Kwa mujibu wa ripoti kutoka ikulu hiyo, Mfalme Albert na mkewe wamekubali mualiko kutoka kwa rais wa nchi hiyo Joseph Kabila, kuzuru nchi hiyo mwezi Juni mwaka huu.
Kwa zaidi ya miongo miwili Congo, ilitawaliwa kama himaya ya kibinafsi ya mfalme wa Ubelgiji, Leopold wa pili, ambaye alijilimbikizia utajiri mkubwa kutokana na mauzo ya zao raba.
Watafiti wa historia wanasema mamilioni ya raia wa Congo waliuawa wakati wa utawala wa mfalme Leopold wa pili.
No comments:
Post a Comment