
Rais wa
Marekani Barrack Obama anasema mshukiwa mkuu wa mashambulizi yaliyotokea
katika Ubalozi wa taifa hilo mjini Bengazi nchini Libya na kusababisha
Balozi wa Marekani nchini humo mwaka 2012 amekamatwa.
Obama
amesema, mshukiwa huyo
Ahmed Abu Khattala (PICHANI) alitiwa mbaroni na
kikosi maalum cha Marekani na tayari ameanza kusafirishwa kwenda
Marekani kujibu tuhuma zinazomkabili, amethibitisha waziri wa mambo ya
nje wa Marekani John Kerry.
Msemaji wa shirika la ujasusi nchini Marekani John Kirby amemtaja Ahmed
Abu Khattala kuwa gaidi nambari moja kaongeza kuwa Khattala ni miongoni
mwa walioratibu mashambulizi kadhaa dhidi ya majengo yanayomilikiwa na
Marekani huko Lybia.
Wakati wa mashambulizi hayo Balozi wa Marekani Chris Stevens na watu wengine watatu walipoteza maisha.
Wakati wa mashambulizi hayo Balozi wa Marekani Chris Stevens na watu wengine watatu walipoteza maisha.
No comments:
Post a Comment