Sunday, December 6, 2020

DKT.ABBASI: BASATA, BODI YA FILAMU NA COSOTA TOENI MSAADA WA KISHERIA KWA WASANII

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (wakwanza kulia) akizungumza na Wanamuziki wa Injili (hawapo pichani) kuhusu azma ya serikali ya kuendeleza sekta ya sanaa hivyo na kuwataka watoe maoni ya mambo gani yaboreshwe kuendeleza tasnia hiyo, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, kufuatia tamko la Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa kwa wanamuziki wa injili alipokuwa akifungua Bunge.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (aliyeketi watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wasanii wa Muziki Injili waliyohudhuria kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa kundi la wanamuziki wa injili, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kikao hicho.
Msanii wa Muziki wa Injili Boniface Mwaitege akitoa ombi kwa serikali kuwasaidia wasanii wa Muziki wa Injili wanao dhulumiwa haki zao na moja ya kampuni (jina limehifadhiwa) ya usambazaji wa nyimbo za injili njia ya mtandao, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa wanamuziki wa injili kufuatia tamko la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa wakati alipokuwa akifungua Bunge.
Msanii wa Muziki wa Injili Christina Shusho akitoa ombi kwa serikali la kuandaliwa kwa Tuzo za Muziki wa Injili nchini ili kutoa hamasa kwa wasanii hao, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa wanamuziki wa injili kufuatia tamko la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa wakati alipokuwa akifungua Bunge.
Mtangazaji wa Kipindi Chomoza kinachotangaza Muziki wa Injili kutoka Televisheni ya Clouds James Temu akitoa ombi kwa serikali la wasanii kupata msaada wa kisheria ili kuwasaidia kupata haki zao kutokana na changamoto za mikataba mingi kuwa ya ulaghai, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao cha kujadili mikakati ya kuendeleza sekta ya sanaa kwa wanamuziki wa injili kufuatia tamko la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la kuendeleza Sanaa wakati alipokuwa akifungua Bunge.
Msanii wa Muziki wa Injili Emmanuel Mgaya akitoa ombi kwa serikali la kuangalia suala la gharama za kusajili Youtube Channel kuwa ni kubwa sana kwa kundi la wasanii, kwani wao hutumia akaunti hizo kutafuta masoko ya kazi zao na siyo kuhabarisha umma, leo Desemba 05, 2020 Jijini Dar es Salaam, katika kikao na Wanamuziki wa Injili kujadili mikakati ya kuendeleza tasnia sekta ya sanaa kufuatia tamko la Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akifungua Bunge.

 

No comments: