Friday, July 26, 2024

RAIS DKT. SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Ll
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Jerry William Silaa kuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Deogratius John Ndejembi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2024.

WATUMISHI WIZARA YA FEDHA WAHIMIZWA KUENDELEA KUCHAPA KAZI



Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akizungumza wakati akifungua Kikao cha Watumishi wa Wizara ya Fedha kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani), kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma, ambapo amewaagiza watumishi kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa mapato na kuratibu upatikanaji wa fedha ili kutoa fedha kwa wakati kwa miradi yote iliyoidhinishwa na Bunge.
Watumishi wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (hayupo pichani), wakati akifungua Kikao cha Watumishi wa Wizara ya Fedha kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (hayupo pichani), kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma.

Na. Saidina Msangi na Farida Ramadhani, WF, Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Fedha wameagizwa kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa mapato na kuratibu upatikanaji wa fedha ili kutoa fedha kwa wakati kwa ajili ya kutekeleza miradi yote iliyoidhinishwa na Bunge.

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MTENDAJI WAK-FINCO YA KOREA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Fedha ya Korea kwa ajili ya Ujenzi (K-Finco) Bibi Eun Jae Lee Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Fedha ya Korea kwa ajili ya Ujenzi (K-Finco) Bibi Eun Jae Lee pamoja na Ujumbe wake mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es Salaam.

RAIS WA ZANZIBAR DKT. HUSSEIN MWINYI AJUMUMUIKA NA WAUMINI WA DINI YA KIISLAM KATIKA IBADA YA SALA YA IJUMAA


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Dini alipowasili katika viwanja vya Masjid Taqwaa Mwanakwerekwe Meli Nne Wilaya ya Magharibi “B” Unguja, kuhudhuria Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid hiyo leo 26-7-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Waumini wa Dini ya Kiislam, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Taqwaa Meli Nne Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 26-7-2024

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wananchi baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa, iliyofanyika katika Masjid Taqwaa Meli Nne Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 26-7-2024

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR AJUMUMUIKA NA WAUMINI WA DINI YA KIISLAM KATIKA SALA YA MAITI


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na wanafamilia na waumini wa Dini ya Kiislamu katika Swala na Dua ya kumuombea marehemu Amour Khalfan Salum aliekuwa mtangazaji Mstaafu wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) iliyofanyika katika msikiti wa Muembe Tanga Wilaya ya Mjini Unguja.

Inna liilahi wainna ilaihi raajiun

Imetolewa na Kitengo cha Habari (OMPR)

Tarehe 26.07.2024

VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA NA WAFANYABIASHARA MTWARA WAPATIWA ELIMU YA FEDHA.



Afisa Mkuu Mwandamizi kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha - Wizara ya Fedha, Bw. Salim Kimaro akitoa elimu ya fedha kwa wanavikundi na wajasiriamali katika ukumbi Shule ya Ufundi ya Sekondari Mtwara (Mtwara Technical Secondary School) Manispaa ya Mtwara.
Afisa Sheria Mwandamizi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Ramadhani Myonza, akitoa elimu ya fedha kwa Wanavikundi na Wajasiriamali katika Ukumbi Shule ya Ufundi ya Sekondari Mtwara (Mtwara Technical secondary school) Manispaa ya Mtwara.
Baadhi ya wajasiriamali na wafanyabiashara wa Manispaa ya Mtwara wakipatiwa mafunzo ya elimu ya fedha na Wizara ya Fedha wakishirikiana na Taasisi za Fedha pamoja na OR TAMISEMI mkoani Mtwara.

UKUSANYAJI WA MAONI YA MPANGO KAZI WA HAKI ZA BINADAMU NA BIASHARA



Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Tanzania, Khatib Mwinyichande Khamis akitoa maelezo kwa waandishi wa habari kuhusu ukusanyaji wa maoni kwa wadau mbali mbali wanaohusika na mambo ya Utalii, Uchumi wa Buluu na Nishati, katika Ukumbi wa Sanaa, Rahaleo.

Na Rahma Khamis 
Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Tanzania, Khatib Mwinyichande Khamis amewataka Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala wa Mikoa kutoa ushirikiano kwa Tume hiyo katika ukusanyaji wa maoni kwa wadau mbali mbali ili kufanikisha utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu na Biashara.

Hayo ameyasema katika Ukumbi wa Sanaa, Rahaleo wakati akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari kuhusiana maandalizi ya mpango huo.

Amesema lengo la ukusanyaji wa maoni hayo ni kuhakikisha linawafikia wadau wanaohusika na mambo ya Utalii, Uchumi wa Buluu na Nishati pamoja na ushirikishwaji na wajumbe wengine katika mikoa yote ya Zanz ibar.
Aidha amefahamisha kuwa Serikali zote mbili ziko katika maandalizi ya mpango huo ambao unaandaliwa chini ya Uratibu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB).

WAITARA AKOSHWA NA UJIRANI MWEMA BAINA YA HIFADHI YA SAADANI NA WAWEKEZAJI





Na Catherine Mbena /Saadani.
Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Jenerali (Mstaafu) George Marwa Waitara, jana Julai 24, 2024 ilitembelea Hifadhi ya Taifa Saadani kwa ajili ya kukagua utendaji kazi ambapo ilipata fursa ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya hifadhi hiyo.

Akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wajumbe wa bodi, Mkuu wa Hifadhi hiyo Afisa Uhifadhi Mkuu, Simon Aweda alisema ushirikiano kati ya Hifadhi ya Taifa Saadani na wawekezaji umewezesha kupiga hatua kubwa kimaendeleo ambapo wadau mbalimbali wamejitokeza kuunga mkono juhudi za uhifadhi na kuchagiza maendeleo ya utalii.

“Wadau wanaozunguka Hifadhi ya Taifa Saadani wamekuwa mstari wa mbele kuunga juhudi za uhifadhi na utalii ambapo kampuni ya sukari ya Bagamoyo sugar ilijitolea kugharamia vifaa pamoja na zoezi la ufungaji wa visukuma mawimbi “collar ” ambapo zaidi ya shillingi milioni 180 zilitolewa na wadau ikiwa ni gharama ya vifaa, wataalam walioshiriki zoezi hilo pamoja na helkopta iliyotumika katika zoezi hilo” alisema Mhifadhi Aweda.

SPIKA TULIA AMUAPISHA MBUNGE BALOZI KOMBO DAR



Na Andrew Chale, Dar es Salaam.
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson amemuapisha Balozi Mahmoud Thabit Kombo kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ofisi ndogo za Bunge, jijini Dar es Salaam.

Balozi Kombo ameapishwa leo Alhamisi Julai 25, 2024, Ofisi hizo huku akiambatana na familia yake, sambamba na kusindikizwa na Wabunge kadhaa pamoja na maafisa wa Bunge n wale wa ofisi ya Mambo ya Nje tukio lililoshuhudiwa na Waandishi wa Habari mbalimbali.

Julai 21, 2024 Balozi Kombo alipoteuliwa kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Rais Samia Suluhu Hassan, kuchukua nafasi ya January Makamba ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Thursday, July 25, 2024

RAIS SAMIA AONGOZA WATANZANIA KUMBUKUMBU YA SIKU YAKO MASHUJAA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa katika Uwanja wa Mashujaa uliopo Mji wa Serikali Mtumba Mkoani Dodoma leo tarehe 25 Julai, 2024.


JESHI LA ZIMAMOTO TANGA WAJA NA PROGRAMU ZA KUELIMISHA UMMA NAMNA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO


Na Oscar Assenga,TANGA
JESHI la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tanga wameanzisha program mbalimbali za kuielimisha Umma kuweza kuwa na utambuzi ili majanga ya moto yanapotokea waweze kukabiliana nayo.

Hayo yalibainishwa leo na Afisa Operesheni wa Jeshi hilo mkoani Tanga Mrakibu Msaidizi wa Jeshi hilo Yusuf Msuya wakati akizungumza na kuhusu namna walivyojipanga kukabiliana na matukio ya moto kwa wananchi.

Alisema katika kuzuia ajali za moto wameamua kuja na mpango huo ambao wanaamini utakuwa na mafanikio makubwa ambao utakwenda sambamba na

ukaguzi wa kinga na tahadhari kwa majanga katika maeneo mablimbali yakiwemo ya biashara,makazi na vyombo bya usafiri na usafirishaji.

“Lengo la ukaguzi huu ni kutambua yale mapungufu na risk zilizopo kwenye majengo ambayo ni hatari na kuyawasilisha kwa mmiliki ikiwemo kumpa mapendekezo na hatua za kufanya ili kuzuia moto usitokee “Alisema

DKT. TAX AKUTANA NA KAIMU NAIBU WAZIRI WA MAREKANI


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), akisalimiana na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass alipokutana naye kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Michael Batle alipomsindikiza Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaamm, kulia ni Katibu Mkuu Balozi Shelukindo akisalimiana na Balozi wa Marekani Mhe. Michael Batle
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb), akizungumza na Kaimu Naibu Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia masuala ya Siasa wa Marekani Mhe. John Bass walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

NEC: KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI


Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza leo tarehe 25 hadi 26 Julai,2024 Mkoani Kagera.
Washiriki wakifatilia hotuba ya ufunguzi.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji ,Erasmi Francis akitoa mada kuhusu uraia wakati wa mafunzo hayo.

Wednesday, July 24, 2024

NANYAMBA YAFIKIWA NA ELIMU YA FEDHA


Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha - Wizara ya Fedha, Bi. Elizabeth Mnzava akitoa elimu ya fedha kwa wanavikundi na wajasiriamali katika ukumbi wa zamani wa Halmashauri, Nanyamba Mkoani Mtwara.
Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha - Wizara ya Fedha, Bw. Kelvin Kalengela, akitoa elimu ya fedha kwa wanavikundi na wajasiriamali katika ukumbi wa Halmashauri ya zamani Nanyamba Mkoani Mtwara.
Afisa Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Masoko ya Mitaji na Dhamana – Wizara ya Fedha, Bw. Godfrey Makiyo, akitoa elimu ya fedha kwa wanavikundi na wajasiriamali katika ukumbi wa zamani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyamba Mkoani Mtwara.

TANZANIA YATOA NENO UKUBWA WA RIBA KIMATAIFA


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika kikao cha Kwanza cha Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ugharamiaji kwa Maendeleo Endelevu (Fouth International Conference on Financing for Deveoplopment - FfD4 ikiwa ni siku ya pili ya Kikao hicho kinachofanyika jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.
Washiriki wa Kikao cha Kwanza cha Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ugharamiaji kwa Maendeleo Endelevu (Fouth International Conference on Financing for Deveoplopment - FfD4, kutoka nchi mbalimbali wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha – Tanzania Bi. Amina Shaaban (hayupo pichani) wakati akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), katika kikao hicho, jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, akiteta jambo na Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha, Idara ya Fedha za Nje, Bw. Patrick Pima katika kikao cha Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa Ugharamiaji kwa Maendeleo Endelevu (Fouth International Conference on Financing for Deveoplopment - FfD4, ambapo licha ya Mawaziri na wawakilishi kuwasilisha hoja mbalimbali, wadau pia watapata fursa ya kujadiliana maeneo yote ya utekelezaji ya Ajenda ya Addis Ababa kutathmini maendeleo yaliyopatikana na kuibua mawazo mapya ili kuziba mapengo yaliyosalia katika utekelezaji wa maendeleo endelevu.

KAGERA, GEITA KUANZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AGOSTI 5,2024



Makamu Mwenyekiti Wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakati akifungua mkutano wa siku moja wa Tume na Wadau wa Uchaguzi uliofanyika leo Julai 24, 2024 Mjini Bukoba Mkoani Kagera.Wadau hao ni pamoja na Viongozi wa vyama vya siasa, Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia, Wahariri wa Vyombo vya habari, Waandishi wa habari, Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri, Wawakilishi wa Makundi mbalimbali ya Vijana, Watu wenye ulemavu, Wanawake na Wazee wa Kimila.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura, Bi. Giveness Aswile akiwasilisha mada.

Na. Waandishi Wetu, Geita na Kagera
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoani Geita na Kagera utafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 05 hadi 11 Agosti, 2024 ambapo vituo vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoani Geita leo tarehe 24 Julai, 2024.

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA WAHASIBU AFRIKA

Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA. Leonard Mkude (Katikati), akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Mikutano katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), kuhusu ujio wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Wahasibu Wakuu wa nchi za Afrika (African Association of Accountants General-AAG Meeting) unaotarajiwa kufanyika tarehe 3 hadi 5 Disemba Mwaka huu, katika Kituo hicho , ambapo washiriki zaidi ya 2,000 kutoka nchi za Afrika na unalenga kujenga Imani ya umma katika Mifumo ya Usimamizi wa Fedha za Umma kwa Ukuaji Endelevu. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wahasibu Wakuu wa Afrika, Bi. Malehlohonolo Mahase, na Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), Bi. Christine Mwakatobe.
Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA. Leonard Mkude, akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Mikutano katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), kuhusu ujio wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Wahasibu Wakuu wa nchi za Afrika (African Association of Accountants General-AAG Meeting), unaotarajiwa kufanyika tarehe 3 hadi 5 Disemba Mwaka huu, katika Kituo hicho cha AICC, na utawashirikisha zaidi ya washiriki 2,000 kutoka nchi za Afrika na mkutano huo unalenga kujenga Imani ya umma katika Mifumo ya Usimamizi wa Fedha za Umma kwa Ukuaji Endelevu.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wahasibu Wakuu wa Afrika ambaye pia ni Mhasibu Mkuu wa Serikali ya Lesotho, Bi. Malehlohonolo Mahase, akizungumza wakati wa Mkutano na wanahabari katika ukumbi wa Mikutano katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), kuhusu ujio wa Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Wahasibu Wakuu wa nchi za Afrika (African Association of Accountants General-AAG Meeting) unaotarajiwa kufanyika tarehe 3 hadi 5 Disemba Mwaka huu, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), ambapo amesema kuwa Mkutano huo utakawakutanisha pia Jumuiya za wafanyabiashara na watapa fursa ya kujua ni namna gani Afrika ipo tayari katika suala la uwekezaji na namna ya kuripoti hali ya Uchumi ya Afrika, jambo ambalo litaongeza uwazi na uwajibikaji.

MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI YA TCAA DKT. HAMIS MWINYIMVUA ATEMBELEA CATC


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TCAA Dkt. Hamis Mwinyimvua akizungumza na uongozi wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) alipotembelea Chuo hicho ili kujionea miundombinu pamoja na kujitambulisha.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TCAA Dkt. Hamis Mwinyimvua akipata maelezo kutoka Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) Aristid Kanje alipotembelea chuo hicho kilichopo chini ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TCAA Dkt. Hamis Mwinyimvua akisaini kitabu cha wageni mara baada ya maelezo kutoka Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) Aristid Kanje alipotembelea chuo hicho kilichopo chini ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).

KIJANA WA MIAKA 19 AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA KWA UBAKAJI NA ULAWITI.


Na John Walter -Babati
Mahakama ya wilaya ya Babati mkoani Manyara imemtia hatiani Kijana Ramadhani Iddi Kipusa (19) kutumikia kufungo cha miaka 30 jela kwa makosa mawili ya kubaka na kumlawiti binti mlemavu (Bubu) mwenye umri wa miaka 19 nakutakiwa kulipa fidia Laki 5 kwa kila kosa.

Hukumu hiyo katika kesi ya jinai namba 5310/ 2024 jamhuri dhidi ya Ramadhani Iddi Kibusa, imesomwa mbele ya Mahakama na hakimu wa mahakama ya wilaya ya Babati Martin Masao.

Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa na jamhuri dhidi Kijana huyo, mahakama imejiridhishwa pasina shaka kuwa Ramadhani Iddi Kipusa alimbaka na kumlawiti binti huyo.

Aidha hakimu Martin Masao amesema mtuhumiwa Ramadhani Iddi Kipusa (19) ametiwa hatiani Kwa makosa mawili ya kubaka na kulawiti ambapo Kwa kosa la kubaka mtuhumiwa ametenda kosa hilo kinyume cha kifungu Cha sheria namba 130 (1) na kifungu kidogo Cha 2 (a) ikisomwa sambamba na kifungu 131(1) ambacho kinatoa adhabu, na kosa la pili la kulawiti kinyume cha kifungu cha sheria namba 154 (1)(a) Cha sheria ya kanuni za adhabu sura namba 6 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

AWESO AZIAGIZA MORUWASA NA BONDE KUSHIRIKIANA KUNUSURU BWAWA LA MINDU


Waziri wa Maji Jumaa Aweso akiangalia mitambo ya kusafirisha maji iliyopo Tumbaku Morogoro
Waziri wa Maji Jumaa Aweso akiangalia mitambo ya kusafirisha maji iliyopo Tumbaku Morogoro
Baadhi wa watumishi wakionekana kukata majani yaliyochomoza kwenye Bwawa la Mindu  

Na Christina Cosmas, Morogoro
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso ameiagiza Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) kushirikiana na Bodi ya maji bonde la Wami Ruvu (WRBWB) kutimiza wajibu wao kwa kuondoa majani yaliyovamia Bwawa la Mindu ambalo ndio roho ya wanaMorogoro na kuliweka katika mazingira safi muda wote.

Waziri Aweso amesema hayo akiwa kwenye ziara ya siku moja mkoa wa Morogoro kukagua bwawa la Mindu na mitambo ya kusafisha na kusafirisha maji iliyopo mkoani hapa.

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR MHE.HEMED AENDELEA NA ZIARA YAKE TUMBATU


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na wananchi wa Kisiwa cha Tumbatu wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Skuli ya Sekondari Tumbatu ikiwa muendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo.

Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema amefurahishwa na ushirikiano unaotolewa na wananchi wa Kisiwa cha Tumbatu kwa wakandarasi wanaojenga miradi mbali mbali ya maendeleo kisiwani humo.

Ameyasema hayo katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa skuli ya Sekondari ya ghorofa ( G+3 ) inayojengwa katika kijiji cha Tumbatu Gomani Mhe. Hemed amesema dhamira ya Serikali ya Awamu ya Nane ( 8) inayoongozwa Rais Dkt. Mwinyi ni kuona wananchi wa Tumbatu wanapata huduma zote za stahiki za kimaendeleo kwa kiwango kinachokubalika sawa na sehemu nyengine.

Makamu wa Pili wa Rais amesema wananchi wa Tumbatu wana kila sababu ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Dkt Mwinyi ikiwemo za kuwaletea maendeleo endelevu katika nyanja mbali mbali ikiwemo Elimu, Afya, Barabara, umeme na maji safi na salama ili ustawi wa wananchi wa Tumbatu uweze kuimarika zaidi.