Thursday, September 26, 2024

RAIS SAMIA AZUNGUMZA NA WANANCHI KATA YA LIKOLA, NAMTUMBO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Kata ya Likola, Wilaya ya Namtumbo, aliposimama eneo hilo kwa ajili ya kuwasalimia, leo asubuhi tarehe 26 Septemba 2024, alipokuwa njiani kuelekea Tunduru, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara yake katika Mkoa wa Ruvuma.

Mhe. Rais Dkt. Samia ameendelea kusisitiza kauli yake ya kuwashukuru wakulima wa Ruvuma na maeneo yote nchi nzima kwa jinsi juhudi zao zimeendelea kuifaharisha nchi kwa usalama wa chakula huku ziada ikitunzwa, nyingine kuuzwa nje ya nchi na kuwa mojawapo ya vyanzo vya pato la taifa na mapato ya fedha za kigeni.
Mbali na kuwashukuru kwa juhudi na ushirikiano wa wakulima, Mhe. Rais Dkt. Samia pia amesisitiza kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi anayoiongoza, itaendelea kutimiza wajibu wake kuwahudumia wakulima hao, hasa kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo, zikiwemo mbolea, huduma za ugani, mbegu bora na masoko ya mazao yao, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 - 2025.

No comments: