Advertisements

Thursday, April 28, 2011

MAISHAMEMA EDUCATION AND TRAINING CENTRE      
Proper knowledge        P.O. BOX 35967,      E-mail:  MAISHAMEMA@GMAIL.Com
          For                     DAR ES SALAAM     Mobile:   0716868425
Genuine Solution                                                             0719268764
                                    Website: http//maishamematanzania.blogspot.com

NAFASI   YA   MAFUNZO   NA  KAZI

Wewe  ni  kijana wa  kike mwenye  umri  wa kati  ya  miaka  18  hadi 35?
Una  elimu  ya  kuanzia  kidato  cha  nne, sita  na  kuendelea?
Unapenda  kufanya  kazi  ya  kuwaelimisha  vijana  wenzako  wa  kike  waliopo  mashuleni, vyuoni  na  magerezani  juu  ya  madhara  ya  vitendo  vya  kisagaji?

Kama jibu  ni  ndio  basi  hii  ni  habari  njema  sana  kwako. Kituo  cha  Elimu, Mafunzo, Utafiti  na  Uimarishaji  Maarifa  cha  MaishaMema  Education &  Training  Center  cha  jijini  Dar  es  salaam  kupitia  katika  mradi  wake  wa “ Sexualitity  Education  &  Awareness  Project  Campaign” ( SEA  Project  Campaign ), kinatangaza  nafasi  hamsini (  50 )  za  mafunzo  na  kazi  kwa  vijana  wa  kike  wa  kitanzania  wenye  sifa  tajwa  hapo  juu   kwa  ajili  ya  kupata  mafunzo  yatakayo  wawezesha  kufanya  kazi  na  kituo  katika  mradi huu.

ADA  YA  MAFUNZO: Mafunzo  yanatolewa  bure  kabisa.
ADA    YA  KUJISAJILI:   Ada  ya  kujisajili  katika  mafunzo  haya  ni  shilingi  Elfu  Thelathini  Tu ( Tshs. 30,000 )  ambayo itajumuisha  gharama  za  kitambulisho  na  T.Shirt..

MUDA  WA  MAFUNZO:
Mafunzo  yatachukua  miezi  miwili. Mwezi  mmoja, mafunzo  ya  darasani  na  mwezi  mmoja  wa  mafunzo  kwa  njia  ya  vitendo (  Field  Trainings )

Baada  ya  mafunzo, wahitimu  watafanya  kazi  na  kituo  katika  mradi  huu.

Mafunzo  yataanza   tarehe  09  MAY  2011. Na  yatakuwa  yakifanyika  katika  shule  ya  sekondari  Perfect  Vision, kuanzia  saa  nane  na  nusu  za  mchana  hadi  saa  kumi  na  mbili  na  nusu  za  jioni.
Mwisho  wa  kujisajili    ni  tarehe  07 MAY  2011.  Endapo  idadi  ya  watu  tunao  wataka  itatimia  kabla  ya  tarehe  07  MAY 2011  tutasitisha  zoezi  la  kusajili..

KUJISAJILI.  Fika  katika  ofisi  zetu  zilizopo  katika  shule  ya  Sekondari  Perfect  Vision, iliyopo  karibu  na  jengo  la  Ubungo  Plaza.


KWA  MAELEZO  ZAIDI.PIGA  0719268764.  AU  O716868425

No comments: