ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, August 23, 2026

WATALII WAFURAHIA UTALII WA BOTI HIFADHI YA NYERERE

 



Hifadhi ya Taifa ya Nyerere imeendelea kuwavutia watalii kutoka ndani na nje ya Tanzania, huku utalii wa boti katika Mto Rufiji ukiwa miongoni mwa shughuli zinazotoa uzoefu wa kipekee kwa wageni.

Wakiwa ndani ya boti, watalii hupata fursa ya kuvuka kwenye mandhari ya kuvutia ya Mto Rufiji na kushuhudia kwa karibu wanyamapori mbalimbali wanaoishi pembezoni mwa mto, wakiwemo viboko, mamba, tembo na ndege wa aina mbalimbali. 

Tabasamu na furaha za watalii zinadhihirisha namna safari hii ya maji inavyobadilisha ziara ya Hifadhi ya Nyerere kuwa kumbukumbu isiyosahaulika.

Nyerere si safari ya kutazama wanyamapori pekee—ni uzoefu wa kuishi na kufurahia uzuri wa asili ya Tanzania kwa njia ya kipekee. 

Karibu Hifadhi ya Nyerere, panda boti, tembelea Mto Rufiji na ujionee Tanzania yenye sura ya kipekee.










Saturday, August 22, 2026

NAIBU SPIKA SILLO APONGEZA VIONGOZI KWA UBUNIFU WA MANYARA TANZANITE MARATHON

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daniel Sillo


Mbio za Hisani za Manyara Tanzanite Marathon zimefanyika leo mkoani Manyara, zikihudhuriwa na watu mbalimbali kutoka maeneo tofauti ya nchi pamoja na viongozi mbalimbali, huku lengo kuu likiwa ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kuokoa maisha ya watoto wachanga na watoto njiti.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daniel Sillo, aliyemwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mbio hizo, amepongeza uongozi wa Mkoa wa Manyara kwa ubunifu wa kuanzisha mbio hizo zinazolenga kuchangisha fedha kwa ajili ya kuimarisha huduma za afya na kuokoa maisha ya watoto wachanga na watoto njiti.

Sillo amesema hatua hiyo ni mfano wa ubunifu unaopaswa kuigwa na maeneo mengine nchini, akisisitiza umuhimu wa kushirikisha jamii na wadau katika kusaidia kuboresha huduma za afya.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Jafari Rajabu, amesema mbio hizo zimeleta tija kubwa katika juhudi za kuokoa maisha ya watoto, akiwataka wananchi na wadau kuendelea kuunga mkono jitihada zinazolenga kuboresha afya ya watoto.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amewashukuru wadau wote walioshiriki na kuunga mkono maandalizi ya mbio hizo, akisema ushiriki wao umewezesha kufanikisha azma ya kuchangisha fedha kwa ajili ya watoto wanaohitaji huduma maalumu za afya.

Baadhi ya washiriki wa mbio hizo wamesema, pamoja na kushiriki kwa ajili ya mazoezi na kuimarisha afya zao, wameona umuhimu wa kuwa sehemu ya harakati za kuchangia maisha ya watoto wachanga na watoto njiti.

Wamesema ushiriki wao katika Manyara Tanzanite Marathon umewapa fursa ya kufanya mazoezi huku wakitoa mchango wa moja kwa moja katika kusaidia kuokoa maisha ya watoto, hivyo kuwataka wananchi wengine kuendelea kushiriki katika matukio yenye malengo ya kijamii na kiafya.



















Monday, August 17, 2026

MASHINDANO YA NGALAWA YANOGESHA MSIMU WA PILI WA FuToPiA ZANZIBAR 2026



ZANZIBAR - Ngalawa ya "Baba Karudi" iliyoongozwa na Hassan Thajo imeibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya mbio za ngalawa yaliyofanyika Bahari ya Fumba.

Mashindano hayo yalishuhudia ushindani mkubwa kutoka kwa ngalawa 12 na ni sehemu ya program ya michezo ya asili katika msimu wa pili wa tamasha la FuToPiA Zanzibar lililofanyika tarehe 8-9 Agosti, 2026.

Katika mbio hizo, Ngalawa ya "Wape Kazi" iliyoongozwa na Nahodha Aboubakari Kondo ilishika nafasi ya pili, huku nafasi ya tatu ikinyakuliwa na Ngalawa ya "Utoto Raha" iliyoongozwa na Nahodha Hussein Thajo.

Akizungumza baada ya mashindano, Mratibu wa Michezo ya Asili wa FuToPiA Zanzibar, Joseph Klanda amesema mashindano hayo yanalenga kuwakaribisha wananchi wa maeneo ya Nyamanzi, Dimani na Fumba Town kujumuika na kufurahia tamasha hilo pamoja.

"Chombo cha 'Baba Karudi' washindi wa kwanza kilipewa nguvu na kampuni ya Fortitude Security. Chombo cha 'Wape Kazi' mshindi wa pili kilipeperusha bendera ya FuToPiA Zanzibar, na chombo cha mshindi wa tatu kilipeperusha bendera ya Clouds Media," amesema Klanda.

Aidha, amesema washindi wote kuanzia nafasi ya kwanza hadi ya 12 walipata zawadi ya fedha taslimu pamoja na shukrani za ushiriki.












TANAPA, GERMANY AGENCIES EXECUTE SH 19 BN COMMUNITY DEVELOPMENT PROJECTS AS THEY SEEK TO BALANCE CONSERVATION AND LIVELIHOOD IN NGORONGORO



By Edmund Salaho, Loliondo–Ngorongoro 


Aug. 17, 2026. Tanzania National Parks (TANAPA), in partnership with Germany’s development agencies, is implementing community development and conservation projects worth about 6.3 million euros ($7.4 million), equivalent to roughly Sh19 billion, in Ngorongoro District, Arusha Region. 

The programme seeks to improve community livelihoods and public services while strengthening conservation of the wider Serengeti ecosystem. 

It is being implemented under the Serengeti Ecosystem Development and Conservation Project (SEDCP), financed by the German government through KfW Development Bank, with support from the Frankfurt Zoological Society (FZS).

During Monday’s inauguration of the Enguserosambu Dispensary, representatives of Germany’s Federal Ministry for Economic Cooperation and Development (BMZ), KfW and other partners witnessed the handover of the facility. 

The state-of-the-art dispensary, located in Enguserosambu Ward, was constructed at a cost of Sh504 million (180,000 euros) and will serve about 5,000 people. 

Nuhu Daniel Massay, TANAPA Assistant Conservation Commissioner–National Parks Development, who also coordinates donor-funded projects, investments and parks planning, said the interventions demonstrate the importance of linking conservation with the wellbeing of communities living alongside protected areas. 

“Conservation cannot be separated from the livelihoods and wellbeing of communities. These investments demonstrate that protecting wildlife and ecosystems must go hand in hand with improving the lives of people living around protected areas,” Massay said. 

He added that better access to education, healthcare, water, markets and sustainable livelihoods could make communities stronger partners in protecting natural resources. 

Joachim Schmitt, Head of Delegation, said he was impressed by the scale and impact of the projects, adding that “the best is yet to come,” while commending Tanzania-Germany cooperation for showing how conservation and community development can reinforce each other.

Across the Serengeti ecosystem, SEDCP has supported 69 social infrastructure projects in Serengeti and Ngorongoro districts. 

These include 14 dispensaries, 16 classrooms, 23 houses for teachers and health workers, one dining hall, one dormitory, six feeder roads and eight charco dams. 

In Ngorongoro District, 36 community development projects have been implemented, with 15 completed and handed over to communities and 21 at various final stages. 

The projects include 11 classrooms, a dining hall, seven dispensaries, 10 houses for teachers and health workers, four feeder roads covering 46 kilometres and three charco dams.

The programme is also supporting livelihoods and sustainable land management through FZS. According to district officials, 23 Community Conservation Banks (COCOBAs) have provided self-employment and income-generating opportunities to 835 people—444 women and 391 men. 

SEDCP has additionally supported village land-use planning, issuance of Certificates of Customary Rights of Occupancy (CCROs) and community-based protection of forests and grazing areas in Serengeti, Ngorongoro, Bariadi, Bunda and Tarime districts. 

Ngorongoro District Administrative Secretary Hamza Hamza said the projects had improved access to education, healthcare and water while strengthening the relationship between conservation and community development. 

“These investments are not merely infrastructure. They have made a real difference in the lives of our people,” Hamza said, adding that communities were becoming more involved in protecting forests, grazing areas and other natural resources.

The German-backed programme is also designed to diversify household livelihoods and reduce pressure on natural resources. 

During Monday’s field visit, the BMZ and KfW delegation inspected the Charco Dam at Olorien Village, where officials explained its benefits to communities and livestock. 

The dam cost Sh1.1 billion (363,363.16 euros) and is located in Olorien Village/Magaiduru Ward, benefiting communities in Olorien and Magaiduru villages. 

It serves a population of 5,011 people and 109,838 livestock, including cows, goats, sheep and donkeys. 

TANAPA is the client, with the Ngorongoro District Executive Director, ward and village leaders, Rural Water Supply and Sanitation Agency (RUWASA) and the District commissioner, among key stakeholders.

The delegation later travelled to Lopolum village, where Maasai community members presented aspects of their traditional way of life and discussed the benefits and challenges of the programme. 

COCOBA groups demonstrated their savings and income-generating activities, while members of the Enguserosambu Forest Trust and village forest scouts explained their work protecting the community forest. 

The partnership brings together TANAPA, BMZ, KfW, the German Embassy, FZS and Tanzanian government authorities. 

Massay said TANAPA would continue working with development partners and local authorities to ensure projects are completed to the required standards and maintained for lasting benefits. 

He said the programme demonstrates the value of Tanzania-Germany cooperation in linking conservation with the socio-economic development of communities living near protected areas.












WAZIRI SORAGA: FuToPiA ZANZIBAR NI JUKWAA LA KUONGEZA UBUNIFU NA KUKUZA UCHUMI WA KIDIJITALI

  


Na: Mwandishi Wetu, Zanzibar


ZANZIBAR - Waziri wa Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu Zanzibar, Mudrik Ramadhan Soraga amepongeza tamasha la FuToPiA Zanzibar kwa kuanzisha jukwaa la ubunifu linalowezesha wadau mbalimbali kutoa mawazo juu ya ukuaji wa uchumi, masuala ya kidijitali na masoko.

Soraga amesema hayo katika jukwaa maalum la ubunifu wakati wa msimu wa pili wa tamasha la Muziki, Utamaduni na Ubunifu la FuToPiA Zanzibar, lililofanyika Fumba Town, Unguja tarehe 8 na 9 Agosti, 2026.

Katika jukwaa hilo, Soraga ameshiriki majadiliano maalum kuelezea mikakati ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, SMZ katika safari ya mageuzi ya kidijitali katika visiwa vya Zanzibar.

Amesema Zanzibar kwa sasa inapitia vipindi tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma kama kisiwa. Uchumi unakua kwa haraka na kila pembe kuna fursa za kiuchumi zinazojitokeza ikiwemo miradi ya maendeleo.

Aidha, amesema wao kama viongozi wa Serikali wanapongeza wadau kuja na majukwaa ya ubunifu kwani yanaisaidia Serikali kufikia malengo yake kwa ushirikiano na wadau.

"Kupitia majukwaa kama haya ya tamasha la FuToPiA Zanzibar, tunapata fursa ya kuelezea harakati na vipaombele vya Serikali tunavyotarajia kuvifanyia kazi kwa wananchi," amesema Soraga.

Ameeleza kuwa Serikali ya SMZ ina mipango ya kuweka miundombinu ya TEHAMA na mawasiliano ili wananchi wote waweze kuunganishwa na mtandao. Hii ni pamoja na kuweka mtandao wa wazi 'Public Wi-Fi' Zanzibar nzima.

Pia amesema Serikali imejipanga kuboresha mifumo ya ulinzi ili kulinda udukuzi wa taarifa katika mitandao ya simu, kibenki na huduma nyingine ili zibaki katika hali ya usalama.

Kuhusu ubunifu hususani kwa vijana wa Zanzibar, Soraga amesema Serikali imeweka nguvu kubwa ya kuunda mazingira bora na rafiki kwa vijana kuonesha vipaji vyao ikiwemo ubunifu wa mifumo na huduma za kidijitali. Amesema vijana watapewa nyenzo na maarifa ili waweze kutengeneza mifumo na kutoa masuluhisho mbalimbali.

Ameongeza kuwa Serikali ipo katika mpango wa kuboresha miundombinu ya msingi ya TEHAMA ikiwemo njia za kimataifa za mtandao wa intaneti 'International Gateway' na kuwa na kituo cha data 'Data Center' cha kuhifadhi taarifa. Amesema Serikali imekusudia kuwekeza zaidi ya dola za Marekani milioni 100 mpaka kukamilika kwa mradi huo.

Katika kuhakikisha huduma zinapatikana kwa urahisi, amesema watafanya kazi ya kuunganisha mifumo ndani ya Serikali hasa ya utoaji wa huduma ili kumsaidia mwananchi.

Kuhusu matumizi ya fedha taslimu, amesema dunia ya sasa inatakiwa kuachana na matumizi ya fedha taslimu na kuelekea kwenye matumizi ya mifumo ya fedha kupitia mitandao.

"Nichukue fursa hii kumpongeza na kumshukuru Rais wetu Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa utashi wake mkubwa na muelekeo alioutoa wa kuona Zanzibar ifikapo 2030 suala zima la matumizi ya fedha taslimu liwe historia na kwamba wananchi wote waweze kulipia huduma zao kwa njia ya mtandao, kibenki na kwenye simu," amesema Soraga.

Tamasha la FuToPiA Zanzibar linaandaliwa na Busara Promotions na linajumuisha muziki, sanaa, ubunifu, masoko na michezo.

Wasanii na ma-DJ mbalimbali walioshiriki ni pamoja na DJ Joozey, DJ Zoro, Baba Kash, Sauti Marley, Ruth Mlawa, DJ LAG kutoka Afrika Kusini, Vania Ice, Hammer Q na wengineo.