwa la vitendo hivyo vinavyotishia ustawi wa jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amefichua takwimu hizo leo alipokuwa akiongoza kikao maalumu kilichowakutanisha viongozi mbalimbali wa serikali, wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Kamati za Usalama, Wakurugenzi, Makatibu Tawala pamoja na wadau wa maendeleo kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kukabiliana na ukatili huo.

Kwa mujibu wa RC Sendiga, kutoka Januari hadi Mei 2025, jumla ya matukio 2,201 ya ukatili yameripotiwa katika mkoa mzima. Wilaya ya Hanang imeongoza kwa kuwa na matukio 668, ikifuatiwa na wilaya nyingine kwa idadi tofauti.

“Kasi ya kuongezeka kwa ukatili ni ya kutisha, tunahitaji kuchukua hatua za haraka, za pamoja na madhubuti kuhakikisha jamii inalindwa dhidi ya vitendo hivi,” amesema RC Sendiga.

Thursday, May 8, 2025

JAMII YATAKIWA KUWA NA HOFU YA MUNGU NA KUKEMEA UKATILI.



Na John Walter -Babati
Siku chache baada ya tukio la kusikitisha la kubakwa na kuuawa kwa mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Ayatsea, uongozi wa SMAUJATA Wilaya ya Babati umetembelea kijiji cha Ayatsea kutoa elimu na kukemea vikali vitendo vya ukatili vinavyoendelea kushamiri kwa kufichwa ndani ya jamii.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa SMAUJATA Wilaya ya Babati, Ezekiel Tlanka, ambaye pia ni Katibu wa SMAUJATA Kanda ya Kaskazini, matukio zaidi ya manne ya ukatili yameripotiwa kutokea kijijini humo, lakini mara nyingi yamekuwa yakimalizwa kifamilia, jambo linalozidi kushusha utu na haki za waathirika.

“Vitendo hivi vinatia aibu na havifai kufumbiwa macho, tunatoa rai kwa jamii kuwa na hofu ya Mungu na kusimama kidete kukemea na kuwafichua wanaojihusisha na tabia hizi chafu,” alisema Tlanka wakati wa ziara hiyo.

Katika hatua ya kushangaza, Tlanka alivamia mkutano wa kina mama uliokuwa ukilenga kufanya usuluhishi wa mgogoro baada ya kijana mmoja kumtukana mama yake kwa matusi makali.

Wednesday, May 7, 2025

MAADHIMISHO YA WIKI YA ZIMAMOTO DUNIANI YAFANA MANYARA.


Na John Walter -Babati

Maadhimisho ya Wiki ya Zimamoto Duniani yamefanyika leo mkoani Manyara, yakiongozwa na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani humo, RFO Gilbert Mvungi.

Maadhimisho hayo yameambatana na shughuli mbalimbali za kijamii na utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu tahadhari na uokoaji katika majanga ya moto.
Kamanda Mvungi ametumia mamlaka aliyopewa kupandisha vyeo baadhi ya maafisa wa jeshi hilo, kuanzia ngazi za chini hadi za kati akieleza kuwa, hatua hiyo inalenga kuongeza motisha kwa askari hao ili waendelee kutoa huduma bora kwa wananchi.

Maafisa wa Zimamoto, wakiwa wamevalia sare zao na kubeba mabango yenye ujumbe wa kaulimbiu ya mwaka huu isemayo "Shujaa wa Moto, Mlinzi wa Maisha: Okoa Maisha na Mali, Piga 114", walipita mitaa mbalimbali ya mji wa Babati wakihamasisha matumizi ya namba hiyo wakati wa dharura.

MWENGE WA UHURU KUPOKEWA NJOMBE MJINI,MWENYEKITI WA HALMASHAURI AELEZA A-Z MAANDALIZI ATAKA WANANCHI KUJITOKEZA


Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe Erasto Mpete amewataka wananchi wa halmashauri hiyo kujitokeza katika maeneo ya miradi yatakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru ili waweze kupokea ujumbe mahususi wa Mwenge na kujionea jinsi halmashauri yao inavyotekeleza miradi ya maendeleo.

Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake Mpete amesema,halmashauri ya mji wa Njombe inatarajia kupokea Mwenge wa Uhuru Mei 8 mwaka huu ukitokea wilayani Ludewa ambapo utatembelea katika kata tano na kumpongeza mkurugenzi wa halmashauri hiyo pamoja na wataalamu kwa maandalizi makubwa ya mapokezi.
"Mwenge wa Uhuru utapita katika kata tano za halamashauri ya mji wa Njombe na utaanza kata ya Luponde kijiji cha Madobole kwa hiyo tunaomba sana wananchi wa Madobole kujitokeza kwa wingi maana yake ndio sehemu ya mapokezi ili kuonyesha kwamba halmashauri ya mji wa Njombe tuko vizuri na baada ya kutoka Madobole Mwenge utakimbizwa kata ya Uwemba katika kijiji cha Ikisa na pale kutakuwa na tukio la kukagua msitu unaoitwa Ilonganjaula na mkimbiza mwenge atakabidhi mizinga ya Nyuki"amesema Mpete

Amesema Mwenge wa Uhuru katika kata ya Mji Mwema utapita katika maeneo mbalimbali ikiwemo katika kiwanda cha uchakataji na kusafirisha mazao ya Parachichi,Kituo cha Afya ambao huduma ya mionzi itazinduliwa na ugawaji wa vyandarua na bima huku pia katika kata hiyo kikietembelewa kikundi cha ujasiriamali wanaojishughulisha na uchoraji na baada ya hapo Mwenge wa Uhuru utaweza kwenda kuzindua madarasa sita katika shule ya sekondari Mpechi.

Tuesday, May 6, 2025

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MAREKANI WAFANYA PASSPORT DC EVENT

 

Joseph Kapinga, afisa ubalozi utalii na siasa ubalozi wachezaji Tanzania nchini Marekani, Washington DC akikaribisha wageni mbalimbali waliojitokeza siku ya Jumamosi May 3, 2025 tamasha la Passport DC ambalo kila ubalozi ulifanya tamasha hilo la kila mwaka kutangaza utalii wa nchi zao.


Monday, May 5, 2025

MKURUGENZI MKUU WA TCAA AFUNGUA RASMI KOZI YA PILI YA CHETI KWA WAKUFUNZI WA USALAMA WA ANGA (AVSEC) KATIKA CHUO CHA CATC, DAR ES SALAAM


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi akizungumza wakati wa kufungua kozi ya pili ya cheti kwa Wakufunzi wa Usalama wa Anga (AVSEC Instructors Certification Phase Two Course) katika Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa anga Tanzania (CATC) Aristid Kanje akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa Kozi ya pili ya cheti kwa Wakufunzi wa Usalama wa Anga (AVSEC Instructors Certification Phase Two Course).