Monday, September 30, 2024

TUKAJIANDIKISHE KWENYE DAFTARI LA MKAZI ILI TUPIGE KURA



Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la Mkazi ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 11 hadi 20, 2024 na upigaji wa kura 27, Novemba 2024 kuchagua viongozi wa serikali za Mitaa.
Vikundi vya Jogging vikiwa vinafanya mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili
Vikundi vya Jogging vikiwa vinafanya mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili
Vikundi vya Jogging vikiwa vinafanya mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili.

Na Fredy Mgunda, Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la Mkazi ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 11 hadi 20, 2024 na upigaji wa kura 27, Novemba 2024 kuchagua viongozi wa serikali za Mitaa.

"Niwaombe vijana wote, niwaombe akina mama, akina Baba tuende tukajiandikishe kwenye daftari la mkazi ili tukaweze kupiga kura "

Wito huo ameutoa leo katika viwanja vya Kilwa Kivinje ambako kivinje Jogging klabu wameandaa bonanza lakualika klabu mbalimbali kutoka maeneo mikoa mbalimbali kama vile Dodoma, Mtwara, Pwani na Dar Es Salaam lenye lengo la kudumisha afya, ushirikiano, upendo, umoja na hamasa ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba 27, 2024.

Mhe. Zainabu Telack ametoa angalizo kwa wananchi ambao hawana taarifa sahihi kuhusu vitambulisho walivbyo navyo na zoezi la kujiandikisha katika daftari la mkazi.

"Wapo wenzetu ambao wanasema tayari wanavitambulisho vya kupiga kura vitambulisho kwahiyo hawaoni sababu ya kujiandikisha tena , vile vitambulisho ni kwa ajili ya uchaguzi wa Mwaka kesho lakini kwa uchaguzi huu wa serikali za mitaa, serikali zamitaa ,vijiji na vitongoji tunakwenda kujiandikisha kwenye daftari la mkazi "
Aidha, amewasihii siku ya kupiga kura wajitokeze mapema kwa ajili ya kutimiza wajibu nahaki ya kupiga kura mapema.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Omary amesema kilammojaazishike tarehe hizo muhimu ambazo tarehe 11 hadi 20 Oktoba , 2024 kwa ajili ya kujiandikisha na tarehe 27 siku ya kupiga kura.

No comments: