ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, April 19, 2015

TASWIRA MBALIMBALI MKUTANO WA JIONI WA WASABATO WATANZANIA WAISHIO NCHINI MAREKANI


Mchungaji Geoffrey Mbwana ambaye pia ni makamu wa Rais wa Wasabato Duniani akielezea hali ya kanisa lilivyo leo huku pia akiongoza kuimbisha nyimbo mbalimbali kwenye mkutano mkubwa wa neno la Mungu wa Wasabato Watanzania waishio nchini Marekani uliofanyika mida ya jioni siku ya Jumamosi April 18, 2015 Silver Spring, Maryland.

Mchungaji Celeb Migombo akielezea somo la wanandoa na vitu gani vya kuepuka vinavyosababisha kuvunja mahusiano ya wapendanao.

Maliyatabu mmoja ya waratibu wa mkutano mkubwa wa neno la Mungu la Wasabato Watanzania waishio nchini Marekani akifafanua jambo.

Noah Manongi toka Massachusetts akiongoza vikundi vya waimbaji wa nyimbo za injili.

Mwimbaji Betty Enoch toka Columbia Maryland akiimba moja ya nyimbo zake za injili kwenye mkutano mkubwa wa neno la Mungu uliofanyika siku ya Jumamosi April 18, 2015 jioni.
 Wanaume singers nao wakiimba moja ya nyimbo za injili
 Kikundi cha kwaya nyimbo za injili cha Sounds of Glory singers kikitoa burudani kwenye mkutano mkubwa wa neno la Mungu.

Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

No comments: