🇲🇦 Morocco — $31.5M
🇪🇬 Egypt — $17.5M
🇸🇳 Senegal — $13.5M
🇩🇿 Algeria — $13.5M
🇨🇩 DR Congo — $13.5M
🇨🇻 Cape Verde — $13.5M
🇨🇮 Ivory Coast — $13.5M
🇿🇦 South Africa — $13.5M
🇬🇭 Ghana — $13.5M
🇹🇳 Tunisia — $10.5M
#WorldCupwithMicky
#FIFAWorldCup
🇲🇦 Morocco — $31.5M
🇪🇬 Egypt — $17.5M
🇸🇳 Senegal — $13.5M
🇩🇿 Algeria — $13.5M
🇨🇩 DR Congo — $13.5M
🇨🇻 Cape Verde — $13.5M
🇨🇮 Ivory Coast — $13.5M
🇿🇦 South Africa — $13.5M
🇬🇭 Ghana — $13.5M
🇹🇳 Tunisia — $10.5M
#WorldCupwithMicky
#FIFAWorldCup
1. Fika muda na siku uliyoambiwa usichelewe hata dakika 5
Kesi yako inaweza kufutwa au kuondolewa dhamana.
2. Toa sauti kubwa unapozungumza
Inakera sana Hakimu/Jaji anapokusikia kwa chini na hutaki kuongeza sauti, kumbuka yeye ndie mtoa maamuzi.
3. Ongea kwa taratibu au kwa kituo.
Ili Hakimu au Jaji apate nafasi ya kuandika, kuwa speed itapelekea ushahidi wako muhimu kwa bahati mbaya unaweza usirekodiwe na kushindwa kesi.
4. Usiikasirikie Mahakama na kuzira.
Tumia maneno yenye hekima na ushawishi kujenga hoja zako.
5. Hakikisha unaushahidi kwa kila hoja unayojenga.
Maamuzi yanatokana na ushahidi zaidi kuliko maneno matupu.
6. Usiongee uongo.
Ukijulikana unadanganya hutoaminika tena
7. Epuka mapozi hasa wanawake.
Mahakamani ni sehemu serious sio sehemu ya kujishebedua na kuonyesha urembo
8. Usitoe Rushwa au kumpa Zawadi Hakimu au jaji.
Hasa kwenye dhamana au ili kushinda, ni kosa kisheria na unaweza kukamatwa on spot.
9. Usikatae kutoa ushahidi na kukaa kimya kwa kiburi unaweza pia kuchukuliwa hatua.
10. Mwisho Uhakimu na Ujaji ni kazi ya MUNGU aliyowapa watu wachache wenye MAADILI kufanya kwa niaba yake katika HAKI
Na. Calvin Katera - Arusha.
Zaidi ya washiriki 500 kutoka ndani na nje ya mipaka ya Tanzania ikiwemo Kenya, Uganda, Uingereza na Ujerumani wachagiza utalii wa ndani kwa kushiriki mbio za Arusha Tourism Marathon zilizorindima ndani ya Hifadhi ya Taifa Arusha ikihusisha mbio ndefu na mbio fupi za kilometa 2.5, kilometa 5, kilometa 10 na kilometa 21, leo Julai 12, 2026, jijini Arusha.
Washiriki hao walitumia tukio hilo kama fursa ya kujionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana ndani ya Hifadhi ya Taifa Arusha, ikiwemo Serengeti ndogo, wanyamapori na ndege mbalimbali, misitu na mandhari ya mlima Meru, jambo lililowapa uzoefu unaounganisha michezo, utalii na uhifadhi.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Arusha Witness Shoo, alisema mbio hizo zimeendelea kuwa jukwaa muhimu la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo hifadhini, kuhamasisha utalii wa ndani na mchango wa michezo na burudani katika kuzitangaza Hifadhi za Taifa, kitaifa na kimataifa.
Kwa upande wake, Bw. Cornell Magoti, Mkurugenzi na Mwanzilishi ya mbio hizo za Arusha Tourism Marathon alisema lengo la mbio hizo ni kuunganisha sekta ya michezo na utalii kwa kuhamasisha watu kutembelea vivutio vya Tanzania, huku zikichochea uchumi wa eneo kupitia ongezeko la wageni wanaotumia huduma mbalimbali za utalii, malazi na usafiri.
Aidha, washiriki walieleza kufurahishwa na mazingira salama na yenye kuvutia ya hifadhi hiyo, wakisema mbio hizo zimewapa fursa ya kipekee ya kufanya mazoezi huku wakifurahia mandhari ya kipekee ndani ya hifadhi, hali iliyowafanya wengi kuahidi kurejea tena pamoja na familia na marafiki zao kutalii na kujiunga na matukio mengine ya kimichezo na burudani yatakaoendelewa kubuniwa na kuibuliwa.
Arusha Tourism Marathon imejenga msingi na kuwa moja ya matukio muhimu ya utalii wa michezo nchini, ikiiunga mkono jitihada za Serikali kupitia TANAPA na wadau wa sekta ya utalii na uhifadhi, kuongeza idadi ya watalii wa ndani na kimataifa, pamoja na kuitangaza Tanzania kama kitovu cha utalii barani Afrika.
📍 Viwanja vya Sabasaba, Dar es Salaam
Matokeo ya tafiti za Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) yanayoonesha kuwa asali ya Tanzania inakidhi viwango vya soko la kikanda na kimataifa kwa kuzingatia ubora wake, yamekua kivutio kwa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Daniel Pancras, alipotembelea taasisi hiyo katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Bw. Pancras alitembelea TAFORI leo Julai 12, 2026, wakati wa ziara yake ya kukagua na kutembelea taasisi na idara zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii zinazoshiriki maonesho hayo yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Akiwa katika banda hilo, alipata maelezo kuhusu tafiti mbalimbali zinazotekelezwa na TAFORI, ikiwemo utafiti uliochambua ubora wa asali inayozalishwa katika maeneo mbalimbali nchini kwa kuzingatia mikoa, hali ya hewa, aina ya udongo na vyanzo vya maua.
Matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa sifa za asali ya Tanzania, zikiwemo utamu, riha na viambata vyake, zinakidhi viwango vya soko la kikanda na kimataifa.
Bw. Pancras pia ameipongeza TAFORI kwa kuendelea kusogeza huduma za kitafiti karibu na wananchi na wadau kupitia ushiriki wake katika maonesho hayo.
TAFORI inaendelea kuwakaribisha wananchi na wadau kutembelea banda lake ndani ya Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii ili kupata elimu, ushauri wa kitaalamu na kufahamu matokeo ya tafiti zinazochochea maendeleo ya sekta ya misitu na nyuki.
Mamia ya wananchi wameendelea kufurika katika Banda la Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba ili kupata huduma mbalimbali za afya, elimu na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa hospitali hiyo.
Wananchi wanaotembelea banda hilo wanapata fursa ya kujionea huduma za kisasa za kibingwa na kibingwa bobezi zinazotolewa na Muhimbili, ikiwemo elimu ya huduma za dharura, uchunguzi wa awali wa afya, ushauri wa kitaalamu pamoja na maonesho ya teknolojia zinazotumika katika utoaji wa huduma za upasuaji.
Baadhi ya wananchi waliofika katika banda hilo wamesema wamevutiwa na namna Muhimbili ilivyowasogezea huduma karibu, hatua iliyowawezesha kupata elimu sahihi ya afya na kuelewa kwa undani zaidi huduma mbalimbali zinazopatikana katika hospitali hiyo ya taifa.
Kutokana na mwitikio huo mkubwa, Hospitali ya Taifa Muhimbili imeendelea kuwakaribisha wananchi kutumia siku zilizobakia za maonesho kutembelea banda hilo ili kupata elimu ya afya, ushauri wa kitaalamu na kujionea ubingwa na ubobezi unaotolewa na hospitali hiyo katika kuimarisha afya na kuokoa maisha ya Watanzania.
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeanza kutekeleza ahadi ya kurejesha ardhi ya misitu iliyoharibiwa kwa kiwango kikubwa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha ardhi inaendelea kuwa hai na yenye uwezo wa kuhimili mifumo ya ikolojia kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Akizungumza katika kikao kazi cha kujadili Mradi wa Urejeshaji endelevu wa Mazingira na Uhifadhi wa Bayonuai, Naibu Katibu Mkuu Muungano kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Abdallah Mitawa, amesisitiza umuhimu wa kutunza mazingira, akieleza kuwa ardhi ndiyo msingi wa maisha na nguzo muhimu ya maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Vyanzo vya Mbegu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Dkt. Fortunata Senya, amesema ushirikishwaji wa wadau, taasisi na mashirika mbalimbali ni nguzo muhimu katika kuhakikisha lengo la kurejesha ardhi iliyoharibiwa linafikiwa kwa ufanisi na kwa matokeo endelevu.
Naye Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Mbegu za Miti wa TFS, Dkt. Hamza Katety, amesema kikao kazi hicho kinatarajiwa kutoa majawabu na mapendekezo yatakayosaidia kuimarisha utekelezaji wa mpango wa urejeshaji wa ardhi ya misitu na kuhifadhi bayonuai nchini.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tamko la Pamoja kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo linafungua njia ya utekelezaji wa uundaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na kuimarisha amani, umoja, mshikamano na maendeleo ya Zanzibar.
Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo baada ya kushuhudia utiaji wa saini wa ajenda zilizokubaliwa kwa pande zote mbili kwa ajili ya kufanyiwa kazi kufuatia Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa Zanzibar baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo katika Viwanja vya Ikulu Zanzibar leo tarehe 09 Julai, 2026.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema maridhiano hayo yanaonesha dhamira ya viongozi kuweka mbele maslahi ya taifa, huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha mchakato huo unadumisha utulivu, utawala bora na maendeleo endelevu.
Halikadhalika, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongeza hatua hiyo akieleza kuwa maridhiano hayo yanafungua ukurasa mpya wa kuimarisha umoja, utulivu na mshikamano miongoni mwa Wazanzibari, na ni ishara ya ukomavu wa kisiasa na dhamira ya kujenga mazingira ya amani na maendeleo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Taifa, Mhe. Othman Masoud Othman, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa kuendeleza mchakato wa maridhiano, akisema umefungua njia ya kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu wa changamoto za kisiasa Zanzibar.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi; Marais Wastaafu wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume na Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein; Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla; Viongozi wa vyama vya siasa, Viongozi wa dini, Viongozi wa Serikali za SMT na SMZ, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mabalozi, Wawakilishi wa Taasisi za Kimataifa pamoja na wananchi mbalimbali.
Na. Calvin Katera - Arusha.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ametoa maagizo sita kwa Kamishna wa Uhifadhi TANAPA Massana Mwishawa leo Julai 09, 2026, jijini Arusha alipokuwa akiongoza zoezi la uapisho kwa aliyekuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Julai 02, 2026 kuchukua nafasi ya Kamishna wa Uhifadhi (Mstaafu) CPA Musa Nassoro Kuji aliyemaliza muda wake.
Akizungumza katika hafla ya uapisho huo Waziri Kijaji amemwelekeza Kamishna Mwishawa kusimamia miundombinu ya hifadhi, kuvutia wawekezaji, kubuni bidhaa mpya za utalii, kusimamia mapato, kuimarisha uhusiano na jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi bila kusahau nidhamu, uadilifu, weledi, ustawi wa watumishi na kusimamia maslahi yao kwa wakati.
Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini TANAPA, Mkuu wa Majeshi (Mst.) Jenerali George Waitara alieleza kuwa Bodi itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati na ushauri wakati wote ili kufanikisha adhma ya kuendeleza sekta ya maliasili na utalii.
Pia alisisitiza kuwa uendeshaji wa shughuli za Shirika zifanywe kwa uwazi na utoaji wa mrejesho uwahusishe maafisa na askari ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kwa upande wake, Kamishna wa Uhifadhi Massana Gibril Mwishawa alibainisha kuwa Hifadhi za Taifa ni hazina kubwa ya kiikolojia, kiuchumi, na kijamii na zinachangia kwa kiasi kikubwa katika mapato ya serikali na miradi ya kimkakati kama uzalishaji wa umeme.
Akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumpa dhamana hiyo, Kamishna Mwishawa aliahidi kutekeleza majukumu yake kwa uzalendo, uadilifu, uwajibikaji, nidhamu, na weledi akishirikiana na watumishi wenzake.
Hafla hii imehudhuriwa na wakuu wa taasisi za uhifadhi ikiwemo NCAA, TFS na wawakilishi kutoka TAWA, viongozi wa Serikali, wadau wa uhifadhi na utalii, viongozi wa dini, Maafisa na Askari wa TANAPA.