
Sadick Mtulya
SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kudokeza ataunda serikali ya watu waadilifu, makini na wachapakazi hodari, wabunge kadhaa wametajwa kuwamo katika baraza jipya la mawaziri linalotarajia kutangazwa hivi karibuni.
SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kudokeza ataunda serikali ya watu waadilifu, makini na wachapakazi hodari, wabunge kadhaa wametajwa kuwamo katika baraza jipya la mawaziri linalotarajia kutangazwa hivi karibuni.
Akitoa hotuba ya kuzindua Bunge la Kumi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma, Alhamisi iliyopita, Rais Kikwete alisema ataunda serikali ya watu wachache ambao wataondoa urasimu watakaokuwa karibu na wananchi na kushirikiana vizuri na wabunge wote bila kujali vyama vya siasa wanavyotoka.
Vyanzo vyetu vya kuaminika, vimeeleza kuwa mbali na sifa alizodekeza Rais Kikwete katika kuteua mawaziri pia amezingatia umri, uzoefu pamoja na uwiano wa mikoa.
“Pamoja na mambo mengine baraza jipya la mawaziri litakuwa na watu wapya, wakongwe pamoja na idadi ya wanawake kuongeza,’’ kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kimemtaja wabunge wanataria kuwmeo kwenye serikali mpya ya Rais Kikwete na majimbo wanayotoka katika mabano kuwa ni Samuel Sitta(Urambo Mashariki) ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dk Harrison Mwakyembe (Kyela), Anne Kilango (Same Mashariki), Januari Makamba (Bumbuli) ambaye alikuwa Msaidizi wa Rais Ikulu katika awamu ya kwanza ya utawala wa Rais Kikwete.
Wengine ni Bernard Membe (Mtama) ambaye katika serikali iliyopita alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Kimataifa na Emmanuel Nchimbi (Songea Mjini) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Mawaziri wengine waliokua katika Serikali iliyopita wanaotajwa kurejeshwa katika kipindi hiki cha mwisho cha utawala wa Kikwete ni Ezikeil Maige (Msalala) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Wiliam Ngeleja (Sengerema) aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini na Adamu Malima (Mkuranga) aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na madini.
Chanzo chetu kimetajwa pia Celina Kombani (Ulanga Mashariki) ambaye alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Profesa Juma Kapuya (Urambo Magharibi), aliyekuwa Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana, Christopher Chiza (Buyungu) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika.
Wengine ni Profesa Mark Mwandosya (Rungwe Mashariki), ambaye alikuwa Waziri Maji na Umwagiliaji, Dk Hussein Mwinyi(Kwahani), aliykuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Shukuru Kawambwa (Bagamoyo), aliyekuwa Waziri wa Miundombinu na John Magufuli (Chato) ambaye alikuwa Waziri wa Maendeleo Mifugo na Uvuvi.
Wabunge wanaotajwa kuingia katika baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza ni Anna Tibaijuka (Muleba Kusini), Salehe Pamba (Pangani), Steven Masele (Shinyanga Mjini), Gerson Lwenge(Njombe Magharibi) na Nyambari Nyangwine (Tarime).
Wengine Shamsi Vuai Nahodha (Mbunge kuteuliwa) na alikuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Angela Mkwizu (Viti Maalum) na Amos Makala(Mvomelo) ambaye ni Mweka Hazina wa CCM, Said Bwanamdogo (Chalinze), Lazaro Nyarandu (Singinda Kaskazini).
Chanzo hicho kimebainisha kuwa Rais Kikwete amedhamiria kuunda baraza dogo la mawaziri litakalo kuwa na tija ikilinganishwa na alilounda wakati akiingia madarakani mwaka 2005, ambalo alilivunja Februari 2008 lilolokuwa na jumla ya mawaziri 60.
Rais Kikwete alilivunja baraza hilo kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kutokana na kashfa ya zbuni tata ya kufuaji umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni ya Richmond.
Hata hivyo, baraza jipya aliloliunda baadaye chini ya Waziri Mkuu mpya, Mizengo Pinda lilikuwa na mawaziri 27 na manaibu mawaziri 21.
Kati ya mawaziri hao wapo walioanguka katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM na wengine waliangushwa katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Sasa wabunge hao wanasubiri huruma ya kuteuliwa na rais katika nafasi kumi ambazo tatu amekwisha zijaza kwa kumteua aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa zamani wa Fedha, Zakia Meghji na Profesa Makame Mnyaa Mbarawa.
Walioanguka katika uchaguzi ni mawaziri watano na manaibu wane, wawili kati yao walishindwa kwenye mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM na wengine saba wakikumbwa na kimbunga cha Uchaguzi Mkuu kwa kubwagwa na wagombea wa vyama vya upinzani.
Mawaziri walioshindwa kutetea viti vyao vya ubunge ni Dk Batilda Burian, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ambaye alipigwa kumbo na mgombea wa Chadema kwenye Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema.
Mwingine ni Lawrence Masha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, yeye alishindwa kutetea kiti chake mkoani Mwanza katika Jimbo la Nyamagana alipoangushwa na mgombea wa Chadema, Ezekiel Wenje.
Katika kundi hilo yumo mwanasiasa mkongwe Philip Marmo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbulu mkoani Manyara kwa miaka mingi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), ambaye aliangushwa na mgombea wa Chadema.
Shamsa Mwangunga, ambaye alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Diodorus Kamara aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mbunge wa Jimbo la Nkenge, walioanguka katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM.
Kwa upande wa manaibu walioanguka katika uchaguzi huo ni Mwantunu Mahiza ambaye alikuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Aisha Kigoda, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Joel Bendera Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk James Wanyancha ambaye alikuwa Naibu Wazara wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.
Wakuu wa mikoa ambao walikuwa pia wabunge walioanguka ni Mohamed Abdul Azizi (Iringa) ambaye alishindwa kutetea jimbo lake la Lindi Mjini kwa kuangushwa na mgombea wa CUF na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega aliyeangushwa na mgombea wa Chadema katikaJimbo la Iringa Mjini.
Uchaguzi wa safari hii pia uliwatupilia mbali wabunge wakongwe akiwamo Getrude Mongela ambaye aliwahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya kwanza na kushika nafasi mbalimbali kwenye taasisi za kimataifa. Pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika. Katika uchaguzi wa mwaka huu aliangushwa na mgombea kutoka Chadema katika jimbo la Ukerewe.
Wengine waliwahi kuwa mawaziri ambo hawakurudi bungeni ni Anthony Diallo aliyewahi kuwa Waziri wa Biashara na Viwanda), Kilontsi Mporogomyi (Naibu, Afya na Ustawi wa Jamii), Lucas Siame (Naibu, Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu), Nazir Karamagi (Waziri, Nishati na Madini) na Ibrahim Msabaha (Waziri, Ushirikiano wa Afrika Mashariki).
Wengine ni Bernard Membe (Mtama) ambaye katika serikali iliyopita alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Kimataifa na Emmanuel Nchimbi (Songea Mjini) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Mawaziri wengine waliokua katika Serikali iliyopita wanaotajwa kurejeshwa katika kipindi hiki cha mwisho cha utawala wa Kikwete ni Ezikeil Maige (Msalala) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Wiliam Ngeleja (Sengerema) aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini na Adamu Malima (Mkuranga) aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na madini.
Chanzo chetu kimetajwa pia Celina Kombani (Ulanga Mashariki) ambaye alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Profesa Juma Kapuya (Urambo Magharibi), aliyekuwa Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana, Christopher Chiza (Buyungu) ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika.
Wengine ni Profesa Mark Mwandosya (Rungwe Mashariki), ambaye alikuwa Waziri Maji na Umwagiliaji, Dk Hussein Mwinyi(Kwahani), aliykuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Shukuru Kawambwa (Bagamoyo), aliyekuwa Waziri wa Miundombinu na John Magufuli (Chato) ambaye alikuwa Waziri wa Maendeleo Mifugo na Uvuvi.
Wabunge wanaotajwa kuingia katika baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza ni Anna Tibaijuka (Muleba Kusini), Salehe Pamba (Pangani), Steven Masele (Shinyanga Mjini), Gerson Lwenge(Njombe Magharibi) na Nyambari Nyangwine (Tarime).
Wengine Shamsi Vuai Nahodha (Mbunge kuteuliwa) na alikuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Angela Mkwizu (Viti Maalum) na Amos Makala(Mvomelo) ambaye ni Mweka Hazina wa CCM, Said Bwanamdogo (Chalinze), Lazaro Nyarandu (Singinda Kaskazini).
Chanzo hicho kimebainisha kuwa Rais Kikwete amedhamiria kuunda baraza dogo la mawaziri litakalo kuwa na tija ikilinganishwa na alilounda wakati akiingia madarakani mwaka 2005, ambalo alilivunja Februari 2008 lilolokuwa na jumla ya mawaziri 60.
Rais Kikwete alilivunja baraza hilo kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kutokana na kashfa ya zbuni tata ya kufuaji umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni ya Richmond.
Hata hivyo, baraza jipya aliloliunda baadaye chini ya Waziri Mkuu mpya, Mizengo Pinda lilikuwa na mawaziri 27 na manaibu mawaziri 21.
Kati ya mawaziri hao wapo walioanguka katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM na wengine waliangushwa katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu.
Sasa wabunge hao wanasubiri huruma ya kuteuliwa na rais katika nafasi kumi ambazo tatu amekwisha zijaza kwa kumteua aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa zamani wa Fedha, Zakia Meghji na Profesa Makame Mnyaa Mbarawa.
Walioanguka katika uchaguzi ni mawaziri watano na manaibu wane, wawili kati yao walishindwa kwenye mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM na wengine saba wakikumbwa na kimbunga cha Uchaguzi Mkuu kwa kubwagwa na wagombea wa vyama vya upinzani.
Mawaziri walioshindwa kutetea viti vyao vya ubunge ni Dk Batilda Burian, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ambaye alipigwa kumbo na mgombea wa Chadema kwenye Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema.
Mwingine ni Lawrence Masha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, yeye alishindwa kutetea kiti chake mkoani Mwanza katika Jimbo la Nyamagana alipoangushwa na mgombea wa Chadema, Ezekiel Wenje.
Katika kundi hilo yumo mwanasiasa mkongwe Philip Marmo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbulu mkoani Manyara kwa miaka mingi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), ambaye aliangushwa na mgombea wa Chadema.
Shamsa Mwangunga, ambaye alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Diodorus Kamara aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mbunge wa Jimbo la Nkenge, walioanguka katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM.
Kwa upande wa manaibu walioanguka katika uchaguzi huo ni Mwantunu Mahiza ambaye alikuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Aisha Kigoda, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Joel Bendera Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk James Wanyancha ambaye alikuwa Naibu Wazara wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.
Wakuu wa mikoa ambao walikuwa pia wabunge walioanguka ni Mohamed Abdul Azizi (Iringa) ambaye alishindwa kutetea jimbo lake la Lindi Mjini kwa kuangushwa na mgombea wa CUF na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega aliyeangushwa na mgombea wa Chadema katikaJimbo la Iringa Mjini.
Uchaguzi wa safari hii pia uliwatupilia mbali wabunge wakongwe akiwamo Getrude Mongela ambaye aliwahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya kwanza na kushika nafasi mbalimbali kwenye taasisi za kimataifa. Pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika. Katika uchaguzi wa mwaka huu aliangushwa na mgombea kutoka Chadema katika jimbo la Ukerewe.
Wengine waliwahi kuwa mawaziri ambo hawakurudi bungeni ni Anthony Diallo aliyewahi kuwa Waziri wa Biashara na Viwanda), Kilontsi Mporogomyi (Naibu, Afya na Ustawi wa Jamii), Lucas Siame (Naibu, Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu), Nazir Karamagi (Waziri, Nishati na Madini) na Ibrahim Msabaha (Waziri, Ushirikiano wa Afrika Mashariki).
CHANZO:MWANANCHI
No comments:
Post a Comment