ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, October 19, 2010

SLAA: NITAJINYIMA WATOTO WASOME

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa.

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa jana alibadili hali ya hewa mkoani Shinyanga baada ya kuutikisha mji kiasi cha kusababisha bendera za CCM zilizotundikwa kwenye maeneo mbalimbali kushushwa, huku akisema kuwa yuko tayari kunyimwa kura kwa kosa la kulazimisha watoto kwenda shule.

Mabasi ya daladala, pikipiki na magari madogo ya abiria (taksi) zinazotoa huduma ya usafiri mjini hapa zilifungwa bendera za Chadema na kufanya usafiri uonekane kama mali ya chama hicho.

Baadhi ya pikipiki ambazo ni maarufu kama bodaboda zilisitisha huduma kwa ajili ya kumsindikiza mgombea huyo wa urais wakati akielekea kuhutubia mkutano wa kampeni.

Jina la Dk Slaa lilitawala mji mzima huku baadhi ya wananchi wakieleza kuwa ikitokea kura za mgombea urais wa Chadema zimezidiwa na mgombea urais wa CCM, wataandamana kwa madai kuwa wanaamini kuwa CCM haipendwi na wananchi wa mkoa huo.

"Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini asiposhinda, basi CCM itakuwa imetenda hujuma kubwa kwa kuwa haina wafuasi na sisi tumeichoka. Chama ni Chadema peke yake ndicho chenye matumaini nasi, CCM imeshindwa kutukomboa," alisema mmoja wa waendesha pikipiki hizo.

chanzo:mwananchi

No comments: