ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, June 9, 2026

KONGAMANO LA TANZANIA NA MISRI LAFUNGUA FURSA MPYA ZA BIASHARA, UWEKEZAJI NA UTALII



Na Mwandishi Wetu, Misri


Mahusiano ya muda mrefu kati ya Tanzania na Misri yameendelea kupata nguvu mpya kufuatia kufanyika kwa Kongamano la Biashara, Uwekezaji na Utalii la Tanzania na Misri, ambalo limewakutanisha viongozi wa serikali, wafanyabiashara, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka mataifa hayo mawili.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara Ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi wakati wa kuhitimisha Kongamano hilo ambalo limetoa fursa za ushirikiano wa kiuchumi na kuimarisha mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Misri. 

Amesema Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania imeendelea kutekeleza mageuzi mbalimbali yaliyolenga kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Mageuzi hayo yameongeza imani ya wawekezaji wa ndani na nje ya nchi na kuifanya Tanzania kuwa moja ya vituo vinavyoongoza kwa kuvutia uwekezaji barani Afrika.

Ametumia  wasaa huo kuwakaribisha wawekezaji kutoka Misri kutumia fursa zilizopo kwa kuwekeza katika hoteli, vituo vya burudani, miundombinu ya utalii wa baharini, taasisi za mafunzo ya ukarimu na huduma za kidijitali zinazohusiana na utalii.

“Ninawakaribisha kuja kutalii Tanzania kwakuwa kwa sasa kuna safari za moja kwa moja za ndege kati ya Cairo na Dar es Salaam, amesema Dkt. Abbasi”.

Naye Naibu Waziri wa Utalii na Mambokale Misri, Mhe. Yomna El Bahar amesema Kuwa Misri ipo tayari kuendeleza mashirikiano baina ya nchi hizo mbili ikiwemo kubadilishana uzoefu kwani Misri imeweza kufikisha watalii milioni 16 hivyo kama Tanzania tuna mengi ya kujifunza ikiwemo namna ya kuendeleza utalii wa utamaduni na kujifunza jinsi wanavyoyatumia kimkakati historia yao kujitangaza.

Kongamano hilo lililoanza Juni 8, 2026 limehitimishwa leo Juni 9, 2026 katika Hoteli ya Sofitel jijini Cairo, Misri.














KILLOLO DC YAVUTIA UTALII IKOLIJIA KILOMBERO, DAS BI. NYAKAJI AONGOZA KAMBI CHUI CAMPSITE



Kilombero Nature Reserve, Iringa


Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kilolo, ikiongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Bi. Nyakaji Etanga, imehimiza wananchi na watumishi wa umma kutumia fursa za utalii ikolojia zilizopo ndani ya Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Kilombero (Kilombero Nature Forest Reserve), baada ya kufanya ziara na kupiga kambi katika kituo cha utalii cha Chui Campsite kilichopo Udekwa.


Ziara hiyo iliyofanyika kuanzia Juni 3 hadi Juni 4, 2026 ilihusisha viongozi wa kamati hiyo waliopata fursa ya kufanya kambi ndani ya hifadhi, hatua iliyolenga kuhamasisha utalii wa ndani na kuongeza uelewa wa uhifadhi wa mazingira kupitia uzoefu wa moja kwa moja wa vivutio vilivyopo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bi. Nyakaji Etanga alisema ameridhishwa na mandhari ya kipekee ya Chui Campsite pamoja na fursa mbalimbali za kiutalii zilizopo ndani ya hifadhi hiyo, akisisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika utalii ikolojia kama njia ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

“Ni fursa kubwa kwa wananchi na watumishi kutumia maeneo haya kwa utalii wa ndani. Kilombero ina hazina ya kipekee inayopaswa kutambulishwa zaidi kitaifa na kimataifa,” alisema Bi. Nyakaji.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Kilombero, COII Ford Mwakalonge, aliwashukuru Bi. Nyakaji Etanga na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kilolo kwa kutembelea hifadhi hiyo na kupiga kambi katika kituo cha utalii cha Chui Campsite.

COII Mwakalonge alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi na wadau wa utalii kuendelea kutembelea hifadhi hiyo, akibainisha kuwa ina fursa mbalimbali za utalii ikolojia zinazoweza kukuza pato la jamii na taifa kwa ujumla.

“Tunawakaribisha wananchi wote kutembelea Kilombero Nature Forest Reserve. Tuna shughuli mbalimbali za utalii ikolojia ikiwemo hiking, camping, bird watching na nyingine nyingi zinazowapa wageni uzoefu wa kipekee wa mazingira ya asili,” alisema Mwakalonge.

Aliongeza kuwa ziara za aina hiyo zinachangia kuimarisha uhusiano kati ya mamlaka za uhifadhi na viongozi wa serikali za wilaya, sambamba na kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira.

Ziara hiyo ilihitimishwa Juni 4, 2026 baada ya washiriki kukamilisha shughuli za kambi katika Chui Campsite, kituo kinachoendelea kujitokeza kama kivutio kipya cha utalii ikolojia ndani ya hifadhi hiyo.

Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Kilombero ni miongoni mwa maeneo yenye bioanuwai kubwa nchini Tanzania, ikijumuisha misitu ya asili, aina mbalimbali za ndege na mandhari ya kuvutia yanayofaa kwa utalii wa asili na utafiti wa mazingira.








MHE. HEMED SERIKALI ITAENDELEA KUIIMARISHA MIFUMO YA USIMAMIZI WA NYARAKA ZA KIELETRONIKI ILI KUHAKIKISHA TAARIFA MUHIMU ZA TAIFA ZINAHIFADHIWA KWA USALAMA ZAIDI

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akipokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Nyaraka na kumbukumbu Zanzibar ndugu Khatibu Suleiman Khatibu wakati alipotembelea eneo maalum la kuhifadhia vitabu vya kumbukumbu na Nyaraka, katika Maadhimisho ya siku ya Nyaraka Duniani yaliofanyika katika Jengo la Makumbusho ya Amani Mnazi Mmoja, Wilaya ya Mjini Unguja.


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) itaendelea kuiimarisha mifumo ya usimamizi wa nyaraka za kieletroniki ili kuhakikisha taarifa muhimu za Taifa zinahifadhiwa kwa usalama, zinapatikana kwa urahisi na zinadumu kwa muda mrefu.

Hayo yamemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abulla katika maadhimisho ya siku ya nyaraka duniani kwa mwaka 2026 yaliyoadhimisha kitaifa katika viwanja vya Makumbusho ya Amani Mnazi mmoja.

Amesema katika kipindi hiki cha maendeleo makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano usimamizi wa nyaraka unahitaji kwenda sambamba na matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidijitali ili kurahisha upatikanaji wa taarifa na kuongeza ufanisi zaidi.

Mhe Hemed amesema kuwa ni matumaini ya Serikali kuwa taasisi zote za umma na binafsi zitaendelea kuzingatia viwango vya kitaalamu katika usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi na kulinda historia ya Taifa la Tanzania.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa Zanzibar imekuwa kitovu muhimu cha elimu, biashara, ustaarabu na utamaduni katika ukanda wa Afrika Mashariki na bahari ya hindi hivyo Serikali itahakikisha kuwa Manuskripti zinaendelea  kuhifadhi maarifa muhimu yanayohusu dini, sheria, elimu, tiba , biashara, utawala na maisha ya jamii kwa ujumla.

Aidha amesema kuwa hati za kale ni ushahidi tosha wa mchango mkubwa wa Zanzibar katika maendeleo ya elimu na ustaarabu wa kiislamu sambamba na kuwa chanzo muhimu cha tafiti kwa watafiti , wanahistoria, wanafunzi na taasisi mbali mbali duniani.

Sambamba na hilo Mhe. Hemed  amesema  ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha kuwa manuskripti na nyaraka adhimu zinalindwa, zinatunzwa na zinaendelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi mbali mbali za ndani na nje ya nchi katika kuhifadhi na kuendeleza urithi huu muhimu kwa Taifa.

Hata hivyo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa wananchi  kuthamini utamaduni wa kutunza kumbukumbu na nyaraka muhimu katika maisha yao binafsi, taasisi na jamii kwa ujumla kwani Taifa lenye utamaduni wa kuhifadhi kumbukumbu zake hujenga msingi imara wa maendeleo, uwajibikaji na utambulisho wa vizazi vyake.

Nae waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Mhe. Dkt. SAADA MKUYA SALUM amesema uwepo wa  taasisi ya Nyaraka huisaidia jamii kujua umuhimu wa nyaraka na kumbukumbu katika kuhifadhi historia, kulinda haki za wananchi, kuimarisha uwazi na uwajibikaji pamoja na kuchangia maendeleo endelevu katika jamii.

Amesema nyaraka ni msingi wa kumbukumbu za Taifa zinazohifadhi ushahidi wa shughuli za Serikali na jamii pamoja na kulinda haki za wananchi, kuimarisha utawala bora na kutoa rejea muhimu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Aidha Dkt. Saada  amefahamisha kuwa katika kuadhimisha siku ya nyaraka duniani taasisi ya nyaraka na kumbukumbu Zanzibar imeandaa na kutekeleza shughili mbali mbali ikiwewmo jukwaa la nyaraka, ziara za kijamii, maonesho ya nyaraka za kihistoria sambamba na maonesho maalumu ya maandiko ya kiislamu na hati za kiarabu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Nyaraka na kumbukumbu Zanzibar ndugu  Khatibu Suleiman Khatibu amesema taasisi hio imejipanga kutoa elimu juu ya matumizi mazuri ya nyaraka na kumbukumbu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na baadae.

Ndugu Khatibu ametumia nafasi hio kuitaka jamii kuitumia taasisi ya nyaraka katika utunzaji wa nyaraka na kumbukumbu pamoja na kupata elimu juu ya utunzaji wa nyaraka na kujiepusha na migogoro isiokuwa na tija katika jamii

Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amekagua mabanda ya maonesho ya vitu vya asili na tamaduni za kizanzibari.

Imetolewa na Kitengo cha Habari ( OMPR )

Leo tarehe 09 / 06 / 2026









FAHAMU ZAIDI KUHUSU PAMBANO DHIDI YA MICHEL SORO NA HASSAN MWAKINYO

 


Michel Soro ni bondia wa kulipwa kutoka Ufaransa mwenye asili ya Côte d'Ivoire. Anapigana katika uzani wa super welterweight (light middleweight).


Amewahi kuwa miongoni mwa mabondia bora wa uzani huo duniani, akiwahi kutajwa ndani ya 10 bora na baadhi ya taasisi za viwango vya ndondi miaka iliyopita. 

Hassan Mwakinyo amewahi kufika karibu na 40 bora duniani kwenye BoxRec katika uzani wa Super Welterweight.


Kwa uzoefu wa kimataifa na kiwango cha wapinzani waliowahi kupigana nao, Michel Soro kwa ujumla anaonekana kuwa na wasifu mkubwa zaidi kuliko Mwakinyo. Lakini Mwakinyo ana nafasi ya kujitangaza zaidi kimataifa akishinda pambano lao la Juni 2026.


Kuhusu nafasi (ranking) ya sasa duniani, Michel Soro na Hassan Mwakinyo hawaonekani katika orodha za juu 15 za mashirika makubwa ya ubingwa wa dunia kama WBA, WBC, IBF na WBO zilizochapishwa mwaka 2026. 


Rekodi yake ya mapambano (professional record):


Ushindi: 38

 Kushindwa: 4

 Sare: 2

Ushindi kwa KO/TKO: 27 (takriban 71%) 


Katika kazi yake amewahi kupigana na mabondia wa kiwango cha juu kama Brian Castaño, Israil Madrimov na Magomed Kurbanov. 


Kuhusu Hassan Mwakinyo:


 Rekodi yake ni ushindi 25 na kushindwa 3.

Ana KO/TKO 18.

 Ni mmoja wa mabondia maarufu zaidi Tanzania katika uzani huo. 


Kwa nini apigane na Hassan Mwakinyo?


Mapambano hayo yanatarajiwa kufanyika tarehe 10 Juni 2026. Sababu kubwa ni kwamba:


1. Mwakinyo anatafuta kuthibitisha uwezo wake dhidi ya bondia mwenye uzoefu mkubwa wa kimataifa.

2. Soro anatafuta kuendelea kupanda kwenye viwango vya dunia kwa kushinda bondia anayeshikilia mafanikio makubwa Afrika.

3. Ni pambano linaloweza kuongeza nafasi ya mshindi kupata mapambano makubwa zaidi ya ubingwa wa dunia


Kwa uzoefu wa kimataifa na wapinzani aliowahi kukutana nao, Soro anaonekana kuwa na uzoefu mkubwa zaidi. Hata hivyo, Mwakinyo ana faida ya kuwa bado yuko kwenye umri mzuri wa ushindani na amekuwa akishinda mapambano yake ya karibuni. 


Je unahisi nani ataibuka mshindi katika pambano hili?.

WAISRAEL NAO WAMERUDI NYUMBANI NGORONGORO


Watalii  zaidi ya 40 kutoka Taifa la Mungu wana wa Israel wamerudi Nyumbani, Kutoka Jerusalem hadi Ngorongoro Tanzania  kuja kujionea maajabu ya Ulimwengu.

Watalii hao  wameshuhudia  maajabu (Wonders) ya uumbaji wa Mungu ikiwemo Kasoko ya Ngorongoro, Bonde la Olduvai na  kupata taarifa kuhusu eneo la Laetoli lenye  Nyayo za Binadamu wa kale.

Watalii hao wakiongozwa na Ellyn Zelikman wamesema kuwa  Ngorongoro imekuwa ndoto ya maisha   na wameamua kujivinjari eneo hilo ili kujionea maajabu ya Dunia.

Wamesema wamezoea  kuona alama za kiroho, Utamaduni wa kisasa wa Mediterania unaozunguka miji mashuhuri na Hifadhi za asili lakini Ngorongoro  imewafanya kufungua ukurasa mpya kwa kuona Simba juu ya miti, Faru pembeni mwa ziwa lenye magadi, Tembo, Nyati, Chui, Ngiri, Pundamilia, Nyumbu na wengineo.

Hifadhi ya Ngorongoro kwa takribani miaka mitano (05) iliyopita imepokea zaidi ya watalii 9,367 kutoka nchini Israel ambapo juhudi za kuongeza watalii wengi zaidi zinaendelea.



HARRISON SIWALE NA RAIS FREDERICK CHILUBA

 

Pichani Harisoni Siwale wa kwanza kushoto

Vijana wa Zambia Walioandika Historia katika mashamba ya Mkonge Tanga


Katika historia ya Tanzania na Zambia kuna simulizi ya kipekee inayounganisha mashamba ya mkonge ya Tanga na mafanikio makubwa yaliyopatikana baadaye nchini Zambia. 


Katika miaka ya 1950 na 1960, mamia ya vijana kutoka Zambia walivuka mipaka na kuja Tanganyika kutafuta ajira katika mashamba ya mkonge, sekta iliyokuwa miongoni mwa nguzo muhimu za uchumi wa nchi wakati huo.


Miongoni mwa vijana hao alikuwapo kijana aliyekuja kujulikana baadaye kama Rais wa Pili wa Zambia, Frederick Chiluba. 


Akiwa na umri mdogo, Chiluba alifanya kazi katika mashamba ya mkonge ya Korogwe mkoani Tanga ambako alipata uzoefu wa maisha ya wafanyakazi, changamoto zao na umuhimu wa mshikamano. 


Uzoefu huo ulimjengea msingi wa harakati zake za kutetea haki za wafanyakazi aliporejea Zambia na hatimaye kumfikisha Ikulu mwaka 1991.


Katika mkumbo huohuo wa vijana wa Zambia waliotafuta maisha Tanga, simulizi za wanamuziki wa zamani pia zinamtaja Harrison Siwale. 


Kabla ya kuhusishwa na muziki wa Afrika Mashariki, Siwale alikuwa ametokea katika mazingira ya Copperbelt nchini Zambia, eneo maarufu kwa migodi ya shaba na utamaduni wake mkubwa wa muziki. 


Migodi hiyo ilitoa nafasi kwa vijana wengi kujifunza uimbaji, upigaji wa vyombo na sanaa za jukwaani.


Ingawa kumbukumbu zilizoandikwa kuhusu safari ya Harrison Siwale kutoka Zambia hadi Tanga ni chache, simulizi za wanamuziki wa kizazi hicho zinaonyesha kwamba mashamba ya mkonge yalikuwa sehemu muhimu ya kukutana kwa tamaduni mbalimbali za Afrika. 


Vijana kutoka Zambia walikuja na muziki wao, lugha zao na mila zao, na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya muziki na maisha ya kijamii katika maeneo ya Tanga.


Jambo la kushangaza ni kwamba kutoka katika mazingira hayo hayo ya kazi ngumu za mkonge, mmoja alikuja kuwa rais wa taifa la Zambia na mwingine akajenga jina katika ulimwengu wa muziki. 


Hii inaonyesha jinsi mashamba ya mkonge ya Tanga yalivyokuwa zaidi ya sehemu za ajira; yalikuwa shule ya maisha iliyozalisha viongozi, wanamuziki na watu waliokuja kuacha alama katika historia ya Afrika.


Leo, simulizi za Frederick Chiluba na Harrison Siwale zinabaki kuwa ushahidi kwamba wakati mwingine historia kubwa huanzia katika maeneo ya kawaida kabisa. 


Mashamba ya mkonge ya Tanga yaliwahi kuwa nyumbani kwa vijana waliotafuta maisha, lakini miongoni mwao walikuwamo watu waliokuja kuwa sehemu ya historia ya Zambia na Afrika kwa ujumla.

.

Makala haya kwa hisani ya : BARIKI NGOWO -MUZIKI HALISI 

PETER TOLL NA HISTORIA YA SIMBA WANYIKA ULAYA PART 2

 

Pichani ni mpiga rithim wa jamhuri Harisoni Siwale na mkewe

Peter Toll anaendelea


Philps to Plydor

"Mwaka 1973 ndiyo mwaka ambao Philips Kenya ilibadilika na kuwa Polygram (Polydor)."


"Polygram ilipoanza kutoa albamu za LP zilizokusanywa kutoka rekodi za 45 RPM, mara nyingi waliandika 'Original Recording – Polygram Studios 1973', kama ilivyo kwenye LP Dunia Haina Wema."


"Lakini hilo lilitokana na ukweli kwamba Polygram haikujali sana au haikuweza kubaini nyimbo hizo zilikuwa zimetolewa lini kwa mara ya kwanza."


Ziara ulaya


Katika makala yake “Wanyika Memories” (The Beat, Vol. 12, No. 4, 1993), Peter Toll anasimulia kuwa wakati Simba Wanyika walipokuwa wakijiandaa kuanza ziara yao ya kwanza Ulaya mwezi Novemba 1989, walikumbana na tatizo kubwa: ndugu Wilson Kinyonga na George Kinyonga pekee ndiyo waliokuwa na pasi za kusafiria.


Africa jambo jambo


Ili kuziba pengo la wanamuziki wengine watatu waliokosekana, waliajiri wanachama watatu kutoka bendi nyingine iliyoitwa Africa Jambo Jambo. Miongoni mwao alikuwa Muitikanda kutoka Uganda aitwaye Sammy Kasule, ambaye alikuwa amewahi kupiga katika makundi mbalimbali na pia kurekodi kazi zake binafsi. 


Les Mangelepa


Wengine wawili walikuwa Wakongo Coco Kanyinda na Micky Jaga Jaga, ambao hapo awali walikuwa wanamuziki wa Orchestra Les Mangalepa.


Peter Toll anaendelea


"Ingawa kundi lililosafiri kwenda Ulaya mwaka 1989 halikuwa Simba Wanyika halisi ya Wilson Peter, walipiga muziki wa Kinyonga pekee, na waliufanya kwa ustadi mkubwa na nguvu nyingi."


"Maonesho yao yalipokelewa kwa sifa nyingi, na kabla ya kurudi Nairobi walirekodi mchanganyiko (medley) wa nyimbo maarufu za Simba Wanyika ambao ulitumika kutangaza ziara kubwa ya Ulaya iliyopangwa kufanyika kipindi cha kiangazi."


Peter anaendelea kueleza kuwa kutokana na mgogoro wa kimkataba kati yake na Polygram Records ya Nairobi, alishindwa kuachia rasmi mkanda huo wa “Wanyika Medley Tape” kama ilivyokuwa imepangwa.


Hata hivyo, mkanda huo ulihamasisha kutolewa kwa albamu ya medley ya Les Wanyika mwaka 1990 iliyoitwa Les Les Non Stop '90 (Polydor POLP 606).


Peter Toll alieleza matumaini yake kwamba siku moja rekodi ya “Live in Europe” itaweza kutolewa rasmi.


Lakini tayari ipo YouTube na aloyeiweka jina linahifadhiwa


NYIMBO ZA ZIARA YA DUNIA YA 1991


Nyimbo zilizorekodiwa nchini Uholanzi wakati wa ziara ya dunia ya Simba Wanyika mwaka 1991 ni:


Mwongele, Wenzako, Pamela

Sikujua Utabadilika, Nakupenda Cherie, Pole Pole, Maria


Wanamuziki waliorekodi pamoja na Wilson na George Kinyonga (waliokuwa waimbaji pamoja na wapiga solo na rhythm guitar) walikuwa, Maneno Shaban Ally  percussion na ngoma, Mike Beche ngoma, Victor Boniface – gitaa la besi


Peter Toll pia aliwahi kusema kuhusu mkanda mmoja uliojitokeza baada ya kifo cha Wilson.........


"Hii si Simba Wanyika halisi. Ni kijana mmoja kutoka Tanzania aliyeniandikia baada ya Wilson kufariki. Alidai kuwa alikuwa ndugu  yao (?) na kwamba angeendelea na Simba Wanyika. 


Alinitumia kaseti hiyo, lakini sikuwahi kusikia tena habari zake."


LES WANYIKA

Mpiga rhythm guitar Omar Shabani, aliyefahamika kama “Professor Omar”, aliondoka Simba Wanyika mwaka 1978 pamoja na:


Tom Malanga (besi) Rashid Juma (ngoma) Elias John (saxophone)

na kwa kushirikiana na Watanzania John Ngereza na mwimbaji Issa Juma, wakaanzisha bendi ya Les Wanyika.


Muda mfupi baada ya kutoa wimbo wao maarufu “Sina Makosa” mwaka 1979, Issa Juma alijitenga na kuanza shughuli zake binafsi.


Katika miaka ya 1980, Les Wanyika walikuwa na mafanikio makubwa sawa na Simba Wanyika. Walitoa nyimbo nyingi zilizotikisa Afrika Mashariki, zikiwemo vibao vikubwa:.......Nilipi la Ajabu (1988)

Nimaru (1989)


Ingawa Omar Shabani ni mmoja wa mwanzilishi wa Les Wanyika na mtunzi wa nyimbo nyingi za bendi hiyo, kufikia mwaka 1990 ilionekana wazi kuwa ushawishi wake ulikuwa unapungua.


Peter Toll anaandika:


"Katika miaka ya 1980 kulikuwa na mvutano wa madaraka kati ya Ngereza na Shabani. Nafikiri Ngereza ndiye aliyeshinda baada ya Polygram kuamua kwamba yeye ndiye mtu ambaye walitaka kufanya naye kazi."


"Nyimbo zake pia zilikuwa zinauza zaidi."


Kutokana na hali hiyo, Omar Shabani alifukuzwa Les Wanyika mwaka 1990 na kujiunga na Everest Kings, kabla ya kurejea tena Les Wanyika miaka michache baadaye.


Kwa masikitiko, Omar Shabani alifariki mwaka 1997, na John Ngereza akafariki mwaka 2002.


SIRI YA WIMBO “SINA MAKOSA”

Katika makala ya Wanyika Memories, Peter Toll anaeleza:


"Ingawa Professor Omar amekuwa akitajwa kama mtunzi wa 'Sina Makosa' na hivyo kupata manufaa ya kifedha kutokana na wimbo huo, ukweli ni kwamba uliandikwa kwa ushirikiano na George Kinyonga walipokuwa bado Simba Wanyika."


"Mstari wa sauti unaonyesha wazi kabisa alama ya George Kinyonga, huku mpangilio wa rhythm na progression ya chords ukifanana sana na wimbo 'Daina' ambao George alikuwa ameutunga hapo awali."


"Huenda kutokana na kufanana huko, ndugu wa Kinyonga waliamua kutourekodi wimbo huo."


"Lakini wanamuziki wao walipoondoka na kuanzisha Les Wanyika, waliuchukua kama mojawapo ya nyimbo zao za kwanza kurekodi."


"Kwa mshangao na huzuni ya George, rekodi hiyo ikawa mafanikio makubwa sana ndani na nje ya Kenya."


LES MOTO MOTO


Nchini Kenya mikataba ya kurekodi haikusainiwa kwa jina la bendi nzima, bali kwa jina la kiongozi wa bendi.


Kwa sababu hiyo, wakati Les Wanyika walipoongozwa na Omar Shabani, John Ngereza hakuwa akipata mirabaha (royalties) za nyimbo alizokuwa akiandika.


Ili kutatua tatizo hilo, Ngereza akaanzisha Les Moto Moto, ambayo kimsingi ilikuwa ni Les Wanyika wakirekodi kwa jina tofauti.


Mpangilio huu ulikuwa sawa kabisa na ule uliotumika kati ya Simba Wanyika na Orchestra Jobiso.


ORCHESTRA JOBISO


Mwaka 1980, George Kinyonga aligombana na ndugu yake Wilson Kinyonga na kuondoka Simba Wanyika.


Wanachama wote wa bendi, isipokuwa William Kinyonga, waliondoka pamoja naye na kuanzisha Orchestra Jobiso, jina lililotokana na mtindo wa dansi ulioonekana kwenye rekodi za Simba Wanyika miaka ya 1970.


Wanamuziki wengine waliojiunga walikuwa:.......Mike Beche (percussion) Saidi Makelele (tarumbeta) ambao wote walikuwa wametoka katika bendi ya Super Volcano ya Mbaraka Mwinshehe.


Bendi hiyo mpya ilipata mafanikio ya haraka kupitia vibao:


Nakupenda Sherry, Pole Jobiso


Mwisho wa mwaka huo, Wilson na George walipatana na George akarudi Simba Wanyika.


Wanachama waliobaki wa Jobiso walijiunga na Issa Juma kuunda Super Wanyika Stars.


Hata hivyo Orchestra Jobiso haikufa.


Peter Toll anaandika:

"Baada ya George kurejea Simba Wanyika, ndugu hao walitatua tatizo la zamani la mkataba wa kurekodi kuwa kwa jina la Wilson pekee."


"Suluhisho lilikuwa kumpa George nafasi ya kurekodi nyimbo zake mwenyewe akiwa na wanamuziki wa Simba Wanyika na kuzitoa chini ya mkataba wake binafsi kama Orchestra Jobiso."


Kwa utaratibu huo zilirekodiwa nyimbo kama:........

.Natafuta Mwali, Tatizo la Pesa

Epuka Kizai-Zai (1984)


SUPER WANYIKA STARS


Baada ya kuimba kwa mafanikio makubwa wimbo “Sina Makosa” mwaka 1979, mwimbaji Mtanzania Issa Juma alijitenga na kuanzisha kundi lake mwenyewe akishirikiana na wanachama waliobaki wa Orchestra Jobiso.


Kundi hilo lilijulikana kwa majina mbalimbali, Waanyika, Wanyika Stars, Super Wanyika na Wanyika Super Les Les


lakini kwa pamoja lilijulikana kama Super Wanyika Stars.


Kwa kipindi fulani waliweza kushindana na makundi mengine ya Wanyika kupitia nyimbo maarufu kama....Ateka, Sigalame


Mwishoni mwa miaka ya 1980 Issa Juma alipitia matatizo mengi binafsi, yakiwemo kufungwa jela kwa miezi sita kwa kufanya kazi bila kibali halali.


Baadaye alihamia Kericho, magharibi mwa Kenya, na kuacha muziki.


Ni katika kipindi hicho alipata kiharusi kilichopooza upande mmoja wa mwili wake.


Issa Juma alifariki mwanzoni mwa miaka ya 1990.


EVEREST KINGS


Mkongwe wa muziki wa Wanyika Abdul Muyonga, akishirikiana na Mohamed Tika na Mahmood Hussein Yassin, aliondoka Mavalo Kings mwishoni mwa miaka ya 1980 na kuanzisha Everest Kings.


Tangu kifo cha John Ngereza mwaka 2002, Everest Kings wamekuwa walinzi wakuu wa urithi wa muziki wa Wanyika nchini Kenya.


Makao yao yamekuwa yakihama kati ya Machakos na Nairobi.


Kwa miaka mingi bendi hiyo imehifadhi sauti ya Wanyika huku pia ikiwakusanya wanamuziki waliotoka katika makundi mbalimbali ya Wanyika.


Miongoni mwa waliowahi kujiunga nayo ni....Omar Shabani, Tom Malanga, Freshley Mwamburi


Mwaka 2003, Freshley Mwamburi na wanachama wengine waliondoka na kujiunga na Great Sounds Band.


Gazeti la Daily Nation la Nairobi liliripoti kuwa baadhi ya waanzilishi wa awali wa Everest Kings, akiwemo Mohammed Hussein, Pius Indimuli na Richard Bangalala, walirejea tena kundini.


Mwaka 2000 Everest Kings walitoa CD Nivishe Pete, iliyokuwa na nyimbo: Nivishe Pete Boaz Olao

Wambua, Panga Mipango


Mwaka 2004 walitoa albamu Stella Wangu, iliyokuwa na nyimbo maarufu: Stella Wangu, Njiwa

Simoni


Albamu hiyo ilichanganya mitindo ya rumba na hip hop.


GREAT SOUNDS BAND


Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la tarehe 13 Machi 2004, Tom Malanga, Freshley Mwamburi na mpiga rhythm guitar Rashid Athman waliondoka Everest Kings mwaka 2003 na kuanzisha Great Sounds Band.


Hata hivyo, haijulikani kwa uhakika bendi hiyo ilikuwa na uhusiano gani rasmi na makundi ya Wanyika, wala kama iliwahi kutoa rekodi zozote rasmi.

 


Itaendelea.............

Makala haya kwa hisani ya : BARIKI NGOWO -MUZIKI HALISI 

SIMBA WANYIKA NA ASILI YAO

 

Pichani ni kundi la vijana wa jamhuri jazz

Makundi yote ya Wanyika yalikuwa yamejikita nchini Kenya, ingawa viongozi wake wakuu, ndugu wa Kinyonga (Wilson na George), Omar Shabani, John Ngereza na Issa Juma wote walitokea Tanzania na walijifunza na kukomaa kimuziki katika mazingira yenye rutuba ya muziki wa Tanzania wa miaka ya 1960 na 1970.

Orodha hii ya kazi za muziki (discography) iliwekwa mtandaoni kwa mara ya kwanza tarehe 10 Julai 2004. 

Taarifa nyingi za awali zilitolewa na Doug Paterson, ambaye ukurasa wake wa East African Music Page ni moja ya vyanzo muhimu vya habari kuhusu muziki wa Kenya na Tanzania.

Baadaye mwandishi aliwasiliana na Peter Toll kutoka Uholanzi, ambaye alidhamini ziara mbalimbali za Simba Wanyika mwishoni mwa miaka ya 1980 na mwanzoni mwa miaka ya 1990. 

Peter Toll aliandika makala mbili muhimu kuhusu Wanyika, The Wanyika Weave (1991) na Wanyika Memories (1993), na pia alikuwa mtayarishaji wa CD ya Simba Wanyika Pepea mwaka 1992.

Peter Toll alitoa taarifa nyingi kuhusu rekodi ambazo hazikuwepo katika orodha ya awali. 

Aidha, makala zake zilitoa maelezo muhimu ya ziada na marekebisho ya taarifa zilizokuwepo.

Kwa msaada wa taarifa zaidi kutoka Doug Paterson na Michael Kieffer, toleo hili jipya la "Discography of the Wanyika Groups" limekuwa zaidi ya mara mbili ya ukubwa wa toleo la kwanza.


John Beadle


JAMHURI JAZZ BAND

Jamhuri Jazz ilianzishwa Tanga, Tanganyika mwishoni mwa miaka ya 1950 na ilikuwa moja ya bendi maarufu zaidi Tanzania.

Wilson Peter Kinyonga na George Peter Kinyonga waliingia katika bendi hiyo mwaka 1966 na walipiga humo kwa miaka minne kabla ya kuondoka Desemba 1970 kuanzisha Arusha Jazz Band.

Maelezo yaliyopo kwenye albamu Simba Wanyika Greatest Hits Vol. 1 yanadai kuwa baada ya wao kuondoka bendi ilisambaratika, lakini jambo hilo si kweli. 

Jamhuri Jazz iliendelea kupiga muziki hadi angalau miaka ya 1970.

Katika kipindi hicho, baadhi ya wanachama wake akiwemo Omar Shabani walichukuliwa na ndugu wa Kinyonga kujiunga na Simba Wanyika.

Baadhi ya nyimbo zake zilikuwa:

Mpenzi Fikiri

Dunia Imenisonga

Bibi Mwenye Chongo

Simba Mwituni

Shingo ya Upanga

Nafikiria Kurudi Shamba

Susana

Magdalena


ARUSHA JAZZ BAND

Arusha Jazz ilianzishwa Arusha mwaka 1971 na Wilson Kinyonga, George Kinyonga, ndugu yao William Kinyonga pamoja na wanamuziki wengine watatu.


Kwa mujibu wa maelezo ya albamu Simba Wanyika Greatest Hits Vol. 1, nyimbo kadhaa ambazo baadaye zilijulikana kama za Simba Wanyika kama:

Pamela

Kenya Yetu

Marceline

zilirekodiwa kwanza chini ya jina la Arusha Jazz.

Mwezi Juni 1971 bendi ilihamia Mombasa, Kenya na kubadili jina kuwa Simba Wanyika (Simba wa Porini).

Hata hivyo jina la Arusha Jazz halikufa mara moja. Peter Toll anaeleza kuwa walipofika Mombasa walikuwa na mabango mawili jukwaani:

Simba Wanyika

Arusha Jazz

George Kinyonga alisema walitumia majina yote mawili kwa muda, lakini kuanzia mwaka 1973 walibaki kutumia jina la Simba Wanyika pekee.

Nyimbo zao za mwanzo zilikuwa:

Mama Suzie

Mary Mtoto

Tutengane Salama

Mama Niache

Eliza Wangu

Jose Twende Zaire

Mwaka 1987 kulitolewa kaseti ya mkusanyiko wa nyimbo zao za zamani iliyoitwa Mama Suzie.

ORCHESTRA SIMBA WANYIKA

Ingawa Simba Wanyika ilikuwa mwendelezo wa Arusha Jazz, kati ya mwaka 1971 na 1973 kulikuwa na mabadiliko mengi ya wanachama.

Peter Toll anaandika kuwa kufikia mwaka 1973 wapiga muziki wa awali walikuwa wamebadilika na:

Rashid Juma (mpiga ngoma kutoka Tanga)

Tom Malanga (mpiga bass kutoka Mombasa)

Katika safari nyingine ya Tanzania, ndugu wa Kinyonga waliwachukua wanamuziki wawili kutoka Jamhuri Jazz:

Elias John (saxophone)

Omar Shabani (rhythm guitar), ambaye baadaye alijulikana kama Professor Omar

Katika kipindi hicho bendi ilisaini mkataba na Polygram Kenya.

Baada ya miaka minne Mombasa, Simba Wanyika ilihamia Nairobi na kwa zaidi ya miaka ishirini ikawa moja ya bendi muhimu zaidi katika maendeleo ya muziki wa Afrika Mashariki.

Mtindo wa Muziki wa Simba Wanyika

Doug Paterson anaeleza kuwa kama bendi nyingi za Tanzania, Simba Wanyika walicheza rumba yenye mashairi ya Kiswahili.

Tofauti na mtindo wa Benga uliokuwa unaibuka Kenya wakati huo, muziki wao ulikuwa:

laini zaidi, mtulivu, unaotiririka

Rekodi zao za mwanzo hazikuwa hata na drum set.

Mdundo ulitokana na:

Congas na Claves na midundo ya Cavacha kwenye hi-hat

Gitaa la rhythm lilikuwa linafanya kazi nyingi lakini kwa sauti ya upole, huku solo guitar na saxophone zikitumika kwa vipindi maalumu tu.

Peter Toll anaeleza kuwa sauti za Wilson na George zilipoimbwa kwa pamoja ziliunda alama maalumu ya Simba Wanyika ambayo iliwavutia mashabiki wengi sana.

MGOGORO NA KUANZISHWA KWA LES WANYIKA

Kama ilivyo kwa makundi mengi ya muziki Afrika, mafanikio yalileta migogoro.


Mwaka 1978 wanachama kadhaa wa Simba Wanyika wakiongozwa na Omar Shabani waliondoka na kuunda Les Wanyika.

Mwaka 1980 mgogoro mwingine kati ya George na Wilson Kinyonga ulisababisha kuundwa kwa Orchestra Jobiso. Hata hivyo mgogoro huo ulimalizika baadaye.

KUREJEA KWA NGUVU KWA SIMBA WANYIKA

Baada ya changamoto hizo, Simba Wanyika ilijikusanya upya. Mwaka 1983 walitoa kibao kikubwa sana:

Shilingi

Kibao hicho kilifuatwa na nyimbo nyingine zilizofanikiwa sana kama:

Halleluya

Baba Asiya


Peter Toll anaeleza kuwa Shilingi iliuza karibu nakala 50,000 wakati ambapo biashara ya muziki ilikuwa tayari imeanza kuathiriwa na uharamia wa kazi za sanaa.


KUONDOKA KWA WANAMUZIKI MUHIMU


Mwaka 1976 wanamuziki hawa waliondoka Simba Wanyika na kurudi Tanzania:

Luiza Elias John (tenor saxophone)

Kassim Mponda Mbwana (mi-solo guitar)

Bindo Bakari Kipanga (rhythm guitar)


Sababu kubwa ilikuwa kusambaratika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ya wakati huo.


Luiza Elias John baadaye alijiunga na Mwenge Jazz ya JWTZ.

Mwandishi Miguel Suleyman aliwahi kusema:  "Luiza Elias alikuwa mwanamuziki aliyesoma zaidi katika historia yote ya Wanyika. 

Linganisha muziki wa Simba Wanyika kabla na baada ya kuondoka kwake."

WIMBO WA NAKUPENDA

Mwaka 1977 Simba Wanyika walitoa wimbo:

Nakupenda

Ingawa uliandikwa na George Kinyonga, haukuwa toleo la awali la Nakupenda Sherry ambayo baadaye ilikuja kuwa hit kubwa ya Orchestra Jobiso.

Peter Toll alisema:

"Huu ulikuwa wimbo wenye nguvu sana uliochezwa katika mdundo wa Moja Moja." Moja moja na simba wa nyika


SIKUJUA UTABADILIKA


Baada ya wanachama wengi kuondoka mwaka 1978 kuunda Les Wanyika, Wilson na George waliunda kikosi kipya chenye:

Joseph Tito (rhythm guitar)

George Madrago (bass)

Maneno Shaban Ally (drums)

Kwa kikosi hicho walirekodi:

Sikujua Utabadilika kama kuthibitisha kuwa Simba Wanyika bado ilikuwa bendi imara licha ya mabadiliko ya wanachama.


ZIARA YA ULAYA

Mwaka 1989 Simba Wanyika ilipojiandaa kwa ziara yake ya kwanza Ulaya ilikumbwa na tatizo kubwa.


Ni Wilson na George Kinyonga pekee waliokuwa na pasipoti.

Kwa hiyo walilazimika kuchukua wanamuziki watatu kutoka bendi ya Africa Jambo Jambo:


Sammy Kasule (Uganda)

Coco Kanyinda (DR Congo)

Micky Jaga Jaga (DR Congo)


Peter Toll anasema kwamba ingawa kikosi hicho hakikuwa Simba Wanyika ya kawaida, kilipiga nyimbo za Kinyonga kwa ustadi mkubwa na kupokelewa vizuri sana Ulaya.


ALBAMU YA PEPEA

Mwaka 1992 Simba Wanyika ilitoa CD ya: Pepea


iliyorekodiwa nchini Uholanzi wakati wa ziara yao ya dunia ya mwaka 1991.


Nyimbo zake zilijumuisha:

Mwongele, Wenzako, Pamela

Sikujua Utabadilika, Nakupenda Cherie, Pole Pole, Maria


Mbali na Wilson na George Kinyonga, wanamuziki wengine walikuwa:

Maneno Shaban Ally

Mike Beche

Victor Boniface


KIFO CHA GEORGE NA WILSON

George Peter Kinyonga alifariki mkesha wa Krismasi mwaka 1992 baada ya kuugua kwa muda mfupi.


Wilson Peter Kinyonga naye alifariki mwaka 1995.


Baada ya vifo vya ndugu hao wawili, Simba Wanyika ilianza kufifia na hatimaye kuvunjika.


Peter Toll alieleza kuwa kaseti moja iliyotolewa baadaye kwa jina la Simba Wanyika haikuwa ya bendi halisi, bali ya mtu kutoka Tanzania aliyedai kuwa ni ndugu wa familia ya Kinyonga na alitaka kuendeleza jina la Simba Wanyika. Hata hivyo hakusikika tena baada ya kutuma kaseti hiyo.


(Sehemu zinazofuata za Les Wanyika, Les Moto Moto, Orchestra Jobiso, Super Wanyika Stars, Everest Kings na Great Sounds 


Itaendelea........


Makala haya kwa hisani ya : BARIKI NGOWO -MUZIKI HALISI 

KITENDAWILI CHA SIMBA WANYIKA

Pichani ni Bindo Kipanga  huyu alijua mpango WA kuanzishwa kwa Simba wanyika, na alikuwa WA kwanza kuwa Kenya.sehemu za Kericho na baadaye alikaa.simba wanyika Muda mfupi na kurudi Dar es salaam kujiunga na Western jazz.


Migogoro ya Ndani, na Mapambano ya Hatimiliki


Historia ya bendi kongwe na maarufu ya Simba Wanyika imejaa mambo mengi yaliyo nyuma ya pazia ambalo hayajawahi kuwekwa wazi kikamilifu. 


Unapochimba kwa undani, unagundua kuwa mafanikio makubwa ya bendi hii yalienda sambamba na dhoruba kali za kimaslahi, migogoro ya kifamilia, na mikataba ya kinyonyaji kutoka kwa makampuni ya kurekodi muziki.


Ili kuelewa vizuri kiini cha kusambaratika kwa ngome hii ya muziki wa dansi, ni lazima uangazie mambo makuu matano yafuatayo:


1. Mkataba wa Siri wa Wilson na Mpasuko wa Ndani


Moja ya migogoro mikubwa iliyotikisa misingi ya Simba Wanyika ni ule uamuzi wa Wilson (Wilson Peter Kinyonga) kuingia mkataba wa siri na kampuni ya kurekodi muziki bila kumshirikisha au kumtaarifu ndugu yake, George Peter Kinyonga. 


Ukweli wa jambo hili ulikuja kubainika kwa mshangao mkubwa wakati bendi ilipokuwa inajiandaa kurekodi nyimbo maalum kwa ajili ya ziara (tour songs). 


Suala hili liliacha jeraha kubwa la kiitikadi na uaminifu ndani ya uongozi wa bendi.


2. Suala la Vyombo: Tuzo au Mtego wa Kampuni?


Kuna maandiko na simulizi za kihistoria zinazodai kuwa Simba Wanyika walikabidhiwa seti ya vyombo vya muziki na kampuni moja ya kurekodi. 


Hata hivyo, "msada" huo haukuwa wa bure; vyombo hivyo vilitolewa kama malipo mbadala (barter trade) ya kazi na hakimiliki za nyimbo zao. 


Hali hii ilichangia kuwanyonya wasanii hao kwani thamani ya nyimbo zao ilizidi mbali gharama ya vyombo walivyopewa.


3. Mpango wa George Kujimwambafai na Hatimiliki

Kama jibu au matokeo ya migogoro ya ndani, George Kinyonga naye alianza kuchukua hatua za kujilinda. 


Kulikuwa na mpango madhubuti wa George kwenda kurekodi na kusajili nyimbo zake binafsi kwa jina lake mwenyewe (kama hakimiliki yake), hatua iliyoashiria wazi kuwa bendi ilikuwa inaelekea ukingoni mwa mgawanyiko.


4. Sakata la Wimbo "Sina Makosa"

Wimbo wa "Sina Makosa" unabaki kuwa moja ya nembo kubwa za muziki wa Afrika Mashariki, lakini nyuma yake kuna utata mkubwa. 


Maandiko mbalimbali ya kihistoria yanathibitisha uwepo wa mgogoro mzito wa kimaslahi na kisheria kuhusu nani hasa alikuwa na haki miliki ya wimbo huo, nani alipaswa kulipwa mirabaha (royalties), na jinsi jina la wimbo wenyewe lilivyobeba ujumbe wa kijembe au majibu ya migogoro yao ya ndani.


5. Njama za Makampuni na Kupendelewa kwa Les Wanyika


Hali ilizidi kuwa mbaya pale kampuni ya kurekodi ikitumia ushawishi wa jina la mfanyakazi wake mmoja wa ndani ilipoanza kuonyesha upendeleo wa wazi. 


Kampuni hiyo ilishikilia msimamo wa kutaka kurekodi na kupromoti nyimbo za Les Wanyika pekee (bendi iliyozaliwa baada ya kumegeka kwa Simba Wanyika), na kuamua kutaka kuipiga kumbo na kuisusa kabisa Simba Wanyika.


Umuhimu wa Kuhakiki Taarifa

Kifupi, zipo habari nyingi sana za Simba Wanyika na bendi zote zilizozaliwa kutoka kwayo (uzao wake) ambazo hazijawahi kusimuliwa ipasavyo, au zimesimuliwa kwa upendeleo. 


Hii ndiyo maana kuna umuhimu mkubwa wa **kuacha kila mwenye taarifa azilete mezani, kisha ije kazi ya ziada na ya kitaalamu ya kuzihakiki (cross-checking) ili kupata ukweli usiopotoshwa.


Mfano mzuri wa umuhimu wa uhakiki ni katika sakata la mwanamuziki Mponda . Katika maandiko fulani, ilielezwa kuwa Mponda alikuwa mmoja wa wajumbe wa Simba Wanyika. 


Hata hivyo, baada ya kufanya ufuatiliaji wa kina na kuwasiliana moja kwa moja na mwandishi wa taarifa hiyo, mwandishi huyo aliomba muda wa siku mbili kufanya utafiti upya. 


Aliporudi, alikiri kuwa taarifa hiyo haikuwa ya kweli na kushauri kipengele hicho kiondolewe kabisa ili kulinda ukweli wa historia.


Hii inadhihirisha kuwa, bila kufanya tafiti za ana kwa ana na kuhoji vyanzo, historia ya muziki wetu inaweza kujaa upotoshaji mkubwa.


Jana niliongea na Luza Jonh, Bindo Kipanga nilipata maelezo mazuri tu.


Makala haya kwa hisani ya : BARIKI NGOWO -MUZIKI HALISI 


KAA TAYARI KWA AJILI YA ZIFF 2026


Pazia la Msimu wa 29 wa Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF 2026) linakaribia kufunguliwa rasmi kuanzia Juni 24 hadi 28, 2026 visiwani Zanzibar! Safari hii mambo ni makubwa, ya kidijitali, na ya kitamaduni kwelikweli! 


Hapa kuna dondoo 4 za moto unazotakiwa kuzijua:


🤖 Akili Unde (AI) Kukutana na Sinema: Chini ya CEO Joseph Mwale, tamasha la mwaka huu linakuja na kaulimbiu ya “Akili Unde (AI) na Sanaa ya Usimuliaji wa Hadithi.” 

Kutakuwa na warsha kali na mada nzito kutoka kwa wataalamu kama Lisa Russell na Robert Mwampembwa, wakijadili jinsi AI inavyoweza kuleta mapinduzi kwenye filamu za Kiafrika licha ya changamoto za kishujaa za mtandao na umeme!

🏹 Uhalisia wa Kutisha: "We Are Hadza": Safari hii hakuna kuigiza! Zaidi ya Wahadzabe 20 watasafiri kutoka porini hadi kwenye mchanga wa Zanzibar kuleta filamu yao ya makala "We Are Hadza" (African Premiere). Kutakuwa na usiku maalum wa Hadzabe Dinner, ngoma za asili, na maonyesho ya kurusha mishale mubashara! 🍖🥁

🏆 Mnyukano wa Filamu 65: Mkurugenzi wa Tamasha, Khatibu Madudu, ametangaza kuwa kati ya filamu zaidi ya 400 zilizowasilishwa duniani kote, ni filamu 65 tu kali zilizopenya kwenye mchujo! Zipo filamu fupi, ndefu, vikaragosi, na zile za kwanza kuonekana Afrika (African Premieres) kutoka Uturuki, Zambia, Uganda, na hapa nyumbani!

🗳️ Tuzo za People’s Choice: Mashabiki mmepewa nguvu! Mwaka huu utapiga kura kuchagua Tamthilia na Waigizaji unaowapenda zaidi kupitia tuzo za People's Choice Awards, mbali na zile tuzo kubwa za kijadi za Golden Dhow Awards.

Kutoka siku 9 hadi siku 5 za burudani safi na ya kiwango cha juu—hili si la kukosa! 🏝️🎥


Kwa hisani ya ✏️ Taarifa na Beda Msimbe, BSKY Media.


#ZIFF2026 #AkiliUnde #HadzaInZanzibar #AfricanCinema #GoldenDhow #FilamuZetu #ZanzibarEvents #SupportLocalCinema

UNESCO NATIONAL COMMISSIONS PREPARE AND ORGANISE STATE PARTY PARTICIPATION IN UNESCO MEETINGS

 


State party participation in the UNESCO meetings including the World Heritage Committee meetings involves a coordinated diplomatic and technical approach.

Delegations to the World Heritage Committee Meetings are typically led by a senior minister (often the Minister of Tourism, Natural Resources, Heritage, Antiquity or Culture) and carefully coordinated by the UNESCO National Commission to ensure alignment with global standards.

Participation in World Heritage Committee Meetings

The roles, structure, and operational framework for this participation include:


1. Key Roles and Responsibilities

Ministerial Delegation Lead

The Minister provides high-level policy direction, advocates for the State’s nominated sites, and votes on crucial inscription decisions. They represent the nation’s broader geopolitical and conservation interests on the global stage.


UNESCO National Commission

This body acts as the primary national coordinator. They manage logistical preparations, coordinate pre-session consultations with relevant government ministries, synthesize scientific and heritage reports, and brief the ministerial delegation.


Technical Experts & Permanent Delegations

Supporting the delegation are technical experts (e.g., conservators, archaeologists) and the State Party’s Permanent Delegation to UNESCO in Paris, ensuring day-to-day engagement with advisory bodies like IUCN and ICOMOS.

Prof. Hamisi Masanja Malebo Executive Secretary UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania



2. Preparation and Coordination Workflow

Briefing & Dossier Review

The National Commission compiles scientific evidence, conservation statuses, and management plans to prepare the Minister for committee debates.


Side Events & Bilateral Meetings

Ministers and the coordinating commission host side events or hold bilateral meetings with other World Heritage Committee member states to garner support for pending site nominations and other pertinent issues.


Decision Making

The Minister casts votes on inscription proposals, reviews the State of Conservation reports of existing World Heritage sites, and allocates funds from the World Heritage Fund.


National Commission Coordinator

The national UNESCO secretariat acts as the primary liaison between the State Party and UNESCO, ensuring logistical coordination and policy alignment across domestic ministries.


Permanent Delegate to UNESCO

An ambassador-level diplomat (or representative) based at the UNESCO headquarters in Paris, who handles ongoing Committee business, preliminary meetings, and day-to-day operations.


Technical Experts

Specialists from state heritage bodies (such as antiquities departments, wildlife services, or environmental agencies) who review scientific and conservation dossiers.


Key Responsibilities at the Committee Meeting

Site Nominations

Presenting and defending the State Party’s own proposals for inscription onto the World Heritage List.


State of Conservation

Responding to, debating, and voting on monitoring reports concerning the health and management of existing World Heritage sites, particularly those threatened by development or conflict.


Policy and Budget

Participating in decisions that allocate the World Heritage Fund and define the convention’s global strategic framework.


A State Party delegation at a UNESCO World Heritage Committee meeting is typically a high-level diplomatic and technical contingent.


Delegations from the 21 elected committee members often include Senior National Ministers, Permanent Delegates to UNESCO, and representatives from the UNESCO National Commission.


Key Components of These Delegations Generally Include:

Delegation Head (Minister/Ambassador)

Led by a relevant cabinet minister (such as the Minister of Tourism, Culture, Natural Resources, Antiquity or Environment) or the State Party’s Ambassador and Permanent Delegate to UNESCO. They deliver high-level national policy statements and vote on key matters.


National Commission Coordination

The UNESCO National Commission frequently acts as the primary focal point. They coordinate the delegation’s preparatory work, liaise between national ministries and ensure alignment with the World Heritage Convention.


Technical Experts

Specialists from bodies such as wildlife services, environmental authorities, and cultural heritage and antiquities. They advise on technical nomination files, boundary modifications, and state of conservation reports.


Written by:

Prof. Hamisi Masanja Malebo, Executive Secretary UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania


Edited by:

Julitha August Mlay, Public Relations and Communications Officer UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania

TANZANIA YASHIRIKI JUKWAA LA UTALII, BIASHARA NA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA MISRI

 


Cairo, Misri, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb) ameshiriki Ufunguzi wa Jukwaa la Utalii, Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Misri Juni 8, 2026 linalofanyika  jijini Cairo, Misri likiwakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za utalii, wafanyabiashara, wawekezaji na wadau mbalimbali kutoka nchi hizo mbili kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kukuza fursa za biashara, uwekezaji na utalii. 

Jukwaa hilo limeandaliwa chini ya kaulimbiu inayohamasisha uhusiano kati ya Bahari ya Mediterania na Bahari ya Hindi kupitia masoko, utalii, biashara na uwekezaji, likitoa fursa kwa wadau kujadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano yenye manufaa kwa pande zote mbili. 

Aidha, washiriki walipata fursa ya kushuhudia video mbalimbali za kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na kufanya mikutano ya kibiashara (B2B) na majadiliano yaliyolenga kuanzisha na kuimarisha ushirikiano kati ya wadau wa sekta binafsi kutoka Tanzania na Misri. 

Jukwaa hilo limehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Utalii na Mambo Kale Misri, Mhe. Yomna El Bahar, Balozi wa Tanzania nchini Misri Meja Jenerali Richard Makanzo na viongozi wengine mbalimbali wa Serikali kutoka nchi zote mbili.






Monday, June 8, 2026

DC LINDI MHE. VICTORIA MWANZIVA ATEULIWA KATI YA WANAWAKE 15 BARANI AFRIKA KUSHIRIKI PROGRAMU YA UONGOZI KWA WANAWAKE YA EJS CENTRE


Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Victoria Mwanziva, ni miongoni mwa Wanawake 15 Barani Afrika waliopata bahati ya kuchaguliwa kwenye program maalum ya Uongozi kwa Wanawake, mafunzo ambayo yanafanyika nchini Liberia na Sierra Leone.

Katika mchujo huo, Mhe DC Mwanziva amebainisha kuwa, amepitia mchujo wa maombi ya zaidi ya Wanawake viongozi 600 Barani Afrika.


Kauli ya Mhe. DC Mwanziva:

"Ninamshukuru Mwenyezi Mungu nimechaguliwa kuiwakilisha Tanzania kushiriki katika Programu mahususi na maalumu ya Uongozi kwa wanawake inayoratibiwa na Rais wa kwanza Mwanamke Barani Afrika- Rais Mstaafu wa Liberia- Mhe Ellen Johnson Sirleaf.

Programu hii inayojulikana kama *“Amujae Leadership Initiative”* chini ya Ellen Johnson Sirleaf Presidential Centre for Women and Development- EJS Centre ninaenda kuungana na wanawake viongozi waliopata fursa na heshima ya kushiriki wakiwemo- Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii wa Namibia Mhe Dkt Esperance Luvindao, Waziri wa Mazingira wa Guinea Mhe Djami Diallo,

Wabunge mbalimbali kama Mbunge kundi la wanawake kutoka Senegal Mhe Anta Diack na wanawake Viongozi wa Mashirika na Taasisi mbalimbali barani Afrika kama Dr Anneline Chetty Mtendaji mkuu wa kituo cha Biashara, Viwanda na Uwekezaji Afrika ya Kusini.


Aidha, nimekuwa miongoni mwa Wanawake 15 Barani Afrika waliochaguliwa kushiriki mafunzo haya nchini Liberia na Senegal- baada ya kupitia mchujo wa maombi ya zaidi ya wanawake viongozi 600 barani Afrika- nikilivutia jopo la mchujo na haswa kilichowavutia juu ya kunichagua ni sababu ya kazi ninazofanya za uongozi wa jamii hususani maeneo ya vijijini na zenye kugusa jamii moja kwa moja na vijana kupitia utendaji wangu kama Mkuu wa Wilaya ya Lindi- nafasi niliyoaminiwa kuteuliwa na Rais wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan.

Programu hii ya kimkakati na kihistoria imelenga kuleta pamoja Wanawake viongozi kutoka barani Afrika na kuwapa uwanda wa kukutana na kujadiliana kwa pamoja masuala ya Uongozi kwa wanawake yenye mrengo wa ajenda za maendeleo barani Afrika.

Mafunzo haya yana tija kubwa kwenye uwakilishi wa nchi ya Tanzania barani Afrika na zaidi kuzidi kufungua fursa za mashirikiano mema baina ya mataifa ya Barani Afrika." Amebainisha DC Mwanziva.



#Tags:

@ejscenter #EllenJohnsonSirleaf #AmujaeInitiative #AmujaeForum #MonroviaLiberia #Tanzania

Sunday, June 7, 2026

UNESCO NATIONAL COMMISSIONS EXPANDED THEIR PORTFOLIOS BEYOND EDUCATION SINCE THE 1960s

Prof. Hamisi Masanja Malebo, Executive Secretary, UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania.


Since the 1960s, UNESCO National Commissions have significantly broadened their portfolios to operate as multidisciplinary catalysts. They have shifted beyond basic education conventions to encompass science, social sciences, culture, communication, and human rights, spearheading initiatives like the Sustainable Development Goals (SDGs), ethics of Artificial Intelligence, and climate change resilience.

Evolution of the Operational Scope

The evolution of their operational scope spans several core areas:

Science and the Environment

Commissions coordinate national participation in the Man and the Biosphere (MAB) Programme, promote UNESCO Global Geoparks, and advance sustainability science.

Culture and Heritage

They lead the domestic implementation of the World Heritage Convention and the Convention for the Safeguarding of the Intangible Cultural Heritage, managing transnational serial nominations and community-based preservation projects.

Information and Communication

They champion press freedom, media literacy, digital skills, and the Memory of the World Register, while tackling emerging global issues such as disinformation and the ethics of Artificial Intelligence.


Interdisciplinary Networks

Commissions foster robust civil society engagement through partnerships with UNESCO Chairs and UNESCO Associated Schools, acting as vital institutional bridges between governments, academia, and the public.


UNESCO’s Expanded Portfolio for National Commissions

UNESCO’s expanded portfolio for National Commissions has pivoted to include specialized science, technology, and cultural diplomacy to address rapidly emerging global issues. With 199 commissions acting as constitutional bridges, they now manage localized challenges including the ethical governance of Artificial Intelligence, climate disruption, and digital disinformation.



Core Focus Areas

*Science and Technology Diplomacy*

Bridging scientific research with international policy. Commissions support cross-border collaboration on transboundary water management, climate change resilience, and the ethical implementation of the global Recommendation on the Ethics of Artificial Intelligence.


Cultural and Heritage Diplomacy

Using international programs such as World Heritage Sites and the List of Intangible Cultural Heritage to foster cooperation across borders. Commissions also facilitate high-level dialogues celebrating linguistic diversity.

Information and Digital Literacy

Tackling the spread of misinformation. Commissions host media and information literacy programs designed to protect independent journalists and equip communities with necessary digital skills.


Peacebuilding and Crisis Management

Leveraging global networks to protect cultural heritage and educational infrastructure in areas threatened by armed conflict and natural disasters.

To strengthen these efforts, UNESCO’s governing bodies have recently launched updated global guidelines to provide practical tools to maximize the impact of National Commissions at the country level.

UNESCO National Commissions as a Bridge Between UNESCO and Member States

UNESCO’s 199 National Commissions (NatComs) operate as a unique bridge between the United Nations and Member States. Recently reinforced by new UNESCO Global Guidelines, their portfolios have expanded beyond basic liaison functions to include active programme execution, localized sustainable development, and targeted capacity building.

Core Expanded Functions

The UNESCO Charter of National Commissions outlines several modernized responsibilities:

Operational Execution

Shifting from pure advisory roles to actively managing and implementing cross-sectoral programmes.

Decentralized Coordination

Strengthening integration between UNESCO and local partners to deliver impactful, community-focused projects.

Standard-Setting and Policy

Advising national governments on UNESCO’s standard-setting work, including the implementation of Open Science and Ethical AI frameworks.

Network Mobilization

Bridging civil society, academia, and the mass media with intergovernmental dialogue to ensure localized impact.

Focus on Priority Areas

The expanded portfolio heavily integrates UNESCO’s global priorities:

Priority Africa

Supporting conservation (e.g., through the African World Heritage Fund), promoting quality education, and advancing science-based solutions.

Gender Equality

Integrating inclusive policies and expanding initiatives to tackle intersectoral issues, such as gender-based violence.


Written by Prof. Hamisi Masanja Malebo, Executive Secretary, UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania.

 Edited by Julitha August Mlay, Public Relations and Communications Officer, UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania.

BARAZA LA TIBA ASILI NCHINI LAFUTA USAJILI DAWA POWAFUL BANANA NA VITAMAX ,LAPIGA MARUFUKU 'JOY' KUINGIZWA SOKONI.

 


Na ABDU MADENGE, WAF - DODOMA 


Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini limefuta usajili wa dawa ya Powaful Banana Medicine, kupiga marufuku uingizwaji na matumizi ya dawa ya Vitamax, pamoja na kuamuru kuondolewa sokoni kwa toleo namba MN1060 la dawa ya Joy. 

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya ukaguzi na vipimo vya maabara kubaini uwepo wa mchanganyiko wa kemikali hatari za kisasa na sumu kuvu kwenye bidhaa hizo kinyume cha sheria.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Prof. Nicolao Joseph Otieno, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Ofisi za Wizara ya Afya Juni 05, 2026 Mkoani Dodoma ambapo ameeleza maamuzi hayo yanajiri kufuatia zoezi maalum la ufuatiliaji wa dawa sokoni (Post Market Surveillance) lililofanyika katika mwaka wa fedha wa 2025/2026, ambalo lilibaini ukiukwaji mkubwa wa Kanuni za Usimamizi wa Dawa za Tiba Asili kifungu cha 13(1)(a) na (b).

Prof. Otieno ameongeza kuwa Uchunguzi wa kimaabara umeonesha dawa ya Powaful Banana (inayotengenezwa na Powaful Products Company Ltd) na Vitamax (kutoka kampuni ya Superfood International ya Malaysia), ambazo zimekuwa zikitumika kuongeza nguvu za kiume, zimechakachuliwa kwa kuongezewa kemikali za kisasa za Sildenafil, Tadalafil, pamoja na dawa za maumivu aina ya Tramadol na Paracetamol. 

“Tunaonya matumizi ya kemikali hizo bila usimamizi wa daktari yanaweza kusababisha magonjwa ya moyo, kufeli kwa ini na figo, shinikizo la damu, na hata vifo vya ghafla.” amesema Prof . Otieno.

Sambamba na hatua hizo, Baraza pia limebaini kuwa toleo namba MN1060 la dawa ya Joy (Usajili Na. TZ25TM0010) lina kiwango kikubwa cha sumu kuvu (mycotoxins) kinachoweza kusababisha saratani ya ini na uharibifu wa figo. Hali hii imetajwa kutokana na kutokuzingatiwa kwa viwango bora vya ukaushaji na uhifadhi wakati wa uzalishaji.

“Baraza tunatoa onyo kali kwa watengenezaji wote nchini ambao dawa zao zimebainika kuwa na mapungufu katika vifungashio, taarifa za lebo, ujazo, na maelezo ya dozi, tunawataka kufanya maboresho ya haraka kulingana na vigezo vya usajili kwa lengo la kulinda afya na usalama wa watumiaji.” amesema na kuongeza  Prof. Otieno.