
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa
Sadick Mtulya
WAZIRI wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa ametaka kupewa maelezo ya kina kuhusu afya ya Rais Jakaya Kikwete ikiwa ni siku chache baada ya kiongozi huyo wa nchi kudondoka wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za CCM kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaa.
Tukio hilo la kuanguka kwa Rais Kikwete la Agosti 21 mwaka huu ni la tatu tangu mwaka 2005 baada ya kuanguka siku ya mwisho ya kampeni za CCM mwaka 2005 na kuishiwa tena nguvu mwaka jana wakati akihutubia waumini wa Kanisa la AIC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba. Pia imeripotiwa kuwa aliwahi kuanguka nchini Ubelgiji wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Alipodondoka mwaka 2005, ilielezwa kuwa ilitokana na kufunga lakini daktari wake alitoa taarifa ndefu baada ya Rais Kikwete kudondoka tena mwaka jana, akieleza kuwa hali hiyo ilitokana na uchovu baada ya kusafiri safari ndefu iliyomtoa Italia, Marekani, Dar es salaam, Arusha na baadaye Mwanza.
Kwa Habari Zaidi Bofya Hapa
No comments:
Post a Comment
bila kutumia lugha ya matusi na kumharibia mtu siku
yake