ANGALIA LIVE NEWS
Friday, March 27, 2026
MAZIKO YA MPENDWA WETU HASSAN NG'ANZO
Friday, January 23, 2026
WATUHUMIWA WA KUSAFIRISHA KILO 20.03 ZA SKANKA KATIKA BASI LA KING MASAI TOURS WASOMEWA MASHTAKA
WATUHUMIWA wawili, Amasha Iddi Mrisho (40), mkazi wa Buza, Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32), raia wa Msumbiji, Januari 22, 2026, wamefikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kujibu tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya skanka.
Akisoma maelezo ya awali ya shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mhe. Lukosi, Mwendesha Mashtaka wa Serikali Wakili Nicas Kihembe akisaidiana na Erick alidai kuwa washtakiwa hao walikamatwa tarehe 08 Desemba 2025 katika mtaa wa Wailes, Temeke, Dar es Salaam na maofisa wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, wakati wa operesheni hiyo, DCEA ilikamata pakiti 20 za Bangi aina ya skanka zenye uzito wa jumla wa kilogramu 20.03, ambazo zilikuwa zimefichwa ndani ya balo la mitumba, kisha kufichwa katika basi aina ya Scania la kampuni ya King Masai Tours, lenye namba za usajili wa Msumbiji AAM 297 CA.
Ilielezwa zaidi kuwa, mashtaka yanayowakabili washtakiwa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 16(I) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, inayokataza umiliki, usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya nchini.
Upande wa mashtaka uliieleza mahakama kuwa, shtaka hilo halina dhamana kutokana na uzito wa dawa za kulevya walizokutwa nazo washtakiwa.
Aidha, kwa mujibu wa wakili wa Serikali, upelelezi wa shauri hilo namba 1535/2026 ya mwaka 2026 bado unaendelea na mashahidi wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo siku itakayopangwa.
Shauri hili lilihairishwa hadi tarehe 05 februari 2026, huku washtakiwa wakirejeshwa rumande.
Mwisho
Saturday, January 10, 2026
TANI 9 ZA DAWA ZA KULEVYA ZAKAMATWA NCHINI TANZANIA
*Raia wa Kenya akamatwa akitumia biashara ya chai kuficha uuzaji wa dawa za kulevya.
*Basi la King Masai linaswa likisafirisha skanka.
*Mirungi iliyofungwa kama majani ya mwarobaini yakamatwa.
*Watumishi wa serikali wanaswa wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini imetekeleza operesheni maalum mwishoni mwa mwezi Desemba 2025 na kufanikiwa kukamata jumla ya kilogramu 9,689.833 za dawa za kulevya, sawa na tani 9. Pia pikipiki 11 na magari matatu yamekamatwa, huku watuhumiwa 66 wakitiwa mbaroni kwa tuhuma za kuhusika na biashara hiyo haramu.
Katika operesheni iliyofanyika Sinza C, mtaa wa Bustani, nyumba namba 16 jijini Dar es Salaam, Jefferson Kilonzo Mwende mwenye umri wa miaka 35, raia wa Kenya, alikamatwa akiwa na gramu 131.88 za heroin. Uchunguzi umebaini kuwa mtuhumiwa huyo, ambaye aliishi Tanzania tangu mwaka 2023, alikuwa akitumia biashara ya kuuza chai kama kificho cha kuendesha mtandao wa uuzaji wa dawa za kulevya.
Katika eneo la Wailes, Temeke jijini Dar es Salaam, mamlaka ilikamata pakiti 20 za skanka zenye uzito wa kilo 20.03, zilizokuwa zimefichwa ndani ya balo la nguo za mitumba na kusafirishwa kwa basi aina ya Scania la kampuni ya King Masai Tours, lenye namba za usajili AAM 297 CA kutoka Msumbiji. Basi hilo hufanya safari kati ya Nampula nchini Msumbiji na Tanzania. Watuhumiwa waliokamatwa ni Amasha Iddi Mrisho mkazi wa Buza, Dar es Salaam, pamoja na Seleman Juma Ally, raia wa Msumbiji.
Katika Kinyerezi, mtaa wa Majoka wilayani Ilala, watuhumiwa watatu Erick Ernest Ndagwa, Paul Blass Henry na Tido Emmanuel Mkude walikamatwa wakiwa wanasafirisha bangi yenye uzito wa kilo 193.66 kutoka Morogoro kwenda Dar es Salaam.
Kadhalika, kupitia ukaguzi uliofanyika katika kampuni za usafirishaji wa mizigo jijini Dar es Salaam, paketi 20 za mirungi zenye uzito wa kilo 9.54 zilikamatwa zikiwa zimefungwa na kufanana na majani ya mwarobaini yaliyokaushwa. Mizigo hiyo ilikuwa ikisafirishwa kutoka Kenya kuelekea Australia.
Katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Tanga, Lindi, Kilimanjaro, Njombe, Kigoma na Arusha, operesheni mbalimbali zilifanikiwa kukamata heroin gramu 37.34, skanka kilo 1.015, bangi kilo 7,969.98 na mirungi kilo 1,363.701. Pia mashamba ya bangi yenye ukubwa wa ekari 14 yaliteketezwa.
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imesisitiza wananchi kutoa taarifa pale wanapoona viashiria vya biashara ya dawa za kulevya na kuepuka kubeba mizigo wasiyoijua. Mamlaka itaendelea na operesheni nchi nzima na kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika wote wa uhalifu huu.
Monday, November 10, 2025
GLORY ASHEREHEKEA BIRTHDAY YAKE NA MARAFIKI ZAKE, DURHAM, NORTH CAROLINA
Saturday, October 4, 2025
MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA YATEKETEZA KILO 4,402 ZA DAWA ZA KULEVYA JIJINI DAR ES SALAAM
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikisha zoezi kubwa la kuteketeza dawa za kulevya zenye uzito wa jumla ya kilo 4,402.02. Zoezi hilo limefanyika Oktoba 3, 2025, katika kiwanda cha saruji cha Twiga kilichopo Wazo, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya DCEA iliyosomwa na Kamishna Jenerali Aretas Lyimo, dawa zilizoteketezwa ni pamoja na kilo 2,168.18 za methamphetamine, kilo 1,064.29 za heroin, gramu 326.95 za cocaine, kilo 515.48 za bangi na kilo 653.74 za mirungi. Zote zilikuwa sehemu ya vielelezo vya mashauri mbalimbali yaliyopo mahakamani; baadhi yakiwa tayari yametolewa hukumu na mengine yakiendelea kusikilizwa.
Miongoni mwa mashauri yanayohusiana na dawa zilizoteketezwa ni kesi ya Najim Abdallah Mohamed iliyohusisha heroin kilogramu 882.71 na methamphetamine kilogramu 2,167.29. Aidha, mashauri yaliyotolewa hukumu ni Pamoja na ya Hassan Azizi aliyepatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha, Salum Shaaban Mpangula aliyehukumiwa kifungo cha maisha, Hemed Juma Mrisho maarufu kwa jina la “Hororo” aliyehukumiwa kifungo cha maisha, Ramadhan Shaban Gumbo aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, Irene Dickson Mseluka aliyehukumiwa miaka mitano jela na Gema Victor Mmasy aliyehukumiwa miaka mitatu jela.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, alisema mamlaka itaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha vita dhidi ya dawa za kulevya inafanikiwa. Aidha, alisisitiza kuwa DCEA haitabaki katika hatua za kisheria pekee, bali pia itatoa nafasi kwa wale wanaojihusisha na biashara hiyo kuachana nayo kwa hiari.
“Tunatoa msamaha kwa wauzaji wa dawa za kulevya watakaoamua kukiri na kuacha. Hatutachukua hatua yoyote dhidi yao, bali tutashirikiana nao ili kufichua mbinu zinazotumika kuficha na kusambaza dawa hizi,” alisema Lyimo.
Kutokomeza zaidi ya tani nne za dawa za kulevya ni hatua kubwa katika kupunguza athari zinazotokana na biashara haramu ya dawa za kulevya nchini. Tukio hili linadhihirisha dhamira ya DCEA kuhakikisha jamii inalindwa dhidi ya madhara ya dawa hizo ambazo zimekuwa zikiathiri afya, uchumi na usalama wa taifa.
Saturday, August 23, 2025
ONA JINSI TANI 18 4 YA SHEHENA YA DAWA MPYA YA KULEVYA NA WATUHUMIWA WALIVYOKAMATWA
SERIKALI YAREJESHA TABASAMU KWA CHIDI BENZ
Thursday, August 7, 2025
TAUS CHOIR CONCERT DMV

DKT. MWAISOBWA AKABIDHIWA PRESSCARD
Dkt. Cosmas Mwaisobwa, Msaidizi wa Makamu wa Rais (Hotuba) akipokea Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Presscard) kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) Wakili Patrick Kipangula.
Dkt. Mwaisobwa amepokea Kitambulisho hicho tarehe 05 Agosti, 2025 katika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam, baada ya kukidhi vigezo vinavyohitajika Kisheria akiwa na Elimu ya juu iliyotajwa katika Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 ya Daktari wa Falsafa ya Mawasiliano kwa Umma.
Mwaisobwa ni miongoni mwa Wataalamu wachache nchini wenye Elimu ya Udaktari wa Falsafa ya Mawasiliano kwa Umma na Uandishi wa Habari waliopewa vitambulisho, akitanguliwa na Dkt. Egbert Mkoko (Mjumbe wa Bodi) na Dkt. Ayoub Chacha Rioba (Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania TBC).
Akizungumza mara baada ya kumkabidhi kitambulisho hicho, Wakili Kipangula amempongeza Dkt. Mwaisobwa kwa kutekeleza takwa la Kisheria na kuwasihi waandishi wengine ambao bado hawajajisajili kuhakikisha wanafanya hivyo ili waweze kuendelea kutekeleza majukumu yako ya kihabari bila kukinzana na Sheria.
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB imepokea maombi zaidi ya 3,200 kwa ajili ya Ithibati na Vitambulisho vya Uandishi wa Habari na tayari maombi 2,109 yameidhinishwa hadi kufikia tarehe 5 Agosti, 2025 huku maombi 43 kati ya hayo yakikataliwa kutokana na kutokidhi vigezo na 674 yakiwa katika mchakato wa kuthibitishwa.
Tuesday, July 29, 2025
MHE. JESCA MSAMBATAVANGU ASHUKURU KAMATI KUU CCM KUREJESHA JINA LAKE UBUNGE URINGA MJINI
Sunday, July 20, 2025
Thursday, July 17, 2025
Sunday, June 29, 2025
OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA IMEFANIKIWA SANA USHIRIKI WAKE KATIKA KESI ZA DAWA ZA KULEVYA
Katika kuhakikisha ufanisi wa mashauri haya, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa mashauri yote ya dawa za kulevya yanakamilika kwa hukumu ndani ya kipindi kisichozidi miezi sita.
Tangu Julai 2024 hadi Juni 2025, jumla ya mashauri 2,785 ya dawa za kulevya yalipelekwa mahakamani ambapo Jamhuri ilishinda mashauri 2,021, sawa na asilimia 63%. Katika kipindi hicho hicho, mafanikio ya jumla ya mashitaka yote ya jinai yaliyosimamiwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ma kusinda yalifikia asilimia 72%.
Hii ni dalili ya utendaji mahiri na juhudi zinazostahili pongezi katika kulinda usalama wa jamii dhidi ya janga la dawa za kulevya.
Kauli mbiu: "Wekeza kwenye Kinga na Tiba dhidi ya dawa za kulevya"
ALLENA AKAMATA NONDO NORTHEN HIGH SCHOOL, DURHAM, NORTH CAROLINA
Thursday, June 19, 2025
RAIS WA YANGA AKUTANA NA WANACHAMA NA MASHABIKI WA YANGA USA
Tuesday, June 10, 2025
MAKAMU WA RAIS DKT. PHILIP MPANGO AMEFUNGUA MKUTANO MAALUM WA MKONDO WA BAHARI WA PEMBA -UFARANSA
WAZIRI MKUU BUNGENI LEO JUNI 10, 2025
Monday, June 9, 2025
SERIKALI IMEENDELEA KUCHUKUA KUKABILI ATHARI ZA MAZINGIRA
WAZIRI MKUU: SERIKALI YATENGA 43BN/- KUIMARISHA MICHEZO SHULENI
Sunday, June 8, 2025
RAIS WA ZANZIBAR DK.HUSSEIN ALI MWINYI ALIHUTUBIA BARAZA LA EID AL ADHAA UKUMBI WA DKT.ALI MOHAMED SHEIN SUZA TUNGUU MKOA WA KUSINI UNGUJA


NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA MWANDUMBYA ATETA NA UJUMBE WA KAMPUNI YA ALSTOM
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwandumbya, akiongoza kikao na ujumbe wa Kampuni ya ALSTOM, ambapo pamoja na mambo mengine walijadiliana kuhusu uendelezaji wa miundombinu jijini Dar es Salaam, kikao hicho kilifanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini, Dodoma.

.jpeg)



.jpg)



.jpg)
.jpg)