Advertisements

Saturday, March 16, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSTUKIZA KUKAGUA UJENZI WA NYUMBA ZA ASKARI MAGEREZA UKONGA NA MAGOMENI KOTA JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na baadhi ya wazee waliokuwa wakaazi wa nyumba za Magomeni Kota jijini Dar es salaam wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kuona maendeleo ya ujenzi wa nyumba za ghorofa alizoziwekea jiwe  la msingi Aprili 15, 2017 ambapo mpaka sasa ujenzi wake umesimama kwa sababu ambazo hazikuweza kujulikana mara moja.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za askari Magereza huko Ukonga jijini Dar es salaam alikofanya ziara ya kushtukiza leo Jumamosi Machi 16, 2019 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimwangalia Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza  Julius Ntembala akipima nguzo wakati akikagua  maendeleo ya ujenzi wa nyumba za askari Magereza huko Ukonga jijini Dar es salaam alipofanya ziara ya kushtukiza leo Jumamosi Machi 16, 2019

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za ghorofa za Magomeni Kota jijini Dar es salaam alizoziwekea jiwe  la msingi Aprili 15, 2017 wakati alipofanya ziara ya kushtukiza leo Jumamosi Machi 16, 2019
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba za ghorofa za Magomeni Kota jijini Dar es salaam alizoziwekea mnamo  Aprili 15, 2017 ambapo mpaka sasa ujenzi wake umesimama alipofanya ziara ya kushtukiza leo Jumamosi Machi 16, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za askari Magereza huko Ukonga jijini Dar es salaam alikofanya ziara ya kushtukiza leo Jumamosi Machi 16, 2019
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wana familia ya moja ya nyumba za askari Magereza huko Ukonga jijini Dar es salaam alikotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za askari hao alipofanya ziara ya kushtukiza leo Jumamosi Machi 16, 2019
PICHA NA IKULU

No comments: