ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, June 7, 2026

UNESCO NATIONAL COMMISSIONS EXPANDED THEIR PORTFOLIOS BEYOND EDUCATION SINCE THE 1960s

Prof. Hamisi Masanja Malebo, Executive Secretary, UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania.


Since the 1960s, UNESCO National Commissions have significantly broadened their portfolios to operate as multidisciplinary catalysts. They have shifted beyond basic education conventions to encompass science, social sciences, culture, communication, and human rights, spearheading initiatives like the Sustainable Development Goals (SDGs), ethics of Artificial Intelligence, and climate change resilience.

Evolution of the Operational Scope

The evolution of their operational scope spans several core areas:

Science and the Environment

Commissions coordinate national participation in the Man and the Biosphere (MAB) Programme, promote UNESCO Global Geoparks, and advance sustainability science.

Culture and Heritage

They lead the domestic implementation of the World Heritage Convention and the Convention for the Safeguarding of the Intangible Cultural Heritage, managing transnational serial nominations and community-based preservation projects.

Information and Communication

They champion press freedom, media literacy, digital skills, and the Memory of the World Register, while tackling emerging global issues such as disinformation and the ethics of Artificial Intelligence.


Interdisciplinary Networks

Commissions foster robust civil society engagement through partnerships with UNESCO Chairs and UNESCO Associated Schools, acting as vital institutional bridges between governments, academia, and the public.


UNESCO’s Expanded Portfolio for National Commissions

UNESCO’s expanded portfolio for National Commissions has pivoted to include specialized science, technology, and cultural diplomacy to address rapidly emerging global issues. With 199 commissions acting as constitutional bridges, they now manage localized challenges including the ethical governance of Artificial Intelligence, climate disruption, and digital disinformation.



Core Focus Areas

*Science and Technology Diplomacy*

Bridging scientific research with international policy. Commissions support cross-border collaboration on transboundary water management, climate change resilience, and the ethical implementation of the global Recommendation on the Ethics of Artificial Intelligence.


Cultural and Heritage Diplomacy

Using international programs such as World Heritage Sites and the List of Intangible Cultural Heritage to foster cooperation across borders. Commissions also facilitate high-level dialogues celebrating linguistic diversity.

Information and Digital Literacy

Tackling the spread of misinformation. Commissions host media and information literacy programs designed to protect independent journalists and equip communities with necessary digital skills.


Peacebuilding and Crisis Management

Leveraging global networks to protect cultural heritage and educational infrastructure in areas threatened by armed conflict and natural disasters.

To strengthen these efforts, UNESCO’s governing bodies have recently launched updated global guidelines to provide practical tools to maximize the impact of National Commissions at the country level.

UNESCO National Commissions as a Bridge Between UNESCO and Member States

UNESCO’s 199 National Commissions (NatComs) operate as a unique bridge between the United Nations and Member States. Recently reinforced by new UNESCO Global Guidelines, their portfolios have expanded beyond basic liaison functions to include active programme execution, localized sustainable development, and targeted capacity building.

Core Expanded Functions

The UNESCO Charter of National Commissions outlines several modernized responsibilities:

Operational Execution

Shifting from pure advisory roles to actively managing and implementing cross-sectoral programmes.

Decentralized Coordination

Strengthening integration between UNESCO and local partners to deliver impactful, community-focused projects.

Standard-Setting and Policy

Advising national governments on UNESCO’s standard-setting work, including the implementation of Open Science and Ethical AI frameworks.

Network Mobilization

Bridging civil society, academia, and the mass media with intergovernmental dialogue to ensure localized impact.

Focus on Priority Areas

The expanded portfolio heavily integrates UNESCO’s global priorities:

Priority Africa

Supporting conservation (e.g., through the African World Heritage Fund), promoting quality education, and advancing science-based solutions.

Gender Equality

Integrating inclusive policies and expanding initiatives to tackle intersectoral issues, such as gender-based violence.


Written by Prof. Hamisi Masanja Malebo, Executive Secretary, UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania.

 Edited by Julitha August Mlay, Public Relations and Communications Officer, UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania.

BARAZA LA TIBA ASILI NCHINI LAFUTA USAJILI DAWA POWAFUL BANANA NA VITAMAX ,LAPIGA MARUFUKU 'JOY' KUINGIZWA SOKONI.

 


Na ABDU MADENGE, WAF - DODOMA 


Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini limefuta usajili wa dawa ya Powaful Banana Medicine, kupiga marufuku uingizwaji na matumizi ya dawa ya Vitamax, pamoja na kuamuru kuondolewa sokoni kwa toleo namba MN1060 la dawa ya Joy. 

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya ukaguzi na vipimo vya maabara kubaini uwepo wa mchanganyiko wa kemikali hatari za kisasa na sumu kuvu kwenye bidhaa hizo kinyume cha sheria.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Prof. Nicolao Joseph Otieno, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Ofisi za Wizara ya Afya Juni 05, 2026 Mkoani Dodoma ambapo ameeleza maamuzi hayo yanajiri kufuatia zoezi maalum la ufuatiliaji wa dawa sokoni (Post Market Surveillance) lililofanyika katika mwaka wa fedha wa 2025/2026, ambalo lilibaini ukiukwaji mkubwa wa Kanuni za Usimamizi wa Dawa za Tiba Asili kifungu cha 13(1)(a) na (b).

Prof. Otieno ameongeza kuwa Uchunguzi wa kimaabara umeonesha dawa ya Powaful Banana (inayotengenezwa na Powaful Products Company Ltd) na Vitamax (kutoka kampuni ya Superfood International ya Malaysia), ambazo zimekuwa zikitumika kuongeza nguvu za kiume, zimechakachuliwa kwa kuongezewa kemikali za kisasa za Sildenafil, Tadalafil, pamoja na dawa za maumivu aina ya Tramadol na Paracetamol. 

“Tunaonya matumizi ya kemikali hizo bila usimamizi wa daktari yanaweza kusababisha magonjwa ya moyo, kufeli kwa ini na figo, shinikizo la damu, na hata vifo vya ghafla.” amesema Prof . Otieno.

Sambamba na hatua hizo, Baraza pia limebaini kuwa toleo namba MN1060 la dawa ya Joy (Usajili Na. TZ25TM0010) lina kiwango kikubwa cha sumu kuvu (mycotoxins) kinachoweza kusababisha saratani ya ini na uharibifu wa figo. Hali hii imetajwa kutokana na kutokuzingatiwa kwa viwango bora vya ukaushaji na uhifadhi wakati wa uzalishaji.

“Baraza tunatoa onyo kali kwa watengenezaji wote nchini ambao dawa zao zimebainika kuwa na mapungufu katika vifungashio, taarifa za lebo, ujazo, na maelezo ya dozi, tunawataka kufanya maboresho ya haraka kulingana na vigezo vya usajili kwa lengo la kulinda afya na usalama wa watumiaji.” amesema na kuongeza  Prof. Otieno.















JUMA THOMAS ZANGIRA: MTANZANIA WA KWANZA NCHINI KUSHTAKIWA KWA UJASUSI



Moja kati ya kesi kubwa za kihistoria nchini Tanzania ni ile kesi ya UJASUSI (ESPIONAGE) iliyomhusu Bw. JUMA THOMAS ZANGIRA ambayo ilirindima nchini mwaka 1977. Hii ilikuwa ni kesi ya aina yake iliyowaacha wananchi wakiwa hawaamini maskio yao kwani hii ilikuwa ni kesi ya kwanza ya ujasusi nchini.

Siku ya Jumapili, tarehe 25.9.1977, Radio Tanzania Dar Es Salaam, katika taarifa yake ya habari saa mbili usiku, ilieleza kwamba Bw ZANGIRA atapelekwa mahakamani kesho yake, jumatatu. Hata hivyo, RTD haikutaja atapelekwa mahakama ipi. Kwavile wananchi walizoea kwamba washtakiwa wa makosa ya jinai hupelekwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jumatatu asubuhi watu wengi walijazana mahakamani hapo kujionea wenyewe Mshtakiwa ZANGIRA yukoje na kusikiliza alifanya vipi ujasusi huo.

Hata hivyo, wananchi hao waliula wa chuya kwani kisheria Ujasusi ni kosa kubwa ambalo ni lazma lisikilizwe na hmu Mahakama Kuu na lazma wawepo Wazee wa Baraza kumsaidia Jaji kama yalivyo makosa mengine makubwa kama vile mauaji au uhaini . Ni kwasababu hiyo basi, Bw. ZANGIRA, jumatatu ya tarehe 26.9.1977 alifikishwa Mahakama Kuu, na si Kisutu, toka gereza la Ukonga akiwa amefungwa pingu chini ya ulinzi mkali.

Kutokana na upekee wa kesi hii, ilibidi Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini(DPP) aiendeshe mwenyewe badala ya Mawakili wa Selikali walio chini yake. Aidha, kutokana na ukweli kwamba kesi hiyo ilikuwa ni ya aina yake, ikabidi isikilizwe na Jaji Mkuu, Mh. FRANCIS NYALALI mwenyewe. Mh. NYALALI alisaidiwa na wazee wa Baraza ambao ni Bw. ZUBEIR ALLY, Bw. HUSSEIN ZAMANI na http://Bw.wengine makubwa kama vile duct iliendeshwa kwa kasi ambapo ndani ya siku 10 tu hukumu ikatolewa.

Mashtaka Dhidi ya Bw. ZANGIRA



Siku hiyo ya kwanza saa 3 asubuhi, DPP MEELA alimsomea Bw. ZANGIRA mashtaka 3:

Shtaka la 1 lilikuwa ni kukusanya habari kisha kuzitoa kwa mzungu aishie Uingereza aitwaye JOHN WILSON kwa nia ya kuvuruga usalama wa nchi yetu na kwamba taarifa hizo zingeweza kutumiwa na mataifa ya nje yanayoichukia Tanzania kuvuruga usalama wa nchi. 

Kosa la 2 ni kumpatia Bw JOHN WILSON habari ambazo zingeharibu jitihada za TANU na vyama vya ukombozi vya SWAPO, FRELIMO, PAC, ANC na ZANU 

Kosa la 3 ni kutoa taarifa za OAU kwa JOHN WILSON. 

Mashtaka haya yote matatu yalidaiwa ni kinyume na Kifungu cha 9(1)(a) na 9(2)(1) vya Sheria ya Usalama wa Taifa, 1970.

Mshtakiwa ZANGIRA, aliyekuwa akitetewa na wakili THOMAS MKUDE wa lililokuwa Shirika la Sheria Nchini (TLC), alikana mashtaka yote hayo 3 ambayo ilidaiwa aliyatenda kati ya mwaka 1971 na Julai 1977.

DPP, ambaye aliileza Mahakama kwamba Bw. ZANGIRA ni Afisa Uhusiano wa hoteli ya Kilimanjaro aliyekuwa pia Afisa Usalama wa Taifa, aliita mashahidi 8.

Shahidi wa kwanza alikuwa ni SASP ALI JUMA GUGURU. Kwa ujumla, maelezo ya mashahidi hao 8 yalikuwa ni kwamba tarehe 27.7.1977, Bw GUGURU alipokea habari za ujasusi na akamtuma Sajin ABDALLAH kuchunguza nani anatumia sanduku la posta 3900 DSM. Sajin ABDALLAH akatumia mbinu za medani na kugundua kwamba anayelitumia si mwingine bali ni Bw. ZANGIRA hivyo wakaanza kumfwatilia nyendo zake kwa karibu.

Siku tatu tu baadaye, yaani tarehe 29.7.1977, saa 2 asubuhi, Bw ZANGIRA aliondoka nyumbani kwake akawa anaenda "mdogomdogo" ofisini kwake kwa kupitia posta bila kujua kuwa alikuwa anafanyiwa "surveillance" kali ya nyendo zake!.

Bw. ZANGIRA alipofika posta akafungua sanduku lake la barua na kutoa barua moja aliyoikuta. Kufumba na kufumbua akanyakwa na polisi!

Bw. ZANGIRA alikiri kuwa barua hiyo ni yake na ilipofunguliwa ilikuwa na £ 150. Barua hiyo ilikuwa imeandikwa na JOHN WILSON wa PARKSIDE, DERRY HILLS, CALNE, WITS, UK ikimtaka Bw. ZANGIRA atafute na kumpa habari juu ya namna uhusiano kati ya China na Tanzania unavyoharibu uhusiano wa Tanzania na majirani. Pia ilimtaka aeleze kuhusu vyama vya ukombozi ambavyo makao yake makuu yako Dar Es Salaam. Aidha, ilimtaka kutotumia jina lake halali na kwamba atalipwa £ 150 kwa mwezi na akileta habari zaidi ataongezewa.

Nyumba ya Bw ZANGIRA ilisachiwa na kisha ofisi yake nayo ilisachiwa ambapo zilipatikana barua 33. Barua zote hizo zilipokelewa mahakamani kama vithibiti.

Barua ya kwanza kuandikwa iliandikwa tarehe 29.11.1971 na ikafuatiwa na zingine tarehe 18.2.1972, 29.2.1972, 11.3.1972, 25.3.1972 na 12.4.1972. Barua hizo zilizungumzia mambo mbalimbali ya ujasusi huku zikionesha ZANGIRA alitumiwa £485.

Aidha, baadhi ya barua hizo zilitoa pongezi kwa Bw ZANGIRA kwa kazi nzuri anayofanya na zingine zilimlaumu baada ya kukaa kimya kwa kipindi kirefu. Pia, Bw ZANGIRA alitakiwa kutoa taarifa kuhusu mambo ya OAU na ziliko kambi za wapigania uhuru hapa nchini na kuulizia iwapo Rais NYERERE alikuwa akipendwa na wapigiania uhuru na ni nani nchini angekuja kuchukua nafasi yake.

Bw ZANGIRA alitakiwa pia kutoa taarifa kuhusu ofisi zote za ubalozi na maeneo zilipo na ni zipi zinawaunga mkono Wapigania uhuru. Barua hizo pia zilionesha alikuwa akipokea fedha mara kwa mara na aliwahi kumwandikia Bw. JOHN WILSON akimtaka ampe fedha za kujenga nyumba na kununulia gari kwani alikuwa amefanya kazi kubwa ya kupeleka taarifa hizo nyeti na alijibiwa kwamba apeleke "Account No." yake na avute subira. Mwisho, barua zilionesha alisafiri kwenda Kenya (22.7.1974) na Chileke, Malawi(7.4.1976) ambako alitajiwa na JOHN WILSON hoteli za kufikia na watu wa kukutana nao.

Utetezi wa Bw. ZANGIRA

Baada ya kesi hiyo kusikilizwa mfululizo kwa siku 4 na upande wa mashtaka kufunga kesi yao, Ijumaa, tarehe 30.9.1977 ikawa zamu ya Bw ZANGIRA kutoa utetezi wake.

Mh NYALALI alimueleza kwamba anayo haki ya kujitetea baada ya kula kiapo ambapo akimaliza kujitetea ataulizwa maswali au anaweza kuchagua kutoa utetezi bila kuapa ambapo hataulizwa swali na Jaji NYALALI, DPP Meela wala Wazee wa Baraza.

Bw ZANGIRA alichagua kutoa utetezi bila kuapa, hivyo hakuulizwa maswali.

Katika utetezi wake, Bw ZANGIRA alikiri kuwa barua hizo zote ni zake na kwamba ni kweli alikuwa akimpelekea habari Bw JOHN WILSON ila alifanya hivyo kama mwandishi wa habari kwani habari hizo zilikuwa ni za kawaida tu na zilipatikana magazetini. Aidha, alidai kwamba habari alizokuwa akituma zilikuwa za mambo ya biashara tu.

Bw ZANGIRA alieleza zaidi kwamba zamani alikuwa akifanyakazi Subuzani Tours & Safaris, Arusha ambapo kazi yake ilikuwa kuwapeleka watalii mbugani.

Alieleza kuwa mwanzoni mwa 1971 alifanya kazi ya kumpeleka mtalii mmoja aitwae WILTSHIRE mbuga ya Mikumi. Bw WILTSHIRE alimwambia kuwa ana rafiki yake yuko UK anatafuta mwandishi hivyo yeye akasema yuko tayari hivyo akampa Bw WILTSHIRE "Contacts" zake. Baada ya miezi michache ndipo alipoanza kupokea barua toka kwa JOHN WILSON.

Bw ZANGIRA alieleza kwamba alikuwa akilipwa kwa habari zote alizokuwa akizipeleka toka 1971 hadi 1977 na kwamba alipigwa bumbuwazi aliposhtukia anakamatwa asubuhi ya tarehe 29.7.1977 mara tu baada ya kuchukua barua kwenye sanduku lake la posta toka kwa JOHN WILSON.



Hukumu

Baada ya ZANGIRA kutoa utetezi wake, Jaji NYALALI aliwaeleza kwa kifupi wazee wa Baraza mlolongo wote wa kesi hiyo ili waweze kutoa maoni yao. Baada ya hapo, Wazee hao wa Baraza walitoa maoni yao ambapo wawili (SIMBA SALUM na HUSSEIN HAMIS waliona mashtaka yamethibitishwa wakati Mzee ZUBERI ALLY aliona mashtaka hayakuthibitishwa).

Mh NYALALI akaahirisha kesi hiyo na kuahidi kutoa hukumu Jumatano ya tarehe 5.10.1977. Siku hiyo, tofauti na ilivyokuwa siku ya kwanza, umati mkubwa ulifurika Mahakamani hapo kuanzia saa moja asubuhi na ulinzi ulikuwa umeimarishwa vilivyo.

Mh. NYALALI aliisoma hukumu hiyo ambapo alimtia hatiani Bw ZANGIRA kwa makosa yote 3 aliyoshtakiwa nayo. Mh NYALALI alisema:  

"JOHN WILSON alikuwa ni Jasusi aliyekuwa akitumiwa na mataifa fulani ili kuangamiza usalama wa Taifa letu. Utetezi wa Bw ZANGIRA kwamba alikuwa anamtumia WILSON habari za biashara hauna mashiko. Hizo habari hazikuwa za kumfaa Mfanyabiashara yeyote bali Haini SMITH na Kaburu VOSTER wa Afrika ya Kusini. Vilevile, kama ni habari za biashara ni kwanini ZANGIRA atakiwe kutumia jina bandia?. Tanzania ni moja ya nchi zilizo mistari wa mbele Kusini mwa Afrika hivyo kitendo cha ZANGIRA kutoa siri za vyama hivyo na za OAU ni sawa na Uhaini".

Baada ya kutiwa hatiani, DPP MEELA aliiomba Mahakama imwadabishe Bw ZANGIRA kwa kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine hasa ukizingania umuhimu wa Tanzania katika ukombozi kusini mwa Afrika.

Nae MKUDE, wakili wa ZANGIRA, aliiomba Mahakama imuhurumie mteja wake kwani hilo ni kosa lake la kwanza na anategemewa na nduguze.

Mh NYALALI, baada ya kusikiliza "Aggravating & Mitigating factors" hizo, alitafakari kwa kina kisha akamuhukumu Bw ZANGIRA kwenda jela miaka 20.

Huyo ndiye JUMA THOMAS ZANGIRA, Mtanzania wa kwanza kushtakiwa na kutiwa hatiani kwa ujasusi.


Makala hii ni kwa msaada wa MAJAMBO, MAKTABA YA GLOBU YA JAMII, (Michuzi blog).

Saturday, June 6, 2026

HII HAPA HOTUBA YA DG WA TET, DKT. ANETH KOMBA KWENYE HAFLA YA UTOAJI WA ZAWADI KWA WASHINDI WA SHINDANO LA TAIFA LA NNE LA STADI ZA UFUNDISHAJI KWA WALIMU NCHINI


Na. Mwandishi Wetu, Dar.


Mgeni Rasmi, Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe (Mb); 

Pamoja n wageni wengine: Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Michezo na Utamaduni Mhe. Husna Sekiboko, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Daniel Mushi;

Walimu; Wanafunzi; Wageni waalikwa;         

Mabibi na Mabwana.

"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!

"Ufundishaji bora________ Taifa imara"

Aidha, kwa niaba ya Menejimenti ya Taasisi ya Elimu Tanzania ambayo ndiyo mwendeshaji wa shindano hili na mwandazi wa hafla hii ninawakaribisha nyote katika Duru ya Nne ya hafla ya Utoaji wa Zawadi kwa washindi wa shindano la Taifa la Nne la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali na Msingi na Duru ya pili ya Utoaji wa Zawadi kwa washindi wa shindano la Taifa la Pili kwa walimu wa Sekondari.

Pili, kipekee kabisa nakushukuru sana wewe binafsi Mhe. Mgeni Rasmi kwa kukubali kuwa Mgeni Rasmi wa hafla hii muhimu ya Utoaji wa Zawadi kwa Washindi wa Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari.

Ninawashukuru sana wafadhili na wadau mbalimbali waliowezesha kufanikisha shindano hili. Kwa Heshima ninaomba niwatambue na niwatambulishe kwako kama ifuatavyo:

Kwanza Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Ndugu Firas Raad, pamoja na wawakilishi wengine kutoka Benki ya Dunia. Tunawashukuru sana kwa kuwezesha shindano hili.

Pili, Shirika la Educate; kwa kuiwezesha TET kuwa na mfumo mahususi wa kidijitali kwa ajili ya kuendesha shindano hili (National Teaching Skills Competitionb System Skills), pamoja na mchango wenu katika kufanikisha ufundishaji na ujifunzaji wa Somo loa Elimu ya Biashara, uendeshaji wa shindano hili kwa walimu wa Somo la Elimu ya Biashara na na utoaji wa Zawadi kwa washindi wote wa Somo la Elimu ya Biashara.

Shirika la Enabel kwa kuwezesha upatikanaji wa zawadi za kompyuta Mpakato Tisa kwa washindi wa elimu ya Sekondari katika masomo ya STEM. Mchango wenu utaendelea kuhamasisha matumizi ya TEHAMA na ubunifu katika elimu.

Project Zawadi kwa kutoa zawadi za kompyuta mpakato Tisa. Mchango wenu ni chachu muhimu katika kukuza ari ya ushiriki na ubunifu wa walimu katika ufundishaji Shuleni.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa ukarimu na ushirikiano wenu na kwa kufadhili hafla hii kwa kupunguza bei halisi ya ukumbi huu ambayo imekuwa ni sehemu ya uthamini wa shindano hili.

Shindano la taifa la Stadi za Ufundishaji kwa Mwaka 2026 ni la nne kwa walimu wa Elimu ya Awali na Msingi, na la pili kwa walimu wa Elimu ya Sekondari na limejumuisha halmashauri zote 184 za Tanzania Bara.


Kwa ngazi ya Elimu ya Awali, shindano hili limejikita katika kuimarisha umahiri wa stadi za awali za kusoma, hususan ufundishaji wa sauti za herufi ambazo zimekuwa zikileta changamoto kwa wanafunzi katika kuzitamka kwa usahihi pamoja na kuzitumia katika kuunda silabi na maneno sahihi.

Kwa ngazi ya Elimu ya Awali, lengo la shindano ni kutatua changamoto za ufundishaji na ujifunzaji wa stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK), ili kuhakikisha wanafunzi wanamudu stadi hizo muhimu wanapofikia Darasa la Tatu. 

Eneo hili la ushindani iinaunga mkono maono na mikakati ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha kuwa watoto wote wanapata wanaweza  kusoma kwa ufasaha wanapofikia Darasa la Tatu.

Katika Elimu ya Msingi, shindano hili lilijikita katika Darasa la Kwanza kupitia umahiri wa somo la Kiingereza wa “Demonstrate mastery of basic English language skills”, Umahiri huu uliteuliwa kwa makusudi ili kuendelea kutatua changamoto zinazojitokeza katika ufundishaji na ujifunzaji za stadi za awali za lugha ya Kiingereza, hususan katika matamshi sahihi ya sauti za konsonanti na irabu.  


Kwa upande wa Elimu ya Sekondari, shindano lilihusisha masomo yafuatayo: 

Somo la ‘Physics’ limehusisha shughuli mahususi ya Describe the concept of motion under gravity; Somo la ‘Mathematics’, shughuli mahususi ya Recognising the point of intersection of two linear equations;

Somo la ‘Computer Science’ shughuli mahususi ya Create an algorithm for a familiar real-life problem; na 

Somo la ‘Business Studies’ katika shughuli mahususi ya explain how to establish a startup, specifically a sole proprietorship.

Maandalizi ya shindano hili yalianza kwa wakuza mitaala wa TET kubainisha  maeneo ya ushindani kwa kutumia taarifa za uchambuzi wa majibu ya watahiniwa inayotolewa na Baraza la Mitihani Tanzania (CIRA) pamoja na kubainisha maeneo ambayo ni mapya klatika mtaala. Baada ya maeneo haya kubainisha tangazo rasmi la shindano liliandaliwa  na kusambazwa kupitia OWM TAMISEMI. Tangazo liliwataka walimu kuandaa  andalio la somo la kipindi na kujirekodi akifundisha katika kipindi  chenye urefu wa kati ya dakika 10-15. Kisha mwalimu alipaswa kujisajili katika  mfumo wa kidijitali unaoitwa National Teaching Skills Competition System na kisha kupakia andalio la somo na video. 





Mfumo huu ulimpa mrejesho mwalimu iwapo video yake imepokelewa na katika ngazi zote za tathimini kuanzia ngazi ya halmashauri hadi taifa. 

Kupitia mfumo huu Jumla ya walimu  3,153 walijisajili lakini waliofanikiwa kupakia video kwa ajili ya tathimini ngazi ya halmashauri/wilaya walikuwa ni 1,263  sawa na asilimia 40.  Baada ya video kupokelewa tathmini ilifanyika katika ngazi tatu: ngazi ya halmashauri, mkoa na Taifa kupitia mfumo kwa kuzingatia vigezo vya ushindani vilivyoandaliwa awali na  majaji.  Majaji walitakiwa kujisajili katika mfumo na kufanya tathimini katika ngazi husika, na kila jaji aliweza kuona video katika ngazi anayotathimini tu. Vigezo vya tathimini vilikuwa ni pamoja na maudhui kuakisi umahiri lengwa, mtiririko wa somo,  matumizi ya mbinu shirikishi, matumizi ya TEHAMA, matumizi ya zana, ukuzaji wa stadi za karne ya 21 sanjari na matumizi ya upimaji endelevu katika mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji.  

Katika ngazi ya halmashauri, video 1,263  zilifanyiwa tathimini na kati ya hizo  video 751 ndiyo zilichaguliwa kuendelea na mchakato wa shindano katika ngazi ya mkoa.  Kati ya Video 751 zilizowasilishwa katika ngazi ya mkoa video 232 ziliteuliwa kuendelea na shindano katika ngazi ya Taifa. Aidha, kati ya Video 232 zilizowasilishwa, video  35 ndizo zilizoshinda katika tathmini ya Taifa na hivyo  washiriki 35 ndio  walioshinda ngazi ya Taifa na hawa walifanya ufundishaji wa ana kwa ana mbele ya majaji wa ngazi ya taifa kwa ajili ya tathmini ya mwisho ili kupata mshindi wa kwanza hadi wa tano kwa kila eneo. 

Washindi hao watano kwa kila umahiri ndio tunaowatunukia zawadi katika hafla ya leo Juni 6, 2026.

Majaji katika shindano hili walikuwa ni wahadhiri wa vyuo vikuu, wakufunzi wa vyuo vya ualimu, wathibiti ubora wa shule na wakuza mitaala wa TET. Kwa nafasi hii ninawashukuru sana majaji wote wa shindano hili kuanzia ngazi ya halmashauri mpaka taifa kwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa hatimaye kupata washindi bora wa shindano letu.






Hakika, mchakato wa tathmini ulifanyika kwa weledi na umakini mkubwa katika kuhakikisha kuwa kila mwalimu anatendewa haki. 

Uzingativu vigezo vya tathimini na matumizi ya mfumo wa kijigidital katika tathmini hii vinathibitisha uhalali na uthabiti wa matokeo ya washindi wa shindano hili kwa mwaka 2026. 

Washindi watapewa zawadi kulingana na nafasi zao za ushindi kama ifuatavyo: 

(a) Mshindi wa kwanza kwa kila nyanja  atapata fedha taslimu Tsh 2,500,000/=, Cheti cha Pongezi, Cheti cha Ushindi na Kompyuta Mpakato moja. Shule anayofundisha itapata Projekta. 

Vilevile, shule zilizotoa mshindi wa kwanza katika maeneo ya Kusoma kwa Darasa la Awali, Kiingereza kwa Darasa la Kwanza, Ufaraguzi wa Zana kwa Darasa la Pili zitapata vibao vya kielektroniki (Electronic Pad) 100 vyenye thamani ya Shilingi 5,000,000/=.

Aidha, video zote za washindi wa nafasi ya kwanza zitarekodiwa upya katika studio za TET na kupakiwa kwenye Mfumo wa Elimu wa Kidijitali (LMS) pamoja na kurushwa kupitia TET Soma Kwanza TV ili kuwapa nafasi walimu wote nchini kujifunza.

(b) Mshindi wa Pili- atapata Shilingi 2,000,000/=, Cheti cha Pongezi, Cheti cha Ushindi na Kompyuta Mpakato na Shule anayofundisha itapata Projekta.

(c) Mshindi wa Tatu- Shilingi 1,500,000/=, Cheti cha Pongezi, Cheti cha Ushindi na Kompyuta Mpakato na Shule anayofundisha itapata Projekta.

(d) Mshindi wa Nne- Kompyuta Mpakato na Cheti cha Pongezi.

(e) Mshindi wa Tano - Kompyuta Mpakato na Cheti cha Pongezi.

Shindano hili lina nafasi muhimu katika kuimarisha Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA) kwa kuwa linatoa fursa kwa walimu kujifunza kwa vitendo, kuonesha umahiri, kubadilishana uzoefu, na kuendelea kujiendeleza kitaaluma wakiwa kazini. Kupitia shindano hili, walimu hujifunza kutoka kwa wenzao, huibua mbinu bunifu za ufundishaji, na kuimarisha matumizi ya mbinu shirikishi, upimaji, TEHAMA pamoja na matumizi ya zana za kufundishia na kujifunzia.

Aidha, shindano hili linaifanya MEWAKA kuwa ya vitendo zaidi kwa kuwa maarifa, uzoefu na bunifu zinazozalishwa kupitia shindano hili hurekodiwa, kuhifadhiwa na kusambazwa kupitia majukwaa ya kujifunzia kama MUK/LMS na TET Soma Kwanza TV, hivyo kuwafikia walimu wengi zaidi nchini. Kwa msingi huo, shindano hili limeendelea kuwa chachu muhimu ya kujenga utamaduni wa kujifunza endelevu, kuimarisha umahiri wa walimu, na kuinua ubora wa ufundishaji na ujifunzaji nchini.”

Nimalizie kwa kuwapongeza walimu wote walioshiriki katika shindano hili kwa mwaka huu 2026. Aidha, Ninawashukuru sana vongozi wote wa wizara  ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kwa miongozo na usimamizi katika kutekeleza afua  za TET kupitia ya miradi wa BOOST na SEQUIP. 

Ninawashukuru pia waratibu wote wa mradi wa BOOST na SEQUIP kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI na TET  kwa kuratibu utekelezaji wa afua hii ya shindano kupitia miradi hii. Kwa namna ya pekee  Ninakushukuru sana wewe Mgeni Rasmi kwa kutenga muda wa kuja kuwa mgeni rasmi katika hafla hii muhimu." Dkt. Aneth Komba.








DKT. KIJAJI: UTALII WA HALAL NI ZAO JIPYA LENYE FURSA ZA KUONGEZA IDADI YA WATALII NA PATO LA TAIFA *

 *


Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.), amesema kuwa Utalii wa Halal (Halal Tourism) ni fursa mpya itakayoongeza idadi ya watalii  na pato la Taifa.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo leo Juni 06,2026 katika kikao kilichofanyika Zanzibar kuhusu uendelezaji na utangazaji wa zao jipya la Utalii wa Halal, kilichoandaliwa na Taasisi ya Samia Foundation, kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.

Ameeleza kuwa Utalii wa Halal ni moja ya mazao mapya ya utalii yatakayochochea ongezeko la watalii nchini, hususani kwa kuvutia wageni wengi zaidi kuitembelea Tanzania na kupanua masoko ya kimataifa. Amesema aina hii ya utalii huvutia wageni wanaohitaji huduma zinazozingatia misingi ya imani, maadili na tamaduni zao wakati wa kutalii ikiwemo fursa za kufanya ibada katika maeneo ya huduma za utalii na malazi,  mapishi na vyakula kwa misingi ya halal, kuepuka matumizi ya vilevi, kuzingatia faragha za jinsia na familia, na fursa za kuandaa vifurushi vya safari kutembelea maeneo ya vivutio.

Ameongeza kuwa Zanzibar tayari imeridhia na kuchukua hatua za kimkakati za kuendeleza utalii wa halal ambapo pia wadau wa Sekta Binafsi  katika mnyororo wa huduma za utalii wameonesha mwitikio mkubwa, sauala ambalo lina fursa muhimu katika kuiwezesha nchi  kufikia malengo ya kuongeza idadi ya watalii na Pato la Taifa.

Kwa upande wake, Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mhe. Mudrick Soraga, amesema kupitia Kamisheni ya Utalii Zanzibar, wataweka taratibu zote muhimu kuhakikisha Utalii wa Halal unatekelezwa na kutangazwa kwa ufanisi wa hali ya juu.

Akiwasilisha mada kuhusu Utalii wa Halal, Sheikh Ismail Bullock kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Dar Al Ber Society yenye Makao Makuu yake jijini Dubai, amebainisha kuwa utalii huo umefanikiwa katika nchi mbalimbali duniani na kwamba kwa Tanzania pia utachangia kuongeza idadi ya watalii, Pato la Taifa na fursa za ajira.

Naye mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi, Richie Wandwi, amesema ni wakati muafaka kwa Tanzania kuendeleza zao la Utalii wa Halal hatua ambayo inakwenda sambamba na utekelezaji wa matakwa ya Sera ya Taifa yappp







Utalii ya mwaka 1999 inayotilia mkazo suala la kuongeza wigo wa mazao ya utalii nchini na utoaji wa huduma bora kwa wageni kwa kukidhi mahitaji ya soko la utalii wa Kimataifa.


TFS YAELIMISHA WAVUNAJI RUFIJI, YASISITIZA UVUNAJI HALALI WA MAZAO YA MISITU



Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki umeendelea kuimarisha usimamizi wa rasilimali za misitu kwa kutoa elimu kwa wavunaji na wafanyabiashara wa mazao ya misitu katika Wilaya ya Rufiji, huku wadau wa sekta hiyo wakiomba kuboreshwa kwa mfumo wa usajili ili kurahisisha shughuli zao za biashara.


Akizungumza katika kikao cha elimu kwa wadau hao Juni 03,2026, Mhifadhi Mkuu wa TFS Kanda ya Mashariki, Mkama Kusaga, alisema mafunzo hayo yanalenga kuongeza uelewa wa sheria, kanuni na taratibu za uvunaji na biashara ya mazao ya misitu ili kuhakikisha shughuli hizo zinafanyika kwa kuzingatia misingi ya matumizi endelevu ya rasilimali za misitu.

Alisema kabla ya kuanza uvunaji, wafanyabiashara na wavunaji wanapaswa kuwasilisha maombi katika vijiji husika, kupata idhini kutoka mamlaka zinazotambulika na kuhakikisha wanamiliki vibali vyote vinavyotakiwa kisheria.

“Tunataka wadau wote wafahamu na kuzingatia taratibu zilizowekwa ili rasilimali za misitu ziendelee kunufaisha wananchi na Taifa kwa ujumla bila kuhatarisha uendelevu wake,” alisema Kusaga.

Aliongeza kuwa uzingatiaji wa sheria na kanuni za misitu utasaidia kupunguza migogoro, kudhibiti uvunaji haramu na kuimarisha uhifadhi wa mazingira.

Wakichangia mjadala katika kikao hicho, baadhi ya wafanyabiashara walieleza kuridhishwa na elimu iliyotolewa na TFS, wakisema imewapa uelewa mpana wa wajibu wao katika kulinda rasilimali za misitu wakati wa kutekeleza shughuli za biashara.

Hata hivyo, waliomba serikali kuangalia uwezekano wa kuwa na mfumo wa usajili unaowaruhusu kujisajili mara moja katika ngazi ya wilaya badala ya kufanya usajili katika kila kijiji wanachofanyia biashara, wakidai hatua hiyo itapunguza urasimu na gharama za uendeshaji wa shughuli zao.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara hao, Mussa Maganga alisema pamoja na kupongeza juhudi za TFS za kutoa elimu, bado kuna haja ya kuimarisha ushirikiano kati ya wafanyabiashara na watumishi wa serikali ili kurahisisha utekelezaji wa shughuli zinazofanyika kwa mujibu wa sheria.

“Tunathamini elimu hii kwa sababu imetupa mwanga kuhusu taratibu za sekta ya misitu. Tunatarajia kuona maboresho zaidi katika usajili na kuendelea kujenga ushirikiano mzuri na TFS,” alisema.

TFS imeendelea kusisitiza kuwa ushiriki wa wadau katika kuzingatia sheria na kanuni za misitu ni muhimu katika kulinda rasilimali za Taifa na kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kuchangia ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii kwa vizazi vya sasa na vijavyo.









PROF. SHEMDOE AWATAKA WALIMU KUONGEZA UBUNIFU KATIKA UFUNDISHAJI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe


-Walimu 35 walioshinda tuzo za ufundishaji kupatiwa viwanja


WALIMU nchini wamehimizwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kujituma na kutumia mbinu bunifu za ufundishaji ili kuimarisha ubora wa elimu na kuchangia maendeleo ya taifa, huku walimu 35 walioibuka washindi katika Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji wakielekezwa kupatiwa viwanja karibu na maeneo yao ya kazi kama sehemu ya motisha.

Akizungumza Juni 6, 2026 jijini Dar es Salaam katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano hilo kwa walimu wa elimu ya awali, msingi na sekondari, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe, amesema walimu wana mchango mkubwa katika kuwalea na kuwaandaa wanafunzi kuwa wananchi wenye maarifa, stadi na maadili mema yanayohitajika katika jamii.

Prof. Shemdoe amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango wa walimu kwa kuweka mazingira bora ya kazi na motisha mbalimbali zinazolenga kuongeza ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji.

Aidha, amewataka walimu kuendelea kutumia mbinu za kisasa na bunifu katika ufundishaji ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kufikiri kwa kina, kubuni na kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.

Amesema tuzo hizo zinalenga kuhamasisha ubora, uwajibikaji, ubunifu na kujituma katika kazi za kufundisha, akisisitiza kuwa maendeleo ya taifa yanategemea kwa kiasi kikubwa ubora wa rasilimali watu inayozalishwa kupitia mfumo wa elimu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Husna Sekiboko


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Husna Sekiboko, amesema mafanikio katika sekta ya elimu yanahitaji ushiriki wa wadau wote, wakiwemo wazazi, walimu, wanafunzi na viongozi wa jamii.

Amesema maboresho yanayoendelea katika mifumo ya uongozi na utawala yanalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za elimu na kuimarisha matokeo ya kujifunza kwa wanafunzi.


Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba, amesema shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji la mwaka 2026 ni la nne kwa walimu wa elimu ya awali na msingi na la pili kwa walimu wa elimu ya sekondari, likihusisha halmashauri zote 184 za Tanzania Bara.

Amesema kwa upande wa elimu ya awali, shindano hilo limejikita katika kuimarisha umahiri wa ufundishaji wa stadi za kusoma, hususan sauti za herufi ambazo zimekuwa changamoto kwa baadhi ya wanafunzi katika kuzitamka na kuzitumia kwa usahihi katika kuunda silabi na maneno.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba


“Lengo la shindano hili ni kusaidia kutatua changamoto za ufundishaji na ujifunzaji wa stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) ili kuhakikisha wanafunzi wanazimudu stadi hizo muhimu wanapofikia Darasa la Tatu. Eneo hili la ushindani linaunga mkono maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha watoto wote wanasoma kwa ufasaha wanapofikia Darasa la Tatu,” amesema Dkt. Komba.

Ameeleza kuwa maandalizi ya shindano hilo yalihusisha uchambuzi wa matokeo ya wanafunzi kupitia taarifa za Baraza la Mitihani la Tanzania pamoja na maeneo mapya yaliyoingizwa katika mtaala ili kubaini maeneo yanayohitaji kupewa kipaumbele.

Kwa mujibu wa Dkt. Komba, walimu walitakiwa kuandaa andalio la somo, kujirekodi wakifundisha kwa muda wa dakika 10 hadi 15 na kupakia video pamoja na andalio hilo katika mfumo wa kidijitali wa National Teaching Skills Competition System kwa ajili ya tathmini.

Jumla ya walimu 3,153 walijisajili katika mfumo huo, huku walimu 1,263 sawa na asilimia 40 wakifanikiwa kupakia video zao kwa ajili ya tathmini katika ngazi ya halmashauri.

Amesema tathmini ilifanyika katika ngazi tatu ambazo ni halmashauri, mkoa na taifa kwa kuzingatia vigezo mbalimbali ikiwemo ubora wa maudhui, mtiririko wa somo, matumizi ya mbinu shirikishi, matumizi ya TEHAMA, matumizi ya zana za kufundishia, ukuzaji wa stadi za karne ya 21 na matumizi ya upimaji endelevu katika mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji.

Katika mchujo wa shindano hilo, video 751 zilifanikiwa kuingia ngazi ya mkoa kutoka video 1,263 zilizotathminiwa katika ngazi ya halmashauri. Kati ya hizo, video 232 zilichaguliwa kuingia ngazi ya taifa.