ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, July 30, 2026

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA NA MKURUGENZI MTENDAJI MUHIMBILI WAWEKA MIKAKATI MADHUBUTI KUBORESHA MFUMO WA MALIPO YA HUDUMA ZA AFYA



Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Dellilah Kimambo, kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za afya na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha mfumo wa malipo ya huduma ili kuwawezesha wananchi kupata huduma kwa urahisi, haraka, kwa ufanisi na kuondoa malalamiko ya wananchi.

Katika kikao hicho, Dkt. Magembe amesisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma za afya, akimtaka Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha mifumo ya TEHAMA ya hospitali inaendelea kuimarishwa ili kurahisisha mchakato wa malipo ya huduma, kuongeza uwazi kwa wananchi, kupunguza usumbufu na muda wa kusubiri kwa wagonjwa, pamoja na kuondoa udanganyifu.

“Mwananchi apate taarifa za malipo anayotakiwa kufanya kiganjani mwake kupitia simu ili kabla ya kulipa ajihakikishie kama malipo hayo ni sahihi au hapana”, amesema Dr Grace. 

Amemwelekeza Mkurugenzi wa Muhimbili kuimarisha usimamizi wa huduma za afya kupitia viongozi walioko chini yake wakiwemo wakurugenzi, mameneja na wasimamizi wote na endapo kutakuwa na watumishi wowote wasiowajibika achukue hatua zilizo chini ya mamlaka yake na mengine yanayohitaji Wizara kufanyia kazi, ayawasilishe ili hatua stahiki zichukuliwe. 

Amepongeza maboresho yanayoendelea kufanyika ikiwemo watumishi wanaofanya kazi kwa kujituma na weledi mkubwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Grace Magembe (kushoto) akifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Dellilah Kimambo


DC KYOBYA MGENI RASMI TUKIO LA KIHISTORIA "HIKE FOR A GIRL CHILD" UDZUNGWA AGOSTI 2

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Msomi Dkt. Dunstan Kyobya


KILOMBERO - 

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Wakili Msomi Dkt. Dunstan Kyobya anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi kwenye tukio la kihistoria la Matembezi ya Vilimani ili kupaza Sauti kwa Ajili ya Mtoto wa Kike, _"Hike for A Girl Child"_.

Tukio hilo lenye lengo la kuvunja ukimya na unyanyapaa masuala ya Hedhi Salama kwa Watoto wa Kike, litafanyika tarehe 2 Agosti 2026, katika Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Udzungwa, Wilaya ya Kilombero, Mkoa wa Morogoro.

Kwa mujibu wa Waratibu wa kampeni hiyo kutoka The Brighter Binti Foundation (TBBF) kwa Kushirikiana na Tanzania Save the Community Initiatives (TASACI),  Dkt. Kyobya anatarajiwa kuzindua daraja la Utalii katika njia ya Sonjo Route tayari kwa matembezi ya vilimani.

"Agosti 2, saa 1:00 Asubuhi, Mkuu wa Wilaya Dkt. Kyobya atazindua rasmi daraja la Utalii, kisha kufanya 'Hike' njia ya maporomoko ya maji ya Sanje ambapo washiriki wote tutajumuika," wamesema waratibu hao.

Mchana, matukio mengine yatafanyika Shule ya Sekondari Sanje ambapo kutakuwa na shughuli mbalimbali zikiwemo: Mawasilisho mafupi juu ya Mwongozo wa Hedhi Salama, Elimu ya Malezi ya Familia, Afya ya Akili na Saikolojia.

Pia kutakuwa na Clinic ya Hedhi Salama kwa Jamii, Wanafunzi na Walimu, Maonesho ya bidhaa za Hedhi, Hotuba fupi ya Dkt. Kyobya kwa Wananchi, Wanafunzi na Wadau, sambamba na Utoaji wa Taulo za Hedhi kwa Shule ya Sekondari Sanje na zile za karibu kuzunguka Hifadhi ya Udzungwa.

The Brighter Binti Foundation wanasema wanaamini mabadiliko huanza na Jamii, hivyo matembezi hayo ya vilimani yataongeza umuhimu wa jamii kwa ujumla katika kuelewa na kuondoa unyanyapaa wa hedhi hapa nchini.

_"Mabadiliko huanza pale jamii inapopata uelewaji sahihi na kuondoa unyanyapaa wa hedhi. Tunapanda mlima huu sio kwa raha tu. Tunapanda kwa ajili ya Mtoto wa Kike"._

The Brighter Binti Foundation imewashukuru wadau wote wakiwemo: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Halimashauri ya Wilaya ya Kilombero, Hifadhi ya Taifa ya Udzungwa - TANAPA, TASACI, RTU, Wizara ya Afya, SAFEPAD, She Foundation Tanzania, ICON, FOCAYO, Next Fox Adventures, ARQ, PEPAIN, ToneHai, ONE DRAIN, SAWA na wadau wengine.



Wednesday, July 29, 2026

SIMBA SC ELIMINATED CECAFA KAGAME CUP 2026

Simba SC are officially out of the competition. 🇹🇿❌

The Tanzanian giants have collected just 2 points from 2 games, with one match remaining against Singida Black Stars.

Even if Simba win their final game, they can only reach 5 points.

That won’t be enough to finish as the best 2nd-placed team and qualify for the semi-finals, with Al Hilal and Rayon Sports already on 6 points.

A disappointing campaign for Simba. 

#CECAFAKagameCup2026 #AfricanFootball

#NguvuMoja

JE KUMBUKUMBU HII INA KUKUMBUSHA NINI?.


Na. Bariki Ngowo, Tanzania.

Baada ya Tanzania kupata uhuru mwaka 1961, serikali ilianza kujenga uchumi unaotegemea umiliki wa umma kupitia sera za Ujamaa na Kujitegemea. 

Sekta ya utalii ilitambuliwa kuwa chanzo muhimu cha mapato ya taifa, hivyo serikali ikaamua kuanzisha taasisi mbalimbali za kusimamia hoteli, safari na huduma za watalii.

Miongoni mwa taasisi hizo ilikuwa State Travel Services Ltd. (STS), iliyoanzishwa mwaka 1970 ikiwa kampuni tanzu ya Tanzania Tourist Corporation (TTC). 

Jukumu lake lilikuwa kutoa huduma za uwakala wa safari, kuhifadhi tiketi za ndege, kupanga safari za watalii, pamoja na kuhudumia serikali, mashirika ya umma na wananchi.

Katika kipindi hicho, TTC ilisimamia mtandao mpana wa hoteli na kampuni za utalii nchini. 

Mbali na STS, ilisimamia Kilimanjaro Hotel, New Africa Hotel, New Safari Hotel, Mwanza Hotel, Mount Meru Hotel pamoja na malazi na lodges nyingi za mbugani. 

Mfumo huu uliifanya serikali kuwa mdau mkuu wa sekta ya utalii nchini.

Ili kuimarisha utalii katika Kanda ya Kaskazini, serikali ilianzisha Mount Meru Hotels Ltd. mwaka 1973, kampuni iliyokuwa chini ya TTC kwa umiliki wa asilimia 80. 

Kampuni hiyo ilisimamia ujenzi na uendeshaji wa Mount Meru Hotel mjini Arusha, ambayo ilikamilika mwishoni mwa miaka ya 1970 na kuwa hoteli muhimu kwa watalii na mikutano ya kimataifa.

Ingawa kuna simulizi zinazodai kuwa Mount Meru Hotel ilijengwa na kampuni ya Israel, hadi sasa hakuna nyaraka rasmi zilizopatikana zinazotaja jina la mkandarasi wa awali. 

Tofauti na Kilimanjaro Hotel, historia ya ujenzi wa Mount Meru Hotel haijawekwa wazi katika kumbukumbu za umma zinazopatikana.

Katika miaka ya 1980, sekta ya utalii ilikumbwa na changamoto za kiuchumi, hivyo serikali ilianza kushirikisha kampuni za kimataifa katika usimamizi wa baadhi ya hoteli zake ili kuboresha huduma na kuongeza ushindani. 

Hatua hizi zilikuwa sehemu ya maandalizi ya mageuzi ya uchumi yaliyofuata.

Kuanzia mwishoni mwa miaka ya 1980 na hasa miaka ya 1990, Tanzania ilianza kutekeleza sera za ubinafsishaji. 

Mashirika mengi ya umma yalivunjwa, kuuzwa au kubadilishwa mfumo wa uendeshaji. 

Hali hiyo iliathiri pia STS, ambayo ilipoteza nafasi yake baada ya kampuni binafsi za usafiri na uwakala wa safari kuingia kwa wingi sokoni.

Mount Meru Hotel nayo iliendelea kupitia mabadiliko hayo. 

Hatimaye kampuni ya Mount Meru Hotel Ltd. ilibinafsishwa mwaka 2004, na baadaye hoteli ikafanyiwa ukarabati mkubwa na kurejea katika hadhi yake kama moja ya hoteli bora za Arusha zinazohudumia utalii na mikutano ya kimataifa.

Historia ya Kilimanjaro Hotel ni ya kipekee. Hoteli hiyo ilifunguliwa mwaka 1965 ikiwa hoteli kuu ya serikali kwa ajili ya kupokea wageni wa kimataifa. 

Mradi huo ulifadhiliwa na Israel na Uingereza, ukajengwa na kampuni ya Israel Solel Boneh, huku usimamizi wa mwanzo ukifanywa na kampuni ya Israel Mlonot. 

Mwaka 1972, hoteli hiyo ilitaifishwa na kuhamishiwa chini ya TTC.

Kwa ujumla, historia ya STS, Mount Meru Hotel na Kilimanjaro Hotel inaonyesha namna serikali ya Tanzania ilivyowekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya utalii baada ya uhuru. 

Taasisi hizo zilikuwa nguzo muhimu za maendeleo ya utalii wakati wa Ujamaa, kabla ya mageuzi ya uchumi na ubinafsishaji kubadilisha kabisa mfumo wa umiliki na uendeshaji wa sekta hiyo nchini.

Tuesday, July 28, 2026

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAKABIDHI TAFORI GARI LA UTAFITI KUIMARISHA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MISITU NA NYUKI



Morogoro | Julai 28, 2026

Serikali kupitia Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kuimarisha uwezo wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) kwa kuikabidhi gari jipya la utafiti litakalosaidia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za utafiti wa misitu na ufugaji nyuki nchini.

Gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser Prado Station Wagon lenye namba za usajili STN 7536 limekabidhiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Bw. Daniel Pancras, kwa kushirikiana na Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF), Dkt. Tuli Msuya, kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI, Dkt. Revocatus Mushumbusi, katika hafla iliyofanyika Julai 28, 2026, Makao Makuu ya TAFORI, Morogoro.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii wakati wa hafla hiyo, Bw. Pancras alisema makabidhiano ya gari hilo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ya kuendelea kuzijengea uwezo taasisi kwa kuimarisha miundombinu na vitendea kazi ili ziweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

"Nashukuru Mfuko wa Misitu Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya sekta hii kwa kuendelea kujengea uwezo taasisi. Nawasihi watumishi wa TAFORI kutunza kitendea kazi hiki ili kiendelee kusaidia taasisi kutekeleza tafiti zenye matokeo chanya kwa maendeleo ya sekta ya misitu na nyuki na kwa maslahi ya taifa," alisema Bw. Pancras.

Kadhalika, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF), Dkt. Msuya, alisema kuwa kukabidhi gari hilo ni sehemu ya jitihada za Mfuko katika kuzijengea uwezo taasisi za sekta ya misitu na nyuki ili ziweze kutekeleza majukumu yake ya kitafiti kwa ufanisi zaidi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI, Dkt. Revocatus Mushumbusi, aliishukuru Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) kwa kuendelea kuiwezesha taasisi hiyo kwa vitendea kazi vinavyorahisisha utekelezaji wa shughuli za utafiti.

"Tunashukuru Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na Mfuko wa Misitu Tanzania kwa kuendelea kutupunguzia changamoto za utekelezaji wa shughuli za utafiti. Gari hili litatuwezesha kuwafikia wadau kwa urahisi zaidi na kutekeleza shughuli za utafiti kwa ufanisi katika maeneo mbalimbali nchini," alisema Dkt. Mushumbusi.





MUHIMBILI NA MEGA WE CARE WATOA CHANJO, VIPIMO BURE MAADHIMISHO YA HOMA YA INI DAR

 

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ini, Dkt. Swaleh Pazi 


Dar es Salaam:

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Mega We Care Tanzania Limited leo Julai 28, 2026 wameanza kambi ya siku mbili ya upimaji na utoaji wa chanjo bure kwa wananchi. Kambi hii inafanyika Muhimbili Sokoine Drive Medical Centre (MNHSDMC) jirani na SGR, kuadhimisha Siku ya Homa ya Ini Duniani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ini, Dkt. Swaleh Pazi amesema ugonjwa wa homa ya ini bado ni tishio kubwa.
Mwaka 2024 pekee watu milioni 1.3 walifariki duniani kote kutokana na ugonjwa huo.

"Kwa hiyo tunawahimiza wananchi wajitokeze kwa wingi kupima na kupata chanjo. Homa ya Ini B inazuilika kwa chanjo, na C ina tiba. Usiogope unyanyapaa. Vipimo hivi ni bure na vinachukua muda mfupi tu," amesema Dkt. Pazi.

Kliniki ya Homa ya Ini ya Muhimbili kwa sasa inahudumia wagonjwa zaidi ya 5,000.
Lengo la kambi hii ni kuwafikia wananchi zaidi ya 1,000 katika siku mbili.

Afisa Habari wa Mega We Care, Bw. Mengi Ntasimba


Kwa upande wake, Afisa Habari wa Mega We Care, Bw. Mengi Ntasimba amesema kampuni hiyo imetoa vifaa vya uchunguzi na dawa kama sehemu ya kurejesha kwa jamii baada ya miaka 20 ya kuhudumu Tanzania.

Mmoja wa waliojitokeza, Joseph Chengula kutoka Kimara, amewapongeza waandaaji na kuwataka wananchi wengine kufika kupata huduma hiyo bure.

Kambi itaendelea hadi tarehe 29 Julai 2026.

#PimaMapema #HomaYaIni #Muhimbili #MegaWeCare






Monday, July 27, 2026

MALIASILI NA UTALII, NMB WAKUTANA KUJENGA UHUSIANO WA KIMKAKATI



Na. Mwandishi Wetu, 

Dodoma.


MENEJIMENTI  ya Wizara ya Maliasili na Utalii ikiongozwa na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Utalii Bw. Nkoba Mabula imekutana na kufanya mazungumzo ya kuimarisha uhusiano na uongozi wa Benki ya NMB ukiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Serikali Makao Makuu ya NMB Dodoma Bi. Vicky Bishubo.

Mazungumzo hayo ya Kimkakati baina ya pande hizo mbili yamefanyika leo Julai 27, 2026 katika Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Mtumba jijini Dodoma.

Akizungumzia kikao hicho, Naibu Katibu Mkuu Mabula amesema kimekuwa na tija kubwa kwani Benki ya NMB ni wadau muhimu wa Wizara ya Maliasili na Utalii hususani katika kuimarisha maeneo yake makuu ya Utalii na Uhifadhi.

“Ugeni huu wa wenzetu kutoka NMB unadhihirisha namna Wizara ya Maliasili na Utalii inavyozingatia umuhimu wa kukutana na wadau mbalimbali kama sehemu ya kujenga uhusiano wa karibu na pia kuimarisha utendaji kazi wa Wizara kwa wadau na wananchi kwa ujumla,” amesema Bw. Mabula.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Serikali NMB Makao Makuu Dodoma Bi. Bishubo amesema lengo la kutembelea Wizara ya Maliasili na Utalii ni muendelezo wa Mpango wa benki hiyo kutembelea wadau mbalimbali kwa nia ya kuimarisha uhusiano baina ya pande mbili husika.

Amesema kupitia Mpango huo, Benki ya NMB inaendelea kujipambanua kwenye soko na kujenga uhusiano wenye tija baina yake na wadau na hivyo kujiimaarisha zaidi katika mnyororo mzima wa utoaji huduma za kifedha nchini.

TUMAINI JIPYA:WATOTO SABA WAFUNGULIWA DUNIA YA USIKIVU MUHIMBILI



Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo, Julai 27, imewasha vifaa vya usikivu (Cochlear Implant) kwa watoto saba waliopandikizwa vifaa hivyo, ikiwa ni mwendelezo wa huduma za kibobezi za upandikizaji huo zilizozinduliwa rasmi mwaka 2017 ambapo hadi sasa hospitali imefanikiwa kuwafanyia upasuaji wa kupandikiza vifaa vya usikivu wagonjwa 115 na kuwa hospitali ya kwanza barani Afrika.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Bw. Emmanuel Tayari, amepongeza hatua hiyo na kubainisha kuwa serikali inaendelea kuweka mikakati thabiti ya kusogeza huduma za kibobezi karibu na jamii ili kuliokoa Taifa dhidi ya changamoto za kiafya zinazoweza kuepukika.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Dkt. Dellilah Kimambo, ameeleza kuwa tangu mwaka 2017 Wizara ya Afya kupitia Muhimbili iliazimia kimkakati kuleta huduma za kibobezi nchini lengo ikiwa ni kuzuia wagonjwa kusafiri nje ya nchi na kupunguza gharama kubwa walizokuwa wakizibeba wananchi na kupunguza rufaa za matibabu nje ya nchi ambayo yalikua yanagharimu takribani shillingi mil 120 kwa mgonjwa mmoja ambapo kwa sasa hivi matibabu hayo yanatolewa hapa hapa Nchini kwa gaharama ya TZS. 45 Mil.

"Sasa hivi duniani inajulikana kwamba mtoto mwenye matatizo ya kusikia akipandikizwa kifaa hiki kwa wakati husika, ataweza kusikia kama kawaida na kuepuka changamoto za kuwa kiziwi tulipoamua kuleta huduma hii hapa nchini, wagonjwa wengi waliokuwa wakikosa huduma hapo awali sasa wamefaidika, na inawawezesha kuendelea na maisha yao ya kawaida,"  amesema Dkt. Kimambo.

Muhimbili inaendelea kuboresha huduma hii ambayo inatajwa kuwa unatajwa kuwa muhimu katika kuhakikisha watoto wanaozaliwa au kupata changamoto za usikivu wanapata fursa sawa ya kusoma na kushiriki katika ujenzi wa Taifa bila kikwazo cha ulemavu wa kutosikia.












DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

 



📍Dar es Salaam,


Kufuatia kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini unaofanywa na Wizara ya Madini kupitia Kikosi Kazi (Taskforce), madini aina ya dhahabu Gramu 4,402.20 yenye thamani ya 

1,238,458,594.42 yamekatwa yakitoroshwa.

Hayo yamesemwa leo tarehe 27 Julai, 2026 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari.

"Serikali kupitia Wizara ya Madini iliunda Kikosi kazi ambacho kinahusisha vyombo vya dola ili kudhibiti biashara haramu ya madini na utoroshaji. Hii ni sehemu tu ya kazi ambazo zimeendelea kufanywa na Kikosi kazi hicho katika kuimarisha mfumo wa ufanyaji biashara ya madini"

"Ndugu zangu, dhahabu hii yenye zaidi ya thamani ya bilioni 1.2 haikupitia katika mfumo rasmi wa ufanyaji biashara ya madini na hivyo kupelekea Serikali kukosa mapato ambayo yangeisaidia kuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi" Alisisitiza Mhe. Mavunde.



Aidha, Waziri Mavunde alibainisha kuwa dhahabu hiyo iliyokamatwa imetaifishwa kwa mujibu wa taratibu za Sheria na imehifadhiwa Benki Kuu ya Tanzania.

Vilevile, Mheshimiwa Mavunde amekielekeza Kikosi Kazi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola kumhoji vizuri mtuhumiwa aliyekamatwa na dhahabu hizo kufahamu alikotoka na alikuwa anapeleka wapi, ili kuweza kutibu kabisa mzizi wa vitendo hivyo na kuvunja mnyororo wa wote wa utoroshaji.

Mhe. Mavunde alisisitiza kuwa, iwapo mtuhumiwa aliyekamatwa alikuwa na leseni ya ufanyaji biashara ya madini kufutiwa leseni hiyo mara moja na kuingizwa kwenye orodha maalum ya wenye makosa (blacklisted) ili asiruhusiwe tena kufanya biashara ya madini nchini.

Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde alitoa rai kwa wananchi wote kuzingatia na kufuata sheria na mifumo ya ufanyaji biashara ya madini ambayo tumejiwekea kupitia masoko ya madini na vituo vya ununuzi ambavyo vimesambaa Nchi nzima.

Sunday, July 26, 2026

MUHIMBILI, CAMBRIDGE WAZINDUA UTAFITI WA VINASABA KULETA MAPINDUZI KATIKA TIBA YA SARATANI YA TEZI KWA WATOTO AFRIKA

  





Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Cambridge cha Uingereza, wameaanzisha utafiti wa vinasaba unaolenga kuboresha matibabu ya saratani ya tezi kwa watoto nchini Tanzania na ukanda wa Afrika.

Akieleza kuhusu utafiti huo, Dkt. Advera Ngaiza, Bingwa wa Uchunguzi wa Magonjwa ya Saratani amesema mradi huo utahusisha uchukuaji wa sampuli za vinasaba na tishu kutoka kwa watoto wenye saratani ya tezi nchini Tanzania. 

Amesema sampuli hizo zitachakatwa katika Maabara Kuu ya MNH, huku uchunguzi wa kina wa kisayansi ukifanyika ili kuelewa kwa nini matibabu ya sasa hayatoi matokeo mazuri kwa watoto wa Kiafrika. 




"Lengo letu ni kugundua dawa salama, sahihi na yenye ufanisi mkubwa zaidi itakayosaidia kutibu saratani ya tezi kwa watoto katika ukanda wa Afrika."

Hatua hii inakuja baada ya kubainika kuwa mifumo mingi ya sasa ya matibabu haitoi matokeo yanayotarajiwa kwa watoto wa ukanda huu wa afrika ikilinganishwa na maeneo mengine duniani. 

Kupitia utafiti huu, watafiti wanatarajia kuweka msingi wa maendeleo ya tiba zinazozingatia tofauti za vinasaba, hatua ambayo inaweza kuleta mapinduzi makubwa katika huduma za matibabu ya saratani kwa watoto barani Afrika.








Tuesday, July 21, 2026

MSIMU WA PILI WA FuToPiA ZANZIBAR KUFANYIKA FUMBA TOWN AGOSTI 8-9


Na: Mwandishi Wetu,

ZANZIBAR.

Tukio la Muziki, Utamaduni na Ubunifu, FuToPiA Zanzibar Msimu wa Pili, litafanyika Fumba Town, Unguja tarehe 8 na 9 Agosti, 2026.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa FuToPiA, Lorenz Herrman, amesema mwaka huu tamasha linarudi kubwa zaidi baada ya mwanzo mzuri mwaka jana. 

“Tiketi zimeshaanza kuuzwa. Raia wa Tanzania Tsh 35,000, Afrika Mashariki Tsh 65,000, Kimataifa Tsh 130,000 na VIP Tsh 260,000,” amesema Herrman.

Tamasha linaloandaliwa na Busara Promotions litajumuisha muziki, sanaa, chakula, afya na soko la Kwetu Kwenu Market ikijumlisha pia Food Art Street, Afya Zone, Wonder Zone kwa watoto na michezo ya asili kwa Wazee.

Mkurugenzi wa FuToPiA, Lorenz Herrman


Wasanii wanaotarajiwa ni DJ Joozey, DJ Zoro, Baba Kash, Sauti Marley, Ruth Mlawa, DJ LAG kutoka Afrika Kusini, Vania Ice kutoka Burundi na wengineo wakiwemo mataifa ya Mexico, Canada, Chile na kwingine.

Mitindo itakayopigwa ni Afro House, Singeli, Afro Pop na midundo ya asili. 

Kutakuwa pia na usafiri wa mabasi maalum kutoka Stone Town na Uwanja wa Ndege wa Zanzibar.

Lengo la FuToPiA ni kuwakutanisha watu, kuwainua wabunifu na wajasiriamali na kuonesha Zanzibar ni zaidi ya fukwe.


Baadhi ya matukio na Wasanii watakaokuwepo Msimu wa pili wa FuToPiA Zanzibar Agosti 8-9.