Advertisements

Saturday, June 3, 2023

ZAIDI YA WATU 200 WAFARIKI KWENYE AJALI YA TRENI INDIA


Zaidi ya watu 200 wamefariki dunia na wengine wengi wamejeruhiwa baada ya treni mbili za abiria na moja ya mizigo kugongana huko nchini India.

Kwa uchache watu 230 wamefariki na wengine 900 kujeruhiwa ambapo vyombo vya habari vya Kimataifa vimeripoti kuwa ajali hiyo inayoelezewa kuwa ni mbaya zaidi katika historian ya ajali za treni nchi India imetokea Mei 2, 2023 katika Jimbo la Odisha .

Zaidi ya magari 200 ya kubeba wagonjwa yalipelekwa kwenye eneo la tukio katika Wilaya ya Balasore, amesema Katibu Mkuu wa Jimbo la Odisha Pradeep Jena.



JKT YAKANUSHA UVUMI WA HABARI ZA UPOTOSHAJI KUHUSU MAFUNZO YA VIJANA KWA MUJIBU WA SHERIA


Na Ezekiel Mtonyole – Dodoma
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limewataka wazazi na walezi wa watoto wanaojiunga na mafunzo ya kwa mujibu wa sheria kupuuza habari za uvumi zilizonea kwenye mitandao ya kijamii ambazo zinalenga kulichafua Jeshi hilo kwa kuonyesha picha zinazoashiria kunyanyaswa kwa vijana hususa ni kwa vijana wa kike.

Akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya JKT Mkoani Dodoma ,Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema,JKT kwa kushirikiana na mamlaka nyingine watachukua hatua kwa waliohusika kutokana na kulichafua Jeshi hilo.

“Kumekuwa na uvumi wa namna hii kila mwaka tunapoita vijana hasa wa mujibu wa sheria unaoashiria JKT kuna manyanyaso,hii siyo kweli taarifa hizo zipuuzwe

JKT limekuwa likichukua vijana wa mujibu wa sheria kila mwaka na wale wa kujitolea kwa lengo la kuwapa vijana mafunzo yaliyoandaliwa ili kuwajenga uzalendo,ukakamavu na kuwajengea ari ya kulilinda Taifa lao kwa nguvu zao zote .”

WAZIRI PROF. MKENDA ATAKA VYUO VIKUU NCHINI KUIMARISHA UBORA WA ELIMU







Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ametoa wito kwa Vyuo Vikuu nchini kuona umuhimu wa kuimarisha ubora wa elimu ya juu ili iweze kuakisi mahitaji ya nchi na watu.

Waziri Mkenda ametoa wito huo Jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga warsha ya kubadilishana uzoefu kwa Wenyeviti na Wajumbe wa Mabaraza, Seneti na Bodi za Vyuo Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki ambapo amesema lengo ni kuwa na wahitimu bora.

Pia amevishauri Vyuo kuona ni namna gani wanaweka viwango vinavyofanana vya ubora kwa vyuo Vikuu vyote na kwamba kama hilo lisipofanikiwa kuwepo na gredi ambazo zitakuwa zikitumiwa na Vyuo Vikuu.

“Kuweka viwango itasaidia mhitimu wa Chuo A asionekane ni tofauti na wa Chuo B ili wawe na nafasi sawa za ajira. Msukumo mkubwa wa Vyuo ni kuwa na wanafunzi wengi, ninawaomba tusicompromise ubora wa elimu,”amesema Prof. Mkenda

Ameongeza kuwa kazi ya Vyuo Vikuu ni kuzalisha na kusambaza uelewa hivyo wahadhiri wa Vyuo vikuu lazima wawe wanafanya kazi za tafiti ili kutafuta ugunduzi mbalimbali wakati wanafundisha.

“Vyuo ni lazima viendele kujenga mazingira mazuri ya wahadhiri wake kufanya utafiti vipo baadhi ya Vyuo ambavyo inaonekana mtizamo wake ni kama utafiti ni chanzo cha mapato haiwezi kuwa hivyo na haitakiwi kuwa hivyo utafiti ni chanzo cha maarifa kwa hiyo lengo la utafiti kwa vyuo vikuu ni kuwa na maarifa mapya,”amesisitiza Prof. Mkenda

AFISA MANUNUZI AWEKWA NDANI MANYONI

Mkuu wa mkoa wa Singida Peter Serukamba amemsweka ndani afisa manunuzi ya halmashauri ya Manyoni Joseph Swila kwa kukiuka maagizo aliyoyatoa jana wakati alipofika kukagua ujenzi wa wodi ya wanawake, wanaume na chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya Manyoni.

RC Serukamba alimuagiza mhandisi wa halmashauri na afisa manunuzi kuongea mafundi ili kuongeza kasi ya ujenzi ambapo unatakiwa kukamilika kabla ya June 30 mwaka huu.

Mara ya kuona utekelezaji wa agizo Serukamba amekerwa na afisa manunuzi Joseph Swila baada ya kuonekana kumtetea mkandarasi anayejenga Majengo hayo huku akiwa hapatikani kwenye simu na haypo site.

KATIBU MKUU WIZARA YA MADINI AKUTANA NA WATENDAJI WA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA YAKE

 

Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Kheri Mahimbali, akiongoza kikao cha Watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Madini leo Juni 2, jijini Dar es Salaam. (Na Mpiga Picha Wetu).
Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali ameongoza kikao cha Watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Madini leo Juni 2, jijini Dar es Salaam. 

Kikao hicho cha Wadau wa Ndani wa Takwimu za Sekta ya Madini kililenga kujadiliana namna Bora ya Uzalishaji, Uchakataji na Usambazaji wa Takwimu na Taarifa zinazohuzu Sekta ya Madini ikiwemo Ukuaji na Mchango wa Sekta katika Pato la Taifa.

 Baadhi ya wadau wakiwa katika kikao hicho.

KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI DAR WAPEWA GARI JIPYA KWAAJILI YA KAZI MBALIMBALI ZA USALAMA BARABARANI

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP. MULIRO J. MULIRO amesema tafsiri ya maendeleo ya kiusalama yanapimwa kwa namna ambavyo watu wanaliami na kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kulisaidia Jeshi hilo kufanya kazi kwa weledi.

SACP. Muliro ameyasema hayo leo Juni 2, 2023 wakati Kamati ya usalama barabarani ya Kanda ya Dar es Salaam ikikabidhiwa gari jipya aina ya Toyota Hilux-Revo lenye thamani ya Tsh Milioni 90 kutoka kampuni ya Motisun group litakalotumiwa na kikosi cha Usalama barabarani  Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwaajili na kazi mbalimbali za usalama barabarani.

Akiongea kwa niaba ya kampuni ya MOTISUN GROUP, Bwana PRITESH KHIMJI amesema kampuni ya MOTISUN GROUP imeamua kutoa msaada huo baada ya kuridhika na hali ya usalama iliyopo |Jijini Dar es salaam ili kuunga mkono jitihada zinafanyika katika kudumisha usalama huo.

WATALII WA UWINDAJI WA KITALII WAONGEZEKA NCHINI, REKODI YAVUNJWA,..HAIJAWAHI KUTOKEA

 

Na Beatus Maganja

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Tanzania kupitia  Sekta ya Utalii imeshuhudia kuvunjwa Kwa rekodi ya idadi ya watalii waliotembelea Nchi Yetu Kwa shughuli mbalimbali za Kitalii wakiwemo watalii wa uwindaji wa kitalii ikiwa ni idadi kubwa kuwahi kuipokea kuliko Wakati wowote katika historia ya kuanzishwa Kwa sekta hiyo.

Ameyasema hayo leo June 2, 2023 akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa Mwaka wa fedha 2023/2024 Jijini Dodoma ambapo ongezeko hilo ni kwa mujibu wa taarifa za miezi 10 tu yaani kuanzia Julai mwaka jana hadi Aprili mwaka huu.
"Mheshimiwa Spika, pamoja na kuongezeka Kwa ujumla Kwa idadi ya watalii Kitaifa, katika kipindi hiki cha utekelezaji, taasisi kubwa za Utalii Nchini zimeshuhudia kuvunjwa Kwa rekodi ya idadi ya watalii katika maeneo yao..." amesema

"..Kwa Upande wa TAWA watalii wa Uwindaji wameongezeka kutoka 541 Kwa Mwaka 2021/22 hadi kufikia watalii wa uwindaji 692 Kwa kipindi Cha miezi 10 tu ya mwaka wa fedha 2022/23" amesema
Katika jitihada za kuendeleza uhifadhi wa rasilimali muhimu Mhe. Mchengerwa amesema Wizara imefanikiwa kupandisha hadhi Mapori Tengefu mawili (2) yaani Kilombero na Pololeti kuwa Mapori ya Akiba

Aidha amesema hatua hiyo imeongeza idadi ya Mapori ya Akiba Nchini kutoka 27 hadi 29 lengo likiwa ni kuimarisha ulinzi na matumizi endelevu ya rasilimali na utunzaji wa vyanzo vya maji.

WAZIRI DKT. CHANA ATETA NA KATIBU MKUU CAF

 

Na Shamimu Nyaki


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Pindi Chana  Juni, 2, 2023  amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika ( CAF) Bw. Veron Mosengo Omba jijini Algiers nchini Algeria.

Mazungumzo hayo pia yamehudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Algeria Meja Jenerali Mstaafu Mhe. Jacob Kingu pamoja na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu  Tanzania (TFF) Ndg. Wallace Karia, ambapo Mhe. Pindi amemshukuru kwa kupokea andiko (bid) la maombi ya Tanzania, Kenya na Uganda kuandaa kwa pamoja mashindano ya AFCON  mwaka 2027.

Mhe. Pindi pia amemuhakikishia Bw. Veron kuwa Tanzania imejipanga kuhakikisha inaandaa miundombinu ya kisasa yenye viwango vya Kimataifa kwa lengo la kukidhi vigezo vya CAF vya kuandaa mashindano hayo.

Bw. Veron ametumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuweka mazingira mazuri ya kufanyika kwa shughuli za michezo.


Thursday, June 1, 2023

SERIKALI IMEWAKARIBISHA WAWEKEZAJI WA BURUNDI KUWEKEZA TANZANIA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akizungumza na Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka nchini Burundi wenye lengo la kuwekeza nchini Tanzania wakati alipowasili katika mji wa Bujumbura nchini Burundi kuhudhuria Mkutano wa Dharura wa 21 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).


MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango amewakaribisha wawekezaji kutoka nchini Burundi kuwekeza Tanzania kutokana na mazingira bora ya biashara yaliopo na kwamba Tanzania ni sehemu salama ya kuwekeza mitaji yao.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifanya mazungumzo na Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka nchini Burundi wenye lengo la kuwekeza nchini Tanzania wakati alipowasili katika mji wa Bujumbura nchini Burundi kuhudhuria Mkutano wa Dharura wa 21 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Amesema tangu kuingia madarakani Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mkazo katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ikiwemo kuhakikisha inatatua changamoto za wafanyabishara kwa lengo la kukuza na kuimarisha biashara na uwekezaji. Ameongeza kwamba hali ya uchumi nchini Tanzania inaendelea vizuri ikihusisha kufanya jitihada kubwa kusimamia sera za fedha na sera za kibajeti na kuhakikisha usalama wa chakula unakuepo.

WAZIRI TAX AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA URUSI NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisalimiana Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara jijini Dodoma kwa mazungumzo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (kulia) katika picha ya pamoja na Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara jijini Dodoma kwa mazungumzo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (kulia) akimsindikiza na Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma kwa mazungumzo.

TASAF KUNUFAIKA NA MSAADA WA SH. BIL 15 KUTOKA UINGEREZA


 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu El- Maamry Mwamba na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, wakionesha Hati ya makubaliano ya msaada wa takribani shilingi bilioni 15 kwa ajili ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF), hafla iliyofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu El- Maamry Mwamba, akizungumza kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini, wakati wa hafla ya makabidhiano ya hati za msaada wa takribani shilingi bilioni 15 kwa ajili ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF), iliyofanyika jijini Dodoma.

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akizungumza kuhusu nchi yake kuendelea kuisaidia Tanzania katika kupunguza umasikini, wakati wa hafla ya kubadilishana hati ya makubaliano ya msaada wa takribani shilingi bilioni 15 kwa ajili ya TASAF, iliyofanyika jijini Dodoma.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu El- Maamry Mwamba (kushoto) na Ujumbe wa Uingereza Ukiongozwa na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, wakati wa hafla ya makabidhiano ya hati ya makubaliano ya msaada wa takribani shilingi bilioni 15 kwa ajili ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF), hafla iliyofanyika jijini Dodoma

WAKUU WA WILAYA NA WAKURUGENZI SIMAMIENI HUDUMA ZA WAZEE NA ZA MAMA NA MTOTO - DKT. MOLLEL

  NAIBU WAZIRI wa afya Dkt. Godwin Mollel ametoa wito kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kusimamia huduma za afya ya mama na mtoto na kuhakikisha vituo vyote vya kutolea huduma za afya  nchini kuanzia zahanati mpaka hospitali ya Rufaa ya taifa kuwa na dirisha maalumu kwaajili ya kuwahudumia wazee ili kuepusha usumbufu unaowakumba.

Ametoa wito huo leo Juni 1, 2023 wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mhe. Bupe Nelson Mwakang'ata katika Bunge la kumi na mbili Mkutano wa kumi na moja kikao cha 38, Jijini Dodoma.

"Kwenye swala la wazee tumeagiza kila kitu cha afya, kila zahanati na kila hospitali kuwepo na dirisha kwaajili ya kuwahudumia wazee, na tunaomba wenzetu Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wasimamie ili eneo ili kuhakikisha takwa la kisera linatekelezwa ipasavyo." Amesema Dkt. Mollel.

Ameendelea kusema, katika kuhakikisha Sera ya afya inatekelezwa vizuri Serikali kupitia Wizara ya Afya imetenga zaidi ya Bilioni 167 ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma muhimu ikiwemo upatikanaji wa dawa na vifaa tiba utaoenda kutatua changamoto ya huduma kwa wazee na mama na mtoto nchini.

RAIS DKT.MWINYI AZINDUA KAMATI YA KUZUIA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA ZANZIBAR

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi akiondoa pazia kuashiria kuzindua Kamati ya Kuzuia Udhalilishaji wa Kijinsia Zanzibar (kushoto ) Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mhe.Mgeni Jailani Jecha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Sheria, Katiba,Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Mhe. Haroun Ali Suleiman.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, akikabidhiwa Kitabu cha Hadidu Rejea, Kanuni, na Mpango Kazi wa Kamati ya Kuzuia Udhalilishwa Kijinsia Zanzibar, akikabidhiwa na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mhe. Mwanamkaa Abdulrahman Mohammed na (kushoto kwa Rais) Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mhe. Mgeni Jailani Jecha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Sheria,Katiba,Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Mhe. Haroun Ali Suleiman, uzinduzi huo uliyofanyika leo 1-6-2023 katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, akikabidhiwa Kitabu cha Hadidu Rejea, Kanuni, na Mpango Kazi wa Kamati ya Kuzuia Udhalilishwa Kijinsia Zanzibar, akikabidhiwa na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mhe. Mwanamkaa Abdulrahman Mohammed na (kushoto kwa Rais) Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mhe. Mgeni Jailani Jecha, uzinduzi huo uliyofanyika leo 1-6-2023 katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

DC SIMANJIRO DK SERERA AZINDUA TUZO YA MALKIA WA MADINI

Na Mwandishi wetu, Mirerani 
MKUU wa wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, Dk Suleiman Serera, amezindua tuzo ya malkia wa madini iliyoandaliwa na chama cha wanawake wachimbaji madini nchini (TAWOMA) itakayoshirikisha mikoa 12.

Dk Serera akizindua mchakato wa tuzo za malki wa madini mji mdogo wa Mirerani, ambapo kilele chake kitafanyika mkoani Geita, amewataka wanawake wachimbaji wajitokeze kwa wingi kushiriki.

Amesema ni heshima ya kipekee kwa tuzo hizo kuzinduliwa kwenye madini ya Tanzanite yaliyopo Simanjiro hivyo mwaka ujao wa 2023 TAWOMA waandae tuzo hizo katika wilaya hiyo.
Mwenyekiti wa TAWOMA, Semeni Malale amesema mshindi wa kwanza atakayenyakua tuzo ya malkia wa madini atapata zawadi ya Sh5 milioni na mshindi wa pili atapata Sh3 milioni.

Amesema mshindi wa tatu atapata Sh2 milioni na mshindi wanne hadi wa 20 watajishindia zawadi zenye thamani ya Sh500,000 kwa kila mmoja.

Wednesday, May 31, 2023

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUENDELEA KUTOA ELIMU KUHUSU CHANJO


Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuwapeleka watoto kupata chanjo mbalimbali zinazotolewa na Serikali kupitia Wizara ya afya.

Rai hiyo imetolewa leo na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Rashid Mfaume wakati wa semina kwa waandishi wa habari wa Mikoa ya Mtwara, Lindi Pwani na Morogoro iliyofanyika kwenye ukumbi wa Anatoglo jijini Dar es Salaama.

Dkt. Mfaume amesema waandishi wa habari ni muhimu katika kuhamasisha masuala yote ya afya hususani chanjo ili kuweza kuwakinga watoto magonjwa yanayozuilika kwa chanjo.

Ameongeza kuwa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuhakikisha huduma za chanjo zinapatikana kila mahali ikiwemo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

"Tunamshukuru Rais wetu kwa uwekezaji mkubwa kwa sekta hii kwa upande wa chanjo tumepata majokofu yanayotumia nishati ya jua hakuna sababu tena ya kituo kukosa chanjo kwa sababu hii".

VIONGOZI WA DINI KAGERA WATAMANI RC FATMA MWASSA AANZE NA HAYA SUGU


Na Lydia Lugakila, Bukoba.
Viongozi wa dini na madhehebu katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera wamekutana na kujadiliana na mkuu wa Mkoa wa Kagera Bi Fatma Mwassa huku shauku yao ni kutamani na kuona baadhi ya kero zilizoonekana sugu kwa muda mrefu zinafanyiwa kazi ili Mkoa huo uinuke haraka kiuchumi.

Viongozi hao wa Dini Wakiongea katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Mkoa huo wamesema wanaamini kuwa kiongozi huyo atajifunga mkanda na kutenda miujiza kwa kuazia alipoishia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Albert John Chalamila kwa kuanza na kero ya Stendi, Soko, upanuzi wa mji wa Bukoba, kumwondolea mkulima wa Kijijini makato na kodi katika kilimo, kuona namna ya kuwaondoa Wanyama aina ya Ngedere wanaoonekana maeneo ya mjini na kushambulia mazao ya Wananchi, pamoja na suala la uchafu utokanao uvunaji wa Senene na mmomonyoko wa maadili kwa vijana.

Viongozi hao wa dini akiwemo Sheikh wa Mkoa wa Kagera Harouna Kichwabuta wameiomba Serikali kumfikilia mkulima wa Kijijini kwa kumpunguzia makato na kodi na kuwa mkulima hawezi kuendelea akiwa anakatwa na kukosa uhuru katika bidhaa zake ikiwa ni pamoja na kumfungulia mipaka ili apate kusafirisha bidhaa zake ili kujipatia kipato.

Sheikh Kichwabuta ameiomba pia Serikali kuona namna ya kurudisha na kuheshimisha somo la dini ili lifundishwe tena kama awali shuleni na mtihani wa somo hilo uingizwe katika orodha ya mitihani ya kitaifa na kumfanya anayelifaulu kupewe kipaumbele hali itakayosaidia kuwa na wasomi wenye maadili mema na kuondokana na maovu yanayoonekana kwa sasa ikiwemo mapenzi ya jinsia moja.

RAIS DKT. MWINYI AZINDUA KAMATI YA MARIDHIANO KATI YA CCM NA ACT -WAZALENDO IKULU ZANZIBAR

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa Chama cha ACT-Wazalendo, wakati  akizindua Kamati ya Maridhiano Kati ya CCM na ACT –Wazalendo, uzinduzi huo uliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 31-5-2023, na (kulia kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla na (kushoto kwa Rais) Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman.(Picha na Ikulu)

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya na Wajumbe wa Kamati ya Maridhiano Kati ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha ACT-Wazalendo, baada ya kuizindua kamati hiyo leo katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar na (kulia kwa Rais)Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ambae pia ni Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman na Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo Mhe. Nossor Ahmed Mazrui na (kushoto kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ambae ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Mhe. Hemed Suleiman Abdulla na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Mohammed Said Dimwa.(Picha na Ikulu)

DKT. NCHEMBA AWAAGIZA WATAALAM WA UCHUMI WA KITAIFA NA KIMATAIFA KUTAFUTA SULUHU YA UPUNGUFU WA DOLA ZA MAREKANI KATIKA SOKO LA FEDHA


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akimsikiliza Kiongozi wa ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Harris Tsangaride wakati wa kikao cha wataalamu wa Wizara hiyo na IMF, waliokuja nchini kufanya tathmini ya Program ya Huduma za Mikopo (EFC), jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akifungua kikao cha wataalamu wa Wizara hiyo na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuhusu tathmini ya Program ya Huduma za Mikopo (EFC), jijini Dodoma.
 
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Kiongozi wa ujumbe kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF), Bw. Harris Tsangaride baada ya kufungua kikao cha wataalamu wa Wizara hiyo na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), waliofika nchini kwa ajili ya kufanya tathmini ya Program ya Huduma za Mikopo (EFC), jijini Dodoma.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM-Dodoma)

 Na Farida Ramadhani-Dodoma


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amewaagiza wataalamu wa Wizara ya Fedha na Mipango na ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kujadili namna ya kushughulikia athari za upungufu wa dola za Kimarekani katika mzunguko wa fedha ili kunusuru uchumi wa nchi zinazoendelea.

Mhe. Dkt. Nchemba (Mb) ametoa maagizo hayo wakati wa kufungua kikao kilichowashirikisha wataalam kutoka Shirika la Fedha na Kimataifa (IMF) waliowasili nchini kwa ajili ya kufanya tathimini ya Program ya Huduma za Mikopo (EFC), kwa kushirikiana na wataalam wa ndani wa Serikali.

Alisema mabadiliko ya Sera za Fedha nchini Marekani ya kubana matumzi na kupunguza dola kwenye mzunguko wa fedha, yameleta athari zinazoonekana mpaka kwenye nchi zinazoendelea, ikiwemo Tanzania.
 
“Tumekuwa tukirejea Uviko na vita baina ya Urusi na Ukraini kama moja ya vitu vinavyoathiri uchumi wa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania lakini upungufu wa dola unaathiri uchumi kwa kiwango kikubwa ikiwemo uagizaji wa mafuta na uagizwaji wa bidhaa mbalimbali zinazotumika katika shughuli za Sekta Binafsi”, alisema Dkt. Nchemba.

Alisema ni vema kutafuta namna ya kushughulikia jambo hilo kisera ili kunusuru nchi zinazoendelea kwa kuwa sekta ya nje ni muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa ndani.

Kwa upande wake Kiongozi wa ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Harris Tsangaride, alisema Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuhakikisha nchi inaendelea kupiga hatua kiuchumi na kijamii.
 
Aliipongeza Serikali kwa Sera zake nzuri ambazo zinaendelea kutekelezwa katika kukabiliana na athari za vita ya Ukraine na kuongeza kuwa ni matarajio yao kuwa zitaendelea kuchokea ukuaji wa uchumi na maisha ya wananchi.

Bw. Tsangaride alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi chache katika kanda ambazo zinafanya vizuri katika kutekeleza programu mbalimbali kwa kushirikiana na Shirika hilo na hivyo katika kikao hicho watajadiliana namna bora ya kuendelea kuiona nchi ikifanya vizuri zaidi. 

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AKUTANA NA RAIS WA BURUNDI NDAYISHIMIYE


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Ikulu ya Bujumbura nchini Burundi leo tarehe 31 Mei 2023. Makamu wa Rais anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura wa 21 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaofanyika nchini Burundi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akizungumza na Rais wa Burundi Mheshimiwa Evariste Nayishimiye mara baada ya kuwasili Ikulu ya Bujumbura nchini Burundi kushiriki Mkutano wa Dharura wa 21 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) leo tarehe 31 Mei 2023.

RAIS DKT. MWINYI AZUNGUMZA NA MWAKILISHI MKAAZI WA UNDP BI.CHRISTINE MUSISI IKULU ZANZIBAR



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar mgeni wake Mwakilishi Mkaazi wa UNDP Nchini Tanzania Bi.Christine Musisi, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 31-05-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na mgeni wake Mwakilishi Mkaazi wa UNDP Nchini Tanzania Bi.Christine Musisi, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 31-05-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Mwakilishi Mkaazi wa UNDP Nchini Tanzania Bi. Christine Musisi, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 31-5-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na mgeni wake Mwakilishi Mkaazi wa UNDP Nchini Tanzania Bi. Christine Musisi (kulia kwa Rais) akiwa na Ujumbe wake wa Maofisa wa UNDP, mazungumzo hayo yaliyofanyika leo 31-5-2023, katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Mwakilishi Mkaazi wa UNDP Nchini Tanzania Bi. Christine Musisi, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar akiwa na Ujumbe wake,mazungumzo hayo yaliyofanyika leo 31-5-2023, katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu)

MATUKIO MBALIMBALI YA WAZIRI MKUU BUNGENI JIJINI DODOMA

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Sikonge Joseph Kakunda kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 31, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Kapteni Mstaafu George Mkuchika, bungeni jijini Dodoma, Mei 31, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Tunduru Kasikazini, Hassan Zidadu Kungu,  bungeni jijini Dodoma, Mei 31, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

SERIKALI KUWEZESHA HUDUMA ZA KIBENKI KIMATAIFA

 

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande akijibu swali bungeni jijini Dodoma.

Na Farida Ramadhani, WFM – Dodoma.

Serikali imesema kuwa itaendelea kutoa ushirikiano kwa benki za biashara nchini kuanzisha kampuni tanzu nje ya nchi ili kusambaza huduma za kibenki katika nchi mbalimbali na kurahisisha ufanyaji wa biashara kati ya nchi na nchi.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Kusini, Mhe. Nashon William Bidyanguze, aliyetaka kujua wakati ambao Serikali itashawishi mabenki kufungua Benki nchini Congo DRC katika Miji ya Kalemie na Uvira ili kurahisisha biashara.

“Mei, 2021 Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania iliipa benki ya CRDB kibali cha kufungua kampuni tanzu Lubumbashi, nchini Congo ambapo inatarajia kuanza kutoa huduma za kibenki mara tu itakapopewa leseni na Benki Kuu ya Congo”, alisema Mhe. Chande.

Alibainisha kuwa katika Mkakati wa Miaka Mitano wa Biashara wa Benki ya CRDB wa Mwaka 2023 - 2028 unaonesha kuwa benki hiyo inatarajia kufungua kampuni tanzu zitakazotoa huduma za kibenki kwenye miji ya Bukavu, Uvira na Kalemie nchini Congo.


DK.MWINYI AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia pichani) akimsikiliza Mwandishi Mwandamizi Ndg.Salim Said Salim (kushoto) akimsikiliza katika mazungumzo yanayohusu masuala ya ziara yake Nchini Qatar hivi karibuni na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbali mbali vya Serikali na Binafsi yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.[Picha na Ikulu] 30/05/2023.

Wasaidizi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, wakifauatilia kwa makini mazungumzo baina ya na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbali mbali vya Habari vya Serikali na Binafsi na Mhe.Rais, yaliyofanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar kuhusu ziara ya Nchini Qatar hivi karibuni.[Picha na Ikulu] 30/05/2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali vya Serikali na Binafsi katika Ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo,ambapo zaidi amezungumzia ziara yake Nchini Qatar hivi karibuni.[Picha na Ikulu] 30/05/2023.
Mwandishi wa Habari wa gazeti la Nipashe hapa Zanzibr Ndg.Rahma Suleiman akiuliza suala wakati wa mazungumzo ya Wahariri na Waandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali vya Serikali na Binafsi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) Ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo yanayohusu masuala ya ziara ya Nchini Qatar hivi karibuni.[Picha na Ikulu] 30/05/2023.